kwa-muda
JF-Expert Member
- Sep 5, 2018
- 2,097
- 5,348
Mkuu plug za dualis bei gani? Maana nshaweka plug nimebadili mara tatu shida ni hiyo ni kama vile inakuwa inashindwa kujua niko gear gani. Mara ya mwisho hadi fundi fulani akasema aah hii itakuwa gearbox badili gear box mkuu unaona inashindwa kutambua iko gear gani. plug nilizoweka nilianza na used za ilala ambazo zimetolewa kwa nissa dualis nyingine, wapi. nikabadili coil wapi, nikawekewa zile zinauzwa 20000 mpya wapi, nikanunua tena nyingine wapi. nishabadili sijui ndo chase ya gearbox wapi. hapa nilikuwa nina mpango wa kubadili gear box yote mwezi ujao.Shida hii ipo karibu kwenye kila gari ila kwenye Nissan Hali ni mbaya mno. mfano wa gari zenye hiyo shida ni Dualis, Xtrail T31, Note, Juke na Tiida.
Gari inawaka vizuri, Ila ukianza kuitafuta 40kph ndio unaona hiyo shida hasa kama hujaikanyagia sana na hasa maeneo ya vilima, hata kama ni kilima kidogo.
Shida huwa ni spark plugs.
Sasa watu wengi wamepata mkanganyiko sababu baada ya kubadili plug gari inaweza kutulia hata kwa siku moja au mbili halafu ikarudia tena hali ile ile ya mwanzo. Ikijitahidi kukaa muda mrefu ni mwezi mmoja au ukipiga safari ndefu hutatoboa hata 2000km.
Sababu ya shida hiyo kujirudia baada ya kubadili plug huwa ni plug feki na ndio nyingi zilizojaa madukani.
Shida hii imepelekea watu kubadili plug hata mara 8 kwa mwaka na wengine kuyakatia tamaa magari yao au hata kuyauza.
Solutions ni kupata Spark Plug original.
Mambo ya kuzingatia
1. Plug iwe original na compatible na hiyo engine
2. Usiruhusu fundi kusafisha plug zako(wengi mmejitia kiherehere kusafisha plug na mwisho wa siku mmeingia kwenye hiyo shida)
3. Kama unafanya gapping kwenye plug usiguse electrodes zake vinginevyo plug haitofaa tena.
5. Funga plug ambazo ni PFE design(mostly ni double iridium) au PSPE(ruthenium). Ni plug hizi mbili tu ambazo zinaingia kwenye kundi la plugs zenye uwezo mkubwa wa kuunguza mafuta.
Kwa wenye dualis na Xtrail zenye MR20DE kama umekosa plug original karibu ninazo High performance NCE spark plugs ambazo zitasolve tatizo lako kwa 80,000Km zijazo.
Shida hiyo pia ipo kwenye engines kama EJ20 ya turbo na FB20 za subaru unapokuwa speed 60km/h mpaka 80km/h
1NR FE toyota
TSI engines za VW
Na gari nyingine nyingi na sababu ni hizohizo za spark plugs.
yani gari ikiwa speed ndogo ndipo kama inaslip slip fulani hivi. ikitembea beyond 60 nimekanyagia hilo tatizo hakuna na wala haiwashi taa ya check engine.
wakati nabadilisha plug iliwasha taa ya check engine, nia mashine ikasoma kuwa plug namba mbili haichomi ndio maana nilizibadili lakini ilikuwa ishaanza kuslip pia.