Uchaguzi 2020 Tathmini yangu juu ya Uchaguzi Mkuu 2020: Hakuna sababu nzuri ya kukataa kuteua wabunge wa Viti Maalum CHADEMA

Uchaguzi 2020 Tathmini yangu juu ya Uchaguzi Mkuu 2020: Hakuna sababu nzuri ya kukataa kuteua wabunge wa Viti Maalum CHADEMA

Tabia ya kushindwa kutofautisha hoja na mleta hoja ni dalili kwamba Watanzania wenye elimu iliyo chini ya kidato cha nne wanafikia 90%, na wewe ni miongoni mwao.

Sio lazima uandike chochote. Ukimya nao unakubalika.
Pole sana! Kuna nyakati elimu inaweza kushindwa kukusaidia hata wewe mleta mada pale unaposhindwa kutofautisha ushabiki na uhalisia baki na ujinga wako! Kaa ukijua hakuna coalition yoyote itasafisha huu uchafuzi mkuu
 
Ndiyo maana polepole aliwaita cjadema Malaghai wakubwa.
 
View attachment 1633150
Tundu Lissu (Mgombea Urais wa Chadema) na Job Ndugai (Spika)

Kuna mdau kanitumia kitabu cha Gene Sharp (2012), kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Yaani, "Safari ya Kutoka Kwenye HImaya ya Kidikteta Kuelekea Kwenye HImaya ya Kidemokrasia: Mawazo Ambayo ni Msingi wa Hoja za Kuendeleza Mapambano ya Ukombozi." (Tafsiri yangu).

Mdau huyu amenitaka nikisome na kisha nijibu swali hili: Kama wabunge wa viti maalum wanatokana na kura za mgombea urais, na kama kura za mgombea urais wa Chadema zilizotangazwa na tume ni sehemu ya kura zote ambazo Chadema wanadai kwamba walipata, uamuzi wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum wa Chadema ili waende Bungeni kula kiapo na kuchapa kazi ya ubunge unachangia vipi katika kuimarisha demokrasia nchini Tanzania?

Nimekisoma kitabu na kukimaliza. Kina kurasa 100, na kimeandikwa kwa Kingereza chepesi. Ninaelewa mengi yaliyojiri katika siku zote za uchaguzi mkuu wa 2020. Pia najua malalamiko kadhaa ya vyama vya upinzani. Baada tafakari nimefikiria kama ifuatavyo:

Mosi, kama mgombea urais wa Chadema (Lissu) alipata kura X, na NEC ikatangaza kwamba Lissu kapata kura Y, ni wazi kwamba kura X ni kubwa kuliko kura Y, yaani X>Y.

Pili, Tofauti kati ya kura X na kura Y, tuseme kura Z, ndizo kura zinazobishaniwa. Chadema wanapinga kutotangazwa kwa kura Z. Yaani, Chadema wanapinga kutangazwa kwa kura Y pekee bila kujumlisha kura Z.

Tatu, kura Y zilizotangawa na NEC ni sehemu ya kura X zinazotamkwa na viongozi wa Chadema.

Nne, wabunge wa viti maalum wa Chadema wanatokana na kura Y, ambazo ni kura halali.

Kwa hiyo, idadi ya wabunge wa viti maalum kupitia Chadema iliyotangazwa na NEC ni idadi ya wabunge iliyotokana na kura halali.

Lakini, kama Chadema wanasema kuwa LIssu alipata kura ambazo ni ndogo kuliko zile zilizotangazwa na NEC, basi hitimisho langu linaporomoka hadi kuwa kifusi; na nitaungana nao katika msimamo wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum.

Nitatoa mifano miwili ili kufafanua hitimisho langu hili.

Mfano wa kwanza, ni mfano wa mtu aliyefukuzwa kazi, akamshitaki mwajiri kwenye Mahakama ya Kazi, Makahaka ikaamuru alippwe Milioni 10 kama fidia. Ikiwa mwajiri atamlipa milioni 3 pekee, anazipokea na kuzitumia kama gharama za kuweka wakili ili ambane mwajiri kwa hoja kwamba malipo ya milioni tatu "pekee" hayatoshi, lakini baada ya kuchukua milioni tatu.

Na mfano wa pili ni wa kifalsafa zaidi. Tunapotaja fasili ya umbo linaloitwa pembetatu tunasema hivi: "Pembetatu ni umbo lenye kona tatu pekee na pande tatu pekee."

Katika fasili hii neno "pekee" ni muhimu sana, kwani hata mraba unazo pembe tatu na kona tatu pia. Lakini mraba hauna pembe tatu "pekee" wala pande tatu "pekee."

Kwa mujibu wa mifano hii miwili, sasa nahitimisha hoja yangu. Katika kura za mgombea urais, Tundu Lissu, Chadema hawadai kura Y pekee, kama ilivyotangazwa na NEC. Wanadai kura Y na kura Z, ambapo tayari wamekwishapatiwa kura Y, lakini bado kupatiwa kura Z, kama watathibitisha kwamba zipo.

Hivyo, Chadema wanaweza, na wanapaswa kupokea kura Y na kuendelea kudai kura Z, kwa kuweka bayana hoja isiyoruhusu hewa wala maji kupenya.

Kwa mantiki hii, Chadema hawapaswi kuona shida kuteua wabunge wa viti maalum ili waende Bungeni kuapa. Nashauri wafanye hivyo leo.

Hapa nimejaribu kufikiri kwa sauti kwa kuzingatia hoja zilizojengwa na Gene Sharp (2012) katika kitabu chake kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Kwa mujibu wa kitabu hiki, kukataa kuteua wabunge wa viti maalum, kama wanavyofanya Chadema kwa sasa, ni aina mojawapo ya udikteta; na majadiliano ya maana hufanyika kati ta "mdikteta" na "mdemokrasia."

Yaani, Chadema inabidi waonyeshe kwa mawazo, maneno na vitendo kwamba wao ni "wademokrasia" ili wapate uhalali wa kumkabili yule anayeitwa "mdikteta."

Nimeambatanisha kitabu hicho hapa chini, kwa ajili ya wale wenye utayari wa kujisomea.

Huu ni mtazamo wangu, na ninawajibika kikamilifu kusanifu hoja hii yenye kutetea mtazamo huu.

Mama Amon,
Sumbawanga Kusini.
Hivi nyinyi watu was CCM si mlipiga kampeni nchi nzima na mwenyekiti wenu akawaambia Nileteeni Gwjimaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa . Sasa mnataka nini tena wakati wapinzani wanakwamisha maendeleo ya nchi kwa mtazamo wa dark ages wa chairman wenu . Sasa hivi nyinyi maccm mfocus vitu viwili , mosi andaeni utetezi wa mashtaka yanayowakabili ICC ambao hata hivyo hamna kwa video zilizotumwa huko , pili andaeni mipango ya kupandisha kodi nyingi sana kwenye bidhaa mbalimbali mwakamue raia mpaka damu , maana mabeberu hawatoi hata mia . Yaani wawasaidie halafu mje na kauli za kishamba na kilimbukeni za palamihogo wenu huyo .
 
Nimependa mtiririko wa mawazo yako.

Kwa hapa itoshe kunukuu sura ya kwanza ya kitabu ambacho nime-attach hapa chini.

Tunasoma:

"When one wants to bring down a dictatorship most effectively and with the least cost then one has four immediate tasks: One must strengthen the oppressed population themselves in their determination, self-confidence, and resistance skills; One must strengthen the independent social groups and institutions of the oppressed people; One must create a powerful internal resistance force; One must develop a wise grand strategic plan for liberation and implement it skillfully." (tazama attachment, sura ya kwanza, chini ya sub-heading hii: "Facing the hard truth ")

Pointi yangu ni kwamba, katika "grand strategic plan for liberation" inayotakiwa tunapaswa kuwa na jukumu la kupeleka wabunge wa viti maalum bungeni, na sio kuwazuia. Hawa watakuwa na kazi nyingi.

Mojawapo ni kwamba watakuwa maafisa vipenyo wetu. Pili, watakiwezesha chama kuwa na nguvu ya kiuchumi kuendeleza mapambano.

Lakini, nisema kwamba, wabunge wa viti maalum wanaweza kutikisa kuliko unavyofikiria.

Baadhi wanazo shahada za uzamivu.

Wengine ni wanasheria.

Wengine ni wabunge wzoefu.

Chadema wachangamke, kijua ndio hichi!

Kwanza, sijui umeielewaje hoja ya mdau Tindo kwamba Bunge letu halina meno. Hata wewe unajua kuwa Bunge linaendeshwa kwa maagizo. Kama ilivyo kwa taasisi nyingine za umma, haliko huru.

Pili, unaeleza kama vile CHADEMA “wamezuia” wabunge wa viti maalum kwenda bungeni. Kama vile unataka kudai kuwa CHADEMA wamekiuka misingi ya demokrasia. Sivyo? Sijui kama una habari za ndani za mchakato wa CHADEMA wa maamuzi kuhusu kupeleka hao viti maalum bungeni. Wewe unajua kama vikao rasmi havijakaa na kuamua wasiwe na wabunge wa viti maalum safari hii? Mimi sijui.

LAKINI, all in all, hiyo hoja kwamba wabunge wa viti maalum watakuwa na sauti ya kudai kura zilizoibiwa na kuwasilisha/kusimamia hoja nyingine muhimu za CHADEMA kwangu mimi ina kila dalili ya “mzaha mbaya”. Maelezo yako hayatoi ushawishi wa kuridhisha. Dikteta aliyepo madarakani safari hii ameweka dhahiri kuwa lengo lake katika awamu yake ni kuufuta upinzani kikamilifu. Na haendekezi mijadala. Hata wanawake mahiri wa CHADEMA kahakikisha wanaporwa ushindi majimboni. It’s a terribly desperate situation.
 
S
Hakuna kiti cha ubunge maalum kinapatikana kwa fadhila.
Ila inawezekana upande wa pili hali ikawa hivyo.
Kwa Chadema hakuna uwezekano huo.
Kwa hiyo neno "fadhila" futa kwenye maelezo yako.
Mkuu Kama MUNGU haishivyo sifuti nakwambia, bila uchuguzi kuvurugwa, hao unaosema kuwa bit mahalum walikua na uwezekano wa kushinda si chini ya asilimia 87,7777 kwa ridhaa ya wenye nchi, I mean wananchi, Sasa vya bure vya nini futeni uchaguzi turudi field ,vinginevyo itakua ni fadhila ,
Usipende kuchukulia mzigo aliobeba mwenzio kuuna rahisi ,Kama Wana nchi ni walewale twende field ,sidhani Kama Kuna mwanamama, wa chadema anapenda kua viti mahalum, tofauti na wale waliokua wamepita viti mahalum mkuu,ila pamoja na hayo wabunge wapo, so acha waendelee achana na vyama vya upinzani
 
View attachment 1633150
Tundu Lissu (Mgombea Urais wa Chadema) na Job Ndugai (Spika)

Kuna mdau kanitumia kitabu cha Gene Sharp (2012), kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Yaani, "Safari ya Kutoka Kwenye HImaya ya Kidikteta Kuelekea Kwenye HImaya ya Kidemokrasia: Mawazo Ambayo ni Msingi wa Hoja za Kuendeleza Mapambano ya Ukombozi." (Tafsiri yangu).

Mdau huyu amenitaka nikisome na kisha nijibu swali hili: Kama wabunge wa viti maalum wanatokana na kura za mgombea urais, na kama kura za mgombea urais wa Chadema zilizotangazwa na tume ni sehemu ya kura zote ambazo Chadema wanadai kwamba walipata, uamuzi wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum wa Chadema ili waende Bungeni kula kiapo na kuchapa kazi ya ubunge unachangia vipi katika kuimarisha demokrasia nchini Tanzania?

Nimekisoma kitabu na kukimaliza. Kina kurasa 100, na kimeandikwa kwa Kingereza chepesi. Ninaelewa mengi yaliyojiri katika siku zote za uchaguzi mkuu wa 2020. Pia najua malalamiko kadhaa ya vyama vya upinzani. Baada tafakari nimefikiria kama ifuatavyo:

Mosi, kama mgombea urais wa Chadema (Lissu) alipata kura X, na NEC ikatangaza kwamba Lissu kapata kura Y, ni wazi kwamba kura X ni kubwa kuliko kura Y, yaani X>Y.

Pili, Tofauti kati ya kura X na kura Y, tuseme kura Z, ndizo kura zinazobishaniwa. Chadema wanapinga kutotangazwa kwa kura Z. Yaani, Chadema wanapinga kutangazwa kwa kura Y pekee bila kujumlisha kura Z.

Tatu, kura Y zilizotangawa na NEC ni sehemu ya kura X zinazotamkwa na viongozi wa Chadema.

Nne, wabunge wa viti maalum wa Chadema wanatokana na kura Y, ambazo ni kura halali.

Kwa hiyo, idadi ya wabunge wa viti maalum kupitia Chadema iliyotangazwa na NEC ni idadi ya wabunge iliyotokana na kura halali.

Lakini, kama Chadema wanasema kuwa LIssu alipata kura ambazo ni ndogo kuliko zile zilizotangazwa na NEC, basi hitimisho langu linaporomoka hadi kuwa kifusi; na nitaungana nao katika msimamo wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum.

Nitatoa mifano miwili ili kufafanua hitimisho langu hili.

Mfano wa kwanza, ni mfano wa mtu aliyefukuzwa kazi, akamshitaki mwajiri kwenye Mahakama ya Kazi, Makahaka ikaamuru alippwe Milioni 10 kama fidia. Ikiwa mwajiri atamlipa milioni 3 pekee, anazipokea na kuzitumia kama gharama za kuweka wakili ili ambane mwajiri kwa hoja kwamba malipo ya milioni tatu "pekee" hayatoshi, lakini baada ya kuchukua milioni tatu.

Na mfano wa pili ni wa kifalsafa zaidi. Tunapotaja fasili ya umbo linaloitwa pembetatu tunasema hivi: "Pembetatu ni umbo lenye kona tatu pekee na pande tatu pekee."

Katika fasili hii neno "pekee" ni muhimu sana, kwani hata mraba unazo pembe tatu na kona tatu pia. Lakini mraba hauna pembe tatu "pekee" wala pande tatu "pekee."

Kwa mujibu wa mifano hii miwili, sasa nahitimisha hoja yangu. Katika kura za mgombea urais, Tundu Lissu, Chadema hawadai kura Y pekee, kama ilivyotangazwa na NEC. Wanadai kura Y na kura Z, ambapo tayari wamekwishapatiwa kura Y, lakini bado kupatiwa kura Z, kama watathibitisha kwamba zipo.

Hivyo, Chadema wanaweza, na wanapaswa kupokea kura Y na kuendelea kudai kura Z, kwa kuweka bayana hoja isiyoruhusu hewa wala maji kupenya.

Kwa mantiki hii, Chadema hawapaswi kuona shida kuteua wabunge wa viti maalum ili waende Bungeni kuapa. Nashauri wafanye hivyo leo.

Hapa nimejaribu kufikiri kwa sauti kwa kuzingatia hoja zilizojengwa na Gene Sharp (2012) katika kitabu chake kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Kwa mujibu wa kitabu hiki, kukataa kuteua wabunge wa viti maalum, kama wanavyofanya Chadema kwa sasa, ni aina mojawapo ya udikteta; na majadiliano ya maana hufanyika kati ta "mdikteta" na "mdemokrasia."

Yaani, Chadema inabidi waonyeshe kwa mawazo, maneno na vitendo kwamba wao ni "wademokrasia" ili wapate uhalali wa kumkabili yule anayeitwa "mdikteta."

Nimeambatanisha kitabu hicho hapa chini, kwa ajili ya wale wenye utayari wa kujisomea.

Huu ni mtazamo wangu, na ninawajibika kikamilifu kusanifu hoja hii yenye kutetea mtazamo huu.

Mama Amon,
Sumbawanga Kusini.
Uko sahihi sana, hata Mwl. Nyerere aliukubali uwaziri mkuu kisha ndio akaendelea kupambania kusaka uhuru....kabla ya jambo kubwa kupewa, MUNGU huanza na dogo kwanza...
 
Tafadhali Chadema huyu mama ametumwa na KIM wa bongo mwangalieni kwa jicho la saba
 
Ukiangalia ni kwamba hatujawahi kuwa na uchaguzi halali na wa haki,sasa hiki wanachofanya sasa chadema nacho pia si sawa na kuhalalisha uharamu wa chaguzi zilizopita?
 
Mama Amon
Naomba kukumbusha jambo moja kupitia mfano wako wa kwanza.
Kupokea mil.3 kama sehemu ya malipo ya fidia iliyoamriwa ambayo ni mil.10 inabadilisha kesi ya msingi kutoka kumlalamikia mwajiri wako kwa kukufukuza kazi hadi kudai kumaliziwa deni la fidia.
Uzito wa kesi hizi mbili ni tofauti sana.

Tukija kwenue hoja ya msingi, inawezekana ni kweli upinzani hasa CHADEMA unahitaji uwakilishi katika nyanja zote kuanzia Bungeni hadi kwenye mabaraza ya Halmashauri. Lakini uwakilishi huu unaweza usisaidie hata kidogo kumaliza matatizo ya upinzani zaidi labda kuugawa zaidi.

Itoshe tu kusema kuna haja kubwa ya kila upande kulegeza msimamo ili kupata suluhu inayoimarisha Umoja & Mshikamano (ndani ya miaka hii5) bila kujali mkwamo wa kisiasa ulipo sasa.
 
Kukubali kuteua viti maalumu ni kukubali uhalamia na ufedhuli uliofanywa na tume kwa maelekezo ya CCM. Mimi nilishiriki kusimamia uchaguzi huu, niliyoyaona yanatisha.

Nimeeleza kidogo tu kuwa kwenye kituo changu nilichosimamia Tundu Antipas Lissu alipata kura 79 na Magufuli alipata kura 31 lakini Lissu akandikiwa kura 6 na Magufuli kura 379 sasa hapo unakubali vipi? Ni bora kuacha tu.
Mie niliyoyaona nitasimulia vizazi vyangu vyote nyaani nitamsimulia mwanangu siku zote ajue kuwa mwaka 2020 kulitokea tukio la kuumiza ,kufedhehesha na kudharaulisha nalo ni uchaguzi mkuu.Nitaandika hata nukuu vizazi vyangu vitasoma kitabu changu kuonesha nilivyoumia

Sent from my TECNO CF8 using JamiiForums mobile app
 
Naona umekuwa "kijana wa kijana " squared hadi ukawa mtoto!
Hakuna mahali hoja yangu inaweza kutumika kuhalalisha uovu wowote.
Kwa taarifa yako, Lissu ni mwanasheria, na anaelewa fika nilichokiandika hapa.
Anaweza kupata shida kuikubali hoja kwa sababu nyingine, lakini sio sababu za kimantiki.
Soma hoja yangu tena.
Bro tumekusoma vema tulichokiona ni kile kinachopinga ukweli kuwa hupaswi kukubali kuunga mkono kudhulumiwa wakati una nafasi ya kureact kwa migomo nk
Wao walioharibu uchaguzi wajenge walipobomoa

Sent from my TECNO CF8 using JamiiForums mobile app
 
Umetoa mfano mzuri unaoimarisha hoja yangu.

Ni hivi:

Kwenye kituo ulichosimamia Tundu Antipas Lissu alipata kura 79 na Magufuli akapata kura 31.

Lakini Lissu alindikiwa kura 6 na Magufuli kura 379.

Kisha unauliza, "sasa hapo unakubali vipi?"

Majibu yangu:

Kama ni kweli, kura 6 alizoandikiwa Lissu ni sehemu ya kura zake halali 79 ulizozishuhudia.

Kwa hiyo, kwa mujibu wa maelezo yako, Lissu aliibiwa kura 73.

Hivyo basi, tunapaswa kukubali kwamba kura 6 ni kura halali, na kuendelea kudai kura 73 kwa kuweka vielelezo mezani.

Hizo kura 6 ambazo tunajua kwamba ni halali ni sehemu ya kura ambazo zimetangazwa na NEC na kuzaa wabunge wa viti maalum 19.

Kwa hiyo, viti maalum 19 vya Chadema ni halali.

Katika kituo chako ulichosimamia, ambacho sio halali, kama kikitibitika, ni kutotangazwa kwa kura 73.

Hizi kura 73 ziendelee kudaiwa bila kuharamisha kura 6 ambazo ni halali.

Wanasheria wote wa Chadema wanaujua ukweli huu.

Tafuta yeyote umwulize na atakwambia ninachokwambia.
Zikadaiwe wapi wakati hata fomu mawakala walinyimwa?

Sent from my TECNO CF8 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom