Uchaguzi 2020 Tathmini yangu juu ya Uchaguzi Mkuu 2020: Hakuna sababu nzuri ya kukataa kuteua wabunge wa Viti Maalum CHADEMA

Uchaguzi 2020 Tathmini yangu juu ya Uchaguzi Mkuu 2020: Hakuna sababu nzuri ya kukataa kuteua wabunge wa Viti Maalum CHADEMA

View attachment 1633150
Tundu Lissu (Mgombea Urais wa Chadema) na Job Ndugai (Spika)

Kuna mdau kanitumia kitabu cha Gene Sharp (2012), kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Yaani, "Safari ya Kutoka Kwenye HImaya ya Kidikteta Kuelekea Kwenye HImaya ya Kidemokrasia: Mawazo Ambayo ni Msingi wa Hoja za Kuendeleza Mapambano ya Ukombozi." (Tafsiri yangu).

Mdau huyu amenitaka nikisome na kisha nijibu swali hili: Kama wabunge wa viti maalum wanatokana na kura za mgombea urais, na kama kura za mgombea urais wa Chadema zilizotangazwa na tume ni sehemu ya kura zote ambazo Chadema wanadai kwamba walipata, uamuzi wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum wa Chadema ili waende Bungeni kula kiapo na kuchapa kazi ya ubunge unachangia vipi katika kuimarisha demokrasia nchini Tanzania?

Nimekisoma kitabu na kukimaliza. Kina kurasa 100, na kimeandikwa kwa Kingereza chepesi. Ninaelewa mengi yaliyojiri katika siku zote za uchaguzi mkuu wa 2020. Pia najua malalamiko kadhaa ya vyama vya upinzani. Baada tafakari nimefikiria kama ifuatavyo:

Mosi, kama mgombea urais wa Chadema (Lissu) alipata kura X, na NEC ikatangaza kwamba Lissu kapata kura Y, ni wazi kwamba kura X ni kubwa kuliko kura Y, yaani X>Y.

Pili, Tofauti kati ya kura X na kura Y, tuseme kura Z, ndizo kura zinazobishaniwa. Chadema wanapinga kutotangazwa kwa kura Z. Yaani, Chadema wanapinga kutangazwa kwa kura Y pekee bila kujumlisha kura Z.

Tatu, kura Y zilizotangawa na NEC ni sehemu ya kura X zinazotamkwa na viongozi wa Chadema.

Nne, wabunge wa viti maalum wa Chadema wanatokana na kura Y, ambazo ni kura halali.

Kwa hiyo, idadi ya wabunge wa viti maalum kupitia Chadema iliyotangazwa na NEC ni idadi ya wabunge iliyotokana na kura halali.

Lakini, kama Chadema wanasema kuwa LIssu alipata kura ambazo ni ndogo kuliko zile zilizotangazwa na NEC, basi hitimisho langu linaporomoka hadi kuwa kifusi; na nitaungana nao katika msimamo wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum.

Nitatoa mifano miwili ili kufafanua hitimisho langu hili.

Mfano wa kwanza, ni mfano wa mtu aliyefukuzwa kazi, akamshitaki mwajiri kwenye Mahakama ya Kazi, Makahaka ikaamuru alippwe Milioni 10 kama fidia. Ikiwa mwajiri atamlipa milioni 3 pekee, anazipokea na kuzitumia kama gharama za kuweka wakili ili ambane mwajiri kwa hoja kwamba malipo ya milioni tatu "pekee" hayatoshi, lakini baada ya kuchukua milioni tatu.

Na mfano wa pili ni wa kifalsafa zaidi. Tunapotaja fasili ya umbo linaloitwa pembetatu tunasema hivi: "Pembetatu ni umbo lenye kona tatu pekee na pande tatu pekee."

Katika fasili hii neno "pekee" ni muhimu sana, kwani hata mraba unazo pembe tatu na kona tatu pia. Lakini mraba hauna pembe tatu "pekee" wala pande tatu "pekee."

Kwa mujibu wa mifano hii miwili, sasa nahitimisha hoja yangu. Katika kura za mgombea urais, Tundu Lissu, Chadema hawadai kura Y pekee, kama ilivyotangazwa na NEC. Wanadai kura Y na kura Z, ambapo tayari wamekwishapatiwa kura Y, lakini bado kupatiwa kura Z, kama watathibitisha kwamba zipo.

Hivyo, Chadema wanaweza, na wanapaswa kupokea kura Y na kuendelea kudai kura Z, kwa kuweka bayana hoja isiyoruhusu hewa wala maji kupenya.

Kwa mantiki hii, Chadema hawapaswi kuona shida kuteua wabunge wa viti maalum ili waende Bungeni kuapa. Nashauri wafanye hivyo leo.

Hapa nimejaribu kufikiri kwa sauti kwa kuzingatia hoja zilizojengwa na Gene Sharp (2012) katika kitabu chake kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Kwa mujibu wa kitabu hiki, kukataa kuteua wabunge wa viti maalum, kama wanavyofanya Chadema kwa sasa, ni aina mojawapo ya udikteta; na majadiliano ya maana hufanyika kati ta "mdikteta" na "mdemokrasia."

Yaani, Chadema inabidi waonyeshe kwa mawazo, maneno na vitendo kwamba wao ni "wademokrasia" ili wapate uhalali wa kumkabili yule anayeitwa "mdikteta."

Nimeambatanisha kitabu hicho hapa chini, kwa ajili ya wale wenye utayari wa kujisomea.

Huu ni mtazamo wangu, na ninawajibika kikamilifu kusanifu hoja hii yenye kutetea mtazamo huu.

Mama Amon,
Sumbawanga Kusini.
1. Asilimia 88 ya mawakala wa CHADEMA walizuiwa/ kutolewa vituoni kabla na baada ya zoezi la kupiga kura.

2. CHADEMA nchi nzima hawakupata nakala za matokeo ya uchaguzi kutokana na mawakala kukatazwa kuingia vituoni au kufukuzwa vituoni hivyo hizo kura X/Y or Z hazifahamiki zipi ni halali na zipi si halali.

3. Wakati wa kuhesabu kura vituo vilivamiwa na maafisa wa polisi kwa kujaza kura zilizokuwa kwenye mabegi na sehemu zingine fomu za matokeo zilijazwa namba tu bila kuzingatia idadi hata ya wapiga kura kwenye kituo husika.

4. Wasimamizi wa uchaguzi kwenye vituo kadhaa waliingia na kura kwenye mabegi zikiwa zimejazwa kwa mgombea wa chama tawala.

5. CHADEMA wanahoji uhalali wa kura zilizotangazwa kwa kuzingatia swali kuwa ni zipi kati ya zilizokuwa kwenye mabegi ya wasimamizi wa uchaguzi au zilizopigwa na wananchi ?

6. Kama CHADEMA hawakuwa na wakala vituoni wakati wa kuhesabu kura je kura halali za kwao ni zipi alizopata mgombea wa ccm au walizopewa wao na tume nani anauthibitisho kuwa ni za kwao wakati hawakuwa na mtazamaji vituoni ?

Kwa kuzingatia kuwa uchaguzi ni mchakato na unahalalishwa na uwazi na haki katika hatua zote msingi wa CHADEMA kukataa kuchagua wabunge wa viti maalumu ni " Mchakato mzima wa kupiga kura na kuhesabu kura" kuwa haukufuata sheria na uligubikwa na mambo ambayo yaliondoa uhalali wa mchakato wenyewe na matokeo ya mchakato.
Hoja ya CHADEMA siyo idadi ya kura ila ni mchakato mzima wa upigaji kura.
 
Wao cdm kama chama waamue watakacho, lakini sisi wafuasi wao tuko wazi kwamba hatukubali washiriki kuhalalisha haramu. Wanaweza kupambana kusaka faida za muda mfupi, lakini wasitegemee tena sisi kujitokeza kupiga kura. Wabaki huku nje tudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya. Haya ni madai halali, na sioni yakipatikana kwa hivyo viti 19 kwenda bungeni. Sio lazima msimamo huu uwe bora, lakini ndio msimamo sahihi kwa mazingira haya.

Mosi, hoja ya kudai Katiba, Tume Huru nk, kwa upande mmoja, na hoja ya kutuma wabunge wa viti maalum bungeni, kwa upande mwingine, ni hoja mbili tofauti.

Pili, kupeleka wabunge wa viti maalum sio kikwazo kwa hoja ya kwanza.

Na tatu, chama kinaendeshwa kwa vikao.

Wananchi walioko nje ya vikao wanapaswa kuonyesha utii kwa maamuzi halali.

Hata viongozi walio kwenye vikao pia wanapaswa kuongozwa na katiba na kanuni, na sio mihemuko.
 
1. Asilimia 88 ya mawakala wa CHADEMA walizuiwa/ kutolewa vituoni kabla na baada ya zoezi la kupiga kura.

2. CHADEMA nchi nzima hawakupata nakala za matokeo ya uchaguzi kutokana na mawakala kukatazwa kuingia vituoni au kufukuzwa vituoni hivyo hizo kura X/Y or Z hazifahamiki zipi ni halali na zipi si halali.

3. Wakati wa kuhesabu kura vituo vilivamiwa na maafisa wa polisi kwa kujaza kura zilizokuwa kwenye mabegi na sehemu zingine fomu za matokeo zilijazwa namba tu bila kuzingatia idadi hata ya wapiga kura kwenye kituo husika.

4. Wasimamizi wa uchaguzi kwenye vituo kadhaa waliingia na kura kwenye mabegi zikiwa zimejazwa kwa mgombea wa chama tawala.

5. CHADEMA wanahoji uhalali wa kura zilizotangazwa kwa kuzingatia swali kuwa ni zipi kati ya zilizokuwa kwenye mabegi ya wasimamizi wa uchaguzi au zilizopigwa na wananchi ?

6. Kama CHADEMA hawakuwa na wakala vituoni wakati wa kuhesabu kura je kura halali za kwao ni zipi alizopata mgombea wa ccm au walizopewa wao na tume nani anauthibitisho kuwa ni za kwao wakati hawakuwa na mtazamaji vituoni ?

Kwa kuzingatia kuwa uchaguzi ni mchakato na unahalalishwa na uwazi na haki katika hatua zote msingi wa CHADEMA kukataa kuchagua wabunge wa viti maalumu ni " Mchakato mzima wa kupiga kura na kuhesabu kura" kuwa haukufuata sheria na uligubikwa na mambo ambayo yaliondoa uhalali wa mchakato wenyewe na matokeo ya mchakato.
Hoja ya CHADEMA siyo idadi ya kura ila ni mchakato mzima wa upigaji kura.

Najua mengi kati ya haya uliyoyaandika.

Lakini, nashauri kutofautisha maembe na machungwa.

Pia nashauri kujiepusha na mantiki ya samaki mmoja akioza wote wameoza.

Turudi kwenye hoja yetu:

Kura za Chadema zilizotangazwa na NEC ni kidogo kuliko uhalisia au ni nyingi zaidi ya uhalisia?

Kama ni kidogo kuliko uhalisia, ni kura halali au kura haramu?

Kama ni kura halali, kwa nini wabunge wa viti maalum wanaotokana na kura hizo wawe haramu?

Nashauri tupeleke wabunge, halafu tuendelee kupigania masuala mengine.

Hakuna athari.
 
Hapa ndipo nimepata kujua kwa nini tunapishana. Kuna mawili:

1. Mtazamo wangu ni kwamba, hizo kura chache zilizotangazwa na NEC ni halali, wakati zile kura nyingi zinazodaiwa kuhamishiwa upande mwingine ni haramu.

2. Lakini, wewe unasema kuwa, kwa vile mchakato mzima ni haramu, na kwa kuwa hizo kura chache ni sehemu ya mchakato haramu, basi hata hizo kura kidogo ni haramu.

Lakini, huoni kuwa mantiki ya samaki mmoja akioza wote wameoza haikubaliki kimantiki na kisheria?

Kwenye hili kila mmoja ana utashi wake, sio lazima kwenye msimamo wangu niwe sahihi, lakini nitakuwa mjinga kuacha ninachoamini, niamini unachoamini ww hata kama sikiamini.
 
Kwenye hili kila mmoja ana utashi wake, sio lazima kwenye msimamo wangu niwe sahihi, lakini nitakuwa mjinga kuacha ninachoamini, niamini unachoamini ww hata kama sikiamini.

Self-imposed irationality aside, lengo la kujenga hoja ni kubadilisha imani ya msikilizaji kwa kutumia nguvu ya ushahidi.

Kwa hiyo, nakualika ukapime uzito wa ushahidi katika hoja zangu.

Kama ukishawishika, sio dhambi kubadili imani yako ya sasa.
 
Fomula ya kukokotoa idadi ya viti maalum hata kama ikihusisha kura za ubunge haina madhara kwa hoja yangu. Pointi yangu ni kwamba, hizi kura kidogo zilizobaki baada ya kitendo kinachoitwa wizi wa kura ndizo zimezaa viti maalum. Ni kura halali na viti maalum ni viti halali. Kura zinazoitwa haramu ni zile zinazodaiwa kuibwa kutoka upande A na kwenda upande B. Hizo ziendelee kutafutwa. Sina shida ni hilo la pili. Umenisoma?
Pengine hoja yako wangeielewa zaidi kama ungewapa maarifa ya namna ya "kukomboa" hizo kura ambazo wanasema ziliibwa.Je wanazikomboaje? maana mfano wa madai kati ya mwajiri na mwajiriwa ambao umeutoa naona ,kwa mawazo yangu,hausadifu kwenye hoja hii.
 
Tujielekeze kwenye hoja.
Tusitoke nje ya mstari.
Achana na hayo mambo madogo.
Jibu lako hili nalifananisha na jibu la mbunge mmoja alipofuatwa na mpiga kura wake alipohoji mambo ya maendeleo mpiga kura akaambiwa achana na siasa wewe kunywa pombe.
 
Pengine hoja yako wangeielewa zaidi kama ungewapa maarifa ya namna ya "kukomboa" hizo kura ambazo wanasema ziliibwa.Je wanazikomboaje? maana mfano wa madai kati ya mwajiri na mwajiriwa ambao umeutoa naona ,kwa mawazo yangu,hausadifu kwenye hoja hii.

Hoja yangu ni rahisi sana.

Haina uhusiano na zoezi la kutafuta kura zinazodaiwa kuibiwa.

Mimi naongelea zile kura chache, ambazo kwa mtazamo wangu, ni kura halali.

Na mfano wangu wa mwajiri na mwajiriwa unafaa katika mipaka hiyo.

Kuhusu kura zinazodaiwa kuibwa kuna nadharia nyingi.

Baadhi ya nadharia ni dhaifu mno.

Nadharia nyingine zina uzito.

Lakini, niseme wazi: mpaka sasa hakuna nadharia ambayo nimeisikia ikitajwa inayoweza kuzalisha ushahidi wa kimahakama unaoweza kusaidia "kukomboa" hizo kura zinazodaiwa kuibiwa.

Lakini, hii sio hoja yangu kwa leo.
 
Jibu lako hili nalifananisha na jibu la mbunge mmoja alipofuatwa na mpiga kura wake alipohoji mambo ya maendeleo mpiga kura akaambiwa achana na siasa wewe kunywa pombe.

Hata hujaelewa nilichosema.
KUna mtu alijaribu kukuondoa kwenye mada.
Ukaanza kuongelea mleta mada badala ya mada ya bandiko hili.
Hivyo tu.
Usiende mbali.
 
View attachment 1633150
Tundu Lissu (Mgombea Urais wa Chadema) na Job Ndugai (Spika)

Kuna mdau kanitumia kitabu cha Gene Sharp (2012), kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Yaani, "Safari ya Kutoka Kwenye HImaya ya Kidikteta Kuelekea Kwenye HImaya ya Kidemokrasia: Mawazo Ambayo ni Msingi wa Hoja za Kuendeleza Mapambano ya Ukombozi." (Tafsiri yangu).

Mdau huyu amenitaka nikisome na kisha nijibu swali hili: Kama wabunge wa viti maalum wanatokana na kura za mgombea urais, na kama kura za mgombea urais wa Chadema zilizotangazwa na tume ni sehemu ya kura zote ambazo Chadema wanadai kwamba walipata, uamuzi wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum wa Chadema ili waende Bungeni kula kiapo na kuchapa kazi ya ubunge unachangia vipi katika kuimarisha demokrasia nchini Tanzania?

Nimekisoma kitabu na kukimaliza. Kina kurasa 100, na kimeandikwa kwa Kingereza chepesi. Ninaelewa mengi yaliyojiri katika siku zote za uchaguzi mkuu wa 2020. Pia najua malalamiko kadhaa ya vyama vya upinzani. Baada tafakari nimefikiria kama ifuatavyo:

Mosi, kama mgombea urais wa Chadema (Lissu) alipata kura X, na NEC ikatangaza kwamba Lissu kapata kura Y, ni wazi kwamba kura X ni kubwa kuliko kura Y, yaani X>Y.

Pili, Tofauti kati ya kura X na kura Y, tuseme kura Z, ndizo kura zinazobishaniwa. Chadema wanapinga kutotangazwa kwa kura Z. Yaani, Chadema wanapinga kutangazwa kwa kura Y pekee bila kujumlisha kura Z.

Tatu, kura Y zilizotangawa na NEC ni sehemu ya kura X zinazotamkwa na viongozi wa Chadema.

Nne, wabunge wa viti maalum wa Chadema wanatokana na kura Y, ambazo ni kura halali.

Kwa hiyo, idadi ya wabunge wa viti maalum kupitia Chadema iliyotangazwa na NEC ni idadi ya wabunge iliyotokana na kura halali.

Lakini, kama Chadema wanasema kuwa LIssu alipata kura ambazo ni ndogo kuliko zile zilizotangazwa na NEC, basi hitimisho langu linaporomoka hadi kuwa kifusi; na nitaungana nao katika msimamo wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum.

Nitatoa mifano miwili ili kufafanua hitimisho langu hili.

Mfano wa kwanza, ni mfano wa mtu aliyefukuzwa kazi, akamshitaki mwajiri kwenye Mahakama ya Kazi, Makahaka ikaamuru alippwe Milioni 10 kama fidia. Ikiwa mwajiri atamlipa milioni 3 pekee, anazipokea na kuzitumia kama gharama za kuweka wakili ili ambane mwajiri kwa hoja kwamba malipo ya milioni tatu "pekee" hayatoshi, lakini baada ya kuchukua milioni tatu.

Na mfano wa pili ni wa kifalsafa zaidi. Tunapotaja fasili ya umbo linaloitwa pembetatu tunasema hivi: "Pembetatu ni umbo lenye kona tatu pekee na pande tatu pekee."

Katika fasili hii neno "pekee" ni muhimu sana, kwani hata mraba unazo pembe tatu na kona tatu pia. Lakini mraba hauna pembe tatu "pekee" wala pande tatu "pekee."

Kwa mujibu wa mifano hii miwili, sasa nahitimisha hoja yangu. Katika kura za mgombea urais, Tundu Lissu, Chadema hawadai kura Y pekee, kama ilivyotangazwa na NEC. Wanadai kura Y na kura Z, ambapo tayari wamekwishapatiwa kura Y, lakini bado kupatiwa kura Z, kama watathibitisha kwamba zipo.

Hivyo, Chadema wanaweza, na wanapaswa kupokea kura Y na kuendelea kudai kura Z, kwa kuweka bayana hoja isiyoruhusu hewa wala maji kupenya.

Kwa mantiki hii, Chadema hawapaswi kuona shida kuteua wabunge wa viti maalum ili waende Bungeni kuapa. Nashauri wafanye hivyo leo.

Hapa nimejaribu kufikiri kwa sauti kwa kuzingatia hoja zilizojengwa na Gene Sharp (2012) katika kitabu chake kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Kwa mujibu wa kitabu hiki, kukataa kuteua wabunge wa viti maalum, kama wanavyofanya Chadema kwa sasa, ni aina mojawapo ya udikteta; na majadiliano ya maana hufanyika kati ta "mdikteta" na "mdemokrasia."

Yaani, Chadema inabidi waonyeshe kwa mawazo, maneno na vitendo kwamba wao ni "wademokrasia" ili wapate uhalali wa kumkabili yule anayeitwa "mdikteta."

Nimeambatanisha kitabu hicho hapa chini, kwa ajili ya wale wenye utayari wa kujisomea.

Huu ni mtazamo wangu, na ninawajibika kikamilifu kusanifu hoja hii yenye kutetea mtazamo huu.

Mama Amon,
Sumbawanga Kusini.
Pili hoja yako ya mgogoro wa Mwajiri na mwajiriwa ni irrelevant kwenye hoja yako ya kura za CHADEMA kwa sababu mwajiriwa ana njia ya kutafuta haki yake wakati CHADEMA hawana tena hiyo Avenue
 
Hata hujaelewa nilichosema.
KUna mtu alijaribu kukuondoa kwenye mada.
Ukaanza kuongelea mleta mada badala ya mada ya bandiko hili.
Hivyo tu.
Usiende mbali.
Umemjibu mtu tofauti na mimi probably
 
Pamoja na maelezo yako marefu, kindendo cha kutojua kwamba wabunge wa viti maalumu wanatokana na jumla ya kura za wabunge wa chama husika na badala yake wewe ukaona wanatokana na jumla ya kura alizopata mgombea wa chama husika, hapo tu tayari hoja yako nzima ni "null and void"

Tafuta hoja nyingine uje nayo.
 
Mosi, hoja ya kudai Katiba, Tume Huru nk, kwa upande mmoja, na hoja ya kutuma wabunge wa viti maalum bungeni, kwa upande mwingine, ni hoja mbili tofauti.

Pili, kupeleka wabunge wa viti maalum sio kikwazo kwa hoja ya kwanza.

Na tatu, chama kinaendeshwa kwa vikao.

Wananchi walioko nje ya vikao wanapaswa kuonyesha utii kwa maamuzi halali.

Hata viongozi walio kwenye vikao pia.
Sioni hoja katiba mpya ikijadiliwa bungeni. Kwenda bungeni ni kuhalalisha uhuni, hilo halibadiliki.

Hatuko tayari kuheshimu maamuzi ya vikao ambayo yatakuwa yanabariki chaguzi za kihuni. Vikao vinapaswa kuheshimu Misimamo yetu wafuasi wao. Tulikaa kimya tukaishia kuletewa Lowasa kwa maamuzi ya vodafasta. Tunaangalia mustakabali wa chaguzi ambazo maamuzi yetu ya kuchagua yataheshimiwa, na sio chaguzi za kihuni zifanyike kisha tuendelee kushiriki kwenye mabunge ya hivyo. Kuliko waende bungeni, bora waende mahakamani kudai kura za wabunge na madiwani zihesabiwe upya, hapo tutawaunga mkono.
 
Najua mengi kati ya haya uliyoyaandika.

Lakini, nashauri kutofautisha maembe na machungwa.

Pia nashauri kujiepusha na mantiki ya samaki mmoja akioza wote wameoza.

Turudi kwenye hoja yetu:

Kura za Chadema zilizotangazwa na NEC ni kidogo kuliko uhalisia au ni nyingi zaidi ya uhalisia?

Kama ni kidogo kuliko uhalisia, ni kura halali au kura haramu?

Kama ni kura halali, kwa nini wabunge wa viti maalum wanaotokana na kura hizo wawe haramu?

Nashauri tupeleke wabunge, halafu tuendelee kupigania masuala mengine.

Hakuna athari.
Kwa hali ilivyo kura halali hazifahamiki ni zipi na majibu nimetoa pale juu.

CHADEMA hawahoji upungufu wa kura au wingi wa kura wanahoji uhalali wa kura zenyewe kutokana na zoezi la kupiga kura kufanyia katika mchakato batili.
 
Kwenda bungeni ni kuhalalisha uhuni, hilo halibadiliki. Hatuko tayari kuheshimu maamuzi ya vikao ambayo yatakuwa yanabariki chaguzi za kihuni. Vikao vinapaswa kuheshimu Misimamo yetu wafuasi wao. Tulikaa kimya tukaishia kuletewa Lowasa kwa maamuzi ya vodafasta. Tunaangalia mustakabali wa chaguzi ambazo maamuzi yetu ya kuchagua yataheshimiwa, na sio chaguzi za kihuni zifanyike kisha tuendelee kushiriki kwenye mabunge ya hivyo. Kuliko waende bungeni, bora waende mahakamani kudai kura za wabunge na madiwani zihesabiwe upya, hapo tutawaunga mkono.

Sorry, unaandika kama vile unadondosha maneno ambayo yanakosa muunganiko wa kimantiki.

Can you paraphrase your argument to make it more formal and palatable?

napendelea hoja zenye muundo haka huu:

Tindo ni mtu (major premise)
KIla mtu atakufa (minor premise)
Kwa hiyo, siku moja, Tindo atakufa (conclusion)

Katika muundo huu inakuwa rahisi kufuatilia anachosema mwenzako.
 
Hakuna atakayemfukuza, na ushauri huo tumeutoa kwa chama, yeye aendelee na wajibu wake lakini ajue fika hatuafiki mchakato huu wa kishenzi. Ni juu yake kusaka maisha ya familia yake, ila sisi tunaangalia mustakabali wa chama.
Hilo ndilo neno kwani uchaguzi umekwisha na waliochaguliwa wameapa wakiendelea kuwajibika kwa wapiga kura. Kinachohitajika ni kwa viongozi wa upinzani, nanyi wafuasi, kutathmini, kwa kina, makosa yaliyofanyika kiasi cha kufanya vibaya SANA kweye Uchaguzi uliomalizika.

Kadiri viongozi wa upinzani, hasa CHADEMA, nanyi wafuasi, mnavyoendelea kulalamikia matokeo na kuilamu NEC, ndivyo mnavyowapa morali viongozi wa CCM kuisimamia vizuri Serikali yake ili Ilani ya Uchaguzi itekelezwe ipasavyo. Na utekelezaji ukifanikiwa, ni wazi Uchaguzi Mkuu, 2025, upinzani usahau kupata hata kata moja.
 
Back
Top Bottom