Tatizo la ajira Tanzania: Nafasi za Ajira ya Ualimu 13,000, waliotuma maombi kuziomba wafikia 80,000+ hadi leo!

Tatizo la ajira Tanzania: Nafasi za Ajira ya Ualimu 13,000, waliotuma maombi kuziomba wafikia 80,000+ hadi leo!

Wanakumbuka shuka wakati kumekucha wanazuoni kila mwaka wanamaliza vyuo ila ajira hakuna wakati yeye mwenyewe alianzia kwenye ualimu mpaka leo akawa raisi ila mwanadamu ni watu wa kusaha wakishapata na kusahau alikotokea
Lissu kawakurupusha kutoka usingizini! Halafu nikasikia mjinga mmoja anauliza ana dhambi gani?
 
Hao walimu hawataajiriwa wata ahirisha hili zoezi, pesa yote iko kwenye kampeni za Magufuli na wenzake.
 
Anayetakiwa kuajiriwa ni yule aliyefaulu kuanzia daraja la kwanza mpaka la tatu, walimu wengi ni watu waliofeli mitihani, tatizo wanazoa zoa tu. Na pia serikali haiwezi kuajiri kila anayehitimu, mambo mengne ni kudanganyana tuu. Vijana wanatakiwa wawe tuned kupambana na mtaa.
Mawazo ya KIJAMAA kwa mjima na upuuzi!! Nani amekwambia vyuo vinatoa vyeti kwa wahitimu waliofeli??. Roho mbaya ndio inawasumbua, F.you
 
Sekta binafsi inakufa kwa kasi kutokana na utegemezi wa mfumo wa kiuchumi ambao hauendani na sera za taifa.

Nchi yetu kimsingi imejijenga kwa mifumo ya kijamaa but tunataka kuoperate kibepari katika sekta za uchumi. Uchumi wa kijamaa mifumo yake ya sheria inategemea sana maamuzi ya serikali katika kuamua matumizi ya rasilimali vile itaona inapendeza.

Mfano, inawezakana kabisa sekta ya mawasiliano ikawa inafanya vizuri na inaajiri watu vema ila viongozi kwa utashi wao wakaona waipige kodi nyingi hadi inakufa halafu akili zao zikawaelekeza kuwa wawekeze kwenye ujenzi wa barabara kwa kodi zile wamekamua. Vijana wakakosa ajira baada sekta ya mawasiliano kufa halafu wao katika vyombo vya habari wakajisifu na kujinadi kuwa serikali inajenga barabara kwa wingi na hayo ni maendeleo kwa wananchi.

Kimsingi magufuri anasimamia sheria na mfumo uliopo katika taifa letu ambao bungeni hawakuwahi kupoteza muda kuuchambua na kuufanyia marekebisho kuendana na uhalisia.

Taifa likiwa na watu/raia wachache mfumo wa ubepari huwa haufai na unakuwa hauna effects. Katika mazingira hayo ya watu wachache ni rahisi sana kwa mfumo wa ujamaa kufanikiwa sababu serikali inaweza ikauza madini, mafuta, au kutumia pesa za utalii kujenga shule, hospitali, mabarabara hata kuwawekea watu pesa kwenye account kama loyalty ya kuwa raia wa nchi husika.

Ila idadi ya watu inaoongezeka tu, rasilimali pamoja na mapato ya serikali ni chache sana kuweza kuwahudumia hao watu wote na kuwapa mahitaji yao ya msingi. Hivyo inabidi natural process ya balance ifanyike kama kuacha soko liwe huria ili watu wajitengenezee ajira na kuajiri watu, serikali inatabakia kuwa msimamizi wa sheria na usalama wa raia,kucontrol supply ya pesa kwenye mzunguko na kuzuia uhujumu uchumi.

Shida ni moja, wengi wa viongozi wetu hawana elimu nzuri ya sociology, uchumi na history. Hizi principles huwa zinawapa uelewa wa namna jamii ina evolve na kubadilika na kuweza kuprededict the next move.

Kwa bahati mbaya, mh. Dkt J.J.P.M yeye ni mtaalamu wa maswala ya kisayansi na principles zake alizosomea ni issue za vipimo ndio maana unamuona katika utendaji wake anakwenda sana na quantity na qualities. Anachagua watu kwenye ranks zake kwa misingi ya ufaulu darasani na miaka ya kazi na kadhalika. Kwa hali ya kiuchumi tuliyonayo sasa hatuhitaji watu kwa misingi hiyo, tunahitaji uwezo na ubunifu.

Sisi hatuhitaji kuwa na kiongozi mwenye mrundikano wa mavyeti ya GPA za 4.5 na aliyesoma Harvard. Tunataka kiongozi ambaye anajua tuna rasilimali watu wa aina gani, na anaye jua kuhesabu tuna list gani ya rasilimali tunazoweza tumia kwa wakati huu kuleta maendeleo na hapo akaweza kuja na sera nzuri za kutuambia watanzania.

But hizi mbwembwe za kupiga pushapu hazitatutoa hapa tulipo. Na ile hali nguvu kazi ya taifa (vijana) wanazidi kuteketea na kupotea..........

Tukitaka kutoka hapa tulipo, inabidi tuapply mixed economy formation ya uchumi, yaani tukubali kuwa serikali na taasisi binafsi zinatakiwa kufanya kazi kwapamoja. Tuweke sheria kali sana kwa viongozi na wafanyabiashara watakaokuwa wakihujumu serikali kwa faida binafsi, familia na jamaa zao.

Tupunguze muda wa kukaa mashuleni sio vijana wanasoma miaka 21 at least mtu akae shule miaka 12 kutoka vidudu hadi chuo kikuu except for baadhi ya taaluma kama udaktari.

Sera za kifedha za benki kuu zibadilishwe na tubadilishe pia sera na masharti ya kibenki ili kuweka clear and direct flow ya pesa kutoka serikalini hadi kwa raia kurudi serikalini tena.


Shkran mkuu! Hii elimu natamani viongozi wote waipate.
Jukwaa linahitaji watu kama wewe.
Kwa hoja zako inaonesha ni jinsi gani tunakwama na wapi tunakwama.

Aproach anayoitumia Rais inafaa sana kwa jamii ya kijamaa sio kwa kipindi hiki cha mfumo wa ubepari.
Sekta binafsi ndio solution pekee ya kuondoa tatizo la jobless kwenye taifa hili, Kuanzia elimu, hospitali, viwanda, kilimo na teknolojia.

Kongore kiongozi
 
Mnaongelea daraja la kwanza kwa level ipi?
O-level? Advance? Au Chuo?

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
sijajua lipi alikuwa anaongelea ila hata akisema daraja la kwanza la kidato cha 4 au 6 bado ngumu watu wengi wanasomea ualimu ili wapate mkopo na kwa miaka ya nyuma wapate ajira kwa urahisi
 
Mawazo ya KIJAMAA kwa mjima na upuuzi!! Nani amekwambia vyuo vinatoa vyeti kwa wahitimu waliofeli??. Roho mbaya ndio inawasumbua, F.you
wanaosema hvyo ni vilaza kwa sababu wanasindwa hata kusoma hata kitabu cha TCU kuona wanachukua watu weny alama zipi
 
Anayetakiwa kuajiriwa ni yule aliyefaulu kuanzia daraja la kwanza mpaka la tatu, walimu wengi ni watu waliofeli mitihani, tatizo wanazoa zoa tu. Na pia serikali haiwezi kuajiri kila anayehitimu, mambo mengne ni kudanganyana tuu. Vijana wanatakiwa wawe tuned kupambana na mtaa.
Kama ujui vitu nyamaza tangu lini kada ya uwalimu ikasomewa na watu waliofeli hivi unajua sifa za kujiunga na kozi ya uwalimu

Nikujuze tu huwezi kukuta mwalimu ana degree alafu ajamaliza kidato cha sita hiyo ina maana gani kidato cha nne alifauru, kidato cha sita au diploma alifauru

Nenda kada nyingine uko ukajionee ndio utajua uwalimu ni complicated kwenye matokeo hawaendi vilaza,

Pitia tovuti ya wizara ya elimu angalia sifa wanazoitaji mtu kujiunga kozi ya uwalimu kuanzia cheti alafu pitia na vyuo vingine angalia kozi nyingine sifa zipi wanaitaji mtu kujiunga na kozi ya cheti alafu ulinganishe ufauru ndio utajua kumbe

Hayo maneno uwalimu wanaenda walioferi hutolewa na mtu asiyejua mambo anayejua division one na two ndio ufauru
 
Anayetakiwa kuajiriwa ni yule aliyefaulu kuanzia daraja la kwanza mpaka la tatu, walimu wengi ni watu waliofeli mitihani, tatizo wanazoa zoa tu. Na pia serikali haiwezi kuajiri kila anayehitimu, mambo mengne ni kudanganyana tuu. Vijana wanatakiwa wawe tuned kupambana na mtaa.
Kipindi cha Kikwete Asilimia kubwa waliajiriwa , walimu, wanajeshi , mpaka secta binafsi ziliajiri, unemployment rate ilikuwa ndogo sana na wasomi waliheshimika mtaani na watu waliona umuhimu wa shule.

Tokea elfu mbili na kumi na tano mpaka sasa ajira hamna.
 
Serikali iwafanyie mchujo mkali wa interview na wachukue walimu waliopata division one form six, bila hivo wataajiri magarasa, pia awamu hii ijifunze kwa Jakaya ilikuwaje miaka yake kumi wote waliosoma ualimu walipata kazi, pamoja na madaktari, nurses iweje awamu hii ishindikanike, pia why sector binafsi inakufa Sana kuliko wakati wote,?
Hatakuwi kupewa mitano tena
 
Hii ni ishara kuwa tatizo la ajira Tanzania ni kubwa sana.

Kati ya nafasi za ajira ya ualimu wa shule za msingi & sekondari 13,000 zilizotangazwa na serikali ikiwa ni kumjibu mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA ndugu, Tundu Lissu, takwimu zinaonesha kuwa mpaka kufikia leo Jumatatu tarehe 14.09.2020 feeder ilikuwa imeshapokea jumla ya maombi 80,000+!

Sijui itakuwaje tu kwa vijana hawa watakaoachwa.

Solution kubwa ya tatizo la ajira hapa nchini kwetu ni kwa serikali kutengeneza mazingira ya watu kuweza kujiajiri, kuilea na kuikuza sekta binafsi kwa sababu kwa vipimo vyote, serikali haiwezi na haina uwezo wa kuajiri watu wote wenye sifa za kuajirika. Hili katika sekta ya elimu linaithibitisha hoja hii.

Inasikitisha kuwa, tangu kuingia madarakani kwa ndugu John Pombe Magufuli 2015, ameitibua tibua sana sekta binafsi kiasi ambacho imetema watu wengi toka kwenye ajira rasmi na yenyewe kudorora kwa kiasi kikubwa.

Matokeo ya Sera za CCM ya Magufuli ni haya. Sasa hawa ni vijana wa taaluma ya ualimu tu waliozagaa mitaani.

Hatujui ni madaktari, manesi, wahasibu, wanasheria, wahandisi nk. Wangapi wamezagaa mitaani bila msaada wowote wa serikali kuwawezesha waajirike au wajiajiri.

Mzee Edward Ngiyai Lowassa kuna wakati fulani alionya kuwa, tatizo la ajira kwa vijana ni BOMU KUBWA linalosubiri kulipuka.
Nadhani hizi nafasi kazi watakuwa wameomba na walioko makazini hasa walio shule za private ndio maana inaonekana waombaji ni wengi
 
Kipindi cha Kikwete Asilimia kubwa waliajiriwa , walimu, wanajeshi , mpaka secta binafsi ziliajiri, unemployment rate ilikuwa ndogo sana na wasomi waliheshimika mtaani na watu waliona umuhimu wa shule.

Tokea elfu mbili na kumi na tano mpaka sasa ajira hamna.
Kapige kura umchague Tundu Lissu akupe ajira
 
Anayetakiwa kuajiriwa ni yule aliyefaulu kuanzia daraja la kwanza mpaka la tatu, walimu wengi ni watu waliofeli mitihani, tatizo wanazoa zoa tu. Na pia serikali haiwezi kuajiri kila anayehitimu, mambo mengne ni kudanganyana tuu. Vijana wanatakiwa wawe tuned kupambana na mtaa.
We mwenyewe umeajiriwa na wakisema unafukuzwa kazi unaweza ukafa hata kwa pressure. afu unasema vijana wapambane mtaani
 
Kama waalimu ambao wanasifa lakini hajaariwa wanafika zaidi ya laki jiulize kada zingine wako wangapi? CCM ni janga la Taifa
 
Hii ni ishara kuwa tatizo la ajira Tanzania ni kubwa sana.

Kati ya nafasi za ajira ya ualimu wa shule za msingi & sekondari 13,000 zilizotangazwa na serikali ikiwa ni kumjibu mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA ndugu, Tundu Lissu, takwimu zinaonesha kuwa mpaka kufikia leo Jumatatu tarehe 14.09.2020 feeder ilikuwa imeshapokea jumla ya maombi 80,000+!

Sijui itakuwaje tu kwa vijana hawa watakaoachwa.

Solution kubwa ya tatizo la ajira hapa nchini kwetu ni kwa serikali kutengeneza mazingira ya watu kuweza kujiajiri, kuilea na kuikuza sekta binafsi kwa sababu kwa vipimo vyote, serikali haiwezi na haina uwezo wa kuajiri watu wote wenye sifa za kuajirika. Hili katika sekta ya elimu linaithibitisha hoja hii.

Inasikitisha kuwa, tangu kuingia madarakani kwa ndugu John Pombe Magufuli 2015, ameitibua tibua sana sekta binafsi kiasi ambacho imetema watu wengi toka kwenye ajira rasmi na yenyewe kudorora kwa kiasi kikubwa.

Matokeo ya Sera za CCM ya Magufuli ni haya. Sasa hawa ni vijana wa taaluma ya ualimu tu waliozagaa mitaani.

Hatujui ni madaktari, manesi, wahasibu, wanasheria, wahandisi nk. Wangapi wamezagaa mitaani bila msaada wowote wa serikali kuwawezesha waajirike au wajiajiri.

Mzee Edward Ngiyai Lowassa kuna wakati fulani alionya kuwa, tatizo la ajira kwa vijana ni BOMU KUBWA linalosubiri kulipuka.
Inaskitisha sana
FB_IMG_1597840970548.jpeg
 
Anayetakiwa kuajiriwa ni yule aliyefaulu kuanzia daraja la kwanza mpaka la tatu, walimu wengi ni watu waliofeli mitihani, tatizo wanazoa zoa tu. Na pia serikali haiwezi kuajiri kila anayehitimu, mambo mengne ni kudanganyana tuu. Vijana wanatakiwa wawe tuned kupambana na mtaa.
Huu ni uongo uliokubuu, nani aliyeachwa kwa kukosa sifa
 
Muheshimiwa kafeli kalimbikiza mno, sasa inakuwa tabu sasa.

Ona sasa tunavyofeli!
Mzee Joni ukimwangalia kwa jicho la tatu, utabaini kuwa anataka kupunguza ukubwa wa tarakimu kwenye payroll. Kumtaka aajiri ni kumpeleka kinyume na malengo yake.
 
Back
Top Bottom