Uchaguzi 2020 Tarehe 28/10/2020: Siku ya kuweka Historia kuu Tanzania

Uchaguzi 2020 Tarehe 28/10/2020: Siku ya kuweka Historia kuu Tanzania

Na wajinga ni mashabiki wakubwa wa ccm, sijui itakuwaje sasa

Sasa sijui wajinga ni kina nani, Chadema na wanao chagua M'kiti, Katibu Mkuu, Naibu katibu Mkuu na mgombea mwenza vilaza. Wajanja wanaongozwa na wajinga, Washika taa hawaoni. Poleni sana.

Wasomi wote katika uongozi wamewakimbia. Na safari hii huyo mnaemwita mshamba ndio atakae teketeza Chadema na upinzani kwa ujumla.

Na CCM yenye viongozi wajinga ndio itatawala miaka 100 ijayo. Vipanga wa CCM Oyeeeeee.
 
Tuwahamishe watu wakapige kura kwa nguvu hapo October mwaka huu ili Tanzania iweke historia mpya mwaka huu
Nimejifunza mengi sana kwenye mkutano fulani mh.lisu watu wako kimya ila wana mengi moyoni nimewaona hata wana ccm ninawafahamu wamemuelewa lisu.tuombe Mungu maana huyu Mungu ni wa wote
 
Hizo zote propoganda. hakuna kosa kubwa kama kumchaguwa mtu mwenye ghadhabu kama Tundu Lissu. Kwanza si mstaarabu. Domo lake limejaa matusi siku zote. Hata sasa hivu yuko kwenye shida kwa kuzuiliwa kutoa matusi, ndiyo maana anapwaya. Mimi na pamoja wengine tumotoka mbali na kuona mengi. Enzi zetu za sekondari tulikuwa trunadhania kumchaguwa mtu mtukutu na asiyesikia ya waalimu ndiyo kunatupa kiranja wa upande wetu.

Lakini ikitokea kumchaguwa kaka wa namna hiyo anageuka mbogo na kutoa vibano kwa wanafunzi. Huyu Lissu hata kabla hajapewa kura tayari ana dharau na majivuno. Nilisikia siku moja akisema yeye mtoto wake hasomi sekondari za kijinga za TZ. Akiingia madarakani ujuwe ndiyo basi elimu itakufa. Hivi Lissu ana uchungu gani na TZ. Uanaharakati na siasa ni vitu mbalimbali. Wanaharakati siku zote ni kutafuta mabaya ya nchi na kuficha mazuri ili agenda yao itimie.

Hao ni watu ambaohugharimiwa na mabeberu , kwa hiyo wakipata pesa wanaambiwa nini cha kutafuta na nam,na ya kukitafuta. Uana harakati ni ajira, ajira kutoka kwa wenye pesa kwenda kwa wenye njaa kama Lissu. Kwa vile uuanaharakati unalipiwa kwa $$$ ndiyo maana unaona watu wanaspiga kelele karibu mishipa ya shingo kupasuka.Do not and never trust mwanaharakati Tundu Lissu.
 
Watz wameshasema hapana..... Hawataki tena dikteta na mharibifu wa uchumi wa nchi na watu wake... magufuli na ccm yake iliyooza na kunuka mtaani
 
Kule mnakoshinda wanayaharibu matokeo kwa kuvipa vyama vileee number isiyokuwepo.

Utaona DP 5%, ADC 7%, NCCR 6%, CHAUMA 10% , ACT 30% ,CCM 15%, Chadema 27%,

Halafu mnabaki mmeduwaa.
 
Kule mnakoshinda wanayaharibu matokeo kwa kuvipa vyama vileee number isiyokuwepo.
Utaona DP 5%, ADC 7%, NCCR 6%, CHAUMA 10% , ACT 30% ,CCM 15%, Chadema 27%,
Halafu mnabaki mmeduwaa.
Nguvu ya umma itaamua mwaka huu!!
 
Hizo zote propoganda. hakuna kosa kubwa kama kumchaguwa mtu mwenye ghadhabu kama Tundu Lissu. Kwanza si mstaarabu. Domo lake limejaa matusi siku zote. Hata sasa hivu yuko kwenye shida kwa kuzuiliwa kutoa matusi, ndiyo maana anapwaya. Mimi na pamoja wengine tumotoka mbali na kuona mengi...
Lissu ana ghadhabu gani?? Embu fafanua??? Sie kama watanzania tulimsikia akiwa kanisani singida akitoa shukrani alisema hatolipa kisasi kamwe kwa yeyote aliyemfanyia mabaya.

Ni matusi gani pia aliyotukana Lissu??? Embu fafanua???

Ni lini Lissu alisema mtoto wake hawezi kusoma shule za Africa??? Alafu kwa mfumo wa Elimu wa a Tanzania unafikiri unawapa elimu bora watoto wa masikini wa Tanzania kwenye karne hii ya sayansi na teknolojia???
 
Nimejifunza mengi sana kwenye mkutano fulani mh.lisu watu wako kimya ila wana mengi moyoni nimewaona hata wana ccm ninawafahamu wamemuelewa lisu.tuombe Mungu maana huyu Mungu ni wa wote
Kweli kabisa. Watanzania wana maamuzi magumu ya kufanya mwaka huu. Na wahasishwe zaidi wasiogope wala kusita kufanya maamuzi magumu mwaka huu!!
 
Kwangu mimi tarehe 28/10/2020 itakuwa ni siku ambayo mfanowe ni tarehe 9/12/1961 tulipopata uhuru na hivyo kujinusuru kutoka mikononi mwa wakoloni weupe waliotukalia kwa miaka karibu 40!

Ninayo matumaini makubwa kuwa siku hiyo tutapata uhuru tena na kuweza kujinusuru kutoka mikononi mwa hawa wakoloni wetu weusi, CCM waliotukalia kwa miaka zaidi ya hiyo 40!

Wengine tunajua kwa nini Magufuli, akiwa hana uwezo, alisukumiziwa utawala wa taifa hili kwa sifa kuu tatu...ujeuri wake, uthubutu wake na uzoefu wake ndani ya tawala zilizomtangulia.

Tahadhari.

Kwa kiongozi mwenye huruma, busara na hekima, anayejali, mfadhili, mtulivu na msikivu, sifa hizi ni kichocheo cha utawala imara na wa maono unaozingatia sheria na katiba, utawala usioyumbishwa katika kutoa haki na utawala usiosita kukiri kosa na kujirekebisha.

Kwa kiongozi asiye na huruma, busara wala hekima, asiyejali, mkatili, anayekurupuka na mwenye kiburi, sifa hizi ni kichocheo cha utawala wa kifashisti na mateso, utawala usioheshimu sheria na Katiba, utawala unaobagua katika utoaji wa haki na utawala usiopenda kukosolewa.

Je kwa sasa tuko wapi?

Mengi yamesemwa na hivyo sitakuwa na haja ya kuyarudia isipokuwa kuhusu moja tu, ufisadi. Kwa miaka mingi ufisadi umekuwa ukidaiwa kupigwa vita, je leo tunaweza kujidai tumeutokomeza ufisadi nchini?

Jibu langu ni hapana, ufisadi haukutokomezwa na badala yake, chini ya Magufuli, aina mpya ya ufisadi ambayo ni mbaya kuliko wa awali uliandaliwa, ukalelewa, ukakua na sasa matunda yake yanavunwa

Ni ufisadi gani huo?

Ni ufisadi wa serikali. Ufisadi huu unaolitafuna taifa sasa hivi ni ule unaoendeshwa na vyombo vya dola vya serikali ikisimamiwa na kiongozi wake mkuu. Wafanya kazi, wakulima, wafanya biashara na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) wote ni waathirika wa ufisadi huu.

Serikali ikiwa ndiyo fisadi mkuu imeamua kuvitumia vyombo vya dola na idara za serikali kuyafisadi makundi haya. Wafanya kazi wanayimwa haki zao, wakulima wanadhulumiwa mazao yao, wafanya biashara wananyang'anywa pesa zao na NGOs kuzuiwa pesa zao.

Hebu fikiria, wote waliowahi kutuhumiwa kwa ufisadi huko nyuma wamekaribishwa ndani ya CCM, chama kinachoongoza serikali na wote wamerudi. Wengi wa watuhumiwa hawa wameteuliwa kugombea ubunge na walioachwa wanaahidiwa ajira kwenye hizi kampeni.

CCM imeamua rasmi kwamba UFISADI ndio sera yake. Ufisadi wa sasa ni state sponsored na vyombo kama TRA, TCRA, TAKUKURU na idara za serikali vimegeuka na kuwa vya unyang'anyi katika mpango kabambe wa kuwafilisi raia wa nchi hii wasiokubaliana na uovu huu.

Magufuli ameweza kufanikisha yote haya kwa ujeuri wa kutisha, uthubutu wa kutisha na uzoefu wa miaka zaidi ya ishirini. Kumbukeni kile alichoapa siku chache baada ya kutangazwa mshindi kwamba wastaafu wasiwe na hofu, walale bila wasiwasi kwani atawalinda.

Na sasa anapita akitaka aongezewe awamu ya pili, kweli! Hapana, Mh. Tundu Antiphas Lissu, njoo uliokoe taifa lako linaloangamia!
 
Nipo kahama hapa submarine panatoka macontainer ya kupogia kura kila siku chadema fuatilieni na kuna watu waccm wanakaa hapa akiwemo kishimba aliyekuwa mbunge wa sasa wa ccm embu fuatilieni mujihakikishie
 
Amani iwe nanyi watu wa Mungu!

Kwa kipindi cha miaka 59 tangu uhuru, Tanzania imekuwa ikiongozwa na Chama cha mapinduzi. Katika miaka hii yote watanzania wamepitia mengi sana ila kila siku maisha ya watanzania yamezidi kuwa ya kuogofya na ya kusikitisha. Umasikini umekuwa donda kuu la watanzania na mbaya zaidi katika kipindi hicho chote, watanzania wamekuwa wakishuhudia wanasiasa wakizidi kujineemisha kwa pesa zao za kodi na mbaya zaidi wamekuwa wakiwafanya watanzania kuwa ombaomba na watumwa kwenye nchi yao.

Tofauti na miaka ya maraisi waliopita ambao pamoja na kujineemisha binafsi ila angalau walijitahidi kuheshimu utu wa mtanzania kwa kumuheshimu na kutomnyanyasa Ila katika kipindi cha miaka 5 watanzania wameshuhudia unyanyasaji mkubwa wa haki zao kutoka kwa watu waliojionesha kwao kuwa watu wazuri kumbe walikuwa chui waliojivika ngozi ya Kondoo!!

Mungu si Athumani alimuokoa mtoto wake Tundu Antiphas Lissu kwenye jaribio la mauaji hapo tarehe 7 mwezi wa 9 mwaka 2017 akiwa amepanga historia kuu iandikwe hapa Tanzania hapo tarehe 28/10/2020. Kwa hiyo ewe mtanzania usikose kuwa sehemu ya historia hii kuu inayoenda kuandikwa hapo tarehe 28/10/2020.

Kwa nini Tarehe 28/10/2020 ni siku ya watanzania kuandika Historia kuu juu ya nchi yao?

1. Kama wewe ni mzazi uliyemsomesha mtoto wako kwa shida hadi akamaliza chuo na hadi leo hajapata ajira, basi tarehe 28/10/2020 nenda kapige kura kuonesha kuwa CCM haistahili kabisa kuendelea kutawala nchi hii kwa sababu mfumo wao na sera zao umefanya mwanao akose ajira. Tarehe hiyo mchague Tundu Antiphas Lissu kuweka historia mpya Tanzania.

2. Kama wewe ni mtanzania uliyefanya kazi katika maisha yako ili uje kuishi vizuri, ila CCM wamefilisi mifuko ya pensheni na kufanya upate pensheni kidogo na kuishi kwa tabu, basi Tarehe 28/10/2020 nenda kaandike historia mpya kwa kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

3. Kama wewe ni kijana uliyesoma kwa shida huku ukiingia mkataba na serikali wa kukukata asilimia 6 mpaka 7 ya mshahara ukipata ajira, ila CCM ya awamu ya tano imekufanya ukatwe asilimia 15 basi nenda kaandike historia tarehe 28/10/2020 kwa kuikataa na kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.

4. Kama Wewe ni Mtanzania ambaye gharama za matibabu zimekuwa kubwa na umekuwa ukipata shida ya gharama za matibabu kwa miaka yote basi tarehe 28/10/2020 nenda kaiadhibu CCM kwa kuinyima kura na uandike historia kwa kumchagua Tundu Antiphas Lissu!

5. Kama Wewe ni mfanyakazi ambaye kwa miaka 5 hukupata haki yako ya kuongezwa mshahara na mwaka huu umeona bima ya afya ikiondoa baadhi ya dawa kwenye mfumo wa bima huku gharama ya maisha ikizidi kupanda basi kaandike historia kuu tarehe 28/10/2020 kwa kuinyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

6. Kama wewe ni mzazi uliyepata shida kumsomesha mtoto wako private na amefika chuo amenyimwa mkopo kwa kusomeshwa private elimu ya chini basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia Kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

7. Kama wewe ulikuwa mfanyakazi uliyeajiliwa sehemu ila Sera za Awamu ya tano ya CCM zikafanya upoteze ajira yako kwa kampuni kufirisika basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

8. Kama wewe ni mfanyabiashara uliyeangaika kupata mtaji ikiwemo kukopa, ila kodi za tra na mnyanyaso ya tra yamekufanya ufunge biashara au ufirisike basi tarehe 28/10/2020 Kawe sehemu ya historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

9. Kama Wewe ni mkulima uliyekuwa ukiuza mazao yako vizuri bila shida ila sera za Chama cha mapinduzi zikakupiga marufuku kuuza mazao nje na kupelekea ukafirisika na kupata hasara basi Kawe sehemu ya historia kuu hapo tarehe 28/10/2020 kwa kuwanyima kura CCM na kumpa kura Tundu Antiphas Lissu.

10. Kama wewe ni kijana ambayo umekuwa ukihangaika bila ajira kwa sababu ya sera mbovu za kiuchumi za Chama cha mapinduzi basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu katika nchi yetu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.

Ewe mtanzania, kumbuka sehemu pekee ya wewe kueleza hisia zako juu ya mwanasiasa yeyote au Sera zozote zinazokuathili kimaisha na kiuchumi ni kwenye Sanduku la Kura. Hivyo Tarehe 28/10/2020 nenda Kawe sehemu ya Historia kuu inayoenda kuandikwa ya kuweka utawala mpya hapa Tanzania kwa maslahi mapana ya nchi yetu na watu wake

Share na mwenzako!
Hilo halina mjadala
 
Kwangu mimi tarehe 28/10/2020 itakuwa ni siku ambayo mfanowe ni tarehe 9/12/1961 tulipopata uhuru na hivyo kujinusuru kutoka mikononi mwa wakoloni weupe waliotukalia kwa miaka karibu 40!

Ninayo matumaini makubwa kuwa siku hiyo tutapata uhuru tena na kuweza kujinusuru kutoka mikononi mwa hawa wakoloni wetu weusi, CCM waliotukalia kwa miaka zaidi ya hiyo 40!

Wengine tunajua kwa nini Magufuli, akiwa hana uwezo, alisukumiziwa utawala wa taifa hili kwa sifa kuu tatu...ujeuri wake, uthubutu wake na uzoefu wake ndani ya tawala zilizomtangulia.

Tahadhari.

Kwa kiongozi mwenye huruma, busara na hekima, anayejali, mfadhili, mtulivu na msikivu, sifa hizi ni kichocheo cha utawala imara na wa maono unaozingatia sheria na katiba, utawala usioyumbishwa katika kutoa haki na utawala usiosita kukiri kosa na kujirekebisha.

Kwa kiongozi asiye na huruma, busara wala hekima, asiyejali, mkatili, anayekurupuka na mwenye kiburi, sifa hizi ni kichocheo cha utawala wa kifashisti na mateso, utawala usioheshimu sheria na Katiba, utawala unaobagua katika utoaji wa haki na utawala usiopenda kukosolewa.

Je kwa sasa tuko wapi?

Mengi yamesemwa na hivyo sitakuwa na haja ya kuyarudia isipokuwa kuhusu moja tu, ufisadi. Kwa miaka mingi ufisadi umekuwa ukidaiwa kupigwa vita, je leo tunaweza kujidai tumeutokomeza ufisadi nchini?

Jibu langu ni hapana, ufisadi haukutokomezwa na badala yake, chini ya Magufuli, aina mpya ya ufisadi ambayo ni mbaya kuliko wa awali uliandaliwa, ukalelewa, ukakua na sasa matunda yake yanavunwa

Ni ufisadi gani huo?

Ni ufisadi wa serikali. Ufisadi huu unaolitafuna taifa sasa hivi ni ule unaoendeshwa na vyombo vya dola vya serikali ikisimamiwa na kiongozi wake mkuu. Wafanya kazi, wakulima, wafanya biashara na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) wote ni waathirika wa ufisadi huu.

Serikali ikiwa ndiyo fisadi mkuu imeamua kuvitumia vyombo vya dola na idara za serikali kuyafisadi makundi haya. Wafanya kazi wanayimwa haki zao, wakulima wanadhulumiwa mazao yao, wafanya biashara wananyang'anywa pesa zao na NGOs kuzuiwa pesa zao.

Hebu fikiria, wote waliowahi kutuhumiwa kwa ufisadi huko nyuma wamekaribishwa ndani ya CCM, chama kinachoongoza serikali na wote wamerudi. Wengi wa watuhumiwa hawa wameteuliwa kugombea ubunge na walioachwa wanaahidiwa ajira kwenye hizi kampeni.

CCM imeamua rasmi kwamba UFISADI ndio sera yake. Ufisadi wa sasa ni state sponsored na vyombo kama TRA, TCRA, TAKUKURU na idara za serikali vimegeuka na kuwa vya unyang'anyi katika mpango kabambe wa kuwafilisi raia wa nchi hii wasiokubaliana na uovu huu.

Magufuli ameweza kufanikisha yote haya kwa ujeuri wa kutisha, uthubutu wa kutisha na uzoefu wa miaka zaidi ya ishirini. Kumbukeni kile alichoapa siku chache baada ya kutangazwa mshindi kwamba wastaafu wasiwe na hofu, walale bila wasiwasi kwani atawalinda.

Na sasa anapita akitaka aongezewe awamu ya pili, kweli! Hapana, Mh. Tundu Antiphas Lissu, njoo uliokoe taifa lako linaloangamia!
Mkuu andiko limeenda shule. Asante sana na Mungu akubariki
 
Nipo kahama hapa submarine panatoka macontainer ya kupogia kura kila siku chadema fuatilieni na kuna watu waccm wanakaa hapa akiwemo kishimba aliyekuwa mbunge wa sasa wa ccm embu fuatilieni mujihakikishie
Jiitahidi utuletre na kaphoto tuwanyoshe hawa. Dawa yao ni timing
 
Kwangu mimi tarehe 28/10/2020 itakuwa ni siku ambayo mfanowe ni tarehe 9/12/1961 tulipopata uhuru na hivyo kujinusuru kutoka mikononi mwa wakoloni weupe waliotukalia kwa miaka karibu 40!

Ninayo matumaini makubwa kuwa siku hiyo tutapata uhuru tena na kuweza kujinusuru kutoka mikononi mwa hawa wakoloni wetu weusi, CCM waliotukalia kwa miaka zaidi ya hiyo 40!

Wengine tunajua kwa nini Magufuli, akiwa hana uwezo, alisukumiziwa utawala wa taifa hili kwa sifa kuu tatu...ujeuri wake, uthubutu wake na uzoefu wake ndani ya tawala zilizomtangulia.

Tahadhari.

Kwa kiongozi mwenye huruma, busara na hekima, anayejali, mfadhili, mtulivu na msikivu, sifa hizi ni kichocheo cha utawala imara na wa maono unaozingatia sheria na katiba, utawala usioyumbishwa katika kutoa haki na utawala usiosita kukiri kosa na kujirekebisha.

Kwa kiongozi asiye na huruma, busara wala hekima, asiyejali, mkatili, anayekurupuka na mwenye kiburi, sifa hizi ni kichocheo cha utawala wa kifashisti na mateso, utawala usioheshimu sheria na Katiba, utawala unaobagua katika utoaji wa haki na utawala usiopenda kukosolewa.

Je kwa sasa tuko wapi?

Mengi yamesemwa na hivyo sitakuwa na haja ya kuyarudia isipokuwa kuhusu moja tu, ufisadi. Kwa miaka mingi ufisadi umekuwa ukidaiwa kupigwa vita, je leo tunaweza kujidai tumeutokomeza ufisadi nchini?

Jibu langu ni hapana, ufisadi haukutokomezwa na badala yake, chini ya Magufuli, aina mpya ya ufisadi ambayo ni mbaya kuliko wa awali uliandaliwa, ukalelewa, ukakua na sasa matunda yake yanavunwa

Ni ufisadi gani huo?

Ni ufisadi wa serikali. Ufisadi huu unaolitafuna taifa sasa hivi ni ule unaoendeshwa na vyombo vya dola vya serikali ikisimamiwa na kiongozi wake mkuu. Wafanya kazi, wakulima, wafanya biashara na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) wote ni waathirika wa ufisadi huu.

Serikali ikiwa ndiyo fisadi mkuu imeamua kuvitumia vyombo vya dola na idara za serikali kuyafisadi makundi haya. Wafanya kazi wanayimwa haki zao, wakulima wanadhulumiwa mazao yao, wafanya biashara wananyang'anywa pesa zao na NGOs kuzuiwa pesa zao.

Hebu fikiria, wote waliowahi kutuhumiwa kwa ufisadi huko nyuma wamekaribishwa ndani ya CCM, chama kinachoongoza serikali na wote wamerudi. Wengi wa watuhumiwa hawa wameteuliwa kugombea ubunge na walioachwa wanaahidiwa ajira kwenye hizi kampeni.

CCM imeamua rasmi kwamba UFISADI ndio sera yake. Ufisadi wa sasa ni state sponsored na vyombo kama TRA, TCRA, TAKUKURU na idara za serikali vimegeuka na kuwa vya unyang'anyi katika mpango kabambe wa kuwafilisi raia wa nchi hii wasiokubaliana na uovu huu.

Magufuli ameweza kufanikisha yote haya kwa ujeuri wa kutisha, uthubutu wa kutisha na uzoefu wa miaka zaidi ya ishirini. Kumbukeni kile alichoapa siku chache baada ya kutangazwa mshindi kwamba wastaafu wasiwe na hofu, walale bila wasiwasi kwani atawalinda.

Na sasa anapita akitaka aongezewe awamu ya pili, kweli! Hapana, Mh. Tundu Antiphas Lissu, njoo uliokoe taifa lako linaloangamia!
Ni kweli kabisa ndugu! Kuna unyang’anyi mkubwa sana unaendelea sasaivi Tanzania dhidi ya watanzania unaofanywa na TAKUKURU, TRA,TCRA na DPP
 
Back
Top Bottom