Tathmini ya mapato ya kilimo cha michungwa 1000 baada ya miaka 3

Tathmini ya mapato ya kilimo cha michungwa 1000 baada ya miaka 3

Zinahitajika ekari ngapi kupanda hiyo michungwa elf moja?
 
kwa kiukweli kaka sina utaalamu wa kujua ni maeneo gani ila maeneo ambayo nina ushahidi nayo ndio hayo niliokwambia na kuhusu mkoa wako kaka bado sijajua mana mm si mtu wa climate

Sasa mkuu wangu kwa nini usifatilie kwanza then ufind out ili uweze kupata watu wa kutosha, maana sisi wengine hayo maeneo hatuna mashamba sasa unadhani hizo extra gharama zisizokuwa na malengo inakuwaje??Fanya utafiti basi...

Mkuu kweli bana mi mwenyewe nimeletwa Songea ardhi ipo yakutosha vijijini ekarimoja mpka elfu 50.da!ngoja jamaa atupe uzoefu hapa

Mkuu wangu kumbe na wewe tupo boti moja mimi nina ekari 80 ndio maana nikamwambia jamaa afanye kwanza mpango kwa kule kama inawezekana...

Hongera sana kwa taarifa. Swali langu ni kuhusu aina ya mchungwa, na jina lake kitaalamu? Je soko la haya machungwa baada ya kuvuna utauza wapi yote uweze maliza shambani bila kuharibika?

Nadhani previous nimeuliza hili swali ila sijaona kujibiwa bado maana naona hapa inabidi kuwa makini kidogo kwenye hii biashara kwa kweli.....

mm si mtaalaam wa irrigation ila rabda nikupeleke sehemu ukaone jamaa walivyofanya irrigation yao nzuri na ni ya kieconimic

Mkuu wangu why kama una nia ya kuwasaidia watu usiilete humu hiyo hiyo ikawa public na kila mtu akatoa points zake??

aina hii ya michungwa mjomba ni magumu makubwa na matamu suala la soko ondoa shaka mm nadhani ningewaonjesha aina hiyo ya machungwa subiri niagizie halafu nitawaambia muje muchukue moja moja kwa ushahidi kisha mtanambia wenyewe!

Hilo soko lipo wapi mkuu wangu???Maana nilikuwa nategemea hasa kuona lugha za kusema kwamba unaweza kusaidia kuanzia mwanzo mwisho ila naona ume base kwenye kufanya biashara zaidi.....

mm sina utaalamu na irrigation ila nikupeleke shambani kwa rafiki yangu halafu uone jinsi alivofanya very intresting na economic

Ongea na jamaaa ajiunge ajee mkuu hala atusaidie na atupe more details kama anavyofanya mkuu wetu Malila

songea sina ushahidi kama aina hii ya michungwa itakubali!

Unaweza kutuulizia mkuu kama itawezekana??

ni kweli tunafanya grafting

So naona vile vile upo kibiashara zaidi, maana hujasemea kwenye hii project advantage and disadvantages naona hujazungumzia kabisa.......

yoyote anaehitaji miche anipe order then nitawataarifu bei mana sasa imekua adimu!

mhhhh sasa kuna maswali mengi sana hujajibu sasa mtu atawezaje kutoa jibu lake wakati hajapata conclusion ya hii project ina make sense kweli??

Tengeneza busindes plan then uiuze!

gud idea ila naweza hatoweza maana hapa naona kama kuna vitu muhimu sana hataki kuviongelea endapo anaulizwa

jamani mm nipo dar hapa hayo mashamba yako tanga nikifika nitawatumia sasa hivi sina picha hapa yaliyopo hapa dar bado ni miaka miwili huko tanga nina michungwa 2000 nitawaonyesha nikifika!

Tutashukuru sana tena sanaaa

mm hapa nafanya biashara kama kuna yoyote aliekua intrest na kilimo hiki tukae mezeni tuongee biashara

Ndio maana kumbe upo kibiashara zaidi mkuu wangu basi watu wataingia hasawa endapo watakubali kuingia kwenye hii project.....
kwani haya si mawazo yangu kama hayakufai achana nayo! na hao walioona yanawafaa washanifata na tumeshaongeoa ni zaidi ya watu 10 wananitosha

ina maana kwenye biashara yako una limit ya watu unaowataka??maana umesema 10 wanakutosha una mean nini hapo hutaki wengine au vipi??still kabla ya kutoa hela yangu mfukoni naona nina maswali mengi sana kuhusu hii project.
 
Last edited by a moderator:
nawajibu maswali yenu wwote kwa wakati mmoja kama kuna mtu ambae ana intrest ila hajaridhika na ufafanuzi wangu anitafute kwa namba ya simu nitamjibu maswali yake yote na ni kweli mm sio malila nafanya kibiashara zaidi kama nikikusaidia wazo kisha baada ya mika 3 utakula na mimi au na familia yako ?
 
kwa sasa wananitosha maana hiyo miche 5700 wameshaimaliza kwa bei ya 3000 na hakuna hata mche mmoja mpaka msimu mwingine nyinyi endeleeni kupiga soga! hao jamaa baada ya miaka mitatu watakua wamewapiga gap la ajabu ninachopokea kutoka sasa ni order tu basi!
 
hao ambao wapo maeneo tofauti niliwaeleza kua sina ushahidi nayo kua michungwa aina hii yanaweza kukubali vizuri na pia mnazidi kuning'ang'ania niseme kama itakubali au vp, jamani mm si mtu wa climate tafuteni wataalamu wa maeneo na kilimo wawasaidie au mnataka niwadanganye mm siwezi kukudanganya kwa sababu hainisaidii na rabda niwaambie kitu kadri mnavyonikwaza kwa maswali ndio mnazidi kunipa changamoto na watu wengi wananipigia simu na tumekutana na kujadili hili swali.
na rabda niseme ukweli watu wengi ambao wanapenda kuuliza maswali yasiyo na msingi hawana kitu mfukoni kwa ajili ya kufanya hii project wenye mihela yao wameshaniona nyinyi mlikua hamna kitu msinisumbue siku mkipata nishtueni
 
pia kuna mambo mengi ambayo kila mtu anataka kuyajua kwa upande wake siwezi kuridhisha matwaka ya kila mtu bila ya kuniuliza face to face mambo mengine hayaelezeki kwa maandhishi ,tatizo mnaogopa kutapeliwa kwani ukiniona nitakuomba hela its freeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!
 
ndio kuna maswali mengi nilikua sijajibu ila sasa nimeyajibu kwasababu mimi sijaajiriwa na jamii forum bali ni sehemu ninayoingia baada ya kumaliza kazi zangu za msingi ikiwa unaona umeuliza swali kisha mda umepita sijalijibu ujuwe nawajibika sehemu nyingine kuridhisha tumbo na uwe na subira mpaka nitakapoingia jamii mm humu sipo masaa 24
 
sihitaji mshiriki katika biashara yangu wala sitoi ajira kama mnataka awafanyie kazi kwa ajili yenu muajirini mimi najitosheleza na familia yangu wala sihitaji kabisaaaa samahanini sana!
 
heee jamani nipo humu kuwasaidia watu ambao wanataka wao wenyewe kujisaidia wala haijawa sababu mm kupoteza muda kuwaelewesha watu ambao hapo shule hawakuelewa!
 
kufatilia maeneo yote yataka utaalamu si kila unakwenda ukiona mchungwa tu basi michungwa aina hii itakubali tumeshawahi kujaribu mwanza ila tumeona kua tunapoteza muda
 
mimi nina shughuli nyingi kweli kila dili mjini nimo cha ajabu ni kipi kwani ni nani niliemwambia kama mm nimebobea katika masuala ya kilimo mm ni mwana kilimo ila kilimo nakijua ,biashara naijua, mission town pia nazijua ww unajua nn?
 
Mkuu vp mbona unashtuka mashetani yako hayapendi kuwa milionea nini? Mi bado nawaza huo mchungwa wenyew uwezo wa kubeba machungwa elfu nne ambayo uzito wake unakaribia tani moja labda huo mchungwa unazaa mara tatu kwa mwaka ukijumlisha uzao wote ndo unatapata hiyo idadi ya machungwa au wenyewe unazaa non stop kila mwezi unavuna hauna msimu mleta mada tafadhali fafanua it's too good to be true

Sabayi umeiona hiyo enh! Taarifa za tafiti zinatueleza kuwa uzito wa matunda huwa hauzidi uzito wa shina na majani yake, hakuna mmea wenye kuzaa matunda hata iwe nafaka ambao jumla ya uzito wa matunda yake inazidi uzito wa shina! Machungwa makubwa 4000 kwa jinsi anavyosifia chungwa moja linaweza kuwa na uzito gramu 200 hadi 300 kwa makadirio ya chini! Machungwa 4000 x gram 200 = 800,000 gram sawa na kilo 800! Au machungwa 4000 x gram 300 = gram 1,200,000 sawa na kilo 1200 au tani 1.2. Kwa mantiki hiyo shina linapaswa kuwa na uzito zaidi ya kilo 800 au zaid ya tani 1.2! Huo ni utaalamu ambao hatuwezi kuupindisha!! Sasa naomba msomaji tafakari shina la mchungwa wenye umri wa miaka 3 lenye uzito zaidi ya tani moja!! Tani moja!!!
 
kwani ww shida yako nini mjomba na kama kweli unafuatilia mbona umekileta nilichokijibu wala hukukileta nilichoambiwa? wacha ufitishaji hizo ni tabia za kina mama, mtu mzima yako akili kuangalia maisha yako, ndio mm nauza daihatsu sasa dili ya daihatsu na michungwa imekujaje kwani kipi kinachokuuma mm kufanya biashara aina tofauti hemu chunga muda wako na ufanye ya maana kukuza kipato chako na kutunza heshima yako na muda wako pia!

Hii ndiyo aina ya market promotion ya kitanzania, unawatangazia watu bidhaa yako huku unawatukana, kukashifu na kuwazodoa wateja, ngoja tufuatilie hii the comedy naona napata burudani poa kabisa daah!!
 
Hii ndiyo aina ya market promotion ya kitanzania, unawatangazia watu bidhaa yako huku unawatukana, kukashifu na kuwazodoa wateja, ngoja tufuatilie hii the comedy naona napata burudani poa kabisa daah!!

Kaka huyu dogo ni Pimbi sana ana majibu ya hovyo sijawahi ona na bado anatoa ideas za Kitapeli humu eti mchungwa unaweza kubeba machungwa makubwa 4000
 
Nimejarubu Ku google kwenye Nchi zinazo ongoza kwa kilimo Cha Machungwa bado sijapata mchungwa wa Kubeba hayo machungwa, Inaonekana itaanzia Tanzania kwa mara ya kwanza
 
Kaka huyu dogo ni Pimbi sana ana majibu ya hovyo sijawahi ona na bado anatoa ideas za Kitapeli humu eti mchungwa unaweza kubeba machungwa makubwa 4000

haa haaa

jf ni kiboko aisee
 
Mkuu kulima kwenye keyboard ni rahisi sana unaweza ukapata hata bil3!! Fanya implementatio tuone weka picha ya michungwa yako!
 
Back
Top Bottom