TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

Wananchi wengi ni wenye kipato cha chini hawana uwezo wa kulipia hiyo Azam, mimi nahisi ni serikali kutaka kuchagua nini waonyeshwe wananchi na nini wasionyeshwe katika yanayotokea bungeni.
Tutakosa fursa ya kuona na kusikia mambo mengi, kipindi kinapo kiwa recorded huko kunafanyika editing pale penye ukakasi basi pataondolewa ili kuuficha huo ukakasi, na hakuna tv nyingine yoyote inayolusha matangazo haya moja kwa moja, hi ni kuwakosea watanzania na kupoka haki yao ya kikatiba kupata habari
Hii ya jioni subiri kuangalia bunge ambalo watakuwa wameli edit kutokana na muongozo kutoka kwa waziri wa habari Nape, usidhani utashuhudia cheche za kina LISU, ZITTO, na wabunge wa upinzani wanapo ibana serikali, tuta nangalia ki makapi tu.

Minaona huyu Nape sasa anatafuta sifa aiseeee.....
Na kama haya ni maagizo kutoka kwa mkubwa wake, naanza kupata maswali na wasiwasi kwamba..... Ni kipi hasa ambacho serikali inakiogopa hasa waTanzania wasikijue kutoka bungeni..!?
 
Hzo bilioni nne ni posho au nini? Yan techonlogia ilivyokubwa hv vikao vya bunge kwa mwaka mipesa yote hyo. Hapo pana jipu Hapo sio bure
Bilioni nne ikitolewa ktk 1.3 trillion inabaki ngapi? Kama ni nyingi wawaache star tv warushe laivu kwa gharama zao!
 
Kama hiyo ni hoja ya msingi.....
Mbona waziri Nape hajasema kwamba hiyo bilioni 4 badala yake itaelekezwa kwenye shuguli zipi?
Kwasababu nina hakika tayari kurugenzi ya TBC tayari ilikua imekwisha tenga gawio la gharama hiyo ya kurusha matangazo ya bunge moja kwa moja toka Dodoma


Bado naendelea kuaminika kuwa Uongozi wa Awamu ya 5 hawataki changamoto.


Ukiwauliza watasema hiyo hela imeelekezwa kwenye Shughuli za Maendeleo
 
Sasa taifa letu litapiga hatua kubwa kimaendeleo,haya maigizo ya bunge yalikuwa yanawachukulia mda mwingi sana wa kufanya kazi wananchi
 
Hapa hakuna suala la gharama wala nini,huo ni udikteta wa JPM muda si mrefu ataonekana kwa rangi zake zote.Badala ya kutafuta vyanzo vya mapato ili wananchi waendelee kupata habari live wanaona ni bora kusitisha matangazo,kwani hiyo ni starehe??na Nape asingetamka hayo bila kuambiwa na JPM,hawataki watu waone live na kusikia kashfa zinazowagusa viongozi wa ccm.utawala huu unakwenda kufanana na wa mkapa kwa namna zote.
 
jana nilimuona mbunge wa ARUSHA vitu maalum mmmh! wacha wee ni kitu cha haja!
 
Zitto

Kuna wanaouliza, USA
wanaonyesha Bunge 'live'?
UK je? Ifahamike kuwa Nchi
hizo mabunge yao yana TV
na yanarusha live mikutano
yao.


Mpaka hapo hilo litafanyika nchini kwetu, TBC wana wajibu wa kuwapa
habari wananchi.


Kuzuia kurusha mikutano ya Bunge 'live' ni dalili za udikteta
 
Tukubaliane jamba moja, kama TBC wanaona ni gharama kurudha bunge live ni kwanini Azam Tv na Star Tv nao wamekatisha matangazo ngafla?

Tanzania sio korea kasikazini, endapo vyombo vya habari vitadhibitiwa kwa mtindo huu ni heri turudi kwenye chama kimoja tusiwe nchi ya kuhoji wala kujadili.

Tunapoelekea hata mtandao wetu pendwa JF nao unaweza pangiwa masharti
huu uoga unatoka wapi? Hii haki ya kupata habari ni ya kikatiba sio hisani ya mtu wala serekali

Rais Magufuli asipoingilia swala hili mapema heshima yake yote aliyoipata itaporomoka.Huu ni aina ya udikteta
 
Magufuli ni uzao wa CCM na ni lazima alinde maslahi ya CCM.

Hii nchi tunaburuzwa sana.

....Matukio mengine yatarekodia ili yaoneshwe baadaye... nafikiri wenye akili wanajua tarayi nini kinatafutwa hapa. Hatutaona tena mijadala mizoto kwenye runinga, ni kama tunavyoonyeshwa na TBC wakati wa taarifa za habari! Ha ha ha, nchi hii ni hatari sana. Tutafika kweli?
 
Hujawahi sikia TV au Radio za Tanzania zikisema sasa tunajiunga na BBC kusikiliza taarifa za habari? Ina maana BBC akizima mitambo yake wewe huwezi kujiunga naye kurusha hicho kipindi.Kama Star tv walikuwa wakijiunganisha na TBC kurusha matangazo automatically TBC wasiporusha Star TV hawezi rusha kwa sababu hawi na mitambo yake eneo husika.Kama BBC wasiporusha kipindi wewe huwezi rusha kwani huna mitambo yako eneo husika ulijiunga tu


StarTv walikua wanarusha kupitia Mitambo yao ila wamekata baada ya mabishano kati ya Zitto na Chenge, Zitto akitaka mjadala wa kujadili hotuba ya Rais usitishwe wajadili ni kwanini TBC ikate matangazo ya moja kwa moja.

Inaonekana wameamrishwa kukata hayo matangazo.
 
Safi sana hiki kilikuwa ni kilio changu siku zote, Watu wafanye kazi na waache kuangalia Bunge, mkirudi nyumbani jioni baada yakazi mtaangalia Bunge tani yenu au kama mmechoka hata wkend!

Safi sana W. Nape!
Watakuwa wame edit kuonyesha mazuri ya CCM tu .,.. Acha tuisome number ... kwa mbali naona awamu hii itakuwa ya hovyo kuliko zote .
 
Kuna hoja ya msingi hapa zaidi ya watu kufanya kazi muda kazi na siyo kuangalia Bunge? Kama Serikali ingekataza kuonyeshwa Bunge kabisa hapo sawa lkn litaonyeshwa lote jioni baada ya kazi, tatizo liko wapi hapo?

Hoja ya msingi yako au ya nape? Maana hoja ya msingi ya nape inahusu gharama za uendeshaji na wala sio watu kuangalia bunge muda wa kazi (according to you)

Na je unauhakika taarifa zinasema kwamba tbc ita-record kipindi kizima cha bunge bila kuki-edit? au ndio muendelezo wako kukurupuka hapa?
 
Kama maamuzi aliyopeleka bungeni kuhusu kusitisha matangazo ya TBC1 hakukushirikisha nawe ukakubali basi ana lengo baya na ni wazi anakuharibia image yako kitaifa na kimataifa.

Ila kama ni ruhusa yako basi hana kosa ila mheshimiwa sasa utaangaliwa kwa jicho la tatu juu ya dhamira yako na kwanini umeonyesha nia ya kuminya wananchi wasione serikali yako inavyo hojiwa bungeni?
 

Ndiyo hivyo pole sana, HAPA KAZI TU!

Naiunga sana hiyo kaulimbiu ya hapa kazi tu. Lakini kwahili Noooooo.......
Ebu ifike wakati tusishabikie mambo kisiasa au kimihemko aiseeee.....
 
Kuna hoja ya msingi hapa zaidi ya watu kufanya kazi muda kazi na siyo kuangalia Bunge? Kama Serikali ingekataza kuonyeshwa Bunge kabisa hapo sawa lkn litaonyeshwa lote jioni baada ya kazi, tatizo liko wapi hapo?

Kama issue ni watu wafanye kazi basi Vituo vyote vya TV Nchini viwe vinaanza kurusha matangazo yao jioni baada ya kazi.
 
Back
Top Bottom