TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

Wengi wanao lalamika ni wafuasi wa UKAWA walio waandaa wabunge wao kugeuza bunge sehemu ya kujipatia umaarufu na kuleta uhuni.

Hongera sana Mh Nape..
 
Kama ni suala la kubana matumizi basi vituo vingine vya television viwe huru kuonyesha live, vinginevyo navyo visipoonyesha itakuwa ni Kama kubana uhuru wa vyombo vya habari
 
Wengi wanao lalamika ni wafuasi wa UKAWA walio waandaa wabunge wao kugeuza bunge sehemu ya kujipatia umaarufu na kuleta uhuni.

Hongera sana Mh Nape..

Pamoja na itikadi yako mkuu, ninaamini uelewa wako ni zaidi ya hiki ulichokiandika.

Sidhani pia kama unamaanisha kumpongeza jamaa kwa uamuzi huo.
 
Si kweli, star tv wanatusha kivyao, hawapitii tbc!
Okey, vipi Azam tv nao?

Well, am not sure now... Kama nakumbuka kuna wakati kulikuwa na mjadala kuhusu nani arushe matangazo ya bunge, then ikawa kwamba indepenndent tv zilinyimwa kibali cha kurusha kivyao?
 
yelewiiiiiiiiiiiiiiiii sasa tutarajie kuona harusi live kwa wingi


hivi itv star na wengine ambao wanajitegemea wanafanyaje aisee hii wizara ni jipu.. badala kufanya ubunifu wapate jinsi ya kutuonyesha jambo hili muhimu kwa taifa wanaleta longolongo piga chini muhusika

Thinking Capacity zao sijui zikoje yaaani hata mtoto wa darasa la saba atajiuli nini maana ya TV ya Taifa na kwanini tunalipa kodi, Menilitegemea wanaboresha kuongeza mitambo ya kisasa zaidi. kumbe wanaturudisha zile enzi za simulizi yaaani tunahamia North Korea sooon

My Take;

Nape amewekwa pale kwa ajili ya kupambana na wapinzani, Serikali gani hiii inataka kuwa MUNGU. Duniani kote ukisha anza tuu kuminya vyombo vya habari tuu ni udikiteta huo, sasa sielewi wao wameisha lewa madaraka hata kabla ya siku 100 za Rais JPM kweli?
 
Well, am not sure now... Kama nakumbuka kuna wakati kulikuwa na mjadala kuhusu nani arushe matangazo ya bunge, then ikawa kwamba indepenndent tv zilinyimwa kibali cha kurusha kivyao?
Labda inatakiwa hivyo kuwa watangaze kupitia tbc ila mpaka sasa azam na star tv wanarusha kivyao, jana baada ya tbc kukata matangazo ya live ya bunge dk tatu baadae star tv wakakata! Walianza azam kukata matangazo, hivyo suala la gharama ni uongo.
 
duuu hi serikali inaweza ikawa mbovu zaidi ya zote,kuzuia TBC maana yake hamna channel yoyote atakayorusha
 
Mnalalamika nini wakati nyie ndio mliowapigia kura tulieni ivyo ivyo dawa iwaingie mana wengine tulishaona haya yakija na bado mengi yatakuja# CCM mbele kwa mbele
 
....leo umenichekesha sana aisee!!!

Penye ukakasi ni hapo kwenye "idol" nadhani urekebishe ulikuwa unamaanisha "idle".

But all in all watz kwa sasa wanapelekwapelekwa kama circus wakisubiri matukio mara tezi dume, mara Eritrea...and the list is long. Fanyeni kazi, tafuteni hobby kama anavyoshauri mdau hapo, kama ni kutazama bunge nenda dodoma kabisa! Ila hii tabia ya kuwa cry babies kutaka TV iwashwe mpate cha kuongea itatumaliza!

Waingereza walituharibu sana, tumekuwa wazungumzaji kuliko kuwa watendaji, jambo dogo linakuzwa kuwa kubwaaa...ndio maana EPL ina publicity kuubwa wakati hamna talent kiivyo ni hichi kihulka cha kuwa na uzungumzaji zaidi ya kuwekeza kwenye the actual work.
 
NAYASEMA HAYA BAADA YA KUGUNDUA WATANCHI TUNAKOSEA KUWACHAGUA WAWAKILISHI WETU BUNGE ,TUNACHAGUA MAVUVUZELA BUNGENI NA WANAOTAFUTA KUONEKANA BUNGENI ILI KUPATA UMAARUFU MAJIMBONI BADALA YA KUWATUMIKIA WANANCHI,
USHAIDI UPO
MFANO HAKUNA MBUNGE AMBAYE AMEJITOKEZA WAZI KUPELEKA HOJA BINAFSI YENYE MASLAI JIMBONI KWAKE ADI SASA, WENGI BADALA YA KUWATUMIKIA WANACHI MAJIMBONI WAMAJIKITA KUPATA SIFA BUNGENI TU,
NAWAKUMBUSHA,ILI BAADA YA KUONA LEO WABUNGE WENGI AKILI ZAO ZIMEJIKITA KWENYE MATANGAZO YA BUNGE AUBUHI KWA KINGEZO CHA WANANCHI KUWAPA HAKI YAO KURIKO WAO KUTOKUTIMIZA HAKI HIYO YA KUWATUMIKIA IPASAVYO WANANCHI,
MAREHEMU
DEO FILIPO LUNJOMBE ALIYEKUWA MBUNGE WA LUDEWA ALIKUWA MBUNGE MWENYE KUJILIKANA SANA NA HESHIMA KUBWA ALIYOIPATA KWA KUFANYA KAZI NA KUWATUMIKIA WANANCHI WAKE JIMBONI KURIKO KUTENGEMEA UMAARUFU WA KWENYE TV ,USIO NA FAIDA KWA WANANCHI MASIKINI,
WABUNGE WOTE ACHANA NA SIFA ZA KWENYE TV JIFUNZE KWA DEO,
 
....leo umenichekesha sana aisee!!!

Penye ukakasi ni hapo kwenye "idol" nadhani urekebishe ulikuwa unamaanisha "idle".

But all in all watz kwa sasa wanapelekwapelekwa kama circus wakisubiri matukio mara tezi dume, mara Eritrea...and the list is long. Fanyeni kazi, tafuteni hobby kama anavyoshauri mdau hapo, kama ni kutazama bunge nenda dodoma kabisa! Ila hii tabia ya kuwa cry babies kutaka TV iwashwe mpate cha kuongea itatumaliza!

Waingereza walituharibu sana, tumekuwa wazungumzaji kuliko kuwa watendaji, jambo dogo linakuzwa kuwa kubwaaa...ndio maana EPL ina publicity kuubwa wakati hamna talent kiivyo ni hichi kihulka cha kuwa na uzungumzaji zaidi ya kuwekeza kwenye the actual work.


Nimeshabadilisha asante kwa kunisahihisha!
 
Huyu waziri nayeye ni jipu linalo hitaji kutumbuliwa. Yeye awewaangalia zaidi watu wachache wa mjini na wenye TV , je itakuwaje yule raia wa kijijini saa mbili ama saa mbili ama saa tatu usiku amekuwa amelala kwa uchovu wa jembe la mkono. Napia raia wengi wa vijijini wanategemea TV kwa jirani huenda wakakosa haki yao ya kupata habari. Hongera chichim kwa weredi wenu.
 
Uko sahihi mkuu lakini pia Kuna mihimili mitatu.kuna Bunge,mahakama,na SERIKALI.Hiyo TV ni mali ya Serikali sio ya bunge.Huwezi lazimisha mali za muhimili mwingine zitumikaje na muhimili mwingine.TBC hawalazimiki kisheria kurusha mijadala ya bunge.
na alivyoagiza Pesa za sherehe za Bunge zikanunue vitanda hakuingilia mhimili mwingine!?
 
ccm ni waoga sana , wameona ni bora kurusha Harusi kuliko vikao vya bunge !
 
Tutakuwa tunaangalia kupitia stations zingine zinazoweza kwenda bungeni kutafuta matangazo otherwise napo wawakataze.
Tired of this Napeeee😡😡😡😡😡
 
Kweli tunaisoma namba,huu ni udikteta wa hali ya Juu..
huu ni udikteta unasema ??? bilioni zote hizo si bora wapeleke watoto wetu wasome bure zaidi. mnasahau kwamba hapa ni kazi tu. hakuna siasa sahiz. siasa zitarudi tena mwaka 2020. watchout! !
 
Katika kauli za Mawaziri, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye, ametangaza kwamba, Kuanzia tarehe 26 Januari mwaka 2016, TBC1 haitaonesha tena Mikutano ya bunge live kutokana na gharama za kuonesha live kufikia bilioni nne kwa mwaka.

Badala yake TBC1 watarekodi na kuonesha katika kipindi maalum usiku kuanzia saa nne hadi saa tano.

Hii itanyima wanchi fursa ya kuona kinachoendelea Bungeni.
=========



Mheshimiwa spika,
Naomba kutoa kauli ya serikali kuhusu TBC kutangaza moja kwa moja vikao vya majadiliano ya bunge. Mheshimiwa spika, shirika la utangazaji Tanzania, TBC lilianza kurusha moja kwa moja matangazo ya vikao vya bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania mwaka 2005. Kabla ya kuanza kurusha moja kwa moja, TBC wakati huo televisheni ya taifa ilikuwa inarekodi matukio yote ya bunge na kurusha usiku katika vipindi maalumu vilivyojulikana kama bungeni leo kwa maana ya yaliyojiri ndani ya bunge kwa siku husika.

Baada ya kuanza kwa utaratibu wa kuanza kurusha matangazo moja kwa moja mwaka 2005, gharama za kufanya kazi hio zimekua zikipanda kwa kasi hadi kufikia Tshs. bilioni 4.2 kwa mwaka kwa maana ya mikutano minne ya bunge.

Shirika limekuwa likigharamia kwa sehemu kubwa matangazo hayo kwa kutumia mapato yake yanayotokana na matangazo madogo madogo ya biashara, ifahamike kuwa asilimia 75 ni vipindi vingi vinavyolenga kutoa elimu kwa umma na asilimia 25 ni burudani.

Mheshimiwa spika, kutokana na hali hii, TBC imeona ni busara kubadilisha mfumo wa utangazaji wa shughuli za bunge ili kukabiliana na kupanda kwa gharama za uendeshaji, hivyo basi, TBC imeona ni busara kuanzia mkutano huu wa bunge iwe inarusha baadhi ya matangazo ya bunge moja kwa moja yaani live ikiwa ni njia ya kubana matumizi.

Chini ya utaratibu huu, TBC itahakikisha kuwa, baadhi ya matukio ya matukio ya bunge yatarushwa moja kwa moja na mengine kurekodiwa na kuandaliwa kipindi maalum kitakachoitwa leo katika bunge. Kipindi hiki kitakua na mambo yote muhimu yaliyojiri ndani ya bunge kwa siku husika. Kipindi hichi kitakuwa kinarushwa kuanzia saa nne usiku hadi saa tano usiku.

Na mheshimiwa spika kipindi hicho kimeanza jana na tayari baadhi ya wananchi wameonyesha kuridhishwa na utaratibu huu na kuwa na kipindi maalum usiku kikishughulikia shughuli za bunge, mheshimiwa spika, uamuzi huu utapunguza gharama za uendeshaji wa shirika na pia kupitia kipindi cha leo katika bunge, watanzania walio wengi watapata nafasi ya kufahamu yaliyojiri bungeni kwani wakati bunge linaendelea mijadala yake, watanzania walio wengi huwa wanakua na kazi za kiofisi au zingine za ujenzi wa taifa kwa mahali walipo.

Mheshimiwa spika nakushukuru.

Kikwete aliwadekeza sana. sasa ngoja muone upande wa pili wa shilingi.
 
NAYASEMA HAYA BAADA YA KUGUNDUA WATANCHI TUNAKOSEA KUWACHAGUA WAWAKILISHI WETU BUNGE ,TUNACHAGUA MAVUVUZELA BUNGENI NA WANAOTAFUTA KUONEKANA BUNGENI ILI KUPATA UMAARUFU MAJIMBONI BADALA YA KUWATUMIKIA WANANCHI,
USHAIDI UPO
MFANO HAKUNA MBUNGE AMBAYE AMEJITOKEZA WAZI KUPELEKA HOJA BINAFSI YENYE MASLAI JIMBONI KWAKE ADI SASA, WENGI BADALA YA KUWATUMIKIA WANACHI MAJIMBONI WAMAJIKITA KUPATA SIFA BUNGENI TU,
NAWAKUMBUSHA,ILI BAADA YA KUONA LEO WABUNGE WENGI AKILI ZAO ZIMEJIKITA KWENYE MATANGAZO YA BUNGE AUBUHI KWA KINGEZO CHA WANANCHI KUWAPA HAKI YAO KURIKO WAO KUTOKUTIMIZA HAKI HIYO YA KUWATUMIKIA IPASAVYO WANANCHI,
MAREHEMU
DEO FILIPO LUNJOMBE ALIYEKUWA MBUNGE WA LUDEWA ALIKUWA MBUNGE MWENYE KUJILIKANA SANA NA HESHIMA KUBWA ALIYOIPATA KWA KUFANYA KAZI NA KUWATUMIKIA WANANCHI WAKE JIMBONI KURIKO KUTENGEMEA UMAARUFU WA KWENYE TV ,USIO NA FAIDA KWA WANANCHI MASIKINI,
WABUNGE WOTE ACHANA NA SIFA ZA KWENYE TV JIFUNZE KWA DEO,
Kumbuka deo ,unaye mjua leo ni kwasababu kipindi chake cha.yale aliyokuwa anafanya bungeni yalirushwa live
 
Back
Top Bottom