Tatizo la masikio: Fahamu kuhusu sehemu za sikio, magonjwa, ushauri na tiba

Tatizo la masikio: Fahamu kuhusu sehemu za sikio, magonjwa, ushauri na tiba

Ndugu wana jamii forum husika na mada hapo juu mke wangu ana tatizo la masikio kutosikia vizuri mwanzo alikuwa anasikia vizuri lakini ndani ya miezi minne baada ya kujifungua limetojitokeza tatizo hili hasikii vizuri hadi uongee kwa kutumia nguvu. tafadhali naombeni msaada wenu kama utakuwa umeguswa na hili.
 
Kuna mtoto ana miaka mitano sasa, mtoto alikuwa mbunifu, mwenye maswali sana, sasa amepata tatizo!

mwanzo alikuwa anasikia vizuri, lakini ametokea kuwa anapoteza uwezo wa kusikia vizuri, ili akusikie lazima awe karibu yako, akiwa mbali hasikii, ingawa masikio hayana usaha.

Nilimpeleka hospitali zetu za kiswahili, akapimwa na akaandikiwa dawa, tena za bei ghali nilizinunua akazitumia wala hazikumpa nafuu yoyote.

Wasamalia wema waliponisikia nikilalama juu ya tatizo hilo walinishauri kumpa amoxiline na dawa ya matone ya kudondoshea, (ingawa siikumbuki jina) ile dawa ilimsaidia akawa anasikia kwa kiasi fulani, lakini baada ya muda mfupi hali ile inarudi.

Naomba msaada wadau, ni dawa gani anatakiwa kupewa mtoto huyo?
 
Pole mkuu, jaribu kumpeleka Hospital kubwa huenda tatizo likawa solved sio hizo za Kiswahili
 
Hospital zetu ndio maana wakubwa hawaendiko kuna dogo mwezi wa nne anameza vdonge kama anaumwa UKIMWI anapimwa na kupewa vidonge tena hospital kubwa hapa MZA lakin hata nafuu hakunq kila akienda matbabu si chini ya elfu 80 tafuta tu hela mkuu mpeleke hospital binafsi kajaribu huko.
 
siwezi guarantee ila kumuona specialist ni kama 30, gharama nyingine ni kutokana na matibabu na vipimo pamoja na dawa. jitahidi uende its worth going there.
Unaweza kumuona daktari labda umasafiri kutoka Kigoma halafu tiba ukaambiwa laki nane!
Ha ha ha ha !
 
Ndugu vipimo vya Kubaini ungonjwa ni hatua ya kwanza na rahisi kutambua lakini kuutibu ungonjwa kunahitaji uchunguzi wa kina hasa baada ya tiba ya awali kutofanya kazi vizuri
Nashauri umpeleke hospitali kubwa (Muhimbili au Mvumi) ili akakutane na wataalamu waliobobea kwenye magonjwa hayo.
 
Daah
Kwa hospital za bongo si serikalini si private. Mwisho wa siku ataishia kupewa hearing aid, sijui haya masikio. hayatibiki
Kuna dawa huwa wanatoa kila ukienda vidonge fulani vyekundu na vyeupe na dawa ya kunyunyizia sikia Hhizo dawa waweza tumia kipindi chote utadhani.muathirika bila mafanikio.

Mh kama una pesa mpeleke nje tu la sivyo nitamkaribisha kuvaa hearing aid masikioni
Pole sana
 
Jaribu na ekenywa hospital
Kumuona Dr kama sikosei 15 vipimo 40 mpaka dawa dawa nilipoteza kama 160 still sisikiii vizuri ila jaribu.

Muhimbili nilipoteza km 400
Regency hospital km nako alinidhamn prof pale UDSM sijui gharama ila bado

Mwisho wa siku unatumia.kifaa kusikia kazi kweli kweli

Ila mpeleke ajaribu
 
zinginary,
Kuna kipindi nakiri kuwa madokta wetu wanafanya kazi kwa kubunia kwa asilimia 80, hii inawezekana ni kwa kukosa vipimo vya kueleweka, mimi sidhani kuwa nchi hii haina wataalamu walio bobea katika maswala ya mfumo wa masikio pia kuna hospital zenye mitambo ya kisasa ya upimaji, kuna hosptal arusha NSK ipo ungalimited, ina vipimo vya kitabibu vya hali ya juu sana japokuwa nasikia gharama zake ni za juu.

upload_2016-10-31_9-17-12.png
 
.....
Nilimpeleka hospitali zetu za kiswahili, akapimwa na akaandikiwa dawa, tena za bei ghari nilizinunua akazitumia wala hazikumpa nafuu yoyote.
.....
Nashauri uende Muhimbili uonane na madaktari bingwa wa ENT na/au Uende EKENYWA ya Dr. Ole pale Nyuma ya Petrol Station ya mwembechai. Dr. Ole na hiyo hospital yake ni mabingwa wa ENT (Ear, Nose & Throat) yaani masikio, Pua na koo.

Pia usisahau sala na maombi ya nguvu kwani Madaktari hutibu ila Mungu ndiye mponyaji.
 
Back
Top Bottom