Tatizo la Kukojoa Kitandani kwa Watoto - Ushauri, Tiba na Namna ya Kukabiliana Nalo

Tatizo la Kukojoa Kitandani kwa Watoto - Ushauri, Tiba na Namna ya Kukabiliana Nalo

Great [emoji106]
Mkuu pole sana ,kwanza nikupongeze kwa kulivalia njuga swala la binti yako umeliwahi ,ukiliacha likaenda ukubwani laweza mletea fedheha kubwa kwenye mahusiano na ndoa yake swala hili linatatulika kwa njia mbili

1. Kidaktari

Kaka nenda hospitali kubwa kutana na daktari bingwa wa masuala ya kibofu ,sisemi dawa za kienyeji hazisaidii ila mara
nyingi ni kubahatisha kuua kindege juu ya screen ya tv waweza ua kindege ukapasua tv ,sababu za hali hiyo ni nyingi
-aweza kuwa ana kisukali cha kuzaliwa (usiogope 80% hutibika)
-Matumizi ya kupitiliza ya carboneted drinks (soda,sparkling waters etc)
-etc
UGONJWA HUU UNATIBIKA KABISA

2. Kiroho

Huu ni moja ya ugonjwa pendwa na walozi au roho chafu kama wewe ni mkristo usimpeleke kwa wauza mafuta ya upako au sijui maji ya uzima ,peleka kwenye makanisa yasiyo binafsi kama mlokole peleka TAG kwenye maombi usisahau kutoa na sadaka kumsihi mungu akuhurumie ,kama wewe ni muislamu usiende kwa hawa wanaojitangaza mara wanamajini,mara nyota huo sio uislamu nenda msikiti unaosali kaongee na imamu atakupa dua stahiki ziombe huku ukifunga ,wa dini za asili usisafiri mbali nenda kaone wazee kijijini kwenu

NB: Wasio wakristo au waislamu wafuate viongozi wao husika sio hawa matapeli wa mitandaoni

Karibu
 
Tumekuwa tukijaribu kufanya hivyo tatizo ni kwamba unaposhtuka uzingizini ili kufanya hivyo unakuta yy keshamaliza tayari. Pia tumakuwa tukimnyima kunywa vimiminika nyakati za jioni hadi usiku ila haijasaidia na ndo unakuta anamwaga kojo jingi kuliko siku nyingine.

Kiakili haya yy mwenyewe hii hali inamtesa sana maana wadogo zake wawili hawakojoi so wamekuwa wakimtania sana dada yao kumuita kikojozi na inabidi awe mnyonge kwao maana ni kweli ni kikojozi.

Hili limedhihirika maana kila dawa ninayomletea nikimwambia ni ya kuzuia kukojoa basi ataitumia kwa umakini mkubwa bila kusahau ila ndo hivyo sijaipata ya ukweli
Mlazimishe kwenda chooni usiku awe hana mkojo au hana mkojo. Fanya hata mara 2 kwa usiku mmoja.
 
I write from experience

1) Apunguze kunywa maji sana, anapoona ni muda wa kulala akakojoe mala ya mwisho then ndio alale.

2) Ajiamshe mwenyewe usingizini, kukojo kunasababishwa na ndoto mtu anaota yupo kama na wenzie anaaga anaenda chooni anakojo kumbe nahuku anakojoa kweli ila ukiwa kwenye stage hii unakuwa Kama na usingizi nusu kwenye njozi unaona mkojo mbona unakojoa kiugumu kumbe huku kwenye uharisia mkojo unazuiliwa na godoro. Ukiwa kwenye hali hiyo jenga mazoea yakujiuliza hapa naota au kweli utakuta unashtuka ukiendelea hivi unaacha.

Ukirudiarudia izo process tabia ya kukojoa inaondoka.
 
Mkuu kuna Pampers inaweza ku absorb mkojo wa mtu wa 9yrs? Mkojo ambao unapenetrate godoro la 6 inch unafika kwenye sakafu na unatiririka kuelekea mlangoni? Twice per night?
pampers ndo dawa achana na waganga wa kienyeji labda psychologist au wa watoto
 
Kama upo serious njoo dm nkupe maelezo ya dawa ya kufanya ndani ya week 3 utaleta mrejesho ni buree
 
Nimekuelewa mzazi
Nina mdogo wangu alikuwa na tatizo hilo ilitumika suluhisho kama hilo ila waafrica tunawaza kutatua tatizo leo tu ,kitaalamu sio huwa ubongo unashindwa kutoa comand ,lazima uelewe kwa miaka 9 tayari huyu mtoto wetu ameanza kudhalilika ni jambo ambalo ni la kibaolojia kuliko kisaikolojia ,huyu kama sio magonjwa nlotaja basi kikawaidi (80%) huwa ni kuchelewa kukomaaa kwa nerves na dawa za kusaidia ukomavu dawa zipo ,ndo maana hakuna mtoto wa 1 year asie kikojozi ,haya ya kumlaza mtoto na nyoka ni masuruhisho ya kale ,zamani walikuwa wanamwambia mama mjamzito asile mayai atazaa mtoto anakipara maskini wajawazito wakawa wanaogopa mayai na kisaikolojia ilipelekea jamii nyingi kudhani wanawake hawapendi mayai na kuwaletea watoto maziwa yasiyo na lishe unazalisha vijana wa hovyo mtaaani kwani mayai yana kemikali inaitwa omega 3 hii huongeza uwezo wa mtoto kufikiri iwapo mzazi atayala kwa wingi,kisasa unamwambia ukweli kuwa kula mayai ila si vyema kuwa na uzito kupitiliza ,atajuaje mwambie ahudhulie klinik.

Natumaini we pia mzazi ,mimi baba yangu alikuwa akitaka tuwahi mahala kama tunapaswa kufika saa 3 basi atatudanganya wanae muda ni saa 2 ,matokeo yake tunafika saa 2 hatujalala vizuri tunajihisi vibaya wenzetu wanakuja saa 2:40 ,hii kwanza ikapelekea tupoteze imani na mzee kwa kuthibitisha ni muongo,sasa akituambia muda ni saa 4 sisi tukawa tunaenda saa 5 maskini kumbe siku hiyo hajadanganya tunaishia kuadhibiwa ,mkuu skuizi hatulei watoto kwa mbinu tunashirikiana nao kwa hoja ,hii itajenga kizazi kidadisi sio cha ndio mzee.
 
1) tumekuwa tukiifanya japo haijatuletea matunda
2) kujiamsha mwenyewe.
Huyu kijana huwa ana usingizi mzito sana, ikatokea amelala kabla hajala ujue huyo3 kalala njaa maana hakuna atakayeweza kumuamsha na akaweza kula. So huu usingizi mzito pamoja na ndoto yaweza ikawa ni sababu, maana inawezekana ubongo unatuma signal kwamba sasa una mkojo unatakiwa ukakojoe ila taarifa hazifiki kwa wakati hadi anajikuta keshamaliza
I write from experience

1)Apunguze kunywa maji sana, anapoona ni muda wa kulala akakojoe mala ya mwisho then ndio alale.

2)Ajiamshe mwenyewe usingizini, kukojo kunasababishwa na ndoto mtu anaota yupo kama na wenzie anaaga anaenda chooni anakojo kumbe nahuku anakojoa kweli ila ukiwa kwenye stage hii unakuwa Kama na usingizi nusu kwenye njozi unaona mkojo mbona unakojoa kiugumu kumbe huku kwenye uharisia mkojo unazuiliwa na godoro...ukiwa kwenye hali hiyo jenga mazoea yakujiuliza hapa naota au kweli utakuta unashtuka ukiendelea hivi unaacha.

Ukirudiarudia izo process tabia ya kukojoa inaondoka.
 
Mkuu kuna Pampers inaweza ku absorb mkojo wa mtu wa 9yrs? Mkojo ambao unapenetrate godoro la 6 inch unafika kwenye sakafu na unatiririka kuelekea mlangoni? Twice per night?
Sisi tuliouguza wazazi kwa miaka wenye matatizo hayo tunajua. Zipo na anaweza kutumia ila cha msingi ni ushauri nasaha ili kujua chanzo cha tatizo. hizo Pampers zipo na size zake. kwenye maduka makubwa kidogo na zina bei lakini kama anatumia usiku tu zitamfaa sababu kama mimi mzazi wangu alikuwa anatumia 24 hours tena kwa both one and two. Shoppers Dar na Kariakoo ni nyingi au mikoani zipo mfano Bk wanazo. asa hivi ni kitu cha kawaida.
 
Noted thanks
Sisi tuliouguza wazazi kwa miaka wenye matatizo hayo tunajua. Zipo na anaweza kutumia ila cha msingi ni ushauri nasaha ili kujua chanzo cha tatizo. hizo Pampers zipo na size zake. kwenye maduka makubwa kidogo na zina bei lakini kama anatumia usiku tu zitamfaa sababu kama mimi mzazi wangu alikuwa anatumia 24 hours tena kwa both one and two. Shoppers Dar na Kariakoo ni nyingi au mikoani zipo mfano Bk wanazo. asa hivi ni kitu cha kawaida.
 
Nina bint wa miaka 9 ila ana tatizo la kukojoa kitandani, yaani anaweza kukojoa hata mara mbili kwa usiku mmoja. Pia hata mchana akilala anaweza akakojoa pia.

Msaada please.

Kwanza jaribu kufuata njia hii.

1. Kila mara kabla ya kulala, hakikisha amejisaidia
2. Usiku mwamshe (weka alarm) at least mara mbili ajisadie. Kwa mfano kama anakwenda kulala saa 4 usiku, hakikisha amejisaidia kabla. Ikifika saa 6 mwamshe. Halafu ilifika saa 8 mwamshe tena na saa 11.
 
Ni kawaida tu bhana, mimi nilikojoa kitandani hadi nafika darasa la saba

kwenye makambi kule shuleni nilikua nakojoa kila siku, ila sikuwahi kugundulika

NB: kukojoa hua ni inshu ya kisaikolojia na hua inatibika kisaikolojia.
 
Ok tutajaribu mkuu ni wazo zuri sana
Kwanza jaribu kufuata njia hii.

1. Kila mara kabla ya kulala, hakikisha amejisaidia
2. Usiku mwamshe (weka alarm) at least mara mbili ajisadie. Kwa mfano kama anakwenda kulala saa 4 usiku, hakikisha amejisaidia kabla. Ikifika saa 6 mwamshe. Halafu ilifika saa 8 mwamshe tena na saa 11.
 
Mawazo yenu yote nunayapokea na nimeshaanza kuyafanyia kazi. Hv nimetoka kuongea naye. Nimejaribu kumuhoji nn kinatokea hadi anajikuta ameshakojoa anasema hakuna kitu anajikuta tayar. Nimemuuliza hujawahi kuota ndoto kama upo chooni then ukakojoa anasema wala haoti.

Nikaamuuliza nilini ulishawahi kustuka kwenyewe usiku ukaamka halafu ukalala tena? Anasema hata siku moja, yaani akiangusha kama ni saa nje ni hadi aamshwe kujiandaa kwenda shule. Hapa ndo na prove kwamba usingizi mzito yaweza ikawa ni sababu kubwa. Suala la kuweka alarms nataka nilianze immediately usiku wa leo then nitatoa mrejesho
[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Mawazo yenu yote nunayapokea na nimeshaanza kuyafanyia kazi. Hv nimetoka kuongea naye. Nimejaribu kumuhoji nn kinatokea hadi anajikuta ameshakojoa anasema hakuna kitu anajikuta tayar. Nimemuuliza hujawahi kuota ndoto kama upo chooni then ukakojoa anasema wala haoti. Nikaamuuliza nilini ulishawahi kustuka kwenyewe usiku ukaamka halafu ukalala tena? Anasema hata siku moja, yaani akiangusha kama ni saa nje ni hadi aamshwe kujiandaa kwenda shule. Hapa ndo na prove kwamba usingizi mzito yaweza ikawa ni sababu kubwa. Suala la kuweka alarms nataka nilianze immediately usiku wa leo then nitatoa mrejesho
[emoji120][emoji120][emoji120]
Fanya Mkuu then leta mrejesho. Nina mdogo wangu wa Kiume yupo Kidato Cha NNE Lakini bado Anakojoa Kitandani.. Ukifanikiwa hili nipe mrejesho.
 
Mawazo yenu yote nunayapokea na nimeshaanza kuyafanyia kazi. Hv nimetoka kuongea naye. Nimejaribu kumuhoji nn kinatokea hadi anajikuta ameshakojoa anasema hakuna kitu anajikuta tayar. Nimemuuliza hujawahi kuota ndoto kama upo chooni then ukakojoa anasema wala haoti. Nikaamuuliza nilini ulishawahi kustuka kwenyewe usiku ukaamka halafu ukalala tena? Anasema hata siku moja, yaani akiangusha kama ni saa nje ni hadi aamshwe kujiandaa kwenda shule. Hapa ndo na prove kwamba usingizi mzito yaweza ikawa ni sababu kubwa. Suala la kuweka alarms nataka nilianze immediately usiku wa leo then nitatoa mrejesho
[emoji120][emoji120][emoji120]
Halafu nakushauri usi panic na kujikuta unafuata ushauri mwingine wa kumuumiza mwanao. Usimkaripie, kumpiga au kumtisha. Pia jiepushe na madawa ya kienyeji. Nimewahi kushuhudia visa vya aina hii. Ni kuwa kama ulivyosema watoto wa namna hii wanakuwa na usingizi mzito sana. Kuna kipindi akikua hali itabadika. Vikojozi wako wengi sana wengine mpaka miaka 14 bado wanalowesha vitanda. Lakini wanakuja kuaacha. Labda kuwe na kitu serious tu. Hata wakati wa kumwamsha usiku utakuja ona kuwa ana usingizi mzito sana.
 
Mawazo yenu yote nunayapokea na nimeshaanza kuyafanyia kazi. Hv nimetoka kuongea naye. Nimejaribu kumuhoji nn kinatokea hadi anajikuta ameshakojoa anasema hakuna kitu anajikuta tayar. Nimemuuliza hujawahi kuota ndoto kama upo chooni then ukakojoa anasema wala haoti. Nikaamuuliza nilini ulishawahi kustuka kwenyewe usiku ukaamka halafu ukalala tena? Anasema hata siku moja, yaani akiangusha kama ni saa nje ni hadi aamshwe kujiandaa kwenda shule. Hapa ndo na prove kwamba usingizi mzito yaweza ikawa ni sababu kubwa. Suala la kuweka alarms nataka nilianze immediately usiku wa leo then nitatoa mrejesho
[emoji120][emoji120][emoji120]
Heshima kwako mkuu, naomba nikupe na mimi uzoefu wangu :

1. Katika hali ya kawaida mtoto akifika miezi 6 hadi 9 anapaswa kuacha kujikojolea

2. Kama atakuwa hawezi kudhibiti mkojo baada ya kufikisha mwaka mmoja basi huyo ana tatizo linalohitaji msaada wa kitaalam

3. Chukua hatua zifuatazo ili kumsaidia

• Ongea nae na mkubaliane asitumie kimiminika chochote baada ya jua kuzama,wakati wa chakula cha jioni anaweza kunywa maji si zaidi ya nusu glass

• Kabla ya kulala hakikisha anaenda kukojoa na uweke utaratibu wa kumuamsha angalau mara mbili usiku ( hapa inabidi uweke Alarm either kwenye simu yako au unaweza kununua saa maalum za mezani zenye alarm) ukimzoesha kufanya hivyo baada ya muda ubongo wake utazoea kuamka hata kabla ya alarm, njia hii ina ufanisi mkubwa sana!

• Kwa Umri wake fahamu tatizo lake linamuumiza sana kisaikolojia, nyie wazazi muonyesheni upendo na kujali na msitangaze tatizo lake kwa watu wala kumuadhibu akijikojolea, anahitaji msaada na nyie ndio mnapaswa kumsaidia

• anzisha utaratibu wa kumpongeza siku asipojikojolea, hii itaongeza self esteem yake na kumtia moyo kwamba mnafuatilia na mpo kwa ajili ya kumsaidia

Ukiweza kufanya haya kwa miezi miwili hadi mitatu tatizo litaisha nina ushahidi wa hili. Kila la heri usisahau kuleta mrejesho!
 
Back
Top Bottom