Uchaguzi 2020 Tathmini yangu juu ya Uchaguzi Mkuu 2020: Hakuna sababu nzuri ya kukataa kuteua wabunge wa Viti Maalum CHADEMA

Uchaguzi 2020 Tathmini yangu juu ya Uchaguzi Mkuu 2020: Hakuna sababu nzuri ya kukataa kuteua wabunge wa Viti Maalum CHADEMA

View attachment 1633150
Tundu Lissu (Mgombea Urais wa Chadema) na Job Ndugai (Spika)

Kuna mdau kanitumia kitabu cha Gene Sharp (2012), kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Yaani, "Safari ya Kutoka Kwenye HImaya ya Kidikteta Kuelekea Kwenye HImaya ya Kidemokrasia: Mawazo Ambayo ni Msingi wa Hoja za Kuendeleza Mapambano ya Ukombozi." (Tafsiri yangu).

Mdau huyu amenitaka nikisome na kisha nijibu swali hili: Kama wabunge wa viti maalum wanatokana na kura za mgombea urais, na kama kura za mgombea urais wa Chadema zilizotangazwa na tume ni sehemu ya kura zote ambazo Chadema wanadai kwamba walipata, uamuzi wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum wa Chadema ili waende Bungeni kula kiapo na kuchapa kazi ya ubunge unachangia vipi katika kuimarisha demokrasia nchini Tanzania?

Nimekisoma kitabu na kukimaliza. Kina kurasa 100, na kimeandikwa kwa Kingereza chepesi. Ninaelewa mengi yaliyojiri katika siku zote za uchaguzi mkuu wa 2020. Pia najua malalamiko kadhaa ya vyama vya upinzani. Baada tafakari nimefikiria kama ifuatavyo:

Mosi, kama mgombea urais wa Chadema (Lissu) alipata kura X, na NEC ikatangaza kwamba Lissu kapata kura Y, ni wazi kwamba kura X ni kubwa kuliko kura Y, yaani X>Y.

Pili, Tofauti kati ya kura X na kura Y, tuseme kura Z, ndizo kura zinazobishaniwa. Chadema wanapinga kutotangazwa kwa kura Z. Yaani, Chadema wanapinga kutangazwa kwa kura Y pekee bila kujumlisha kura Z.

Tatu, kura Y zilizotangawa na NEC ni sehemu ya kura X zinazotamkwa na viongozi wa Chadema.

Nne, wabunge wa viti maalum wa Chadema wanatokana na kura Y, ambazo ni kura halali.

Kwa hiyo, idadi ya wabunge wa viti maalum kupitia Chadema iliyotangazwa na NEC ni idadi ya wabunge iliyotokana na kura halali.

Lakini, kama Chadema wanasema kuwa LIssu alipata kura ambazo ni ndogo kuliko zile zilizotangazwa na NEC, basi hitimisho langu linaporomoka hadi kuwa kifusi; na nitaungana nao katika msimamo wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum.

Nitatoa mifano miwili ili kufafanua hitimisho langu hili.

Mfano wa kwanza, ni mfano wa mtu aliyefukuzwa kazi, akamshitaki mwajiri kwenye Mahakama ya Kazi, Makahaka ikaamuru alippwe Milioni 10 kama fidia. Ikiwa mwajiri atamlipa milioni 3 pekee, anazipokea na kuzitumia kama gharama za kuweka wakili ili ambane mwajiri kwa hoja kwamba malipo ya milioni tatu "pekee" hayatoshi, lakini baada ya kuchukua milioni tatu.

Na mfano wa pili ni wa kifalsafa zaidi. Tunapotaja fasili ya umbo linaloitwa pembetatu tunasema hivi: "Pembetatu ni umbo lenye kona tatu pekee na pande tatu pekee."

Katika fasili hii neno "pekee" ni muhimu sana, kwani hata mraba unazo pembe tatu na kona tatu pia. Lakini mraba hauna pembe tatu "pekee" wala pande tatu "pekee."

Kwa mujibu wa mifano hii miwili, sasa nahitimisha hoja yangu. Katika kura za mgombea urais, Tundu Lissu, Chadema hawadai kura Y pekee, kama ilivyotangazwa na NEC. Wanadai kura Y na kura Z, ambapo tayari wamekwishapatiwa kura Y, lakini bado kupatiwa kura Z, kama watathibitisha kwamba zipo.

Hivyo, Chadema wanaweza, na wanapaswa kupokea kura Y na kuendelea kudai kura Z, kwa kuweka bayana hoja isiyoruhusu hewa wala maji kupenya.

Kwa mantiki hii, Chadema hawapaswi kuona shida kuteua wabunge wa viti maalum ili waende Bungeni kuapa. Nashauri wafanye hivyo leo.

Hapa nimejaribu kufikiri kwa sauti kwa kuzingatia hoja zilizojengwa na Gene Sharp (2012) katika kitabu chake kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Kwa mujibu wa kitabu hiki, kukataa kuteua wabunge wa viti maalum, kama wanavyofanya Chadema kwa sasa, ni aina mojawapo ya udikteta; na majadiliano ya maana hufanyika kati ta "mdikteta" na "mdemokrasia."

Yaani, Chadema inabidi waonyeshe kwa mawazo, maneno na vitendo kwamba wao ni "wademokrasia" ili wapate uhalali wa kumkabili yule anayeitwa "mdikteta."

Nimeambatanisha kitabu hicho hapa chini, kwa ajili ya wale wenye utayari wa kujisomea.

Huu ni mtazamo wangu, na ninawajibika kikamilifu kusanifu hoja hii yenye kutetea mtazamo huu.

Mama Amon,
Sumbawanga Kusini.
Mbona hoja tulishaifunga? Nyie mnawashwa na CHADEMA. Mbona tulishawashauri mchukue wanawake wa ofisi ya NEC, wa polisi na wa wakurugenzi wa wilaya.
 
Sikutarajia kama mama Aron unaweza kuhalalisha uharamia hata kama una nia njema.

Hujasoma hoja yangu.

Kura za Chadema zilizotangazwa, inadaiwa ni kidogo kuliko kura halisi.
Wabunge wa viti maalum wanatokana na kura hizo kidogo.
Kwa hiyo, kupeleka wabunge hakuna uhusiano na kura zinazodaiwa kuibiwa.
Kura zinazodaiwa kuibiwa zinahusiana na wagombea ubunge wa jukwaani.
Umenisoma?
 
Mbona hoja tulishaifunga? Nyie mnawashwa na CDM. Mbona tulishawashauri mchukue wanawake wa ofisi ya NEC, wa polisi na wa wakurugenzi wa wilaya.
Unadai "hoja tulishaifunga."
Ilifungwa kwa mujibu wa kikao gani?
Mbona kura za vikao vya Kamati Kuu ya Chadema haziungi mkono unachokisema?
Fanya utafiti kwanza.
No reserach no right to speak.
 
Ndugu Mama Amon, uelekeo wa upinzani uko 'crystal clear'. Hawakubali kupoozwa kwa nafasi zozote za uongozi na serikali hii kwani machoni pao ni serikali batili.

Strategy iliyopo ni kuwaachia kila kitu CCM kisha kuomba pressure kutoka nje. Mambo yatakapo anza kuwa magumu, wananchi watailaumu CCM na serikali yake pekee. Katika wakati huu wa udhaifu wa dola, upinzani utakua na nafasi nzuri zaidi ya kudai mabadiliko.
 
Umetoa mfano mzuri unaoimarisha hoja yangu.

Ni hivi:

Kwenye kituo ulichosimamia Tundu Antipas Lissu alipata kura 79 na Magufuli akapata kura 31.

Lakini Lissu alindikiwa kura 6 na Magufuli kura 379.

Kisha unauliza, "sasa hapo unakubali vipi?"

Majibu yangu:

Kama ni kweli, kura 6 alizoandikiwa Lissu ni sehemu ya kura zake halali 79 ulizozishuhudia.

Kwa hiyo, kwa mujibu wa maelezo yako, Lissu aliibiwa kura 73.

Hivyo basi, tunapaswa kukubali kwamba kura 6 ni kura halali, na kuendelea kudai kura 73 kwa kuweka vielelezo mezani.

Hizo kura 6 ambazo tunajua kwamba ni halali ni sehemu ya kura ambazo zimetangazwa na NEC na kuzaa wabunge wa viti maalum 19.

Kwa hiyo, viti maalum 19 vya Chadema ni halali.

Katika kituo chako ulichosimamia, ambacho sio halali, kama kikitibitika, ni kutotangazwa kwa kura 73.

Hizi kura 73 ziendelee kudaiwa bila kuharamisha kura 6 ambazo ni halali.

Wanasheria wote wa Chadema wanaujua ukweli huu.

Tafuta yeyote umwulize na atakwambia ninachokwambia.
Chadema hawaja argue kuhusu uhalali wa hizo kura chache bali hawaungi mkono mchakato mzima kutokana na kasoro nyingi zilizojitokeza, kwahiyo uelewa ni muhimu ktkt hili.
 
Kwa heshima, sikubaliani na kauli yako hii hapa.
Kwani mwajiriwa aliyelipwa milioni tatu hapo juu, akazipokea, na kisha akaendelea kudai ziada, alikuwa ameunga mkono ufedhuli wa mwajiri mkorofi?

Mfano wako ni disingenous. Katika Bunge lililopita kulikuwa na takriban wabunge 115 wa upinzani kati ya jumla ya wabunge 384 ( asilimia 30 ya wabunge walikuwa wa upinzani) lakini bado walikuwa wanaburuzwa tu. Wakikubali kuteua wabunge 19 wa viti maalum, jumla itakuwa 21 ambayo ni asilimia 5.8 ya wabunge wote. Kwa mfano ulioutoa ni kama huyo mwajiriwa akubali kupewa shilingi 580,000.00 wakati anastahili milioni 10, kiasi ambacho hakitoshi kumlipa mwanasheria wa kumtetea. Na mwajiriwa akipokea hiyo 580,000 ndio ajue hatapata zaidi maana mwajiri anajua kuwa ana njaa.Ni bora akatae na arudi Mahakamani ili mwajiri abanwe ili alipwe stahili yake yote. Ndio maana wapinzani wanagomea viti hivyo unavyotaka wapokee. Kwa idadi hiyo bora wajikalie nje tu wakati wanatafuta njia mbadala wa kudai stahili yao.

Amandla...
 
View attachment 1633150
Tundu Lissu (Mgombea Urais wa Chadema) na Job Ndugai (Spika)

Kuna mdau kanitumia kitabu cha Gene Sharp (2012), kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Yaani, "Safari ya Kutoka Kwenye HImaya ya Kidikteta Kuelekea Kwenye HImaya ya Kidemokrasia: Mawazo Ambayo ni Msingi wa Hoja za Kuendeleza Mapambano ya Ukombozi." (Tafsiri yangu).

Mdau huyu amenitaka nikisome na kisha nijibu swali hili: Kama wabunge wa viti maalum wanatokana na kura za mgombea urais, na kama kura za mgombea urais wa Chadema zilizotangazwa na tume ni sehemu ya kura zote ambazo Chadema wanadai kwamba walipata, uamuzi wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum wa Chadema ili waende Bungeni kula kiapo na kuchapa kazi ya ubunge unachangia vipi katika kuimarisha demokrasia nchini Tanzania?

Nimekisoma kitabu na kukimaliza. Kina kurasa 100, na kimeandikwa kwa Kingereza chepesi. Ninaelewa mengi yaliyojiri katika siku zote za uchaguzi mkuu wa 2020. Pia najua malalamiko kadhaa ya vyama vya upinzani. Baada tafakari nimefikiria kama ifuatavyo:

Mosi, kama mgombea urais wa Chadema (Lissu) alipata kura X, na NEC ikatangaza kwamba Lissu kapata kura Y, ni wazi kwamba kura X ni kubwa kuliko kura Y, yaani X>Y.

Pili, Tofauti kati ya kura X na kura Y, tuseme kura Z, ndizo kura zinazobishaniwa. Chadema wanapinga kutotangazwa kwa kura Z. Yaani, Chadema wanapinga kutangazwa kwa kura Y pekee bila kujumlisha kura Z.

Tatu, kura Y zilizotangawa na NEC ni sehemu ya kura X zinazotamkwa na viongozi wa Chadema.

Nne, wabunge wa viti maalum wa Chadema wanatokana na kura Y, ambazo ni kura halali.

Kwa hiyo, idadi ya wabunge wa viti maalum kupitia Chadema iliyotangazwa na NEC ni idadi ya wabunge iliyotokana na kura halali.

Lakini, kama Chadema wanasema kuwa LIssu alipata kura ambazo ni ndogo kuliko zile zilizotangazwa na NEC, basi hitimisho langu linaporomoka hadi kuwa kifusi; na nitaungana nao katika msimamo wa kukataa kuteua wabunge wa viti maalum.

Nitatoa mifano miwili ili kufafanua hitimisho langu hili.

Mfano wa kwanza, ni mfano wa mtu aliyefukuzwa kazi, akamshitaki mwajiri kwenye Mahakama ya Kazi, Makahaka ikaamuru alippwe Milioni 10 kama fidia. Ikiwa mwajiri atamlipa milioni 3 pekee, anazipokea na kuzitumia kama gharama za kuweka wakili ili ambane mwajiri kwa hoja kwamba malipo ya milioni tatu "pekee" hayatoshi, lakini baada ya kuchukua milioni tatu.

Na mfano wa pili ni wa kifalsafa zaidi. Tunapotaja fasili ya umbo linaloitwa pembetatu tunasema hivi: "Pembetatu ni umbo lenye kona tatu pekee na pande tatu pekee."

Katika fasili hii neno "pekee" ni muhimu sana, kwani hata mraba unazo pembe tatu na kona tatu pia. Lakini mraba hauna pembe tatu "pekee" wala pande tatu "pekee."

Kwa mujibu wa mifano hii miwili, sasa nahitimisha hoja yangu. Katika kura za mgombea urais, Tundu Lissu, Chadema hawadai kura Y pekee, kama ilivyotangazwa na NEC. Wanadai kura Y na kura Z, ambapo tayari wamekwishapatiwa kura Y, lakini bado kupatiwa kura Z, kama watathibitisha kwamba zipo.

Hivyo, Chadema wanaweza, na wanapaswa kupokea kura Y na kuendelea kudai kura Z, kwa kuweka bayana hoja isiyoruhusu hewa wala maji kupenya.

Kwa mantiki hii, Chadema hawapaswi kuona shida kuteua wabunge wa viti maalum ili waende Bungeni kuapa. Nashauri wafanye hivyo leo.

Hapa nimejaribu kufikiri kwa sauti kwa kuzingatia hoja zilizojengwa na Gene Sharp (2012) katika kitabu chake kiitwacho "From Dictatorship to Democracy: A Conceptual Framework for Liberation."

Kwa mujibu wa kitabu hiki, kukataa kuteua wabunge wa viti maalum, kama wanavyofanya Chadema kwa sasa, ni aina mojawapo ya udikteta; na majadiliano ya maana hufanyika kati ta "mdikteta" na "mdemokrasia."

Yaani, Chadema inabidi waonyeshe kwa mawazo, maneno na vitendo kwamba wao ni "wademokrasia" ili wapate uhalali wa kumkabili yule anayeitwa "mdikteta."

Nimeambatanisha kitabu hicho hapa chini, kwa ajili ya wale wenye utayari wa kujisomea.

Huu ni mtazamo wangu, na ninawajibika kikamilifu kusanifu hoja hii yenye kutetea mtazamo huu.

Mama Amon,
Sumbawanga Kusini.
Ni mwandishi mzuri na umeshawishi vizuri, asante. Lakini bado sijaelewa kwa nini umeegemea upande mmoja wa kura za Urais na kusahau kura za Ubunge?

Kilichowapa CHADEMA viti 19 wasivyostahili (wamepunjwa) si kura za Urais kama unavyojaribu kudadavua, kilichopelekea CDM kupewa hizo nafasi 19 ni kura za Wagombea Ubunge wote wa CDM isipokuwa katika majimbo ambayo hakukuwa na uchaguzi wa nafasi hiyo baada ya kuenguliwa wagombea wao kwa hila.

Sasa unaiba kura za chama A kwenye majimbo na kuwaongezea chama B, unawatangaza washindi haramu wa chama B, kisha unatumia kura haramu ulizowapunja chama A kuwapa Wabunge wa viti maalum? Hebu kasome wanavyopatikana Wabunge wa viti maalum halafu rudi tena na hoja yako.
 
Ndugu Mama Amon, uelekeo wa upinzani uko 'crystal clear'. Hawakubali kupoozwa kwa nafasi zozote za uongozi na serikali hii kwani machoni pao ni serikali batili. Strategy iliyopo ni kuwaachia kila kitu CCM kisha kuomba pressure kutoka nje. Mambo yatakapo anza kuwa magumu, wananchi watailaumu CCM na serikali yake pekee. Katika wakati huu wa udhaifu wa dola, upinzani utakua na nafasi nzuri zaidi ya kudai mabadiliko.

Tuanzie hapo kwenye msitari. Pressure kutoka nje ni mkakati dhaifu sana kwa mujibu wa Gene Sharp (kitabu nimeambatanisha). Pili, Bunge sio serikali. Serikali sio mahakama. Hapa tuongelee Bunge. Kupeleka wabunge wa iti maalum Bungeni ni sehemu ya mkakati wa ndani ya nchi. Tuanzie ndani, sio nje. Na tatu, soma kitabu hiki kwa umakini halafu tupanue mjadala (attached)...
 

Attachments

Ni mwandishi mzuri na umeshawishi vizuri, asante. Lakini bado sijaelewa kwa nini umeegemea upande mmoja wa kura za Urais na kusahau kura za Ubunge?
Kilichowapa CHADEMA viti 19 wasivyostahili (wamepunjwa) si kura za Urais kama unavyojaribu kudadavua, kilichopelekea CDM kupewa hizo nafasi 19 ni kura za Wagombea Ubunge wote wa CDM isipokuwa katika majimbo ambayo hakukuwa na uchaguzi wa nafasi hiyo baada ya kuenguliwa wagombea wao kwa hila. Sasa unaiba kura za chama A kwenye majimbo na kuwaongezea chama B, unawatangaza washindi haramu wa chama B, kisha unatumia kura haramu ulizowapunja chama A kuwapa Wabunge wa viti maalum? Hebu kasome wanavyopatikana Wabunge wa viti maalum halafu rudi tena na hoja yako.
Fomula ya kukokotoa idadi ya viti maalum hata kama ikihusisha kura za ubunge haina madhara kwa hoja yangu. Pointi yangu ni kwamba, hizi kura kidogo zilizobaki baada ya kitendo kinachoitwa wizi wa kura ndizo zimezaa viti maalum. Ni kura halali na viti maalum ni viti halali. Kura zinazoitwa haramu ni zile zinazodaiwa kuibwa kutoka upande A na kwenda upande B. Hizo ziendelee kutafutwa. Sina shida ni hilo la pili. Umenisoma?
 
Moja ya kazi ngumu kwa sasa nchi hii ni kuwashauri CHADEMA kuhusu hili. Wakubwa wamekosa ugali huku kukiwa na fursa ya wadogo kupata ugali.
 
Hujasoma hoja yangu.

Kura za Chadema zilizotangazwa, inadaiwa ni kidogo kuliko kura halisi.
Wabunge wa viti maalum wanatokana na kura hizo kidogo.
Kwa hiyo, kupeleka wabunge hakuna uhusiano na kura zinazodaiwa kuibiwa.
Kura zinazodaiwa kuibiwa zinahusiana na wagombea ubunge wa jukwaani.
Umenisoma?
CHADEMA hawatambui MCHAKATO MZIMA hivyo hata hiyo halali unayosema wewe kwao ni batili kwa kuwa sio walichotarajia. Hivyo viti maalum 19 wawape TISS tu hakuna namna.
 
Ni bora akatae na arudi Mahakamani ili mwajiri abanwe ili alipwe stahili yake yote. Ndio maana wapinzani wanagomea viti hivyo unavyotaka wapokee. Kwa idadi hiyo bora wajikalie nje tu wakati wanatafuta njia mbadala wa kudai stahili yao.

Nilichofanya ni reasoning by analogy. Utaratibu huu unaanzia kwenye ufanano, na sio kwenye utofauti. Pointi yangu ni kwamba, hivyo viti 19 ni haki ya chadema ambayo inaweza, na inapaswa, kuchukuliwa ili kiwe kianzio cha kudai haki baki. Wabunge hawa wataongeza nguvu ya uchumi ya chama, lakini sio kwa sababu wamependelewa na serikali. Bali kwa kuwa wanayo haki ya kuwa wabunge kutokana na kura halali za Chadema. Wale wagombea ubunge wa jukwaani wanaodai kwamba waliporwa waendelee na hoja. Tena waombe msaada wa kifedha kutoka kwa wabunge hawa wa viti maalum ili kuimarisha mapambano. Umenisoma?
 
Hujasoma hoja yangu.

Kura za Chadema zilizotangazwa, inadaiwa ni kidogo kuliko kura halisi.
Wabunge wa viti maalum wanatokana na kura hizo kidogo.
Kwa hiyo, kupeleka wabunge hakuna uhusiano na kura zinazodaiwa kuibiwa.
Kura zinazodaiwa kuibiwa zinahusiana na wagombea ubunge wa jukwaani.
Umenisoma?

Mama Aron nimekupata sana sikuwa na shaka na ulichomaanisha toka mwanzo. Mchakato mzima kwetu ni haramu, kwa hiyo hata hizo kura chache kwetu ni sehemu ya hilo zoezi haramu. Kitendo chochote cha kwenda kushiriki ni kuhalalisha huo uharamia. Kitendo cha kushiriki ni kukubaliana na mchakato mzima, hakuna nafasi yoyote ya kufafanua hilo kwa wananchi huku nje, ndio itakuwa ndani ya hilo bunge kibogoyo? Ukiniambia unashauri wakale hela hapo sawa, sio kwa hizo sababu zako nzuri.
 
Tuanzie hapo kwenye msitari. Pressure kutoka nje ni mkakati dhaifu sana kwa mujibu wa Gene Sharp (kitabu nimeambatanisha). Pili, Bunge sio serikali. Serikali sio mahakama. Hapa tuongelee Bunge. Kupeleka wabunge wa iti maalum Bungeni ni sehemu ya mkakati wa ndani ya nchi. Tuanzie ndani, sio nje. Na tatu, soma kitabu hiki kwa umakini halafu tupanue mjadala (attached)...
Kwa serikali hii bunge + mahakama + serikali = SERIKALI.

Kwani walitumbia wenyewe A + B + C = C pia

C + A + B = A mwisho A + C + B = B

Hence A = B = C.
 
Nianzie kwenye signature yako...

"We define things as we are, and not as they are.." by Anais.

Huyu Ananias anakupotosha, achana naye.

Katika mtazamo wa realism, tunaongozwa na correspondence theory of truth.

Truth is out there to be discovered.

Sasa turudi kwenye hoja.

Wewe na mimi tunajua fika kwamba pale NEC HQ kuna dawati la TISS.

Ulishawahi kufuatilia dawati hili kazi zake?

Huenda hapana, na sio lazima.

Lakini, kubwa ni kwamba, kuna lawama zinaelekezwa kwa NEC kimakosa.

Natamani kusikia na sijasikia:

Chadema wanasema walipata kura ngapi? (X)
NEC wametangaza kura ngapi? (Y)
Nani ameshikilia tofauti ya kura kati ya X na Y, yaani Z=X-Y?
Aliwezaje kuzishikilia?
Tunaweza kumnyang'anya kura hizo ili ziende kwa Chadema?

Maswali ni mengi...

Tuzidi kutafakari pamoja...
Mama Amon, theories huwa zinakinzana dada, sijaamua ktk hili suala nitumie theory gani; hichi wanachofanya Chadema na ACT kinaweza kuwa msaada mkubwa kwa nchi siku zijazo, kuchezea uchaguzi na kura za watu ni hatari kwa amani na mustakabali wa nchi.

Kwa kuzingatia signature yangu wewe uko sahihi na Chadema wako sahihi, nami pia niko sahihi maana "we define things as we are, not as they are".

Vv
 
Unadai "hoja tulishaifunga."
Ilifungwa kwa mujibu wa kikao gani?
Mbona kura za vikao vya Kamati Kuu ya Chadema haziungi mkono unachokisema?
Fanya utafiti kwanza.
No reserach no right to speak.

Wao cdm kama chama waamue watakacho, lakini sisi wafuasi wao tuko wazi kwamba hatukubali washiriki kuhalalisha haramu. Wanaweza kupambana kusaka faida za muda mfupi, lakini wasitegemee tena sisi kujitokeza kupiga kura. Wabaki huku nje tudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya. Haya ni madai halali, na sioni yakipatikana kwa hivyo viti 19 kwenda bungeni. Sio lazima msimamo huu uwe bora, lakini ndio msimamo sahihi kwa mazingira haya.
 
Mchakato mzima kwetu ni haramu, kwa hiyo hata hizo kura chache kwetu ni sehemu ya hilo zoezi haramu.
Hapa ndipo nimepata kujua kwa nini tunapishana. Kuna mawili:

1. Mtazamo wangu ni kwamba, hizo kura chache zilizotangazwa na NEC ni halali, wakati zile kura nyingi zinazodaiwa kuhamishiwa upande mwingine ni haramu.

2. Lakini, wewe unasema kuwa, kwa vile mchakato mzima ni haramu, na kwa kuwa hizo kura chache ni sehemu ya mchakato haramu, basi hata hizo kura kidogo ni haramu.

Lakini, huoni kuwa mantiki ya samaki mmoja akioza wote wameoza haikubaliki kimantiki na kisheria?



 
Back
Top Bottom