The Palm Beach
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 1,967
- 4,267
- Thread starter
- #21
Kwanza, asante kwa observation yako. Nimepokea na hicho kipengere cha kuingiza siasa kidogo, nimekirekebisha kwa kujiondoa kabisa ili niwakere watu...
Kwa hiyo ni sahihi kusema tatizo hili ni hujuma ya baadhi ya viongozi dhidi ya wananchi...!
Tufanyeje sasa tunapokuwa na viongozi wa dizaini hii wanaohujumu wananchi wao...?
Kama ni tiba, tunapaswa kuielekeza dawa mahali hapo...
Huyu Rais anapenda kupokea maneno tu. Hataki kutembea field aone mwenyewe uhalisia wa kile anachoambiwa...
Hili ndilo tatizo hasa ukiachilia mbali changamoto ya mfumo wa kiutawala na kisiasa wa Tanzania kuwa wa hovyo usiosukuma tabia ya uwajibikaji kwa viongozi wa umma wanaoshindwa kutekeleza wajibu wao...
Exactly ndivyo ilivyokuwaUmeandika jambo zuri bahati mbaya ukaja kuharibu baada ya kuingiza vyama, kwani hapo wavivu wa kufikiri watakomea kwenye kujadili vyama badala ya kulizungumzia tatizo husika ulilolitaja, hasa chanzo na nini kifanyike ili kulimaliza.
Mimi kwa upande wangu nitulie hapo ulipozungumzia tatizo wakati wa JPM halikuwa kubwa kama lilivyo wakati huu wa Samia, naamini hapa ndipo penye chimbuko la tatizo, na kutokana na hilo chimbuko, basi tunaweza kuijua solution.
Ooh, kumbe...Kwa upande wangu kinachotuumiza ni mindset tofauti za viongozi waliopo madarakani, na wale wanaopewa hiyo wizara kuiendesha, kuna wale wanaopewa na kujiona wamepewa keki hivyo wanajiamulia waanze kuitafuna upande upi[ bahati mbaya hawa ndio wengi zaidi].
Hawa watatengeneza vikwazo vya kila aina ilimradi kuufanya umeme usipatikane wa uhakika, ili waitumie nafasi hiyo kufanya biashara zao za majenereta, ni watu waliotawaliwa na ubinafsi wa hali ya juu, wasiokula wakashiba, ajabu huyo waziri kila siku anakuja na maneno ya uongo kuhusu chanzo cha kukatika umeme.
Kwa hiyo ni sahihi kusema tatizo hili ni hujuma ya baadhi ya viongozi dhidi ya wananchi...!
Mfano, alishatudanganya wanafanya maintanance, kwamba wakati ule wa JPM palikuwa hapafanyiki maintanance ndio maana umeme ukawa haukatiki hovyo, sasa ajabu ni kwamba, wakati huu ambapo maintanance imekuwa inafanyika, hali ndio imekuwa mbaya zaidi, kumbe sababu ya maintanance ni uongo.
Akaja na sababu nyingine, mabwawa ya umeme yanakauka maji kutokana na upungufu wa mvua, hii kauli yake ikaja kupingana na meneja anayeendesha moja ya bwawa la kuzalisha umeme [simtaji jina yasijekumkuta] akadai maji yaliyokuwepo yalikuwa yanaweza kuzalisha umeme kwa muda mrefu ujao, huu nao ukawa uongo wa waziri.
Tufanyeje sasa tunapokuwa na viongozi wa dizaini hii wanaohujumu wananchi wao...?
Kama ndivyo hivi, ni wazi kuwa tatizo ni la mkubwa wake - Rais Samia Suluhu..Kwa hiyo mifano michache hapo juu, inaonesha vile wizara ya nishati amepewa mtu asiye na weledi wa kuiongoza, lakini hata sababu anazotoa kuhusu kukatika umeme, nazo zinamfanya apoteze uaminifu kwa jamii.
Lakini bahati mbaya aliyemuweka hana habari, anamuona kijana wake ni mchapakazi, anaonesha vile asivyomfuatiliaji wa wasaidizi wake, au anawafuatilia wale asio na urafiki nao, kwangu wizara ya nishati inamuhitaji mtu mwingine aje kuiongoza, asiyekuwa na makandokando ili kurudisha imani kwa watanzania, sio huyu mfanyabiashara aliyepo sasa.
Kama ni tiba, tunapaswa kuielekeza dawa mahali hapo...
Huyu Rais anapenda kupokea maneno tu. Hataki kutembea field aone mwenyewe uhalisia wa kile anachoambiwa...
Hili ndilo tatizo hasa ukiachilia mbali changamoto ya mfumo wa kiutawala na kisiasa wa Tanzania kuwa wa hovyo usiosukuma tabia ya uwajibikaji kwa viongozi wa umma wanaoshindwa kutekeleza wajibu wao...