Tarakilishi
JF-Expert Member
- May 19, 2013
- 2,181
- 2,448
Dr Kimario pia anapatikana kwenye clinic yake pale mbuyuni. Ni jirani kabisa na moroco. Ukifika mbuyuni uliza clinic ya masikio utapelekwa. Ni pembezoni mws barabara mkono wa kulia kama unaenda mwengeHii kama ni ya muda mrefu inaitwa chronic otitis media, kwa kuwa umeshatumia dawa nyingi then hapa siwezi kukushauri utumie dawa gani, ila nenda hospital kitengo cha ENT kama alivyosema King'asti. Pale muhimbili wapo wengi mfano Dr Edwin, Dr Kimario au Prof. Mushi kama hajastaafu. Wacheki hawa watakusaidia.
Asante mkuu,manake mimi pia ni mteja sana kwenye hizi pamba za kusafisha masikio,ngoja nibadilike nahofu ukiziwi unaninyemelea kwa haya niliyosoma toka kwako....ila up to this moment i'm ok....View attachment 331044
1. Kwanza husukuma ndani zaidi uchafu
sikioni(ear wax),ule utando unaotoka ndani
ya sikio.
Unapochokonoa sikio kwa pamba huupeleka
uchafu kuingia ndani zaidi ya sikio, hii
husababisha vijidudu kushambulia kuta za
ndani ya sikio na ngoma ya sikio, hupelekea
mtu kutosikia vizuri.
2. Pia kutumia pamba kusafishia sikio
huatarisha kutokwa damu masikioni.
Unaposukuma ndani zaidi pamba kwenye
kuta za sikio ni ngozi laini, unaweza kuona
viti damu kwenye pamba, hii hutokana na
pamba kukwangua kuta za sikio lako.
3. Kutoka maji maji yanayowasha au usaha
sikio.
Hizi pamba huweza kubakia sikioni na ikikaa
kwa muda mrefu itakuwa inazuia uchafu wa
sikio kutoka,pia kuharibu ngoma ya sikio,
huu
utando unaotoka sikioni kazi yake kulinda
sikio lisishambuliwe na vijidudu(bacter ia) na
uchafu mwingine unaoingia sikioni kama
vumbi, pamba ikiziba huchafu hautoki
kuweza kuoza na kutoa maji maji(usaha) na
sikio kuwasha.
4. Kuharibu kuta za ndani zaidi ya sikio.
Ni mara ngapi umeingiza pamba mpaka
mwisho ndani kabisa ya sikio, na hapo
ikigusa ndani zaidi mwisho tundu la sikio
karibia na ngoma ya sikio utasikia maumivu,
hii ni kwasababu ya pamba kuumiza kuta za
ndani ya sikio mpaka kwenye ngoma ya sikio
inaweza kuchanika hii ni hatari zaidi.
5. Kukwaruza kuta za siko.
Baada tu ya kutumia pamba kusafisha sikio
utasikia muwasho ndani ya sikio hii
inamaanisha umekwaruza kuta za sikio na
pamba zinazotumika ni kavu, apo mtu
huendelea kusafisha ili mradi asisikie
muwasho matokeo yake ni kukwaruza zaidi
kuta za sikio hii naweza kusababisha
vidonda
ndani ya sikio.
N.B- Ushauri, ni vizuri ukangoja uchafu au
utando wa sikio ukatoka wenyewe nje apo
ukautoa kirahisi zaidi kuliko kulichokonoa
sikio, ukishindwa hii njia tumia kipande cha
nguo safi kiloweshe maji na taratibu usafishe
sikio lako, kwa watoto usimwingize pamba
masikioni kama umeshindwa kumtoa utando
wa sikioni kwa njia niliyoshauri apo juu ni
bora humpeleke hospitali kuna njia salama
zaidi (bulb syringe) hii hufanya kwenye
mahospitali chini ya uangalizi maalumu wa daktari!!
Sitaki Biasharaya Pambastick ife ila mimi huwa ninawatahadharisha watu madhara ya kutumia hiyo Pambastick. Kwani wewe hujuwi kuna ugonjwa wa Ukimwi na watu kila siku wanazini?hili mbona geni? unataka biashara ya pambastick ife chief??!
Ni kweli chief... ila hapo kwenye ugonjwa wa ukimwi mh! haka kaugonjwa kamekaa sehemu mbaya! hakuna namna itabidi tu kaendelee kuwepo tu, maana kamekaa kwenye utamuu!🙂^_^Sitaki Biasharaya Pambastick ife ila mimi huwa ninawatahadharisha watu madhara ya kutumia hiyo Pambastick. Kwani wewe hujuwikuna ugonjwa waUkimwi na watu kila siku wanazini?
Hapana Mkuu, Linaunguruma tu na ni la upande mmoja tuPole mkuu
Je ni kiziwi ?
Kamulia bangi mbichi ni siku tatu tu sikio liko poa..ila side effect ni kupoteza usikivu kwa muda kidogo then unakaa sawa
Unaweza kutumia Kitunguu saumu.
DAWA ZA KUJITIBU MARADHI YA MASIKIO:
i. Nyunyiza juisi ya Kitunguu saumu katika sikio linalouma
ii. Nenda Hospitali ukapigwe bomba ili maji na uchafu upate kutoka
iii. Pasha moto mafuta ya Zaituni (Olive oil) na yasubiri yapowe na ujitie drops mbili hadi 3
Nenda Hospitali ukapigwe bomba ili maji na uchafu upate kutokaKitunguu saumu na olive oil vinawezaje kuondoa uchafu sikioni mkuu?
Hapa kwenye Jukwaa la Afya sio Hospitali na ukimuona mpaka mtu amekuja hapa kutaka ushauri sio kama hajakwenda Hospitali huenda amekwenda hospitali hajapona ndio anakuja hapa kutaka ushauri wa Jukwaa letu. Tunapo mpa ushauri wetu tunatumia pia ujuzi wetu kwa hiyo usilete dharau na Tiba mbadala iko siku na wewe utakuja kutaka ushauri wetu hapa hapa jukwaani.Tina mbadala sawa TATIZO chanzo hutojua kama ni bacteria infection, fungal infection or viral infection na kila chanzo kina tiba tofauti si kweli eti kila sikio litoalo usaha litatibiwa na juice ya kitunguu swaumu. Kuna ndugu ameshakua kiziwi kwa kutumia herbal medicine kutibu sikio litoalo usaha. Specialists wapo (ENT) hebu nendeni mka waone kwanza ikishindikana huko mje kwenye mbadala .. Ni ushauri tu.