Wivu tu hao.Jamaa amepambana sn mpaka kufika hatua ile.Nimeona documentary yake aisee ametoka zero.Sema Mungu alimpa kipawa cha kufundisha neno na kuaminika sn
Si vyote visivyoweza kuthibitisha havipo.
Lakini wewe unajuaje hiki hakiwezi kuthibitishwa kwa sababu hakipo na hiki hakiwezi kuthibitishwa lakini kipo?
Mathalani, unajuaje Mungu yupo, hawezi kuthibitishwa tu?
Umeshawahi kufikiri kwamba pengine Mungu hawezi kuthibitishwa kwa sababu hayupo, ni hadithi za kutungwa na watu tu?
Siyo tu Mungu huyu hawezi kuthibitishwa kuwepo, bali pia uwepo wake unakuwa contradicted na hali halisi kwa namna ambayo inaonesha hayupo.
Unaambiwa Mungu ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote.
Aliweza kuumba dunia isiyo na kifo, mabaya, magonjwa, etc.
Lakini hakuumba hiyo, akaumba hii ya ma pandemic na matetemekonya ardhi na ma tsunami.
Kwa nini Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote awe mkatili hivyo kwa viumbe wake?
Wivu tu hao.Jamaa amepambana sn mpaka kufika hatua ile.Nimeona documentary yake aisee ametoka zero.Sema Mungu alimpa kipawa cha kufundisha neno na kuaminika sn
Mkuu.Ni vigumu sana kuamini Binadamu na uhai kwa ujumla ulizuka tu kutoka michakato asilia ya kifizikia na kikemikali, hapo ndipo Mungu anapoingia kwenye picha.
Nimeelewa sana mantiki ya mfano wako. Una maana kwamba huwezi kuafiki jambo lisilowezekana hata kama hufahamu ama hujui jambo linalowezana. Hata mimi pia niko hivyo.Umeelewa mantiki ya huo mfano?
Mtu A akisema mama yako mzazi ni binti wa miaka mitano, mtu mwingine B akabisha na kusema binti wa miaka mitano hawezi kuwa mama yako mzazi, wewe utabisha na kumwambia mtu B ingependeza aseme Mama yako mzazi ni nani kabla ya kusema binti wa miaka mitano hawezi kuwa Mama yako mzazi?
Unaelewa ndicho unachofanya hapa?
Unaelewa naweza kuju jibu fulani si sahihi hata kabla ya kujua jibu sahihi ni lipi?
Unaelewa kwamba naweza kujua binti wa miaka mitano haw3mezi kuwa mama yako mzazi, hata kama simjui mama yako mzazi ni nani?
Unaelewa nikijua Washington DC ni mji ulio Marekani, na ili mji uwe mji mkuu wa nchi ni lazima uwe ndani ya nchi hiyo, mtu akiniambia Washington DC ni mji mkuu wa nchi ya Chad, naweza kujua Washington DC si mji mkuu wa Chad bila ya kujua mji mkuu wa Chad ni mji gani?
Unaelewq kwamba mimi nakuambia Washington DC si mji mkuu wa Chad, kwa sababu Washington DC ni mji ambao uko Marekani, si Chad. Wewe unanilazimisha nitaje mji mkuu wa Chad.
Hata kama sijui mji mkuu wa Chad, hilo haliondoi ukweli kwamba Washington DC si mji mkuu wa Chad, kwa sababu Washington DC uko Marekani.
Kwa hiyo, kama tunatafuta mji mkuu wa Chad, na tunafanya "elimination method" kuitoa miji yote ambayo haipo Chad, Washington DC tunautoa. Haupo Chad. Hauwezi kuwa mji mkuu wa Chad.
Habari ya Mungu kuwepo ina cintradiction. Inatolewa kwa elimination method. Huko kwingine sijakwambia najua nini kimeniweka, na kutokujua huko hakunizuii kujua kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote hayupo.
Kama vile kutokujua mji mkuu wa Chad ni mji gani hakunizuii kujua kwamba Washington DC, mji uliopo Marekani, si mji mkuu wa Chad.
Unakubali kwamba sihitaji kujua jibu sahihi ili kujua kwamba jibu fulani si sahihi?
Kwani mimi nimekataa huyo mtu hana mzazi? Sijakataa huyo mtu hana mzazi.Nimeelewa sana mantiki ya mfano wako. Una maana kwamba huwezi kuafiki jambo lisilowezekana hata kama hufahamu ama hujui jambo linalowezana. Hata mimi pia niko hivyo.
Halikadhalika pia nakubaliana nawe kuwa kujua jawabu lisilosahihi hakutegemei ujue kwanza jawabu lililosahihi. Mfano wako mzuri ni wa binti wa miaka 5 kuzaa mtoto wa miaka 60. Hilo sio sahihi hata kama hatujui umri wa mama yake. Kutomjua ama kutojua umri wa mama yake huyo mtu wa miaka 60, hakuhalalshi kuwa binti wa miaka 5 ndiye mzazi wake.
Pamoja na hayo, ujue pia ya kwamba kutojua au kutofahamu jambo fulani, hakuhalalishi kutokuwapo kwa jambo husika. Kutojua jambo fulani kunafunika akili yako ya ufahamu na kudhani kwamba jambo hilo halipo.
HIVYO BASI:
Kutomfahamu mama mzazi wa huyo mtu wa miaka 60, hakuhalalishi kwamba huyo mtu hakuwa na mzazi. La hasha!
Kutofahamu mfumo uliokufanya uwepo hapa duniani, hakuhalalishi kwamba hakuna mfumo huo. La hasha!
Kutofafahamu kuthibitisha kuwa Mungu yupo , hakuhalalishi kuwa Mungu hayuoo. La hasha!
Kimsingi, kutofahamu jambo fulani hakuhalalishi kuwa jambo hilo halipo. Kutojua kwako kuwa Mungu yupo kusihalalishe kuwa Mungu hayupo. Kuna mambo mengi sana hapa duniani hatuwezi kuyathibitisha uwepo wake lakini yapo. Ni mengi sana.
Kwa sasa huna ufahamu kwamba Mungu yupo. Utakapota ufahamu, utakiri hadharani kuwa Mungu yupo.
Je, haujui ya kwmba ukishakubali Mungu ana uwezo wote unajifunga kukubali anaweza kufanya yote.Kwani mimi nimekataa huyo mtu hana mzazi? Sijakataa huyo mtu hana mzazi.
Nimekataa mtu wa miaka 60 kuwa na mzazi binti wa miaka 5.
Mimi sijakataa kwamba ulimwengu una mwanzo.
Nimekataa kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ndiye chanzo cha ulimwengu.
Sababu ile ile inayonifanya niseme mtoto binti wa miaka 5 hawezi kuwa mama wa mwanamme wa miaka 60, ndiyo ile ile inayonifanya niseme Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hawezi kuwepo na kuwa muumba wa ulimwengu huu.
Sababu hiyo ni logical inconsistency na inherrent contradiction.
Ukikubali Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote yupo, ni sawa na umekubali binti mtoto wa miaka 5 ni mama wa mwanamme wa miaka 60.
Mimi sijakubali Mungu ana uwezo wote, hiyo ni dhana ya kufikirika ambayo haithibitishiki, na pia ina contradictions ndani yake.Je, haujui ya kwmba ukishakubali Mungu ana uwezo wote unajifunga kukubali anaweza kufanya yote.
Ndio maana Yesu amezaliwa na Bikra, je kuna Bikra anayeweza kuzaa bila kuingiliwa na mwanaume (scientifically and logically)?.
Kama jibu ni hapana, Basi unakubali kuwa Mungu anaweza kufanya lolote, na kuweza kwake kufanya yote hakukufanyi umpangie cha kufanya.
Tukija kwenye mfano wa kibin-adamu, Sote tunajua Bakhressa ni tajiri mkubwa sana, lakini kwa vile ni tajiri wewe uje useme kama Bakhressa ni tajiri kwanini haendeshi Buggati?, unahama kwenye hoja ya utajiri wake unakuja kwenye hoja mpya ya kumpangi cha kufanya.
Umenena vyema.Mimi sijakubali Mungu ana uwezo wote, hiyo ni dhana ya kufikirika ambayo haithibitishiki, na pia ina contradictions ndani yake.
Ukisema Mungu ana uwezo wote, kuna swali dogo tu litadhihirisha hii dhana ni ya kufikirika na haina uhalisia.
Utaulizwa, Je, Mungu ana uwezo wa kuumba jiwe ambalo litakuwa zito kiasi yeye mwenyewe ashindwe kulibeba?
Ukisema ana uwezo huo, jibu hilo maana yake Mungu huyo hatakuwa na uwezo wote, maana hilo jiwe hataweza kulibeba.
Ukisema hataweza kuumba jiwe hilo, Mungu anaweza kubeba kila jiwe, bado Mungu huyo atakuwa si muweza yote, kwa sababu atakuwa hawezi kuumba jiwe ambalo hawezi kulibeba.
Hivyo, swali hili linatuonesha habari nzima ya "Mungu muweza yote" ni hadithi ya kufikirika tu.
Ukisema Mungu anam buwezo wote, lakini kuna vitu hawezi kuvifanya, hapo umeji contradict.Umenena vyema.
Lakini swali lako/mfano wako umejengwa katika dhana ambayo si ya kweli.
Nakupa Mfano.
Ukisoma kitabu cha wabrania 6:18 na timotheo 2:13 unapata kuona kuwa kuna vitu Mungu hawezi kuvifanya, kujikana mwenyewe, kusema uongo n. k
Kwa hiyo ni kweli kabisa Mungu ana uwezo wote, lakini kuna mambo hawezi kuyafanya na si sababu kuwa hana uwezo ila ni kwa sababu mbali mbali.
mfano wa hizo sababu mbalimbali.
1. Kujikufuru mwenyewe 2. Kupinga neno lake mwenyewe 3.Kwenda Kinyume na neno lake.
Kuna wengine wanaweza kuja na mfano wakisema ' kama Mungu anaweza yote kwanini asiumbe Mungu mwingine kama yeye ili tuthibitishe kuwa anaweza vyote'
!?
Utaona kabisa mifano na maswali yote yanayotaka Mungu akipe kiumbe au kitu kingine sifa zake itamcontradict Mungu mwenyewe kwa kuwa ameenda kinyume na neno lake mwenyewe.
Hivyo kabla ya kusema Mungu anajicontradict, maswali yenu ndiyo yanayojicontradict.
Tunarudi pale pale, labda nikuulize kwanini Mungu ajikufuru?. akishajikufuru anakuwa sio Mungu tena, hapo unampa sifa za kiumbe kingine kwa sababu Mungu mwenye uwezo wote hawezi kujikufuru kwa kuumba kitu chenye sifa zake zote au asichekiweza.Ukisema Mungu anam buwezo wote, lakini kuna vitu hawezi kuvifanya, hapo umeji contradict.
Mungu wako anaweza kuumba jiwe zito sana kiasi akawa hawezi kulibeba?
Akiweza kuumba hilo jiwe, hqtaweza kulibeba. Hivyo hawezi yote.
Asipoweza kuumba hilo jiwe, hapo napo hawezi yote.
Hivyo, Mungu muweza yote hayupo, ni hadithi tu.
Labda nikupe mfano uone ni kwa namna gani swali lako linajicontradict.Ukisema Mungu anam buwezo wote, lakini kuna vitu hawezi kuvifanya, hapo umeji contradict.
Mungu wako anaweza kuumba jiwe zito sana kiasi akawa hawezi kulibeba?
Akiweza kuumba hilo jiwe, hqtaweza kulibeba. Hivyo hawezi yote.
Asipoweza kuumba hilo jiwe, hapo napo hawezi yote.
Hivyo, Mungu muweza yote hayupo, ni hadithi tu.
Nguvu za Mungu wako zisizo mwisho ni sawa na utajiri wa Elon Musk wenye mwisho?Labda nikupe mfano uone ni kwa namna gani swali lako linajicontradict.
Mfano:
Ellon Musk ni tajiri zaidi katika matajiri wote ambao utajiri wao unafahamika katika vyanzo vya mashirika makubwa duniani.
Swali, Je kwa kutumia fedha ama utajiri wake Ellon Musk anaweza kumfanya mtu awe tajiri kushinda yeye?
Jibu, Ndio, lakini endapo atafanya hivyo atakuwa sio tena tajiri zaidi duniani.
Tuje kwa Mungu sasa : Kama Mungu akiumba jiwe ambalo hawezi kubeba, au akaumba Mungu mwingine mwenye nguvu kumshinda yeye automatically anakuwa sio Mungu tena, Hivyo basi swali lako linalenga kumuondolea Mungu sifa za uungu wake na sio kumpima kama yeye ndiye Mungu wa kweli.
Natumai umeelewa
Mungu mwenye uwezo wote, upendo wote na ujuzi wote hawezi kuwepo.Tunarudi pale pale, labda nikuulize kwanini Mungu ajikufuru?. akishajikufuru anakuwa sio Mungu tena, hapo unampa sifa za kiumbe kingine kwa sababu Mungu mwenye uwezo wote hawezi kujikufuru kwa kuumba kitu chenye sifa zake zote au asichekiweza.
Maana mfano sio jiwe tu, unaweza ukauliza kusema pia kama Mungu ana uwezo wote, ataweza kuumba Mungu mwingine mwenye sifa kama zake (uwezo na maarifa yote, kuwapo kote n. k)
Swali lako umelijenga katika dhana inayomuondolea Mungu uungu wake, hivyo wewe ndio unajicontradict wala sio Mungu.
Kilicho sababisha usione upendo wa Mungu Ni uchaguzi wetu sis binadamu , kutaka kuish kwa maamuz yetu wenyewe , tulipenda kuishi kwa hiari yetu wenyewe Ila Mungu mwanzo alituonya madhara ya uamuz wetu . Mfano ww Ni mwalimu unafundsha hesabu , upo darasan unasolve swali akatokea mwanafunz akasema mwl ww haujui kitu Hilo swal mm naliweza ww kma mwl mwenye hekma utampa chaki alifanye then akishndwa ndo unamwadhibu , Ila ukimwadhibu kabla haujampa ajarbu wanafunz wengne wataona mwalmu haujatenda haki , ndicho alichokifanya Mungu upendo wake umetufanya sisi wanadamu tuwe na hiari ya kuchagua Ila katka vile tunachagua vinatusababishia madhara Alisha tuonya mda , vyote ulivyovitaja majnga ya asili , njaa ulemavu magonjwa na mengne mengi ni matokeo ya maendeleo ya binadamu (teknowlogle)Mungu mwenye uwezo wote, upendo wote na ujuzi wote hawezi kuwepo.
Kwa sababu, upendo wake wote utamzuia yeye kujifanya Mungu juu ya wengine. Akij8fanya yeye Mungu juu ya wengine hapo ata contradict upendo wake wote. Itakuwa kajipendelea na kafanya uchoyo. Hizi si sifa za mwenye upendo wote.
Yani awaumbe watu awapendele wengine wawe na akili, wengine vichaa, aumbe wengine vinyama vinaishi kwa kula uchafu, vingine vinazaliwa na vilema.
Aumbe watu ambao hajawapa neema ya kumjua, kisha awachome moto milele kwa kuwa hawajamjua.
Huyo Mungu hana upendo wote, na hawezi kuwepo.
Kimantiki, Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote ama ataumba wote wawe miungu sawa na yeye, ama hataumba kitu.
Tumeona sisi si Miungu, na ulimwenguni kuna kitu.
Hivyo, Mungu muweza yote, mwenye ujuzi wote na upendo wote hayupo.
Unaelewa kwamba hujajibu hoja za kimantiki nilizoziandikaKilicho sababisha usione upendo wa Mungu Ni uchaguzi wetu sis binadamu , kutaka kuish kwa maamuz yetu wenyewe , tulipenda kuishi kwa hiari yetu wenyewe Ila Mungu mwanzo alituonya madhara ya uamuz wetu . Mfano ww Ni mwalimu unafundsha hesabu , upo darasan unasolve swali akatokea mwanafunz akasema mwl ww haujui kitu Hilo swal mm naliweza ww kma mwl mwenye hekma utampa chaki alifanye then akishndwa ndo unamwadhibu , Ila ukimwadhibu kabla haujampa ajarbu wanafunz wengne wataona mwalmu haujatenda haki , ndicho alichokifanya Mungu upendo wake umetufanya sisi wanadamu tuwe na hiari ya kuchagua Ila katka vile tunachagua vinatusababishia madhara Alisha tuonya mda , vyote ulivyovitaja majnga ya asili , njaa ulemavu magonjwa na mengne mengi ni matokeo ya maendeleo ya binadamu (teknowlogle)
Ni nadharia ipi unayoiami iliyodhibitishwa kisayns ya uwepo wa binadamu na dunia ?Unaelewa kwamba hujajibu hoja za kimantiki nilizoziandika
Unahubiri tu.
Andika vizuri.Ni nadharia ipi unayoiami iliyodhibitishwa kisayns ya uwepo wa binadamu na dunia ?