Tatizo la Mabaka, Mba na Fungus (Fangasi) sugu na kuwashwa sehemu za siri kwa wanaume na wanawake- Fahamu chanzo, Dalili na Matibabu yake

mmmmmh mbavu zangu hadi mayonaise mtasema ni dawa
 
Jamani naomba mnisaidie uti na fungus husababishwa na nini and dalili na jinsi ya kujizuia na dawa zake.

MAAMBUKIZI YA NJIA YA MKOJO (URINARY TRACT INFECTIONS -UTIs)


Neno U.T.I si geni masikioni mwa wengi, kwani ni wengi leo utawasikia “naumwa U.T.I”. Japo si wote hulitumia kisahihi. Wengine wana tatizo ambalo ni tofauti na U.T.I, lakini anaweza akaenda hata duka la dawa na kuomba

apatiwe dawa za U.T.I. Leo nimeona tubadilishane elimu juu ya hili tatizo, angalau kila mmoja awe na uelewa U.T.I ni nini hasa, inasababisha na nini, na ni jinsi gani anaweza kujikinga.

U.T.Is, ni kifupisho cha Urinary Tract Infections, ambayo kwa lugha yetu ni maambukizi ya njia ya mkojo. Kama linavyojieleza, kwamba maambukizi ni lazima yawe ni kwenye njia ya mkojo ndipo tunaita ni U.T.I, na si pengine popote. Una uchafu unatoka ukeni, hiyo ni kitu kingine tofauti nk. Tunapozungumzia njia ya mkojo, ni kutoka eneo la

nje hadi kwenye kibofu, na kutoka kwenye kibofu hadi kwenye figo.

Kama maambukizi yako eneo la kutoka kwenye kibofu hadi kwenye figo(ikihusisha na figo pia), inaitwa Lower Urinary Tract Infect. Na ikihusisha eneo la juu ya kibofu, inaitwa Upper Urinary Tract Infection.

Tatizo hili huwapata wote, wanaume na wanawake. Lakini huwapata zaidi wanawake kutokana na tofauti za kimaumbile. Hii ni kwa sababu kuu mbili, i)njia ya haja ndogo ya mwanamke iko jirani zaidi na njia ya haja kubwa

ambapo vijidudu vingi visababishao U.T.I ndipo vinapoishi, ii) mrija wa mkojo (urethra) wa mwanamke ni mfupi ukilinganisha na wa mwanaume, hivyo kufanya iwe rahisi kwa maambukizi kufika kwenye kibofu kwa mwanamke kuliko kwa mwanaume.

Visababishi
Tatizo hili husababishwa kwa kiasi kikubwa na bacteria ambao makazi yao ya kawaida utumbo mpana, na hivyo huwa wanapatikana pia kwenye haja kubwa, mfano Escherichia coli na wengineo. Pia, linaweza likasababisha na ‘fungus’ na visababishi vingine, japo ni mara chache sana.


Vihatarishi na Njia ya Maambukizi
a)Kwa wanawake
• Kujamiiana –hii huweza kuamisha bacteria walio kwenye uume moja kwa moja, ama watokanao na maambukizi ya ukeni kuingia moja kwa moja njia ya mkojo
• Kuchezea ama kuchezewa na mikono michafu maeneo ya uke kunaweza kusababisha maambukizi
• Njia mbaya ya kujisafisha baada ya haja kubwa au ndogo inaweza kuhamisha bacteria walio ktk njia ya haja kubwa na kuingia njia ya mkojo
• Matumizi ya pedi za kike zenye kemikali ya kukata harufu ambao huua bacteria wa asili wa eneo la uke na kukaribisha bacteria wanaosababisha maradhi kuzaliana kwa wingi

Vifuatavyo pia vinaweza vikachangia
• Ujauzito –mara nyingi hushusha kinga ya mwili ya mjamzito
• Upungufu wa homon ya ya kike Oestrogen husababisha bacteria wasababishao U.T.I kuzaliana kirahisi


b)Kwa wanaume
• Matatizo ya tezi ya kiume(prostate) mabapo husababisha mrija wa mkojo kuziba, ama kutopitisha mkojo vizuri na kuruhusu bacteria kujenga makazi
• Kutotahiriwa, ambapo nyama ya mbele inaweza kuhifadhi bacteria wasababishao U.T.I
• Kujamiiana kinyume cha maumbile huingiza kirahisi bacteria walio njia ya haja kubwa kwenye njia ya mkojo
• Kujamiiana bila kinga na mwanamke ambaye ana maambukizi ukeni
• Kuwa na VVU ambapo hupunguza uwezo wa mwili kupambana na maambukizi


c)Kwa wote
• Kutokunywa maji na vinyaji kwa wingi –kunywa maji mengi husababisha mkojo kuzalishwa kwa wingi, na kukojoa mara kwa mara na hivyo kusafisha njia ya mkojo
• Kuwekewa mirija inayosaidia kutoa mkojo nje inaweza pia kukaribisha maambukizi
• Matatizo ya figo na mengine kwenye njia ya mkojo yanayoweza kuziba njia ya mkojo
• Kisukari ambapo hudhoosha kinga ya mwili na pia kuharibu mfumo wa figo wa uchujaji


Dalili za U.T.I
a) Kwa eneo la chini la njia ya mkojo
i. Hali ya kujisikia kutaka kukojoa muda wote
ii. Maumivu, au hali ya kujisikia kuchoma choma wakati wa kukojoa
iii. Kukojoa mara kwa mara na mara zote mkojo ni mdogo
iv. Mkojo unaweza kuonekana una ukungu, na mara nyingine unatoa harufu kali
v. Maumivu ya nyonga kwa wanawake
vi. Maumivu ya rektamu(rectum) kwa wanaume
vii. Na mara nyingine damu kwenye mkojo


b) Kwa eneo la juu la njia ya mkojo
i. Maumivu ya tumbo(hasa eneo la juu kwa pembeni –chini ya mbavu)
ii. Homa kali
iii. Kutetemeka na kujihisi baridi
iv. Kichefuchefu na /au kutapika


Vipimo na matibabu
Mara nyingi kipimo cha mkojo kinaweza kuonyesha tatizo.
Matibabu ni antibiotic baada ya daktari kubaini tatizo

Madhala yatokanayo na U.T.I isipopata tiba sahihi
• Inaweza ikasababisha maambukizi makubwa ya figo(pyenephritis) ambayo yanaweza kusababisha uharibifu wa kudumu wa figo na hivyo kutishia maisha
• Kwa wajawazito inaweza kuhatarisha maisha ya wote mama, na motto aliye tumboni
• Bakteria wanaweza kuingia mfumo wa damu na kusababisha ama kwenda kusababisha madhala mengine
• Inaweza kusababisha shinikizo la damu kuwa kubwa kwenye figo na hata kusababisha ufanyaji wa kazi mbovu wa figo


Tiba mbadala nyumbani kabla ya kumwona daktari
Unaweza kutibu, ama kupunguza tatizo nyumbani kabla ya kumwona daktari pale uonapo dalili ya awali ya U.T.I, ambayo ni maumivu na kuchomachoma wakaji wa kukojoa. Fanya yafuatayo
i. Kunywa maji mengi hasa saa 24 za kwanza baada ya kuona dalili. Hii itasaidia kuzalisha mkojo kwa wingi na

kusafisha njia ya mkojo
ii. Kojoa mara kwa mara na hakikisha ni hadi mkojo unaisha ili kibofu kiwe tupu
iii. Kwa maumivu ya mlango wa mkojo, oga na kuosha kwa maji ya moto, kutapunguza maumivu


Njia za Kujikinga na U.T.I

Kunywa maji na vinywaji kwa wingi kila siku. Hii itakusaidia ukojoe mara kwa mara na kutoruhusu bacteria kujenga makazi kwenye njia ya mkojo
Kojoa kila ujisikiapo mkojo na usiubane kwa muda mrefu

Kwa wanawake

Nenda ukakojoe mara tu umalizapo tendo la kujamiiana. Hii itasaidia kutoruhusu bacteria kuingia na kujenga makazi kwenye njia ya mkojo.
Badili pedi mara kwa mara uwapo hedhini

Epuka kujisafisha ukeni na maji yarukayo kwa kasi, pia epuka kupilizia marashi ukeni, ama kutumia pedi zenye kemikali ya kukata harufu. Hizo huua bacteria wa asili wa ukeni hali ambayo hukaribisha bacteria wa maradhi kuzaliana kwa wingi

Ujisafishapo baada ya kujisaidia anzia mbele kwenda nyuma kuepusha kuhamisha bacteria walio eneo la haja kubwa kuingia njia ya mkojo

Kwa wale walio katika kipindi cha ukomo wa hedhi, wanaweza kushauliana na daktari juu ya kutumia oestrogen ya ukeni kuwasaidia kujikinga na maambukizi

Kwa wanaume

Kuhakikisha maeneo ya ncha ya uume ni masafi mara zote, hasa ikiwa hujatahiriwa kuepusha kujihifadhi na kuzaliana kwa vijidudu visababishao maradhi.

Kondom wakati wa kujamiiana nayo ni kinga nzuri

Asanteni kwa kutenga muda wenu kupata elimu hii
 
AFYA YA NGOZI : Magonjwa ya fangasi sehemu za wazi.


KWA UFUPI

  • Eneo lenye maradhi pia hubadilika rangi na kuwa na rangi tofauti kidogo na rangi ya ngozi ya eneo ambalo halijaathirika na maambukizi.


Kama mwendelezo wa makala yetu ya maradhi ya ngozi, tuendelee kuangalia maradhi ya ngozi yanayosababishwa na fangasi hasa wale wanaoshambulia sehemu za wazi za mwili, yaani Tinea corporis.

Fangasi wa ngozi ya mwili

Aina hii ya fangasi huathiri sehemu zisizojificha (sehemu za nje za mwili), tofauti na aina ya fangasi tuliozungumza wiki zilizopita ikiwemo wiki iliyopita tulipotazama fangasi wanaokaa sehemu za siri za mwili na zile zilizojificha kama vile, katikati ya vidole au chini ya kucha.

Aina hii ya fangasi huathiri sehemu za mwili ambazo ziko wazi kwa mfano tumboni au mgongoni.

Fangasi hawa hushambulia sehemu gani?

Fangasi wa aina hii huwa na uwezo wa kushambulia sehemu kubwa zaidi ya mwili kama mikono, miguu, uso na kiwiliwili.

Mwonekano wake

Fangasi wa aina hii huonekana kwenye mwili wakiwa na muundo wa duara mfano wa sarafu (mitaani tumezoea kusema shilingi) na ngozi ikiwa imevimba kwenye uzio wa eneo ambalo fangasi amevamia, yaani ukiangalia eneo lenye athari utaona kuna ka duara, mfano wa sarafu ambako kamevimba kwenye kingo za duara hilo mfano wa pete.

Eneo lenye maradhi pia hubadilika rangi na kuwa na rangi tofauti kidogo na rangi ya ngozi ya eneo ambalo halijaathirika na maambukizi. Mfano, mtu ambaye ana ngozi ya maji ya kunde eneo ambalo limeathirika linaweza kuwa na rangi nyeusi zaidi au likawa na rangi nyaupe zaidi.

Dalili za maambukizi

Aina hii ya fangasi huwa na dalili chache sana na kubwa ni muonekano wake kama nilivyouelezea hapo juu. Ila vifuatavyo huonekana :-

• Kubadilika kwa rangi ya ngozi ya eneo lenye maambukizi • Eneo la ngozi lenye maambukizi huwa lina muundo wa duara mfano wa sarafu ya fedha.
• Ngozi kubanduka kwenye eneo lenye maambukizi

• Ngozi kukauka kwenye eneo lenye maambukizi

• Inawezekana kabisa kupata muwasho kwenye eneo lililo na maradhi ingawa si sehemu zote za mwili zenye maambukizi zinaonyesha dalili hii.

Husambaa vipi

Kati ya aina zote za fangasi aina hii ni rahisi zaidi kuambukizwa kutoka kwa mtu mwenye maradhi kwenda kwa Yule asiye na maradhi.

Maradhi haya huambukizwa kwa njia zifuatazo:

• Kugusana na mtu mwenye maambukizi ya fangasi hawa

• Kugusa vitu vilivyobeba fangasi wa aina hii kama vile nguo ikiwemo nguo za ndani, chanuo la nywele, mikufu, vifaa vya kuogea, viatu, soksi

• Unaweza kupata maambukizi pia kwa kugusa sehemu ambazo mwenye maradhi amegusa kama ukuta, viti, makochi na vitu vingine.

• Wanyama wa kufugwa pia wanaweza kubeba vimelea hivi vya fangasi.

Nani yuko hatarini Watu ambao huweza kupata maambukizi ya fangasi wa aina hii ni kama wafuatao:
• Wale wanaofanya kazi zinazohusisha kugusana na watu wenye maambukizi ya fangasi

• Wanaolala kitanda kimoja na wenye maambukizi ya fangasi wa aina hii

• Wanaoshiriki mapenzi na wenza wenye maambukizi ya fangasi hao.





 

Attachments

  • 3589745_f248.jpg
    9.9 KB · Views: 1,176
  • f11.jpg
    12 KB · Views: 390
  • mkono.jpg
    31.6 KB · Views: 399
  • vidole.jpg
    4.9 KB · Views: 386
Mkuu Mzizimkavu,

Hebut tusaidie kutwambia matibabu ya hizo fungus inakuwaje?

Tiba
 
Jamani naomba mnisaidie uti na fungus husababishwa na nini and dalili na jinsi ya kujizuia na dawa zake.

Mkuu Mzizimkavu,

Hebut tusaidie kutwambia matibabu ya hizo fungus inakuwaje?

Tiba
Dawa ya kutibu Fangasi mbona Ma-Hospitalini ipo bibie? Dawa ya kutibu Maradhi ya UTI na

Maradhi ya Fangasi na Minyoo Dawa ya Tiba Mbadala ni Kitunguu Saumu. Unatumia njia hii hapa chini:

Unapo amka Asubuhi kabla ya kula au kunywa kitu Nunua kitunguu swaumu.Menya chote kama vile uandaavyo kwa ajili

ya kupikia.Twanga ama saga,vikishasagika changanya na maji ya uvuguvugu kidogo kipimo cha kijiko cha chai ili

vilainike.Chota msagiko wote wa vitunguu na uvimeze.


Tahadhari,jitahidi uwe na mfuko ama sehemu ya maliwatoni maana kama hauna tumbo zuri unaweza

tapika.(Mara chache

sana hutokea kutapika)


Ukishakaa kama dk 15 hali yako kutotapika itarudi kawaida.Baada ya SIKU 7 ,utaona Minyoo,UTI na

hakuna tena fungus wote

wamekauka!Kwisha kabisa!!!!


Pia kama una presha ya kushuka usitumie hii dawa maana huwa inashusha sana presha,labda unywe na

kahawa baada ya kuinywa dawa hii ili kuipandisha tena presha! Tumia kisha uje unipe feedback.



 

Asante mkuu nitakupa feedback.

Tiba
 
Hii itapata shavu kama mtu mmoja akiongezea ushuhuda kuwa heshima ya ndoa yake nayo imerudi, ha haha ha!
 
Ndo nimepiga hiyo kitu saa hii, duh! si kazi ndogo kihivyo saa hizi nasikilizia matokeo.

Mkuu uliona ehe? Hii kitu sio ya mchezo. Inabidi uwe strong enough kutumia hiyo dawa. Nilitumia, tumbo likawaka moto, nikawa restless na kujilaumu kwa nini nimekunywa hiyo kitu. Kwa sasa nasikilizia matokeo. Lakini kwa mtu ambaye yuko weak, simshauri atumie hii dawa hata kidogo.

Tiba
 
Duuh Mungu anipe ujasiri na mimi niitumie hii tiba, coz hizo reactions zinanitisha sana

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Asante jamiii forum na mkuu ulieanzisha huu uzi napenda kuthibitisha hii dawa nimetumia.mm na.matokeo nimeyaona wakuu tumieni hii kitu mimi nimejipangia kila mwezi at least mara moja nakula hii kitu
 
Ngoja leo niifanyie kazi kachumbali hizi tunazo kula ni balaa

Umeona eeeh? Siku mbili tatu zilizopita nilipata majanga ya minyoo ya ajabu, kuja kuchunguza kumbe ni banda-made kachumbariz
 
Yaani hata minyoo ama fungus wawe sugu vipi,watakufa muda hiyo dawa ifikapo tumboni!

Kwa minyoo,hakikisha unainywa hiyo dawa ukiwa na njaa ili kuikomesha.
Mkuu hao fungus ni mpaka wale wa vishilingi?
 
Nina rafiki yangu(jina kapuni)anasumbuliwa sana na fangasi za Ikuru.Ameshakwenda hospitali mara kwa mara napewa dawa,ugonjwa unatoweka kwa zaidi ya mwaka halafu unarudi kwa kasi ya ajabu.Sasa anaomba msaada nini dawa ya kuu tokomeza kabisa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…