TBC wamekata matangazo ya Bunge kuficha Sheria ya Manunuzi inayoruhusu Serikali kununua ndege, treni na meli za mitumba?

TBC wamekata matangazo ya Bunge kuficha Sheria ya Manunuzi inayoruhusu Serikali kununua ndege, treni na meli za mitumba?

Hiyo ni bajeti ya jeshi la polisi
Mbona huwa mna majibu mepesi sana mnadhani watu wote ni wa hovyo hivyo tu? Kuna bajeti ya keshi la polis au bajeti ya wizara ya mambo ya ndani? Huwa shule mnaenda kufanya nini?
Vipi kuhusu bajeti ya Tume ya uchaguzi?
Kwahiyo bajeti ya uchaguzi ni bajeti ya keshi la polisi? Duh!
 
Tunaiponda serikali wakati sisi wenyewe tunajipongeza na kujiona tumepiga hatua za kimaendeleo kwa kununua Magari mitumba, nguo za mtumba, vyombo vya majumbani vya mitumba. Wanaotuongoza hawatoki mwezini ni miongoni mwetu ndo maana sishangai wala kuwalaumu kwa hiyo sheria hao ndio sisi sasa. Kama wewe huwezi kununua gari 0 kilometre kuna mazingira pia serikali inaweza kushindwa kutumia fedha nyingi kwaajili ya kupata kipya ambapo vipo mitumba yake ambayo vinaweza kusukuma siku wakati huo uwezo wa kiuchumi wa kununua vipya unakusanywa
Duh, hiyo hiyo ingenunua mpya ungejipiga kifua
 
Una hela ya kununua vipya!?..Kodi unakwepa,tozo ulizisakama,kukopa unapigia kelele, kuwekeza bandari unafanyia maombi lisiwezekane
Hiyo used tunapigwa mara 2 ya bei mpya huoni ulivyo fala.kitu kikiwa mtumaba unawezije kupata thamani halisi
 
Ukute wanafanya hivyo kwa lengo la kujustify mitumba ya escape from sobibo waliyonunua na zitakazofuata.
Ndio hivyo kuna mkubwa ameshaaharisha inatafutwa njia ya kusafisha kinyesi chake kama ilivyokuwa kwa DP W
 
Madalali wa kimataifa wameshafanya lobbying ya kutosha hadi kubadilisha sheria. Hakuna mtumba wenye warranty. Kwa sheria hii, tumekwisha, watu watakufa, hakuna uwajibikaji wa mnunuzi, makampuni ya insurance yatakwepa kulipa fidia etc. Muuzaji wa ndege au train kukuu huuza zikiwa zimechoka na kuna uwezekano wa kuuziwa zisizofaa kwa matumizi tena.
Pia uanwezaje kupata bei halisi ya mitumba kam sio serikali iliyofeiled ni ninijamani
 
Enzi za Nyerere ATC iliwahi kukodi ndege marehemu toka kwa mpalestina George Hallack, siku ya uzinduzi wa safari yake ya kwanza toka Dar es Salaam kwenda London ndege ilikuwa kama Dar Express, ilikwenda mpaka mwisho wa uwanja ikagoma kuruka! Ilibidi basi la uwanja wa ndege likawachukue abiria na kuwarudisha mjengoni, hiyo ndege iliishia hapo uwanjani na hakuna mtu yeyote aliyechukuliwa hatua. Magufuli, aliagiza meli kwa ajili ya abiria kati ya Dar na Bagamoyo, meli ilianza safari kwa mbwembwe zote za kiccm, ilichukua saa mbili toka bandarini Dar mpaka Kunduchi! Magufuli akateremka na kurudi mjini, meli ilitelekezwa bandarini na hakuna aliyechukuliwa hatua, pia kuna manyangarakasha mengine mengi tu yaliyokula pesa zetu huku tukiongezewa kodi kufidia hasara.
Tukigoma kulipa kodi sio kosa kwa Kweli hautwezi kulipa kodi manyangau yakazifaidi
 
Mwigulu Nchemba amependekeza kwenye Sheria mpya ya Manunuzi Serikali inunue Ndege, Vichwa vya Treni, Mabehewa ya Treni, Meli zilizotumika badala ya kuagiza mpya na wabunge wanasherehekea bungeni kwa sababu wanajua wananufaika na nini kufanya maamuzi hayo.

Sheria hii ikipita iko siku taifa litakuja kuomboleza msiba mkubwa utakaosababishwa na maamuzi ya leo pale Meli zitapakuja kuzama, ndege kuungua angani, treni kuua watu wakati huo Mwigulu yuko zake ughaibuni hayuko tena tanzania. Sisi familia zetu zinakwenda kupoteza maisha kwa maamuzi ya leo kisa tu watu wamekula rushwa kufanya maamuzi hayo.

Hii Sheria ni moja ya Sheria mbovu na iliyojaa mazingira ya rushwa kwa watu wachache wenye madaraka kwa sasa kina mwigulu na washirika wake.

Tuliombee taifa letu tuko kwenye hatari kubwa.

Mbaya zaidi Bunge haliko live kwenye TV ili watanzania wasijue kinachojadiliwa na kupitishwa na Bunge.
Daaah 🤔🤔!! Hivi kuna wakati utafika wananchi wajivunie wabunge wao? Au ndo mpaka angalau katiba mpya ipatikane kwanza na tume huru isiyokua nominated na Rais!!
 
Mbona huwa mna majibu mepesi sana mnadhani watu wote ni wa hovyo hivyo tu? Kuna bajeti ya keshi la polis au bajeti ya wizara ya mambo ya ndani? Huwa shule mnaenda kufanya nini?
Vipi kuhusu bajeti ya Tume ya uchaguzi?
Kwahiyo bajeti ya uchaguzi ni bajeti ya keshi la polisi? Duh!
Sasa hiyo bajeti ya uchaguzi ni kwa ajili ya makaratasi ya kupigia kura na wino!?..we una mgogoro Sana kichwani na ugonjwa wa akili wa kujiona unajua
 
Pia uanwezaje kupata bei halisi ya mitumba kam sio serikali iliyofeiled ni ninijamani
Mtumba ni hatari sana kwenye sekta ya uma.
Wafanyabiashara wazawa au wa kimataifa wanajua kuwa mahali ambapo hakuna mwenyewe na ambapo unaweza kuhonga ukapitisha chochote ni sekta ya uma.
Sekta binafsi hongo siyo rahisi kwani mmiliki anajilinda. Rushwa mara nyingi huhusisha sekta ya uma au serikali, hivyo kununua mitumba ni kuhamasisha au kuweka mazingira mazuri ya rushwa. PCCB wapo wapi kuishauri serikali?
 
Hiyo mipango na bajeti za miradi na manunuzi zilikosewaje kiasi cha kulazimika kubadili sheria ya manunuzi. Yaelekea uwajibikaji ni wa kiwango cha chini sana.
Wasafiri toka ughaibuni huenda watasita kupanda ndege za shirika lisiloweza kununua ndege mpya.
Anyway, Tz itakuwa dampo la chuma chakavu.
 
Mwigulu Nchemba amependekeza kwenye Sheria mpya ya Manunuzi Serikali inunue Ndege, Vichwa vya Treni, Mabehewa ya Treni, Meli zilizotumika badala ya kuagiza mpya na wabunge wanasherehekea bungeni kwa sababu wanajua wananufaika na nini kufanya maamuzi hayo.

Sheria hii ikipita iko siku taifa litakuja kuomboleza msiba mkubwa utakaosababishwa na maamuzi ya leo pale Meli zitapakuja kuzama, ndege kuungua angani, treni kuua watu wakati huo Mwigulu yuko zake ughaibuni hayuko tena tanzania. Sisi familia zetu zinakwenda kupoteza maisha kwa maamuzi ya leo kisa tu watu wamekula rushwa kufanya maamuzi hayo.

Hii Sheria ni moja ya Sheria mbovu na iliyojaa mazingira ya rushwa kwa watu wachache wenye madaraka kwa sasa kina mwigulu na washirika wake.

Tuliombee taifa letu tuko kwenye hatari kubwa.

Mbaya zaidi Bunge haliko live kwenye TV ili watanzania wasijue kinachojadiliwa na kupitishwa na Bunge.
Legacy
 
Seriously kabisa umewasha Tv na kuweka channel ya tbc? Na pia unadiriki kuanzisha Uzi humu kuhusu utendaji wa tbc??
 
Tunaiponda serikali wakati sisi wenyewe tunajipongeza na kujiona tumepiga hatua za kimaendeleo kwa kununua Magari mitumba, nguo za mtumba, vyombo vya majumbani vya mitumba. Wanaotuongoza hawatoki mwezini ni miongoni mwetu ndo maana sishangai wala kuwalaumu kwa hiyo sheria hao ndio sisi sasa. Kama wewe huwezi kununua gari 0 kilometre kuna mazingira pia serikali inaweza kushindwa kutumia fedha nyingi kwaajili ya kupata kipya ambapo vipo mitumba yake ambayo vinaweza kusukuma siku wakati huo uwezo wa kiuchumi wa kununua vipya unakusanywa
Usichojua au kama unajua labda umesahau,mwanzoni mwa miaka ya tisini magari na vifaa vingine yalikua yananunuliwa mapya kabisa na vyenye quality....upuuzi wa watawala wetu ndio umeturudisha nyuma kuanza kununua vitu vya mtumba na low quality.
 
Una hela ya kununua vipya!?..Kodi unakwepa,tozo ulizisakama,kukopa unapigia kelele, kuwekeza bandari unafanyia maombi lisiwezekane
Magari ya Mawaziri je hela zipo au hii ni kwa public tu haiwahusu nyinyi??
 
Back
Top Bottom