Tetesi: Tarehe 21/12/2024 Mbowe atatangaza rasmi kutogombea uenyekiti na atamuunga mkono Tundu Lissu


Chama cha ukanda, ukabila, udini na utaifa katika ubora wake, ccm itaendelea kutawala japo ina madhaifu yake
 
Hii ndoto ya mchana ,anataka mbwai na iwe mbwai huyo na lipumba baba yao mmoja tusubiri
 
Natamani iwe hivyo
 
Hii ni tetesi kama tetesi zingine.Mzee wa miaka 20 ya kukomaa
 
Haahaa nitaamini nikiona, wale machawa kina boni yai na yeriko itakuwaje?
Unaweza kumtetea tajiri kwa kumtukana mshindani wake, tajiri akakushangaza siku ukiwakuta wako meza moja na uliyemtukana kwa niaba yake wanakula bia na kucheka😄
 
Approch ya Lissu kuutaka uwenyekiti ilikuwa na walakini - hajui kutumia uugwana, hana lugha ya ki diplomasia anapayuka sana.

Kwa hiyo awe tayari kujipima ubavu ya Jabari.
 
Agombee kife
 
Atakuwa amefanya vyema sana
 
Ruzuku tamu sitegemei kuona Mbowe akiachia kiti na nikichanganya na maigizo ya jana ndio sina imani kama hilo jambo litatokea.
 

Nazikubali harakati za Lissu. Ila asipopunguza makali kidogo kuna uwezekano wa harakati zake kubackfire. Hiyo itapunguza sana umaarufu wa CHADEMA. Kama mass itasupport then Samia itabidi aback down na hiyo itakuwa a plus kwenye movement. Hiyo itafanikiwa tu kama ataachana na kutoambilika kwake. He is bit stubborn by character. Wasawahili wanasema, JASILI HAACHI ASILI.
 
Mandela anaheshimika mpaka leo na jina lake litaendelea kuwa reference katika kupigania haki, kujitoa kwaajili ya watu , siyo kwa sababu alikaa madarakani kwa muda mrefu, bali kwa sababu ya kuwaonesha njia wananchi wa Afrika Kusini.

Mbowe ataheshimika na kukumbukwa nyakati zote kama atachukua uamuzi huo kuliko kufanya vinginevyo.

Hajachelewa sana kufanya hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…