Tarehe 9-12-1961 ilikukuta wapi?


Ndio ujinga huu na kasumba tulionao watanzania tulio wengi.

Kwa hiyo kwenda nchi za nje mfano huko Middle East nakadharika ndo unaona ni jambo la ajabu?
Pole sana maana pamoja na kwenda huko nje bado
Unafikra za kizamani mno.

Nchi za nje sasa hivi kila mtu anaenda na hata kusoma nimesomea huko pia kwa hiyo bado nina pata mashaka mpaka karne hii unaona jambo la kwenda ughaibuni kama fimbo.

Et una kazi yako na maisha mazuri sasa hivyo vimefata nini nikuone wivu mtu kama wewe ambaye sikufahamu na ID yako fake? I’m better than that au unafikiri kila mtu ni wakupenda sifa hapa jukwaani na kuanza ku brag?


Mtu mzima anajielewa hawezi kuwa na maneno kiasi hicho ukweli ni dhahiri kwamba ulichokisema ni uongo mtupu.
 
Halafu unadiriki kuandika kuwa ya kwako ni kweli kuwa umesoma nje na kutembea sawa ila sithubutu kukuita muongo kwa sababu sikufahamu
Wewe umesema mimi ni wa 80 kwa uhakika kabisa na mimi nikakuambia miaka hiyo nilikuwa nimeishatoka nje ya nchi
Sasa kuna nini cha ajabu nikisema nilikuwa nje wakati huo maana nimejibu kadiri ya maneno yako ulivyoandika
Mimi sibishani hapa ila nimeandika part of my life, that's all why should I lie about it
BTW kuwa na amani mkuu humu kama ulivyosema hatujuani lakini umediriki kuniita muongo wakati hatujuani, sasa huoni kama kuna tatizo hapo

Uwe na mchana mwema na uwe na amani maana hasira zinaleta kashfa na matusi na kuvunjiana heshima wakati mtu mwenyewe humjui
Have a great day
 
Kuna wengine ni kizazi cha uongo tu kwa asili.
Na kweli mkuu na ndio wanaharibu mpaka vizazi na vizazi
Hapo unakuta moja wameandika 50 nyingine 60 na kuna moja imewekwa eti ni siku ya Uhuru na hapo hapo mwingine kaandika ni sikukuu ya Eid waislam wanaandaa mahitaji yao
Hii hapa picha ila ina maelezo kibao ya kariakoo
 
Nilikuwa heaven na wanangu akina petrol tunapiga story kuwa hii nchi maendeleo yatakuwa goi goi
 
Sio kwamba tu jinsi ambavyo mahali hiyo siku iliponikuta bali naweza kukuelezea jinsi ambavyo ninaikumbuka...

Wakati huo nilikuwa mdogo kiumri na sikutambua sana kama wazungu ni watawala wa kikoloni, nilikuwa naamini ni miongoni mwa jamii za Tanganyika lakini ni watu wenye uelewa zaidi yetu kwa sababu hata nilipobahatika kuwaona wazungu, walikuwa ni watu wenye kutumia magari na vitu vingine ambavyo kwa pale kijijini kwetu havikuwepo...

Baada ya miaka kadhaa, ndipo nilipotambua ya kwamba wazungu walikuwa ni watawala baada ya kuanza kusikia harakati za Mwalimu Nyerere za kudai uhuru...

Pia kukawa na habari kama hizo nchi jirani haswa Kenya ambapo wao kulikuwa na machafuko ya Maumau ambapo wazalendo wa huko Kenyatta na Kimathi na wengineo...

Ile siku ya uhuru wa Tanganyika ilikuwa tumefunga shule, ambapo tulitangaziwa kwamba sherehe rasmi za uhuru zitafanyika Dar es Salaam...

Baadaye nilisikia wazee wangu wakisema kwamba sambamba na sherehe kubwa ya uhuru huko Dar es Salaam, kila kijiji kitafanya sherehe na wakoloni walitoa takribani shilingi 1000 au 1500 (wanaokumbuka wataweka sawa) kama bajeti ya sherehe kwa kila kijiji...

Mwisho, ilipofika mida ya usiku mzee wangu na wazee wengine na watu wengine walienda kwenye ukumbi wa mahakam ya mkoloni ambapo huko waloenda kuungana kwa pamoja kwenye zoezi la kushusha bendera ya mkoloni na kuipandisha ile ya Tanganyika, zoezi lililoambatana pia na kutoa picha za Malkia Elizabeth wa pili na kuiweka ile ya Mwalimu Nyerere...

Mwisho...
 

Mwandiko wa Mtu wa 80s huu
 

Hata ningekuwa nakufahamu kwa jina halisi siwezi kukuchukia. Ila ulimbukeni na uongo uache


Have a fabulous weekend!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…