Tetesi: TBC wafanya kikao usiku wa manane, kimeisha saa 11 alfajiri

Tetesi: TBC wafanya kikao usiku wa manane, kimeisha saa 11 alfajiri

Kuna yule Mama anatangaza habari za michezo anazingua balaa sijui anaitwa nani??????
Sijui alisoma chuo gani cha Habari ni shida kweli kweli Tema mate chini
 
Kiukweli huwa nasahau kama kuna channel inaitwa TBC..
Kukubalika tena kwa hii, labda baadae sana..
 
Wewe ni NP katika Id tofauti, unaambiwa watu wamekaa hadi usiku Wa manane wanajadili kudorora kwa ufanisi Wa chombo hiki cha wananchi. Wanatafuta sababu za kwa nini watazamaji hawakithamini kama vyombo vingine wewe unakuja na ngonjera ya "wana OB van ya kisasa"? Ama kweli nyie wapigania 'UHURU" wa siku hizi ni vipofu. Na wewe Unadhani kwa maneno hayo umetoa mchango murua Wa kuboresha TV ya Taifa.? Hili liko wazi TV ya wananchi haipendwi na wananchi, ni wajibu Wa waliopewa dhamana ya kuisimamia kujiuliza kwa nini watu hawapendi chao. Tutoke na ushauri Wa kuwapa ili kurekebisha hii hali maana ni wazi kama TV hii isingekuwa inapata Ruzuku ikategemea mapato yake kujiendesha ingeshafungwa miaka 3 iliyopita. Baada ya Tido aliyeletwa kuondolewa ubunifu ulikosekana. Waliowashauri Viongozi wetu kumwondoa Tido kwa sababu za kisiasa hawakuangalia faida ya kibiashara na kimvuto waliyokuwa wanaipoteza kwa kumwondoa Mr. TM. Chombo cha habari kitavutia matangazo yanayokiingizia faida kwa kuwa kinapata watazamaji wengi, na kitapata watazamaji wengi pale tu kitakapokidhi matakwa na mapenzi ya watu wenye mitazamo tofauti. Kutangaza kwa kuremba habari za upande mmoja na wakati mwingine watazamaji wakiona wazi zinapotoshwa kwa masililahi ya upande huo ambayo obviously siyo maslahi ya taifa per se,kunawaondoa na kuwapoteza watazamaji makini hata Wa upande huo. Katika ulimwengu Wa sasa Wa utandawazi ambapo taarifa husafirishwa kwa njia mbalimbali si rahisi kuwadanganya watu. TBC angalieni mlipojikwaa msiangalie mlipoangukia, tafuteni kilichorudisha imani ya watazamaji wakati Wa Tido na mkiboreshe, hata kama kitakuwa kinaudhi baadhi ya wakubwa lakini kinaleta mvuto wenye manufaa na faida kwa shirika letu kichukueni na muwaeleze wakubwa wanaokwazwa na kitu hicho manufaa yake. Msikubali TV ya Taifa kuitwa TV ya Chama, ondoeni mawazo hayo vichwani mwa watazamaji kwa kubalance story zinazohusu pande zote na matokeo mtayaona. Iboresheni TBC kuwa TV halisi ya Taifa.
Nashukuru kwa ushauri wako mzuri tu na unaonekana uko makini na kuna ujumbe unataka ufike mahali.

Lakini TBC itabaki na Sera yake ya kuhakikisha Serikali na majukumu yake kwa Wanainchi yanatangazwa na si ushindani wa mbwembwe na kibiashara na TV zingine.

Kile ni chombo cha umma kinatoa Huduma kwa umma kama ilivyo shule,hospitali. n.k

Waache hao ITV Clouds na wengine waendelee na mbwembwe na unayoyataka wewe kuyaona lakini TBC itabaki na msingi yake.

Labda ushauri tu ni kuongeza ubunifu zaidi ktk baadhi ya maeneo ili kuendana na technology.
 
Nashukuru kwa ushauri wako mzuri tu na unaonekana uko makini na kuna ujumbe unataka ufike mahali.

Lakini TBC itabaki na Sera yake ya kuhakikisha Serikali na majukumu yake kwa Wanainchi yanatangazwa na si ushindani wa mbwembwe na kibiashara na TV zingine.

Kile ni chombo cha umma kinatoa Huduma kwa umma kama ilivyo shule,hospitali. n.k

Waache hao ITV Clouds na wengine waendelee na mbwembwe na unayoyataka wewe kuyaona lakini TBC itabaki na msingi yake.

Labda ushauri tu ni kuongeza ubunifu zaidi ktk baadhi ya maeneo ili kuendana na technology.
Unataka TBC ibakie na misingi yake hata kama ni ya hovyo? Iendelee na misingi yake hata hakuna mwenye hamu ya kukitazama kituo hicho?

BBC, CNN ni vituo vya TV vya kitaifa lakini vinapendwa na asilimia kubwa ya watu wote Duniani? TBC kama inataka kuwa chombo cha umma, ijifunze kutoka kwa waliofanikiwa kuliko kushikilia misingi isiyo na manufaa kwa umma.

Nini sababu ya viongozi wengi kutumia vituo vya umma kuliko TBC? Jibu ni wazi, kama unataka watu wengi wakusikie unaenda kwenye kituo kinachosikilizwa na watu wengi.

Hata ukiwa na biashara, utakuwa mjinga kama utapeleka tangazo lako la biashara kwenye gazeti la UHURU wakati unajua kuna wasomaji wachache sana wa gazeti hilo, tena wale ambao wanalazimishwa kulinunua.
 
Huwa najiuliza, kama kweli CCM inaungwa mkono na watanzania wengi, iweje sasa hao wananchi wengi wanaoipenda hawachangamkii kuvitazama na kusoma magazeti yake, hali inayofanya vidorore na kukosa watumizi. Ina maana mashabiki wa ccm hawavutiwi na habari za chama chao?
Something of an irony, isn't it?
 
Unataka TBC ibakie na misingi yake hata kama ni ya hovyo? Iendelee na misingi yake hata hakuna mwenye hamu ya kukitazama kituo hicho?

BBC, CNN ni vituo vya TV vya kitaifa lakini vinapendwa na asilimia kubwa ya watu wote Duniani? TBC kama inataka kuwa chombo cha umma, ijifunze kutoka kwa waliofanikiwa kuliko kushikilia misingi isiyo na manufaa kwa umma.

Nini sababu ya viongozi wengi kutumia vituo vya umma kuliko TBC? Jibu ni wazi, kama unataka watu wengi wakusikie unaenda kwenye kituo kinachosikilizwa na watu wengi.

Hata ukiwa na biashara, utakuwa mjinga kama utapeleka tangazo lako la biashara kwenye gazeti la UHURU wakati unajua kuna wasomaji wachache sana wa gazeti hilo, tena wale ambao wanalazimishwa kulinunua.
Mkuu gazeti la uhuru halina tofauti karatasi ya kuchambia kinachooandikwa mle ni upuuzi mtupu
 
Bias kwenye habari zao nyakati za uchaguzi,ila hilo hata wao wanalijua wasitafute mchawi
 
Hamna vipindi vya kuvutia ndani ya TBC yaan azam amekuja na wamewapiku wamewaacha mbali
 
Back
Top Bottom