Tatizo kubwa la Prof. Kabudi ni uongo na ulaghai na hana sifa ya kujiongeza ambayo ni sifa mama ya waziri wa diplomasia akiwa na Rais aina ya Magufuli

Tatizo kubwa la Prof. Kabudi ni uongo na ulaghai na hana sifa ya kujiongeza ambayo ni sifa mama ya waziri wa diplomasia akiwa na Rais aina ya Magufuli

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Waziri wa mambo ya nchi za nje kuwa muongo na mlaghai kama alivyo Prof. Kabudi ni hatari kwa afya. Waziri ambaye hawazi mbali kuhusu majukumu yake inafikirisha sana.

Nakumbuka aliyoongea kwenye sakata la madini siyo tunayoona sasa.Aidha alitoa uongo wa awamu tatu. Wa majadiliano ya tume, wa tulichotegemea kupata na mwingine wa yanayoendelea sasa. Ilikuwa ni maigizo matupu. Haya leo hayanihusu!

Juzi wakati wa msiba wa mzee Mkapa, tulisema wazi kuwa upo mgogoro wa kidiplomasia ambao ulipelekea ndege ya Kenya kugeuza angani na kuwarudisha wajumbe wa kutoka Kenya waliokuja kuhudhuria mazishi yale. Mbiombio Kabudi akaja na taarifa eti ndege hiyo ilikumbwa na hitilafu, tena alizungumza palepale msibani. Mbiombio akaagiza ubalozi wa Tanzania nchini Kenya kutoa taarifa kama yake. Ila Kenya hawakutoa taarifa yoyote kuhusu tukio lile. Tukasema huku kuwa lipo tatizo ila kama kawaida ya wafuasi wasioelewa wakaendelea kushupaza shingo!

Siku mbili baadaye ukweli umedhihirika! Ukweli umewekwa hadharani kuwa upo mgogoro mkali wa kidiplomasia kati ya Kenya na Tanzania.

Kiukweli siyo uungwana hata kidogo kwa kilichofanyika juzi! Hizo ni siasa za kitoto na sijui nani anazianzisha, kwa malengo gani?

Kwanza mimi nashangaa sana, lini ndege ya Tanzania imewahi kutangaza hata kivutio kimoja tu cha utalii kilichopo Kenya? Mbona ndege za Kenya zimeandika hadi hifadhi ya Ngorongoro? Tumewahi hata kuwapa wakenya asante ya mdomo hadharani kwa kututangazia vivutio vyetu vya utalii huko duniani?

Enzi ya utawala wa JK na Mkapa Kenya na Tanzania walikuwa ndugu. Nakumbuka enzi ya Mkapa kila shughuli ya kitaifa marais wote watatu wa nchi za EAC lazima wawepo. Leo kuna nini? Lazima tukiri kuwa lipo tatizo la kimfumo. Rais Magufuli ana hulka ambayo waziri wake wa mambo ya nje anahitaji kujiongeza sana na kuzuia yale maboko ambayo yakitoka kwake yanaleta madhara.

Mbaya zaidi zipo taarifa kuwa mgogoro kati ya Kenya na Tanzania umetanuka hadi kwa mataifa ya Uganda na Rwanda. Pia na wao wameshaacha kushirikiana na Tanzania kwenye mambo mengi.

Ni lazima tuelewe kuwa Rais wa Tanzania ana tatizo kubwa sana la ubaguzi ambalo alianza kuwaita watu weupe "Mabeberu ( Sifa mbaya sana kwa mkuu wa nchi) . Hivyo anahitaji kuwa na waziri anayejua sana kujiongeza na kumshauri ila siyo huyu Kabudi ambaye anacheza kila ngoma ya Magufuli na kutuletea uongo na ulaghai.

Kama nchi ni lazima tukiri kuwa tunatumia njia ya aina yake kuishi na Corona ambayo ni vigumu sana kuaminika usoni pa mataifa mengi. Lazima tuje na mikakati ambayo tutawaeleza wenzetu watuelewe na siyo eti tunapiga Nyungu au miujiza. Ni lazima tujue tupo ndani ya dunia ya aina gani.
 
Ni wajinga pekee ndio watakaoshangilia na kufurahia haya yanayoendelea. Nazani viongozi wa nchi zetu zote mbili waache unafiki kwani mwisho wa siku wanaoathirika na upuuzi huu ni wananchi wa kawaida ambao hawawezi tena kufanya biashara baina ya nchi hizi mbili. Mgogoro huu hauna afya yoyote zaidi ya hasara.
 
Hii ni hatari sana. Bwana Yile hatki kuwa kwenye Jumuiya yeuote ile kwani hapendi mawazo tofauti na yake. Ni suala la muda tu tutasikia Tanz imejiondoa kwenye Jumuiya Afrika Mashariki kama ilivyofanya kwenye Mahakama ya Afrika.
 
Ni wajinga pekee ndio watakaoshangilia na kufurahia haya yanayoendelea. Nazani viongozi wa nchi zetu zote mbili waache unafiki kwani mwisho wa siku wanaoathirika na upuuzi huu ni wananchi wa kawaida ambao hawawezi tena kufanya biashara baina ya nchi hizi mbili. Mgogoro huu hauna afya yoyote zaidi ya hasara.
Kwanini kwa muda mrefu tumekuwa tukishirikiana iweje iwe leo kwenye awamu hii ya tano??

Tumekuwa tukipigia kelele ubaguzi wa wazi wazi wa Bw Yule anaowafanyia Watz wenye mawazo mbadala. Sasa ubaguzi wake umeshavuka mipaka. Ni hatari kweli kweli.
 
Kiukweli siyo uungwana hata kidogo kwa kilichofanyika juzi! Hizo ni siasa za kitoto na sijui nani anazianzisha, kwa malengo gani?
Unauliza aliyeanzisha mgogoro?

Kama ulikuwa hujui, labda nikufahamishe, aliyeleta migogoro ya nchi na nchi, chanzo kabisa ni Corona, baada ya hapo, ni wivu wa maendeleo na diplomasia ya Uchumi hasa swala la utalii katika nchi zetu hizi

Licha ya hivyo, Bado Wenzetu hawaepuki Lawama zote za mgogoro huu, walianza na mipakani, nawaziri wakakaa, wakakubaliana, lkn kabla hata ya wiki kuisha, Wao wakazuwia tena, hapo Nani mgomvi

Kabudi Pr, Chapa kazi, Wakati mwingine migogoro hii suluhu yake ni kudindishiana tu basi
 
Wajinga wakiwa wengi , werevu ndio huwa wajinga. ( Ujinga: kutofahamu jambo). Mkuu tujitahidi kufahamu mambo na kuyachuja kwa kupitia chujio la mawazo ya kupata habari na majawabu sahihi ( Hypothesis analysis pamoja Synthesis analysis).

Bila kufanya hicho tutakumbatia ujinga na tukadhani tuko sahihi katika uchambuzi wa maoni yetu.
 
Unauliza aliyeanzisha mgogoro?

Kama ulikuwa hujui, labda nikufahamishe, aliyeleta migogoro ya nchi na nchi, chanzo kabisa ni Corona, baada ya hapo, ni wivu wa maendeleo na diplomasia ya Uchumi hasa swala la utalii katika nchi zetu hizi

Licha ya hivyo, Bado Wenzetu hawaepuki Lawama zote za mgogoro huu, walianza na mipakani, nawaziri wakakaa, wakakubaliana, lkn kabla hata ya wiki kuisha, Wao wakazuwia tena, hapo Nani mgomvi

Kabudi Pr, Chapa kazi, Wakati mwingine migogoro hii suluhu yake ni kudindishiana tu basi
Kabla ya Corona waliwahi kuwa na mgogoro hadi wakausuluhishia Chato. Uwe na kumbukumbu sahihi!
 
Tatizo hapa:
Mkuru mwenyewe,,,populism"'
Kabudi anafanya kumfurahisha mkuru sio taifa.
Kabudi anamuogopa mkuru analinda maslahi yake mwenyewe.
 
Unauliza aliyeanzisha mgogoro?

Kama ulikuwa hujui, labda nikufahamishe, aliyeleta migogoro ya nchi na nchi, chanzo kabisa ni Corona, baada ya hapo, ni wivu wa maendeleo na diplomasia ya Uchumi hasa swala la utalii katika nchi zetu hizi

Licha ya hivyo, Bado Wenzetu hawaepuki Lawama zote za mgogoro huu, walianza na mipakani, nawaziri wakakaa, wakakubaliana, lkn kabla hata ya wiki kuisha, Wao wakazuwia tena, hapo Nani mgomvi

Kabudi Pr, Chapa kazi, Wakati mwingine migogoro hii suluhu yake ni kudindishiana tu basi
Nikurejeshe nyuma kidogo Mkuu: unakumbuka Serikali ya Tanz iliwahi kutaifisha mifugo toka Kenya?? Unakumbuka Tanz iliwahi kuwaunguza na kuwateketeza vifaranga wapatao elfu tano toka Kenya mpakani Namanga?? Unakumbuka Tanz iliwahi pia kuyapiga pini malori ya Kenya yaliyokuwa yamebeba mahindi Wilayani Rombo??
 
Nimeona WAJINGA-WAJINGA wengi wamepongeza TANZANIA kuzuia ndege za Kenya bila kujua undani wa mgogoro huu....
Ila mwisho wa siku kabudi atajikuta anatembea Kwenye bonde la umauti
Hichi hichi ulichokiandika, ndio ishara ya majibu juu ya wajinga Fulani huko kwenu kwamba eti watakinukisha Kura zao zikiibiwa!

Unajikomba nini Kwa jirani yako asiyekupenda? Maloli mipakani yalizuwiwa na sasa ndege, Bado unasema eeeh wallah!!
 
Watanzania tuache ujinga wa kutetea hata vitu vya kijinga Kisa Kenya ni nchi jirani.

Hebu tupeni sababu za msingi za Kenya kuzuia Ndege za Tanzania kutua Kenya halafu iruhusu Ndege zake kutua Tanzania.?

Kama ishu ni maambukizi ya Korona ilibidi wazuie Ndege zote kuingia na kutoka pande zote mbili.

Je hizo za kwao zinavyokuja na kutoka Tanzania zilikuwa hazichukui wenye korona na kupeleka kwao..

Jirani gani anazuia watoto wako kwenda kwake kisa Kuna magonjwa Ila anaruhusu wake kuja kwako.

Nafikiri Tanzania imewasaidia tu wakenya kuwa haina haja ya kuja kubeba korona huku uzidi kuhangaika nayo, baki salama na familia yako...

Kenya ameruhusu Uganda, Rwanda China zenye maambukizi makubwa lakini imeizuia Tanzania.

USA, Russia na Mataifa kadhaa makubwa raia wanaingia na kutoka Tz bila shida lakini Kenya ndio anajiona Standard sana.

Najua haya maamuzi yana athari kubwa Sana kwa nchi zote mbili hasa kwa wafanyabiashara lakini hakuna namna.

Kama ni kulinda ushirikiano tuulinde wote sio upande mmoja tu ndio uwajibike.

Uzuri Tanzania inajibu mashambulizi haianzishi mashambulizi, hivyo kiwewe kitabaki kwa anaejibiwa.

Binafsi nipo pamoja na serikali kwenye kutetea maslahi na hadhi ya nchi popote pale.

Kenya sio Ndugu yetu ni mshirika Mwenzetu kibiashara.
 
Waziri wa mambo ya nchi za nje kuwa muongo na mlaghai kama alivyo Prof. Kabudi ni hatari kwa afya. Waziri ambaye hawazi mbali kuhusu majukumu yake inafikirisha sana.

Nakumbuka aliyoongea kwenye sakata la madini siyo tunayoona sasa.Aidha alitoa uongo wa awamu tatu. Wa majadiliano ya tume, wa tulichotegemea kupata na mwingine wa yanayoendelea sasa. Ilikuwa ni maigizo matupu. Haya leo hayanihusu!

Juzi wakati wa msiba wa mzee Mkapa, tulisema wazi kuwa upo mgogoro wa kidiplomasia ambao ulipelekea ndege ya Kenya kugeuza angani na kuwarudisha wajumbe wa kutoka Kenya waliokuja kuhudhuria mazishi yale. Mbiombio Kabudi akaja na taarifa eti ndege hiyo ilikumbwa na hitilafu, tena alizungumza palepale msibani. Mbiombio akaagiza ubalozi wa Tanzania nchini Kenya kutoa taarifa kama yake. Ila Kenya hawakutoa taarifa yoyote kuhusu tukio lile. Tukasema huku kuwa lipo tatizo ila kama kawaida ya wafuasi wasioelewa wakaendelea kushupaza shingo!

Siku mbili baadaye ukweli umedhihirika! Ukweli umewekwa hadharani kuwa upo mgogoro mkali wa kidiplomasia kati ya Kenya na Tanzania.

Kiukweli siyo uungwana hata kidogo kwa kilichofanyika juzi! Hizo ni siasa za kitoto na sijui nani anazianzisha, kwa malengo gani?

Kwanza mimi nashangaa sana, lini ndege ya Tanzania imewahi kutangaza hata kivutio kimoja tu cha utalii kilichopo Kenya? Mbona ndege za Kenya zimeandika hadi hifadhi ya Ngorongoro? Tumewahi hata kuwapa wakenya asante ya mdomo hadharani kwa kututangazia vivutio vyetu vya utalii huko duniani?

Enzi ya utawala wa JK na Mkapa Kenya na Tanzania walikuwa ndugu. Nakumbuka enzi ya Mkapa kila shughuli ya kitaifa marais wote watatu wa nchi za EAC lazima wawepo. Leo kuna nini? Lazima tukiri kuwa lipo tatizo la kimfumo. Rais Magufuli ana hulka ambayo waziri wake wa mambo ya nje anahitaji kujiongeza sana na kuzuia yale maboko ambayo yakitoka kwake yanaleta madhara.

Mbaya zaidi zipo taarifa kuwa mgogoro kati ya Kenya na Tanzania umetanuka hadi kwa mataifa ya Uganda na Rwanda. Pia na wao wameshaacha kushirikiana na Tanzania kwenye mambo mengi.

Ni lazima tuelewe kuwa Rais wa Tanzania ana tatizo kubwa sana la ubaguzi ambalo alianza kuwaita watu weupe "Mabeberu ( Sifa mbaya sana kwa mkuu wa nchi) . Hivyo anahitaji kuwa na waziri anayejua sana kujiongeza na kumshauri ila siyo huyu Kabudi ambaye anacheza kila ngoma ya Magufuli na kutuletea uongo na ulaghai.

Kama nchi ni lazima tukiri kuwa tunatumia njia ya aina yake kuishi na Corona ambayo ni vigumu sana kuaminika usoni pa mataifa mengi. Lazima tuje na mikakati ambayo tutawaeleza wenzetu watuelewe na siyo eti tunapiga Nyungu au miujiza. Ni lazima tujue tupo ndani ya dunia ya aina gani.
Umeongea mambo ya msingi sana. Tatizo watanzania wengi uelewa wao ni mdogo! Hakuna risky assessments before making decisions so wengi watakuponda ila wachache tumekuelewa sana.
 
Si uhamie kenya kama huku kuna wajinga wengi walioanza kuzuia ndega ni wakina nani halafu unakuja huku unalialia
 
Mfupa uliomshinda Mwanadiplomasia nguli hayati Mzee Mahiga, Prof Kabudi ataweza kweli kumshauri boss kubwa?.

Prof kilichombakisha ni kuganga njaa na kulinda heshima feki ya kuitwa Waziri!.

Tatizo la Raia namba moja wetu ni kujiamini kupita kiasi ambapo kunapelekea yeye kuona kila kitu anakijua na anakiweza!.

Na mpaka sasa hivi hana wasaidizi wa kuweza kuwa na uthubutu wa kumshauri na kama ushauri unatolewa basi unatolewa kwa hofu kubwa!.

Baraza la Mawaziri linaishia kupokea maelekezo tu kutoka kwa boss, na kibaya zaidi na Bunge ambalo lingesaidia kumu shape nalo ndio hilo!.

Hapa aliyekuwa amebaki wa kuweza kumumdu huyu mzee ni mtoto pendwa maana mzee hakohowi, ila nae ndio huyo amekuwa akimshauri mambo ya kuvuruga amani na mshikamano wa Taifa.

Kwa huu uongozi wa one man show sijui nini hatima ya huko tunakoelekea kama Taifa!.
 
Uyo kabundi inaonekana alikuwa anafundisha ujinga mtupu pale UDSM

Yaani jamaa muongo muongo tu na macho yake yale kama kanywa viroba
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hahahah nimekumbuka Mdee alimchana bungeni live, kuwa anajuta kufundishwa na Kabudi, ili hali huyo mfundishaji hana uelewa wowote juu ya anachokifundisha.
 
Back
Top Bottom