Tathmini ya mapato ya kilimo cha michungwa 1000 baada ya miaka 3

Tathmini ya mapato ya kilimo cha michungwa 1000 baada ya miaka 3

nimekujbu lkua sina utaalamu wa kujua maeneo ila nimeona katika mkoa wa pwani,dar, tanga na morogoro nimesikia sasa maeneo mengine waulize wataalamu wa climate
 
nashkuru sana kwa maelezo yako ila nakuomba nikwambie kitu kwamba usikatae mm nina baba angu tangu enzi za ukoloni ishu zake ni michungwa ila sasa ameng'oa michungwa ya aina zote ikiwemo valencia,jaffer na msasa na amepanda aina hii ya michungwa ninayokueleza hemu google machungwa toka brazil then angalia idadi kuna michungwa inazaa mpaka 16000 kwa kila mchungwa jaribu kufuatilitilia kilimo vizuri wacha kukurupuka

mkuu ... ni hatari sana kufanya kilimo katika mazingira yetu kwa kutumia google

swali moja tuu kwako ..... hichi unachotuambia ni idea tu au umeshakifanya kwa kiwango fulani hata kama ni kidogo,

pia nina mashaka na bei ya kuuzia machungwa .... hapa dar wakati wa msimu machungwa sokoni huuzwa hadi sh.50 bei ya reja reja .... je bei yako ya kuuzia uliyotoa ina uhalisia?
 
nimekujbu lkua sina utaalamu wa kujua maeneo ila nimeona katika mkoa wa pwani,dar, tanga na morogoro nimesikia sasa maeneo mengine waulize wataalamu wa climate

Mkuu ni ukubwa gani wa Shamba unahitajika? vipi mtu akiwa na heakari kama Tano zinatosha? na vipi bei ya Mche mmoja wa hiyo aina unayo sema,
 
sikiliza machungwa aina hii ni makubwa na matamu ndio yale unayouziwa 300 mjini kwa matenga na kwa quality yake waweza kuuza hata super market na aliekua na muda aje nimpeleke akaone nilipofikia nimeanza na miche 300 ila sasa nina michungwa 21000 na sina eneo kubwa ila ningepanda hata kama ni michungwa milioni na nia na madhumuni ya kukupeni wazo hili nataka kuwauzia miche ili na nyinyi mufaidike bado nazalisha miche na shamba langu limejaa hapa natafuta soko la miche
 
kwa heka tano ni miche makadirio ni kama miche 350 zinatosha na tadhmini ya miche 350 kila mwaka unaweza kuingiza 400,000,000
 
ila ni baada ya miaka mitatu miche huanza kuzaa na pia inahitaji ushughulikiaji na katika miezi 14 ya mwanzo kila siku kila mche umwagiliziwe liter mbili
 
Mkuu kahtan Ahamed heshim sana,

Nimepitia bandiko lako nikaona yapo baadhi ya mambo yanahitaji kuboreshwa kidogo.

Kwanza hakuna mchungwa unaweza kuzaa chungwa 4,000.Uzoefu wangu wa kulima machungwa wa zaidi ya miaka mitano mti mmoja ni kati ya chungwa 600 - 800 katika msimu mmoja.

Kuna aina nyingi za chungwa zinazolimwa Tanzania hasa mikoa ya ukanda wa Pwani ie Tanga,Pwani,Dar na Morogoro.

[1] Msasa (Kubwa na Ndogo) hii ni aina nzuri ya chungwa,inaweza kusafirishwa umbali mrefu bila kuharibika.Soko lake kubwa ni Kenya na miji ya Dar,Arusha,Kilimanjaro ....

[2] Valensia ni aina ya chungwa linaloweza kusafirishwa mbali.Aina hii ya Chungwa ipo kwa wingi Muheza na kidogo limeanza kulimwa maeneo ya Korogwe na Handeni (Michungwani,Kwedi Zinga na Kabuku) Uzuri wa Valensia msimu wake mara nyngi unatokea wakati msimu wa chungwa umekwisha au machungwa yanakuwa hayapo sokoni kwa wingi.Wakulima wengi wanapendelea kulima aina hii ya chungwa kwasababu za kibiashara zaidi.

[3] Jaffar ni aina ya chungwa kubwa zinazozaa sana mara nyingi msimu wake wa mavuno unagongana na Msasa.Jaffa ni kubwa,lina maji mengi,ni tamu sana,linaweza kuliwa hata kama halijaiva vizuri.Ubaya pekee wa Jaffa ni kuharibika kwa wingi linaposafirishwa mbali.wafanyabiashara wengi hawapendi kuyanunua kwa wingi kwa kuhofia kuharibika yanapofika sokoni.Jaffa si chungwa zuri kwa biashara lakini si vibaya ukayachanganya kidogo shambani let say katika eka 13 ukaweka eka 1.

Nitarejea baadae kukupatia uzoefu wangu wa namna bora ya kuanzisha shamba la michungwa,miembe na minanasi ukipenda stay tune.

Usichukue muda mrefu mkuu tafadhali urudi kutoa uzoefu
 
dah .... ndugu yangu

Mkuu vp mbona unashtuka mashetani yako hayapendi kuwa milionea nini? Mi bado nawaza huo mchungwa wenyew uwezo wa kubeba machungwa elfu nne ambayo uzito wake unakaribia tani moja labda huo mchungwa unazaa mara tatu kwa mwaka ukijumlisha uzao wote ndo unatapata hiyo idadi ya machungwa au wenyewe unazaa non stop kila mwezi unavuna hauna msimu mleta mada tafadhali fafanua it's too good to be true
 
sikiliza machungwa aina hii ni makubwa na matamu ndio yale unayouziwa 300 mjini kwa matenga na kwa quality yake waweza kuuza hata super market na aliekua na muda aje nimpeleke akaone nilipofikia nimeanza na miche 300 ila sasa nina michungwa 21000 na sina eneo kubwa ila ningepanda hata kama ni michungwa milioni na nia na madhumuni ya kukupeni wazo hili nataka kuwauzia miche ili na nyinyi mufaidike bado nazalisha miche na shamba langu limejaa hapa natafuta soko la miche

Weka picha basi mkuu tuone ulivyo fanya mbona maneno mengi???
 
jamani mm nipo dar hapa hayo mashamba yako tanga nikifika nitawatumia sasa hivi sina picha hapa yaliyopo hapa dar bado ni miaka miwili huko tanga nina michungwa 2000 nitawaonyesha nikifika!
 
Mkuu vp mbona unashtuka mashetani yako hayapendi kuwa milionea nini? Mi bado nawaza huo mchungwa wenyew uwezo wa kubeba machungwa elfu nne ambayo uzito wake unakaribia tani moja labda huo mchungwa unazaa mara tatu kwa mwaka ukijumlisha uzao wote ndo unatapata hiyo idadi ya machungwa au wenyewe unazaa non stop kila mwezi unavuna hauna msimu mleta mada tafadhali fafanua it's too good to be true

Aweke picha tuuone ukiwa shambani kwake maana nahisi huu mchungwa utakua mkubwa kama mkaratusi!machungwa 4000 tena kwa mbwembwe anasema ni makubwa!Ni mchungwa wa bustani ya EDEN au?!
 
jamani mm nipo dar hapa hayo mashamba yako tanga nikifika nitawatumia sasa hivi sina picha hapa yaliyopo hapa dar bado ni miaka miwili huko tanga nina michungwa 2000 nitawaonyesha nikifika!
Hata huo wa Dar tupia tu sio mbaya kwa kuazia then ukifika huko Tanga tupia wala haitobadili maana...
 
Mkuu Kahtan Ahmed naomba jina la hayo machungwa itakuwa rahisi kwangu kuelewa.Unajua Brasil wanalima machungwa ya aina nyingi kama ilivyo Tanzania.

nashkuru sana kwa maelezo yako ila nakuomba nikwambie kitu kwamba usikatae mm nina baba angu tangu enzi za ukoloni ishu zake ni michungwa ila sasa ameng'oa michungwa ya aina zote ikiwemo valencia,jaffer na msasa na amepanda aina hii ya michungwa ninayokueleza hemu google machungwa toka brazil then angalia idadi kuna michungwa inazaa mpaka 16000 kwa kila mchungwa jaribu kufuatilitilia kilimo vizuri wacha kukurupuka
 
Last edited by a moderator:
Niliwahi kununua chungwa fulani hivi pale MSAMVU katikati ya mwaka jana na niliuziwa kwa tsh300 per pc,bila shaka ndio machungwa hayo na kama ndiyo yenyewe basi this is a big deal maana ni matamu sana.
Mkuu:Kahtan Ahmed"Ebu tupe jina la huo mchungwa ili tu google tupate some more details.
But hongera kwa kazi nzuri na ntakutafuta kwa msaada zaidi.
 
sasa hii ni biashara mm nauza wazo la biashara sasa kama nikikutajia na jina si biashara ndio imekufa kama unahitaji tukae kwenye meza tuongee biashara!
 
mm hapa nafanya biashara kama kuna yoyote aliekua intrest na kilimo hiki tukae mezeni tuongee biashara
 
kama unajiona una ardhi maeneo hayo nilisema na una nia ya kilimo hiki na pesa unayo kwa ajili ya gharama na kunilipa mm nitafute tuake mezani ww unataka jina kwani mm nilietafuta hizi details na kuzifanyia kazi nimepoteza muda wangu na gharama zangu wacha kung'ang'ania jina siwezi kuwapa jina hata siku moja na nikifika tanga nitawapa picha za hiyo michungwa
 
Mkuu vp mbona unashtuka mashetani yako hayapendi kuwa milionea nini? Mi bado nawaza huo mchungwa wenyew uwezo wa kubeba machungwa elfu nne ambayo uzito wake unakaribia tani moja labda huo mchungwa unazaa mara tatu kwa mwaka ukijumlisha uzao wote ndo unatapata hiyo idadi ya machungwa au wenyewe unazaa non stop kila mwezi unavuna hauna msimu mleta mada tafadhali fafanua it's too good to be true

mkuu ... kwa mchanganuo huu wa mapato .... ukipeleka business plan banki wataita polisi
 
mm nina uhakika na niliyokwambia kua mche mmoja unazaa mpaka 4000 na isipokua wakulima waliowengi hata hao wanaopanda valencia hawafuati masharti ya kilimo cha machungwa michungwa ya aina ninayokwambia ni kwamba inauwezo wa kuzaliasha 4000 ikiwa utafuata masharti niliyokueleza katika gharama hasa katika umwagiliziaji

Ni vizuri ukaendelea na udalali wa ile gari Tarios kwenye thread yako nyingine kuliko kuleta porojo kwenye kilimo. Nikuelimishe kuwa machungwa na jamii nyingi za citrus family unapofanya 'budding' ni kweli kuwa unapunguza muda wa kuanza kuzaa matunda. Lakini kwa miaka michache ya mwanzo matunda huwa ni kidogo, kwa vile mti unajaribu kuzaa kulingana na uwezo wake in terms of strength, ndio maana ukiwa mkulima mzuri unashauriwa kupunguza baadhi ya maua au later matunda ili mti usielemewe na kuvunjika. Sasa kimantiki si kweli mchungwa wa miaka mitatu kubeba machungwa 4000, labda machungwa hayo yawe na saizi kama karanga....!
 
Back
Top Bottom