Kwa mujibu wa taasisi ya kimarekani ya National Health and Nutrition Examination Survey (NHANES) hadi kufikia mwaka 2016 nchi ya Tanzania ilikuwa ina kiwango cha unene uliopitiliza (Obesity Rate) kwa 8.4% ya idadi ya watu wake. Huku USA ikiwa na 42.1% ya idadi ya watu wake. Hii ni kumaanisha kuwa hadi 2016 kulikuwa na watu 8 kati ya 100 wenye tatizo la unene Tanzania. Huku wamarekani wanne kati ya 10 wakiwa na tatizo la unene.
Pia kwa mujibu wa ripoti za benki ya dunia kwa mwaka 2021 asilimia 23.5 ya idadi ya watu nchini Tanzania walikuwa na tatizo la ukosefu wa chakula cha kutosha (undernourishment). Inamaanisha kulikuwa na watu 24 kati ya 100 waliokuwa wanapata lishe duni. Na hadi 2020 asilimia 34 ya watoto wa chini ya umri wa miaka 5 walikuwa na tatizo la chronic malnutrition nchini Tanzania kwa mujibu wa USAID.
Hizo ni ripoti ambazo ziko mtandaoni na yeyote anaweza kujisomea. Nimeandika huu uzi nikiwa na masikitiko kuona kumeibuka kampeni kubwa ya kuwaaminisha wananchi kuwa kwa sasa hatuna tatizo lolote linalosababishwa na lishe duni ila tuna matatizo yanayosababishwa na matumizi mabaya ya lishe tele iliyopo. Kila mwanaharakati wa afya akiibuka ni kusema kitu fulani msile ni kibaya kwa afya wakati hata hicho anachotaja watu wanakipata kwa kubahatisha.
Ukienda mitaa ya uswazi tatizo kubwa linalowasumbua ni vidonda vya tumbo kutokana na kutopata chakula cha kutosha kwa wakati. Udumavu wa watoto ni mkubwa. Watu wengi tuna maumbo madogo kwa sababu ya kutopata lishe sahihi. Jana waziri wa mifugo kahimiza watu wale na nyama na maziwa ila akaibuka mfuasi wa Mbowe (nyumbu) ndugu Lema na kumpinga kwa kudai angewaona kwanza madaktari kabla ya kuhimiza.
Dr Janabi na wanaharakati wengine ingependeza kama mngeweka nguvu kuhakikisha watanzania wanapata chakula bora. Pongezi za dhati kwa mbunge Neema Lugangira kwa jitihada zake kuhusu lishe.
Pia kwa mujibu wa ripoti za benki ya dunia kwa mwaka 2021 asilimia 23.5 ya idadi ya watu nchini Tanzania walikuwa na tatizo la ukosefu wa chakula cha kutosha (undernourishment). Inamaanisha kulikuwa na watu 24 kati ya 100 waliokuwa wanapata lishe duni. Na hadi 2020 asilimia 34 ya watoto wa chini ya umri wa miaka 5 walikuwa na tatizo la chronic malnutrition nchini Tanzania kwa mujibu wa USAID.
Hizo ni ripoti ambazo ziko mtandaoni na yeyote anaweza kujisomea. Nimeandika huu uzi nikiwa na masikitiko kuona kumeibuka kampeni kubwa ya kuwaaminisha wananchi kuwa kwa sasa hatuna tatizo lolote linalosababishwa na lishe duni ila tuna matatizo yanayosababishwa na matumizi mabaya ya lishe tele iliyopo. Kila mwanaharakati wa afya akiibuka ni kusema kitu fulani msile ni kibaya kwa afya wakati hata hicho anachotaja watu wanakipata kwa kubahatisha.
Ukienda mitaa ya uswazi tatizo kubwa linalowasumbua ni vidonda vya tumbo kutokana na kutopata chakula cha kutosha kwa wakati. Udumavu wa watoto ni mkubwa. Watu wengi tuna maumbo madogo kwa sababu ya kutopata lishe sahihi. Jana waziri wa mifugo kahimiza watu wale na nyama na maziwa ila akaibuka mfuasi wa Mbowe (nyumbu) ndugu Lema na kumpinga kwa kudai angewaona kwanza madaktari kabla ya kuhimiza.
Dr Janabi na wanaharakati wengine ingependeza kama mngeweka nguvu kuhakikisha watanzania wanapata chakula bora. Pongezi za dhati kwa mbunge Neema Lugangira kwa jitihada zake kuhusu lishe.