asakuta same
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 14,829
- 5,035
Wadau napenda kutanguliza shukrani za dhati kwenu nyote nimepona ugonjwa wa fungus wa mwili niliokuwa nao kwa muda takribani miaka 12..nimetibiwa hospital ya masista Kawe unashukia kituo kinaitwa kanisani kama ukipanda daladala.jaribu nawe kama una tatizo kama langu thanks so much JFmEMBER
mbona aliyepona kapotea??? wengine tutahitaji details maana tupo mikoani. hata kawe hatupajui zaidi ya kumjua halima mdee
sioni jf inahusika vipi hapo..........
ufafanuzi tafadhali..........
Atueleze alikuwa anaumwa fungus wa aina gani na alipewa dawa gani na pia ushauri huo aliupata kwenye sredi gani? Ili na mie npate somo.
duh!.
Kweli hujaelewa uhusiano uliopo?
Tahadhari: fungus wapo aina nyingi wengine ni wagumu sana kutibika 'resistant' na njia pekee ni kumchukua huyo na kumfanyia wanayoita 'culture and sensitivity test' hapo utapata dawa sahihi. Kitunguu swaumu ni sawa na limau au tangawizi. Asali ni tofauti imethibitika kisayansi kuwa antibacterial na siyo wote pia
Labda una utumbo wa Mamba fanya check up!!
Msaada wana Jf
Nina tatizo nikiwa na hasira nashikwa na mkojo sana je hili ni tatizo gani nifanyeje ili lisinitokee
naomba majibu ya kweli sio dhihaka na dharau tafadhalini wadau
asante mkuu nitajaribu
Kiongozi naomba kuuliza ..ivi hii fungus ya maps like dawa yake exactly ni ipi? Maana mi nnayo miaka 5 saivi dawa kibao najaribu ila wapi,,,msaada
Kwa hao sugu ni vizuri ukifanya culture and sensitivity test.....ukienda maabara watachukua sampuli wazipime kuliko kubahatisha dawa
Shukrani mkuu..mi naishi moro kwani hiyo huduma inapatikana maabara za dispensary yoyote ? Km siyo kwa hapo dar huduma hiyo inatolewa km wapi vile?
Hapo Moro hebu jaribu kucheki na jamaa mmoja anayo lab (maabara) hapo karibu na Mt Uluguru Hotel. Hapa DSM maabara kibao unaweza kupata huduma hiyo. Matokeo yatachukua kuanzia siku 2 siyo chini ya hapo
Halafu na haya masuala ya kuchanganya na asali sijui limao nani kayaleta tena hapa?!!Hivi jamani mmeona maelezo yangu vizuri ama mnatunga tu na nyie yenu maana tusije kulaumiana baadaye ikitokea sumu!Nimetaja vitunguu swaumu peke yake,SIJATAMKA LIMAO ama ASALI!Sasa wewe kama unaamua sijui kuwekeka sukari,chumvi ama asali utakuwa unajihatarisha mwenyewe.Wengine wanasema eti wanatengeneza juice,kha!!Kama umeona hukufuata maelezo yangu tafadhali usije kulalamika kwamba haikufanya kazi wala kukusababishia hamu ya vitu vingine.Tuwe makini tafadhali wakuu.
TIBA NA USHAURI:
Kwanza,Hakikisha sehemu husika inakuwa kavu masaa 24.
Pili pakaa poda yoyote ya kutibu fangasi asubuhi na usiku kwa wiki 4 mfululizo MYCOTA inaweza kukufaa.
Tatu,tafuta na meza antibiotic eg cloxacillin 250mg(2 x 3 siku 5) kama sehemu yenyewe imekwa kama kidonda ili uweze kukausha
haraka.
Nne usivae boxer/chupi bali vaa bukta yenye kuruhusu hewa kupita na jikaushe vizuri baada ya kuoga(ni vizuri kusubiri ukauke kabla ya kuvaa nguo).
Usitumie sabuni zenye dawa kwani zitakusaidia kwa muda lakini zitafanya ngozi kupoteza uwezo wake wa asili wa kujilinda dhidi ya vijidudu(ngozi ina uwezo wa kujilinda kiasili,haiitaji msaada, na uwezo wake unaongezeka kadiri inavyoshambuliwa na vijidudu-)
Tano hakikisha unabadili nguo ya ndani kila siku na unavaa nguo safi na ikibidi uipige pasi kila siku.
Sita,tumia cream inayoitwa QUADRIDERM X 2 KWA SIKU 14 lakini ipake sehemu ikiwa kavu na kaa dk 15-30 kabla ya kuvaa nguo Mwisho,Muone daktari kwa ushauri na tiba zaidi.
DAWA YA KUTIBU MARADHI YA FANGASI
Nunua Kitunguu Swaumu.Menya chote kama vile uandaavyo kwa ajili ya
kupikia.Twanga ama saga,vikishasagika changanya na maji ya uvuguvugu kidogo
kipimo cha kijiko cha chai ili vilainike.Chota msagiko wote wa vitunguu na uvimeze.
Tahadhari,jitahidi uwe na mfuko ama sehemu ya maliwatoni maana kama hauna
tumbo zuri unaweza tapika.(Mara chache sana hutokea kutapika)
Ukishakaa kama dk 15 hali yako kutotapika itarudi kama kawaida.Baada ya SIKU 14
utaona minyoo hakuna tena na fungus wote wamekauka!Kwisha kabisa!!!!
Pia kama una presha ya kushuka usitumie hii dawa maana huwa inashusha sana
presha,labda unywe na kahawa baada ya kuinywa dawa hii ili kuipandisha tena
presha! Usisite kuja kutoa ushuhuda wako hapa.