Uchaguzi 2020 Tathmini yangu juu ya Uchaguzi Mkuu 2020: Hakuna sababu nzuri ya kukataa kuteua wabunge wa Viti Maalum CHADEMA

Uchaguzi 2020 Tathmini yangu juu ya Uchaguzi Mkuu 2020: Hakuna sababu nzuri ya kukataa kuteua wabunge wa Viti Maalum CHADEMA

Mama Amon, natumaini umesimama kwenye uaminifu (honesty) unapotoa hilo pendekezo.

Umeainisha sentenso ya muamala kama wa kibiashara vile kuonyesha faida watakayopata CHADEMA kwa kupeleka wabunge wa viti maalum. Kwamba watakuwa nyenzo ya kudai kura zilizoibiwa!

Naamini unao uelewa mkubwa kuweza kutambua kuwa alichofanya Mwenyekiti wa CCM ni kufifisha nguvu ya CHADEMA kwa kuwapoka ushindi wao kwenye urais na kwenye majimbo na kuhakikisha wabunge wake maarufu hawarudi bungeni.

Kisha kawapa mbunge mmoja tu wa jimbo asiye na historia ya “kutikisa” sana. Sasa anachotaka ni CHADEMA kuwa na uwakilishi dhaifu wa viti maalum kuhalalisha dhulma kubwa iliyofanywa kwa chama hicho na kwa Watanzania kwa ujumla.

Aidha, wewe kama ni mama (ke) kweli umeshasikia kejeli inayoshamirishwa na wabunge wanawake wa CCM wakishangiliwa na spika kuwa wanaopata viti maalum CHADEMA sharti “wadhalilishwe” na mwenyekiti wa chama hicho!

Halafu kweli unaamini hao viti maalum wataweza kudai kura za CHADEMA zilizoibwa?

Usishangae ukiona wadau hapa JF wakikutilia mashaka makubwa kuhusu nia yako halisi (real motive) ya kuleta bandiko hili.
 
Sorry, unaandika kama vile unadondosha maneno ambayo yanakosa muunganiko wa kimantiki.

Can you paraphrase your argument to make it more formal and palatable?

napendelea hoja zenye muundo haka huu:

Tindo ni mtu (major premise)
KIla mtu atakufa (minor premise)
Kwa hiyo, siku moja, Tindo atakufa (conclusion)

Katika muundo huu inakuwa rahisi kufuatilia anachosema mwenzako.

Mama Aron jitahidi ukija huku jukwaani usije na marking scheme, maana utapoteza muda wako bure. Unaweza ukasababisha na mimi nikawa nataka kila mtu ajadili kwa mtiririko niutakao mimi na sio aonavyo yeye.
 
Pili hoja yako ya mgogoro wa Mwajiri na mwajiriwa ni irrelevant kwenye hoja yako ya kura za CHADEMA kwa sababu mwajiriwa ana njia ya kutafuta haki yake wakati CHADEMA hawana tena hiyo Avenue

Ndugu, analogical argument inayo anatomia yake, kama ifuatavyo:

1. Members of class X have properties making up set P and more;
2. Members of Class Y have properties making up set Q and more;
3. Members of Set P are similar to members of set Q;
4. Thus, what is true of class X is true of class Y.

Nje ya mfumo huu wa ufananisho, analogical argument fails.
Kwa hiyo, usijielekeze kwenye tofauti.
Zingatia ufanano.
 
Mama Aron jitahidi ukija huku jukwaani usije na marking scheme, maana utapoteza muda wako bure. Unaweza ukasababisha na mimi nikawa nataka kila mtu ajadili kwa mtiririko niutakao mimi na sio aonavyo yeye.

Mie ni mleta bandiko, na hivyo ni moderator wa mjadala huu.
Unataka kuninyang'anya haki yangu hiyo?
 
Mie ni mleta bandiko, na hivyo ni moderator wa mjadala huu.
Unataka kuninyang'anya haki yangu hiyo?

Ni kweli unachosema wala sipingi, Ila sio moderator kwa kile ulichosema.
 
View attachment 1633150
Tundu Lissu (Mgombea Urais wa Chadema) na Job Ndugai (Spika)

Kuna mdau kanitumia kitabu cha Gene Sharp (2012), kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Yaani, "Safari ya Kutoka Kwenye HImaya ya Kidikteta Kuelekea Kwenye HImaya ya Kidemokrasia: Mawazo Ambayo ni Msingi wa Hoja za Kuendeleza Mapambano ya Ukombozi." (Tafsiri yangu).

Mdau huyu amenitaka nikisome na kisha nijibu swali hili: Kama wabunge wa viti maalum wanatokana na kura za mgombea urais, na kama kura za mgombea urais wa Chadema zilizotangazwa na tume ni sehemu ya kura zote ambazo Chadema wanadai kwamba walipata, uamuzi wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum wa Chadema ili waende Bungeni kula kiapo na kuchapa kazi ya ubunge unachangia vipi katika kuimarisha demokrasia nchini Tanzania?

Nimekisoma kitabu na kukimaliza. Kina kurasa 100, na kimeandikwa kwa Kingereza chepesi. Ninaelewa mengi yaliyojiri katika siku zote za uchaguzi mkuu wa 2020. Pia najua malalamiko kadhaa ya vyama vya upinzani. Baada tafakari nimefikiria kama ifuatavyo:

Mosi, kama mgombea urais wa Chadema (Lissu) alipata kura X, na NEC ikatangaza kwamba Lissu kapata kura Y, ni wazi kwamba kura X ni kubwa kuliko kura Y, yaani X>Y.

Pili, Tofauti kati ya kura X na kura Y, tuseme kura Z, ndizo kura zinazobishaniwa. Chadema wanapinga kutotangazwa kwa kura Z. Yaani, Chadema wanapinga kutangazwa kwa kura Y pekee bila kujumlisha kura Z.

Tatu, kura Y zilizotangawa na NEC ni sehemu ya kura X zinazotamkwa na viongozi wa Chadema.

Nne, wabunge wa viti maalum wa Chadema wanatokana na kura Y, ambazo ni kura halali.

Kwa hiyo, idadi ya wabunge wa viti maalum kupitia Chadema iliyotangazwa na NEC ni idadi ya wabunge iliyotokana na kura halali.

Lakini, kama Chadema wanasema kuwa LIssu alipata kura ambazo ni ndogo kuliko zile zilizotangazwa na NEC, basi hitimisho langu linaporomoka hadi kuwa kifusi; na nitaungana nao katika msimamo wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum.

Nitatoa mifano miwili ili kufafanua hitimisho langu hili.

Mfano wa kwanza, ni mfano wa mtu aliyefukuzwa kazi, akamshitaki mwajiri kwenye Mahakama ya Kazi, Makahaka ikaamuru alippwe Milioni 10 kama fidia. Ikiwa mwajiri atamlipa milioni 3 pekee, anazipokea na kuzitumia kama gharama za kuweka wakili ili ambane mwajiri kwa hoja kwamba malipo ya milioni tatu "pekee" hayatoshi, lakini baada ya kuchukua milioni tatu.

Na mfano wa pili ni wa kifalsafa zaidi. Tunapotaja fasili ya umbo linaloitwa pembetatu tunasema hivi: "Pembetatu ni umbo lenye kona tatu pekee na pande tatu pekee."

Katika fasili hii neno "pekee" ni muhimu sana, kwani hata mraba unazo pembe tatu na kona tatu pia. Lakini mraba hauna pembe tatu "pekee" wala pande tatu "pekee."

Kwa mujibu wa mifano hii miwili, sasa nahitimisha hoja yangu. Katika kura za mgombea urais, Tundu Lissu, Chadema hawadai kura Y pekee, kama ilivyotangazwa na NEC. Wanadai kura Y na kura Z, ambapo tayari wamekwishapatiwa kura Y, lakini bado kupatiwa kura Z, kama watathibitisha kwamba zipo.

Hivyo, Chadema wanaweza, na wanapaswa kupokea kura Y na kuendelea kudai kura Z, kwa kuweka bayana hoja isiyoruhusu hewa wala maji kupenya.

Kwa mantiki hii, Chadema hawapaswi kuona shida kuteua wabunge wa viti maalum ili waende Bungeni kuapa. Nashauri wafanye hivyo leo.

Hapa nimejaribu kufikiri kwa sauti kwa kuzingatia hoja zilizojengwa na Gene Sharp (2012) katika kitabu chake kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Kwa mujibu wa kitabu hiki, kukataa kuteua wabunge wa viti maalum, kama wanavyofanya Chadema kwa sasa, ni aina mojawapo ya udikteta; na majadiliano ya maana hufanyika kati ta "mdikteta" na "mdemokrasia."

Yaani, Chadema inabidi waonyeshe kwa mawazo, maneno na vitendo kwamba wao ni "wademokrasia" ili wapate uhalali wa kumkabili yule anayeitwa "mdikteta."

Nimeambatanisha kitabu hicho hapa chini, kwa ajili ya wale wenye utayari wa kujisomea.

Huu ni mtazamo wangu, na ninawajibika kikamilifu kusanifu hoja hii yenye kutetea mtazamo huu.

Mama Amon,
Sumbawanga Kusini.
Mama Amon nafasi zipo zote 19 chukua viti kiasi unachotaka usijali, lakini aliyekataliwa kwa kuporwa kura hana sababu ya kuingia bungeni.
 
View attachment 1633150
Tundu Lissu (Mgombea Urais wa Chadema) na Job Ndugai (Spika)

Kuna mdau kanitumia kitabu cha Gene Sharp (2012), kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Yaani, "Safari ya Kutoka Kwenye HImaya ya Kidikteta Kuelekea Kwenye HImaya ya Kidemokrasia: Mawazo Ambayo ni Msingi wa Hoja za Kuendeleza Mapambano ya Ukombozi." (Tafsiri yangu).

Mdau huyu amenitaka nikisome na kisha nijibu swali hili: Kama wabunge wa viti maalum wanatokana na kura za mgombea urais, na kama kura za mgombea urais wa Chadema zilizotangazwa na tume ni sehemu ya kura zote ambazo Chadema wanadai kwamba walipata, uamuzi wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum wa Chadema ili waende Bungeni kula kiapo na kuchapa kazi ya ubunge unachangia vipi katika kuimarisha demokrasia nchini Tanzania?

Nimekisoma kitabu na kukimaliza. Kina kurasa 100, na kimeandikwa kwa Kingereza chepesi. Ninaelewa mengi yaliyojiri katika siku zote za uchaguzi mkuu wa 2020. Pia najua malalamiko kadhaa ya vyama vya upinzani. Baada tafakari nimefikiria kama ifuatavyo:

Mosi, kama mgombea urais wa Chadema (Lissu) alipata kura X, na NEC ikatangaza kwamba Lissu kapata kura Y, ni wazi kwamba kura X ni kubwa kuliko kura Y, yaani X>Y.

Pili, Tofauti kati ya kura X na kura Y, tuseme kura Z, ndizo kura zinazobishaniwa. Chadema wanapinga kutotangazwa kwa kura Z. Yaani, Chadema wanapinga kutangazwa kwa kura Y pekee bila kujumlisha kura Z.

Tatu, kura Y zilizotangawa na NEC ni sehemu ya kura X zinazotamkwa na viongozi wa Chadema.

Nne, wabunge wa viti maalum wa Chadema wanatokana na kura Y, ambazo ni kura halali.

Kwa hiyo, idadi ya wabunge wa viti maalum kupitia Chadema iliyotangazwa na NEC ni idadi ya wabunge iliyotokana na kura halali.

Lakini, kama Chadema wanasema kuwa LIssu alipata kura ambazo ni ndogo kuliko zile zilizotangazwa na NEC, basi hitimisho langu linaporomoka hadi kuwa kifusi; na nitaungana nao katika msimamo wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum.

Nitatoa mifano miwili ili kufafanua hitimisho langu hili.

Mfano wa kwanza, ni mfano wa mtu aliyefukuzwa kazi, akamshitaki mwajiri kwenye Mahakama ya Kazi, Makahaka ikaamuru alippwe Milioni 10 kama fidia. Ikiwa mwajiri atamlipa milioni 3 pekee, anazipokea na kuzitumia kama gharama za kuweka wakili ili ambane mwajiri kwa hoja kwamba malipo ya milioni tatu "pekee" hayatoshi, lakini baada ya kuchukua milioni tatu.

Na mfano wa pili ni wa kifalsafa zaidi. Tunapotaja fasili ya umbo linaloitwa pembetatu tunasema hivi: "Pembetatu ni umbo lenye kona tatu pekee na pande tatu pekee."

Katika fasili hii neno "pekee" ni muhimu sana, kwani hata mraba unazo pembe tatu na kona tatu pia. Lakini mraba hauna pembe tatu "pekee" wala pande tatu "pekee."

Kwa mujibu wa mifano hii miwili, sasa nahitimisha hoja yangu. Katika kura za mgombea urais, Tundu Lissu, Chadema hawadai kura Y pekee, kama ilivyotangazwa na NEC. Wanadai kura Y na kura Z, ambapo tayari wamekwishapatiwa kura Y, lakini bado kupatiwa kura Z, kama watathibitisha kwamba zipo.

Hivyo, Chadema wanaweza, na wanapaswa kupokea kura Y na kuendelea kudai kura Z, kwa kuweka bayana hoja isiyoruhusu hewa wala maji kupenya.

Kwa mantiki hii, Chadema hawapaswi kuona shida kuteua wabunge wa viti maalum ili waende Bungeni kuapa. Nashauri wafanye hivyo leo.

Hapa nimejaribu kufikiri kwa sauti kwa kuzingatia hoja zilizojengwa na Gene Sharp (2012) katika kitabu chake kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Kwa mujibu wa kitabu hiki, kukataa kuteua wabunge wa viti maalum, kama wanavyofanya Chadema kwa sasa, ni aina mojawapo ya udikteta; na majadiliano ya maana hufanyika kati ta "mdikteta" na "mdemokrasia."

Yaani, Chadema inabidi waonyeshe kwa mawazo, maneno na vitendo kwamba wao ni "wademokrasia" ili wapate uhalali wa kumkabili yule anayeitwa "mdikteta."

Nimeambatanisha kitabu hicho hapa chini, kwa ajili ya wale wenye utayari wa kujisomea.

Huu ni mtazamo wangu, na ninawajibika kikamilifu kusanifu hoja hii yenye kutetea mtazamo huu.

Mama Amon,
Sumbawanga Kusini.
Sawa huo ni mtazamo wako.

Maswali magumu pengine tukuulize Ndg. mwandishi:

1. Endapo CHADEMA wakakukubali kuteua wabunge wa viti maalum, Je? hii itakuwa imesaidia nini katika kujenga Demokrasia huru na utawala wa haki nchini?
2. Je unadhani nani atakuwa mnufaika mkubwa wa hayo maamuzi endapo yatafanyika kati ya "waliyotengeneza hayo mazingira" au Demokrasia ya nchi yetu.

3. Je umewahi kujiuliza imekuwakuwaje Chadema wakapata kiti kimoja cha ubunge wa kuchaguliwa (kupitia mwanamke) na kuachiwa hivyo viti maalum. Unahisi hii ilikuwa ni bahati mbaya? kwamba haukuwa mpgango maalum? na kama ni mpango maalum nini lilikuwa lengo lao waliofanya hivi?

4.Je unadhani Chadema wakikubali huo "mtego" ulioandaliwa mahususi baina ya Chama tawala,Tume ya uchaguzi na vyombo vya usalama, Je haka kamchezo ka "kudidimiza" upinzani katakuwa kamepata dawa kuelekea demokrasia makini?

5 Mwisho kabisa japo sio kwa umuhimu. Chadema wakikubali haka kamtego. Wahisani pamoja na marafiki wa dunia watakuwa na sababu tena ya kutunyooshea mkono juu ya uminywaji wa Demokrasia katika nchi yetu? Namalizia kwa mfano wa mwisho. Ikatokea ukamfumania mkeo na mwanaume mwingine kitandani kwako (kama umeoa), arafu akaanzisha ugonvi na bado kama haitoshi akatumia na vyombo vya dola kukukandamiza ili uonekana wewe ndio mshari na unayeleta chokochoko kwenye ndoa, Je utakubali ushauri wa kurudi mezani myamalize kundelea kukaa naye nyumba moja kwa sharti kwamba ukubali kuwa yeye ndiye mshindi? ila wewe ndio ulitaka kuleta chokochoko na kuharibu amani ya ndoa yenu na pengine unatumika na Mabeberu (watu wenye lengo baya dhidi ya ndoa yenu ndio maana ya neno beberu kwa mfano huu pekee)
 
View attachment 1633150
Tundu Lissu (Mgombea Urais wa Chadema) na Job Ndugai (Spika)

Kuna mdau kanitumia kitabu cha Gene Sharp (2012), kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Yaani, "Safari ya Kutoka Kwenye HImaya ya Kidikteta Kuelekea Kwenye HImaya ya Kidemokrasia: Mawazo Ambayo ni Msingi wa Hoja za Kuendeleza Mapambano ya Ukombozi." (Tafsiri yangu).

Mdau huyu amenitaka nikisome na kisha nijibu swali hili: Kama wabunge wa viti maalum wanatokana na kura za mgombea urais, na kama kura za mgombea urais wa Chadema zilizotangazwa na tume ni sehemu ya kura zote ambazo Chadema wanadai kwamba walipata, uamuzi wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum wa Chadema ili waende Bungeni kula kiapo na kuchapa kazi ya ubunge unachangia vipi katika kuimarisha demokrasia nchini Tanzania?

Nimekisoma kitabu na kukimaliza. Kina kurasa 100, na kimeandikwa kwa Kingereza chepesi. Ninaelewa mengi yaliyojiri katika siku zote za uchaguzi mkuu wa 2020. Pia najua malalamiko kadhaa ya vyama vya upinzani. Baada tafakari nimefikiria kama ifuatavyo:

Mosi, kama mgombea urais wa Chadema (Lissu) alipata kura X, na NEC ikatangaza kwamba Lissu kapata kura Y, ni wazi kwamba kura X ni kubwa kuliko kura Y, yaani X>Y.

Pili, Tofauti kati ya kura X na kura Y, tuseme kura Z, ndizo kura zinazobishaniwa. Chadema wanapinga kutotangazwa kwa kura Z. Yaani, Chadema wanapinga kutangazwa kwa kura Y pekee bila kujumlisha kura Z.

Tatu, kura Y zilizotangawa na NEC ni sehemu ya kura X zinazotamkwa na viongozi wa Chadema.

Nne, wabunge wa viti maalum wa Chadema wanatokana na kura Y, ambazo ni kura halali.

Kwa hiyo, idadi ya wabunge wa viti maalum kupitia Chadema iliyotangazwa na NEC ni idadi ya wabunge iliyotokana na kura halali.

Lakini, kama Chadema wanasema kuwa LIssu alipata kura ambazo ni ndogo kuliko zile zilizotangazwa na NEC, basi hitimisho langu linaporomoka hadi kuwa kifusi; na nitaungana nao katika msimamo wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum.

Nitatoa mifano miwili ili kufafanua hitimisho langu hili.

Mfano wa kwanza, ni mfano wa mtu aliyefukuzwa kazi, akamshitaki mwajiri kwenye Mahakama ya Kazi, Makahaka ikaamuru alippwe Milioni 10 kama fidia. Ikiwa mwajiri atamlipa milioni 3 pekee, anazipokea na kuzitumia kama gharama za kuweka wakili ili ambane mwajiri kwa hoja kwamba malipo ya milioni tatu "pekee" hayatoshi, lakini baada ya kuchukua milioni tatu.

Na mfano wa pili ni wa kifalsafa zaidi. Tunapotaja fasili ya umbo linaloitwa pembetatu tunasema hivi: "Pembetatu ni umbo lenye kona tatu pekee na pande tatu pekee."

Katika fasili hii neno "pekee" ni muhimu sana, kwani hata mraba unazo pembe tatu na kona tatu pia. Lakini mraba hauna pembe tatu "pekee" wala pande tatu "pekee."

Kwa mujibu wa mifano hii miwili, sasa nahitimisha hoja yangu. Katika kura za mgombea urais, Tundu Lissu, Chadema hawadai kura Y pekee, kama ilivyotangazwa na NEC. Wanadai kura Y na kura Z, ambapo tayari wamekwishapatiwa kura Y, lakini bado kupatiwa kura Z, kama watathibitisha kwamba zipo.

Hivyo, Chadema wanaweza, na wanapaswa kupokea kura Y na kuendelea kudai kura Z, kwa kuweka bayana hoja isiyoruhusu hewa wala maji kupenya.

Kwa mantiki hii, Chadema hawapaswi kuona shida kuteua wabunge wa viti maalum ili waende Bungeni kuapa. Nashauri wafanye hivyo leo.

Hapa nimejaribu kufikiri kwa sauti kwa kuzingatia hoja zilizojengwa na Gene Sharp (2012) katika kitabu chake kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Kwa mujibu wa kitabu hiki, kukataa kuteua wabunge wa viti maalum, kama wanavyofanya Chadema kwa sasa, ni aina mojawapo ya udikteta; na majadiliano ya maana hufanyika kati ta "mdikteta" na "mdemokrasia."

Yaani, Chadema inabidi waonyeshe kwa mawazo, maneno na vitendo kwamba wao ni "wademokrasia" ili wapate uhalali wa kumkabili yule anayeitwa "mdikteta."

Nimeambatanisha kitabu hicho hapa chini, kwa ajili ya wale wenye utayari wa kujisomea.

Huu ni mtazamo wangu, na ninawajibika kikamilifu kusanifu hoja hii yenye kutetea mtazamo huu.

Mama Amon,
Sumbawanga Kusini.
Natofautiana mtizamo na wewe,kwanza umekiri uwepo wa kasoro kama sii malalamiko au mapungufu.Mapungufu haya hayakuwa ya bahati mbaya,ila ya kimkakati kwa kushisha pande mbalimbali.Hivyo kukubaliana na hali hiyo ni kuhalalisha mapungufu ya kupangwa.
 
Ndugu, analogical argument inayo anatomia yake, kama ifuatavyo:

1. Members of class X have properties making up set P and more;
2. Members of Class Y have properties making up set Q and more;
3. Members of Set P are similar to members of set Q;
4. Thus, what is true of class X is true of class Y.

Nje ya mfumo huu wa ufananisho, analogical argument fails.
Kwa hiyo, usijielekeze kwenye tofauti.
Zingatia ufanano.
Hakuna ufanano hapo ni sawa na kuanzisha race kati ya Mlamavu wa miguu na mlemavu wa masikio simply kwa sababu wote ni walemavu watashindana !!
 
Nilichofanya ni reasoning by analogy. Utaratibu huu unaanzia kwenye ufanano, na sio kwenye utofauti. Pointi yangu ni kwamba, hivyo viti 19 ni haki ya chadema ambayo inaweza, na inapaswa, kuchukuliwa ili kiwe kianzio cha kudai haki baki. Wabunge hawa wataongeza nguvu ya uchumi ya chama, lakini sio kwa sababu wamependelewa na serikali. Bali kwa kuwa wanayo haki ya kuwa wabunge kutokana na kura halali za Chadema. Wale wagombea ubunge wa jukwaani wanaodai kwamba waliporwa waendelee na hoja. Tena waombe msaada wa kifedha kutoka kwa wabunge hawa wa viti maalum ili kuimarisha mapambano. Umenisoma?
Nimekusoma Sana tu,
kwa mtizamo wa faida ya haraka na muda mfupi CDM wakubali kupeleka majina ya kujaza hizo nasafi.....

Ila kwa mtizamo wa muda mrefu na na faida kuu, CDM intakiwa kuwa na msimamo wakutopeleka majina badala yake waandae list ya madai yao tena ikiwa umeandikwa kwa ufasaha na mantiki, vitu zitakavyoweza kutatua haya Mambo hata kwa chaguzi zijazo mfano
✓tume huru, mchakato unaanze Mara moja
✓matokeo ya Uchaguzi ya ngazi zote kupingwa makamani
✓kufumua muundo wa jeshi la polisi liwe la kulinda raia Bila kupokea maagizo ktk kwa wanasiasa
✓kuipa mahakama nguvu zaidi iweze kusikiliza mashauri na kutoa maamuzi bila mshinikizo wa serikali
✓maboresho makubwa ya katiba, kupunguza nguvu na mamlaka ya Rais, kuongeza Uhuru wa mihimili ya bunge,mahakama na other overnight bodies.
✓katiba mpya

Hii ndo italeta solution ya kudumu kwa kero zitokanazo na uchaguzi na siasa nchini,Leo na kesho


Ila Kama lengo ni posho, mishahara ya ubunge na ruzuku CDM wapeleke hayo majina ili tuwajue rangi ya harisi, ili waje wapuuzwe baadaye watakapoanza kujifanya wanatetea sijui demokrasia na Uhuru maoni, mawazo nchini.

Hi
 
Mama Amon, natumaini umesimama kwenye uaminifu (honesty) unapotoa hilo pendekezo.

Umeainisha sentenso ya muamala kama wa kibiashara vile kuonyesha faida watakayopata CHADEMA kwa kupeleka wabunge wa viti maalum. Kwamba watakuwa nyenzo ya kudai kura zilizoibiwa!

Naamini unao uelewa mkubwa kuweza kutambua kuwa alichofanya Mwenyekiti wa CCM ni kufifisha nguvu ya CHADEMA kwa kuwapoka ushindi wao kwenye urais na kwenye majimbo na kuhakikisha wabunge wake maarufu hawarudi bungeni.

Kisha kawapa mbunge mmoja tu wa jimbo asiye na historia ya “kutikisa” sana. Sasa anachotaka ni CHADEMA kuwa na uwakilishi dhaifu wa viti maalum kuhalalisha dhulma kubwa iliyofanywa kwa chama hicho na kwa Watanzania kwa ujumla.

Aidha, wewe kama ni mama (ke) kweli umeshasikia kejeli inayoshamirishwa na wabunge wanawake wa CCM wakishangiliwa na spika kuwa wanaopata viti maalum CHADEMA sharti “wadhalilishwe” na mwenyekiti wa chama hicho!

Halafu kweli unaamini hao viti maalum wataweza kudai kura za CHADEMA zilizoibwa?

Usishangae ukiona wadau hapa JF wakikutilia mashaka makubwa kuhusu nia yako halisi (real motive) ya kuleta bandiko hili.

Nimependa mtiririko wa mawazo yako.

Kwa hapa itoshe kunukuu sura ya kwanza ya kitabu ambacho nime-attach hapa chini.

Tunasoma:

"When one wants to bring down a dictatorship most effectively and with the least cost then one has four immediate tasks: One must strengthen the oppressed population themselves in their determination, self-confidence, and resistance skills; One must strengthen the independent social groups and institutions of the oppressed people; One must create a powerful internal resistance force; One must develop a wise grand strategic plan for liberation and implement it skillfully." (tazama attachment, sura ya kwanza, chini ya sub-heading hii: "Facing the hard truth ")

Pointi yangu ni kwamba, katika "grand strategic plan for liberation" inayotakiwa tunapaswa kuwa na jukumu la kupeleka wabunge wa viti maalum bungeni, na sio kuwazuia. Hawa watakuwa na kazi nyingi.

Mojawapo ni kwamba watakuwa maafisa vipenyo wetu. Pili, watakiwezesha chama kuwa na nguvu ya kiuchumi kuendeleza mapambano.

Lakini, nisema kwamba, wabunge wa viti maalum wanaweza kutikisa kuliko unavyofikiria.

Baadhi wanazo shahada za uzamivu.

Wengine ni wanasheria.

Wengine ni wabunge wzoefu.

Chadema wachangamke, kijua ndio hichi!
 

Attachments

Nimekusoma Sana tu,
kwa mtizamo wa faida ya haraka na muda mfupi CDM wakubali kupeleka majina ya kujaza hizo nasafi.....

Ila kwa mtizamo wa muda mrefu na na faida kuu, CDM intakiwa kuwa na msimamo wakutopeleka majina badala yake waandae list ya madai yao tena ikiwa umeandikwa kwa ufasaha na mantiki, vitu zitakavyoweza kutatua haya Mambo hata kwa chaguzi zijazo mfano
✓tume huru, mchakato unaanze Mara moja
✓matokeo ya Uchaguzi ya ngazi zote kupingwa makamani
✓kufumua muundo wa jeshi la polisi liwe la kujikuta kulinda raia Bila kupokea maagizo ktk kwa wanasiasa
✓kuipa mahakama nguvu zaidi iweze kusikiliza mashauri na kutoa maamuzi bila mshinikizo wa serikali
✓maboresho makubwa ya katiba, kupunguza nguvu na mamlaka ya Rais, kuongeza Uhuru wa mihimili ya bunge,mahakama na other overnight bodies.

Hii ndo italeta solution ya kudumu kwa kero zitokanazo na uchaguzi na siasa nchini


Ila Kama lengo ni posho, mishahara ya ubunge na ruzuku CDM upeleke hayo majina ili tuwajue rangi ya harisi, ili waje wapuuzwe baadaye watakapoanza kufinya wanatetea sijui demokrasia na Uhuru nchini.
Tusome pamoja:

"When one wants to bring down a dictatorship most effectively and with the least cost then one has four immediate tasks: One must strengthen the oppressed population themselves in their determination, self-confidence, and resistance skills; One must strengthen the independent social groups and institutions of the oppressed people; One must create a powerful internal resistance force; One must develop a wise grand strategic plan for liberation and implement it skillfully." (tazama attachment, sura ya kwanza, chini ya sub-heading hii: "Facing the hard truth ")
 

Attachments

Natofautiana mtizamo na wewe,kwanza umekiri uwepo wa kasoro kama sii malalamiko au mapungufu.Mapungufu haya hayakuwa ya bahati mbaya,ila ya kimkakati kwa kushisha pande mbalimbali.Hivyo kukubaliana na hali hiyo ni kuhalalisha mapungufu ya kupangwa.
Be specific ili niweze kukujibu kwa mtindo wa pointi counter point
 
Kwa heshima, sikubaliani na kauli yako hii hapa.
Kwani mwajiriwa aliyelipwa milioni tatu hapo juu, akazipokea, na kisha akaendelea kudai ziada, alikuwa ameunga mkono ufedhuli wa mwajiri mkorofi?
Chadema, hawapangiwi ,viti mahalum hakuna, na ilisha , kwa mazingira yoyote yale kupata kitu kwa fadhila sio Jambo zuri, na ikiamua kitu na kuludi nyuma ,tena katika madai ya msingi mungu mwenyewe atakuchoka ,pamoja na yesu kusulubiwa msalabani, Bado hakukana kile anacho kuamini,Sasa binadam sie ni nani mpaka tuwe wepesi kiasi hicho, hakunaa mkuu,
 
Chadema, hawapangiwi ,viti mahalum hakuna, na ilisha , kwa mazingira yoyote yale kupata kitu kwa fadhila sio Jambo zuri,
Hakuna kiti cha ubunge maalum kinapatikana kwa fadhila.
Ila inawezekana upande wa pili hali ikawa hivyo.
Kwa Chadema hakuna uwezekano huo.
Kwa hiyo neno "fadhila" futa kwenye maelezo yako.
 
Dalili zote zinaonyesha kuwa wewe ni miongoni mwao wakiuka demokrasia.
Kiukweri hoja zako hazina mantiki yeyote kwetu sisi ambao ninyi na wabunge wenu mnatuita mambwa. Tumewaachia bunge lenu bakini wenyewe.
 
Nilichofanya ni reasoning by analogy. Utaratibu huu unaanzia kwenye ufanano, na sio kwenye utofauti. Pointi yangu ni kwamba, hivyo viti 19 ni haki ya chadema ambayo inaweza, na inapaswa, kuchukuliwa ili kiwe kianzio cha kudai haki baki. Wabunge hawa wataongeza nguvu ya uchumi ya chama, lakini sio kwa sababu wamependelewa na serikali. Bali kwa kuwa wanayo haki ya kuwa wabunge kutokana na kura halali za Chadema. Wale wagombea ubunge wa jukwaani wanaodai kwamba waliporwa waendelee na hoja. Tena waombe msaada wa kifedha kutoka kwa wabunge hawa wa viti maalum ili kuimarisha mapambano. Umenisoma?

Ndio maana nikasema mfano wako hauna mantik. Kutokana na uchache wa hao wabunge sababu pekee inayofanya wahitajike sana kwenye Bunge ni kuleta taswira ya kuwa bado ni Bunge la vyama vingi.

Mimi hata sielewi unawezaje kusema kuwa wataongeza vipi uchumi wa chama maana hata kama kila mmoja akichangia milioni moja watapata shilingi milioni 19 ambazo ni kidogo sana ukiangalia gharama za kuendesha chama. Kitu kibaya zaidi ni kuwa watapoteza legitimacy kwa wale waliowapigia kura.

Aidha, hata huo uteuzi wa majina utaleta mpasuko zaidi kwenye chama. Tukiendeleza analogy yako ni kama vile unayemdai shilingi milioni kumi akakupa 500,000 halafu akakuambia sikulipi tena na hamna unachoweza kunifanya. Na mbaya zaidi, ile milioni kumi ni sehemu yako ya mkopo wa shilingi milioni 20 mliokopa pamoja. Jamaa anakula za kwake na zako halafu anakutupia makombo!

Ikifikia mahali chama kitegemee hisani ya wabunge wake ili kiweze kudai haki yake basi hakistahili kuwepo. Unachosema ni wakubali kula makombo ya chakula ambacho walitakiwa kushiriki wakiwa meza kuu.

Hapana, sijakusoma.

Amandla...
 
Wao cdm kama chama waamue watakacho, lakini sisi wafuasi wao tuko wazi kwamba hatukubali washiriki kuhalalisha haramu. Wanaweza kupambana kusaka faida za muda mfupi, lakini wasitegemee tena sisi kujitokeza kupiga kura. Wabaki huku nje tudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya. Haya ni madai halali, na sioni yakipatikana kwa hivyo viti 19 kwenda bungeni. Sio lazima msimamo huu uwe bora, lakini ndio msimamo sahihi kwa mazingira haya.
Mkuu kama ungekua karibu na CDM au kuweza kufikisha ushauri kwao, nadhani CDM wanatakiwa kuwa more serious this time than any other time. Una hoja nzuri sana. Nimekufuatilia comments zako zinafaa CDM na vyama vya upinzani makini wazifanyie kazi. Without tume huru ya uchaguzi na katiba mpya, there is no general election in Tanzania. Zaidi tutaendelea na hiki kinachotokea miaka yote na zaidi hiki cha mwaka huu 2020, ambacho hata CCM wenyewe bado wako kwenye mshangao.
 
Sawa huo ni mtazamo wako.

Maswali magumu pengine tukuulize Ndg. mwandishi:

1. Endapo CHADEMA wakakukubali kuteua wabunge wa viti maalum, Je? hii itakuwa imesaidia nini katika kujenga Demokrasia huru na utawala wa haki nchini?
2. Je unadhani nani atakuwa mnufaika mkubwa wa hayo maamuzi endapo yatafanyika kati ya "waliyotengeneza hayo mazingira" au Demokrasia ya nchi yetu.

3. Je umewahi kujiuliza imekuwakuwaje Chadema wakapata kiti kimoja cha ubunge wa kuchaguliwa (kupitia mwanamke) na kuachiwa hivyo viti maalum. Unahisi hii ilikuwa ni bahati mbaya? kwamba haukuwa mpgango maalum? na kama ni mpango maalum nini lilikuwa lengo lao waliofanya hivi?

4.Je unadhani Chadema wakikubali huo "mtego" ulioandaliwa mahususi baina ya Chama tawala,Tume ya uchaguzi na vyombo vya usalama, Je haka kamchezo ka "kudidimiza" upinzani katakuwa kamepata dawa kuelekea demokrasia makini?

5 Mwisho kabisa japo sio kwa umuhimu. Chadema wakikubali haka kamtego. Wahisani pamoja na marafiki wa dunia watakuwa na sababu tena ya kutunyooshea mkono juu ya uminywaji wa Demokrasia katika nchi yetu? Namalizia kwa mfano wa mwisho. Ikatokea ukamfumania mkeo na mwanaume mwingine kitandani kwako (kama umeoa), arafu akaanzisha ugonvi na bado kama haitoshi akatumia na vyombo vya dola kukukandamiza ili uonekana wewe ndio mshari na unayeleta chokochoko kwenye ndoa, Je utakubali ushauri wa kurudi mezani myamalize kundelea kukaa naye nyumba moja kwa sharti kwamba ukubali kuwa yeye ndiye mshindi? ila wewe ndio ulitaka kuleta chokochoko na kuharibu amani ya ndoa yenu na pengine unatumika na Mabeberu (watu wenye lengo baya dhidi ya ndoa yenu ndio maana ya neno beberu kwa mfano huu pekee)

Ndg Kasenene,

Asante kwa maswali yaliyonyooka. Najibu kawa mtindo wa bandika bandua kama ifuatavyo:

1. Endapo CHADEMA wakakukubali kuteua wabunge wa viti maalum, Je? hii itakuwa imesaidia nini katika kujenga Demokrasia huru na utawala wa haki nchini?

Jawabu: Uwepo wa wabunge wa viti maalum bungeni kutoka Chadema kutaimarisha mfumo wa demokrasia ya Kibunge. Kamati za Bunge zinazopaswa kuongozwa na wapinzani zitapata wenyeviti. Pia, Mawaziri kivuli wanaweza kuwepo kwa ajili ya kuandaa bajeti vivuli zenye maudhui boreshi. Kwa sasa, bunge limenasa katika kipingele hiki, ama kwa kujua au kwa kutojua.

2. Je unadhani nani atakuwa mnufaika mkubwa wa hayo maamuzi endapo yatafanyika kati ya "waliyotengeneza hayo mazingira" au Demokrasia ya nchi yetu.

Jawabu: Watu "waliyotengeneza hayo mazingira" ya kamati kadhaa kuongozwa na wapinzani ni Bunge zima lililotunga kanuni za kudumu za Bunge. Bunge ni chombo cha Taifa. Kwa hiyo, Taifa litanufaika na uamuzi wa Chadema kupeleka wabunge wa viti maalum. Pia Chadema watanufaika kwa njia ya kupata mgao kutoka kwenye posho za wabunge kwa mujibu wa kanuni za Chama.

3. Je umewahi kujiuliza imekuwakuwaje Chadema wakapata kiti kimoja cha ubunge wa kuchaguliwa (kupitia mwanamke) na kuachiwa hivyo viti maalum. Unahisi hii ilikuwa ni bahati mbaya? Kwamba haukuwa mpgango maalum? na kama ni mpango maalum nini lilikuwa lengo lao waliofanya hivi?

Jawabu: Sio kwamba nimewahi kufikiria. Najua kila kilichotokea kwenye kila hatua ya mchakato wa uchaguzi. Najua malalamiko ya Chadema. Najua matokeo yaliyotangazwa na NEC. Najua kwamba mgombea ubunge wa kwanza kutangazwa ni Mbowe, kwamba ameshindwa, And a lot more. Lakini, haya yote sio hoja yangu katika uzi huu. Hapa naongelea zile kura chache zilizotangazwa na NEC, na ambazo kwa mujibu wa udadavuzi wangu ni kura halali za Chadema. Na kwa hiyo, tunao wabunge halali wa viti maalum waliotokana na kura hizo. Natamani waende Bungeni leo ili kutekeleza majukumu yao, halafu chama kiendelee kushughulikia masuala hayo mengine kuhusu kura zinazodaiwa kuibwa na watu wasiojulikana!

4.Je unadhani Chadema wakikubali huo "mtego" ulioandaliwa mahususi baina ya Chama tawala,Tume ya uchaguzi na vyombo vya usalama, Je haka kamchezo ka "kudidimiza" upinzani katakuwa kamepata dawa kuelekea demokrasia makini?

Jawabu: Mtego gani unaongelea? Utaratibu wa kupeleka wabunge wa viti maalumu Bungeni sio mtego kwa Chadema. Ni matakwa ya Kikatiba. Mtego ambao nauona mimi ni huu wa kuwa na Tume ya Uchaguzi ambaye ni Mtumwa wa serikali na chama tawala. Lakini, hiyo ni hoja tofauti na kinachojadiliwa katika bandiko langu.

5. Mwisho kabisa japo sio kwa umuhimu. Chadema wakikubali haka kamtego. Wahisani pamoja na marafiki wa dunia watakuwa na sababu tena ya kutunyooshea mkono juu ya uminywaji wa Demokrasia katika nchi yetu? Namalizia kwa mfano wa mwisho. Ikatokea ukamfumania mkeo na mwanaume mwingine kitandani kwako (kama umeoa), arafu akaanzisha ugonvi na bado kama haitoshi akatumia na vyombo vya dola kukukandamiza ili uonekana wewe ndio mshari na unayeleta chokochoko kwenye ndoa, Je utakubali ushauri wa kurudi mezani myamalize kundelea kukaa naye nyumba moja kwa sharti kwamba ukubali kuwa yeye ndiye mshindi? ila wewe ndio ulitaka kuleta chokochoko na kuharibu amani ya ndoa yenu na pengine unatumika na Mabeberu (watu wenye lengo baya dhidi ya ndoa yenu ndio maana ya neno beberu kwa mfano huu pekee)

Jawabu: "Haka kamtego" ka NEC ambayo imewekwa kwapani na serikali wahisani wanakajua vizuri kuliko wewe. Lakini, pia wahisani wanapaswa kupigwa shule juu ya mienendo ya siasa za ndani ya Tanzania kwa kuzingatia kanuni za ukweli na uwazi. Hoja yangu hapa, yenye kutofautisha uhalali wa kura zilizozalisha wabunge wa viti maalum wa Chadema, na kura zinazodaiwa kuibwa kwa faida ya CCM, ni hoja inayoeleweka, na inayoweza, na inayopaswa kukubalika kwa wahisani wenye akili timamu.


Karibu kwa swali la nyongeza.
 
Back
Top Bottom