TCRA yatolea ufafanuzi sheria ya umiliki wa laini moja iliyoanza kutumika leo

TCRA yatolea ufafanuzi sheria ya umiliki wa laini moja iliyoanza kutumika leo

Hatari sana na mwaka huu wa uchaguzi TCRA ndo wanaamka wakati bado wana usingizi
 
... yaani kila mwaka haya majamaa lazima yapigishe watanzania foleni hadi inakera! Ndani ya miaka hii mitano hatujawahi kupumua mifoleni yahusianayo na simu/SIM card!

Kwamba leo ndio kwanza umeona sheria ya aina hii ilipitishwa na Bunge sio wewe tu; tuko wengi mimi ni juzi (3 days ago) niliona kwa mara ya kwanza humu humu JF. You know why? Bunge la gizani ndio matokeo yake haya.

You know why? Bunge la gizani ndio matokeo yake haya
 
Sheria ya umiliki wa laini moja ya simu kwa kila mtandao imeanza kutumika leo Julai Mosi 2020 ambapo ndio siku ya kwanza ya mwaka wa fedha wa serikali.

Hata hivyo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuwa sheria hiyo haimzuii mtu kumiliki laini zaidi ya moja kwa mtandao mmoja, isipokuwa atalazimika kutolea ufafanuzi laini ya ziada, na kwamba lengo la sheria hiyo ni kudhibiti umiliki holela wa laini za simu na kudhibiti uhalifu.

“Kuna wengine wanasajili [laini zaidi ya moja] kwa ajili ya matumizi ya biashara au majumbani, hivyo huwezi kuwafunga kwa kuwaambia wamiliki laini moja,” amenukuliwa Msemaji wa TCRA, Semu Mwakyanjala wakati akizungumza na Gazeti la Mwananchi.

Kifungu cha 18 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, sheria ya usajili wa laini za simu ya mwaka 2020 inaeleza kuwa mtu anatakiwa kumiliki laini moja ya simu kwa mtandao kwa ajili ya matumizi ya kupiga, kutuma jumbe na huduma za intaneti.

Sheria hiyo inaeleza kuwa mtu atakayemiliki laini zaidi ya moja kwa mtandao kinyume cha sheria atatozwa faini ya TZS 5 milioni au kifungo jela kwa miezi 12 au vyote kwa pamoja.

Na katika kila siku ambayo laini ya ziada ilitumika mhusika atalipa faini ya TZS 75,000 kwa siku.

Aidha, sheria hairuhusu kampuni kumiliki laini zaidi ya 30 ambazo zitatumika katika kupiga, kutuma jumba au huduma ya intaneti. Endapo kampuni itakiuka sheria hiyo, itatozwa faini isiyopungua TZS 50 milioni pamoja na TZS 175,000 kwa kila siku ambayo laini za/ya ziada ilitumika.

Wananchi kupitia mitandao ya kijamii wameonekana kuilalamikia sheria hiyo ambayo baadhi wamedai kuwa inaminya uhuru wao.

View attachment 1494501
View attachment 1494502

Pia soma > Ukimiliki laini zaidi ya moja ya mtandao mmoja utalipa faini Tsh 5M au kufungwa gerezani kwa miezi 12 au vyote kwa pamoja kuanzia 1 Julai, 2020

Naheshimu sana wasomi na wataalamu wetu lakini kuna baadhi ya maamuzi yananifanya nitilie mashaka weledi wao.

Kwanza, kuna sababu gani ya msingi mtu kuzuiwa kumiliki line zaidi ya moja iwe tu kwa mtandao mmoja? Kama suala ni kudhibiti watu kuwa na laini nyingi, kwa nini waruhusiwe kumiliki line nyingine za mitandao mingine?
Ikiwa mantiki ni kuwa na line moja kwa matumizi ya kupiga, message na data - basi hawakutakiwa kujali ni mtandao gani. Ama sivyo, basi kuna uwezekano mtu kusajili mtandao A kwa matumizi binafsi, na mtandao B na C kwa uhalifu.

Pamoja na hayo yote, suala la kuzuia uhalifu kwa kukataza watu kusajili line zaidi ya moja HALINA MANTIKI. Zoezi la kusajili, tena kwa kutumia kitambulisho cha taifa, linatosha kabisa kuwa na taarifa sahihi za mtu pasipo kujali amesajili line ngapi.

Kama kuna sheria kali ambayo TCRA walipaswa kuweka ni kukataza mtu kutumia kitambulisho chake kusajili line ambayo haitumii yeye. Hapo wangeweza kuweka namna ya watu kuona vitambulisho vyao vimesajili namba zipi na kuweka jukumu kwa raia kuhakikisha wanatoa ripoti pale wanapobaini kitambulisho chao kimetumika kusajili line zisizo zao.

Pili, idadi ya line 30 kwa kampuni imewekwa kwa kuzingatia nini? Kitu cha msingi sio namba ya line, ni utaratibu wa usajili. Kampuni zinatofautiana sana miundo yao na aina za biashara wanazofanya. Kwa mfano, siku hizi kuna mapinduzi makubwa kwenye sekta ya customer care. Kitengo tu cha customer care kinaweza kuwa na watu zaidi ya 30. Je, serikali inataka kuingingiza urasimu kwenye kusajili kila laini zitazoongezeka? Kwa nini kusiwe zisichukuliwe taarifa za kutosha wakati wa kusajili na suala la udhibiti wakaachiwa kampuni?
Kwa nini adhabu kali ya matumizi mabaya ya line isiwekwe juu ya kampuni iliyosajili ili kuhakikisha wanasimamia waajiriwa wao ipasavyo? Nani alikuja na hiyo 'magic number' 30?

Tatu, ikiwa TCRA wanataka nieleze matumizi yangu ya line - kwa nini wasiweke hilo swali wakati wa usajili? Mtu akiwa anasajili angeweza kuchagua baina ya 'mawasiliano binafsi', 'biashara', 'simu ya nyumbani', 'kifaa cha electroniki' na kadhalika. Kuna ulazima gani ya kuweka urasimu wa kujaza maelezo baadae ikiwa yangeweza kuchukuliwa wakati wa usajili? Je, TCRA wana watu wa kutosha kupitia maelezo yetu sote? - Kutakuwa na mabaraza ya kukubali ama kukataa maelezo?

Matumizi ya line za simu ni muingiliano wa mambo mengi ikiwemo uhuru wa watu kuwasiliana na kuchagua njia ya mawasiliano, biashara ya baina makampuni ya simu na kwa ujumla kutafuta namna ya kurahisisha maisha, biashara na maendeleo. Udhibiti ni jambo jema maana ni kweli kuna watu wanania ya kutumia mitandao vibaya. Lakini njia za udhibiti zisisababishe urasimu usio na sababu, zisilazimishe watu kutumia mitandao wasiochagua na wala zisionyeshe muelekeo wa kuingilia biashara huria za makampuni ya simu.
Kitambulisho cha NIDA ni njia sahihi ya kusajili line za simu. Tena kwa kutumia fingerprint, inakupa uhakika kuwa ni lazima mwenye kitambulisho mwenyewe alikuwepo siku ya usajili. Serikali iangalie mapungufu machache iyafanyie kazi - isianze kutapa tapa na utitiri wa sheria, matakwa na urasimu ikidhani kwamba ndio njia ya kuboresha kumbe inaharibu.
Tuendelee na NIDA inatosha sana, na sio kwenye simu tu na hata mahala pengine pote. Tukianza leo kutapa tapa kama taifa lisilo na mwelekeo, kesho tutaamuru kila mwanachi awe na akaunti moja benki.
 
Naheshimu sana wasomi na wataalamu wetu lakini kuna baadhi ya maamuzi yananifanya nitilie mashaka weledi wao.

Kwanza, kuna sababu gani ya msingi mtu kuzuiwa kumiliki line zaidi ya moja iwe tu kwa mtandao mmoja? Kama suala ni kudhibiti watu kuwa na laini nyingi, kwa nini waruhusiwe kumiliki line nyingine za mitandao mingine?
Ikiwa mantiki ni kuwa na line moja kwa matumizi ya kupiga, message na data - basi hawakutakiwa kujali ni mtandao gani. Ama sivyo, basi kuna uwezekano mtu kusajili mtandao A kwa matumizi binafsi, na mtandao B na C kwa uhalifu.

Pamoja na hayo yote, suala la kuzuia uhalifu kwa kukataza watu kusajili line zaidi ya moja HALINA MANTIKI. Zoezi la kusajili, tena kwa kutumia kitambulisho cha taifa, linatosha kabisa kuwa na taarifa sahihi za mtu pasipo kujali amesajili line ngapi.

Kama kuna sheria kali ambayo TCRA walipaswa kuweka ni kukataza mtu kutumia kitambulisho chake kusajili line ambayo haitumii yeye. Hapo wangeweza kuweka namna ya watu kuona vitambulisho vyao vimesajili namba zipi na kuweka jukumu kwa raia kuhakikisha wanatoa ripoti pale wanapobaini kitambulisho chao kimetumika kusajili line zisizo zao.

Pili, idadi ya line 30 kwa kampuni imewekwa kwa kuzingatia nini? Kitu cha msingi sio namba ya line, ni utaratibu wa usajili. Kampuni zinatofautiana sana miundo yao na aina za biashara wanazofanya. Kwa mfano, siku hizi kuna mapinduzi makubwa kwenye sekta ya customer care. Kitengo tu cha customer care kinaweza kuwa na watu zaidi ya 30. Je, serikali inataka kuingingiza urasimu kwenye kusajili kila laini zitazoongezeka? Kwa nini kusiwe zisichukuliwe taarifa za kutosha wakati wa kusajili na suala la udhibiti wakaachiwa kampuni?
Kwa nini adhabu kali ya matumizi mabaya ya line isiwekwe juu ya kampuni iliyosajili ili kuhakikisha wanasimamia waajiriwa wao ipasavyo? Nani alikuja na hiyo 'magic number' 30?

Tatu, ikiwa TCRA wanataka nieleze matumizi yangu ya line - kwa nini wasiweke hilo swali wakati wa usajili? Mtu akiwa anasajili angeweza kuchagua baina ya 'mawasiliano binafsi', 'biashara', 'simu ya nyumbani', 'kifaa cha electroniki' na kadhalika. Kuna ulazima gani ya kuweka urasimu wa kujaza maelezo baadae ikiwa yangeweza kuchukuliwa wakati wa usajili? Je, TCRA wana watu wa kutosha kupitia maelezo yetu sote? - Kutakuwa na mabaraza ya kukubali ama kukataa maelezo?

Matumizi ya line za simu ni muingiliano wa mambo mengi ikiwemo uhuru wa watu kuwasiliana na kuchagua njia ya mawasiliano, biashara ya baina makampuni ya simu na kwa ujumla kutafuta namna ya kurahisisha maisha, biashara na maendeleo. Udhibiti ni jambo jema maana ni kweli kuna watu wanania ya kutumia mitandao vibaya. Lakini njia za udhibiti zisisababishe urasimu usio na sababu, zisilazimishe watu kutumia mitandao wasiochagua na wala zisionyeshe muelekeo wa kuingilia biashara huria za makampuni ya simu.
Kitambulisho cha NIDA ni njia sahihi ya kusajili line za simu. Tena kwa kutumia fingerprint, inakupa uhakika kuwa ni lazima mwenye kitambulisho mwenyewe alikuwepo siku ya usajili. Serikali iangalie mapungufu machache iyafanyie kazi - isianze kutapa tapa na utitiri wa sheria, matakwa na urasimu ikidhani kwamba ndio njia ya kuboresha kumbe inaharibu.
Tuendelee na NIDA inatosha sana, na sio kwenye simu tu na hata mahala pengine pote. Tukianza leo kutapa tapa kama taifa lisilo na mwelekeo, kesho tutaamuru kila mwanachi awe na akaunti moja benki.

Hivi kuna vifaa vingine vinavyotumia laini za simu (sim card) zaidi ya simu za mkononi?
Je ni vifaa gani hivyo?
 
Hivi kuna vifaa vingine vinavyotumia laini za simu (sim card) zaidi ya simu za mkononi?
Je ni vifaa gani hivyo?
mi nnazo mashine kibao zipo site, zinatumia sim card, kuwasha/kuzima vifaa kwa sms
not to mention mita smart za maji, zinatumia sim card for internet access
 
Sheria ya umiliki wa laini moja ya simu kwa kila mtandao imeanza kutumika leo Julai Mosi 2020 ambapo ndio siku ya kwanza ya mwaka wa fedha wa serikali.

Hata hivyo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuwa sheria hiyo haimzuii mtu kumiliki laini zaidi ya moja kwa mtandao mmoja, isipokuwa atalazimika kutolea ufafanuzi laini ya ziada, na kwamba lengo la sheria hiyo ni kudhibiti umiliki holela wa laini za simu na kudhibiti uhalifu.

“Kuna wengine wanasajili [laini zaidi ya moja] kwa ajili ya matumizi ya biashara au majumbani, hivyo huwezi kuwafunga kwa kuwaambia wamiliki laini moja,” amenukuliwa Msemaji wa TCRA, Semu Mwakyanjala wakati akizungumza na Gazeti la Mwananchi.

Kifungu cha 18 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, sheria ya usajili wa laini za simu ya mwaka 2020 inaeleza kuwa mtu anatakiwa kumiliki laini moja ya simu kwa mtandao kwa ajili ya matumizi ya kupiga, kutuma jumbe na huduma za intaneti.

Sheria hiyo inaeleza kuwa mtu atakayemiliki laini zaidi ya moja kwa mtandao kinyume cha sheria atatozwa faini ya TZS 5 milioni au kifungo jela kwa miezi 12 au vyote kwa pamoja.

Na katika kila siku ambayo laini ya ziada ilitumika mhusika atalipa faini ya TZS 75,000 kwa siku.

Aidha, sheria hairuhusu kampuni kumiliki laini zaidi ya 30 ambazo zitatumika katika kupiga, kutuma jumba au huduma ya intaneti. Endapo kampuni itakiuka sheria hiyo, itatozwa faini isiyopungua TZS 50 milioni pamoja na TZS 175,000 kwa kila siku ambayo laini za/ya ziada ilitumika.

Wananchi kupitia mitandao ya kijamii wameonekana kuilalamikia sheria hiyo ambayo baadhi wamedai kuwa inaminya uhuru wao.

View attachment 1494501
View attachment 1494502

Pia soma > Ukimiliki laini zaidi ya moja ya mtandao mmoja utalipa faini Tsh 5M au kufungwa gerezani kwa miezi 12 au vyote kwa pamoja kuanzia 1 Julai, 2020

Ni makosa kwetu wananchi kutoshirikishwa kwenye utungaji sheria wao wakishakaa utunga Sheria na kutuletea,wasiwe na dhana moja tu ya uhalifu twajua wawasaka wakosoaji mhalifu mwenye nia ya uhalifu hazuiliki kwa kumiliki line moja pekee.
Waweke wazi hayo maelezo ya kutaka kumiliki zaidi ya line moja wanayatolea wapi TCRA,polisi, kampuni za simu
 
Laini zaidi ya moja inaweza kuwa fursa kwa serikali,watwambie tu tutakuwa tunalipia kiasi gani kila mwezi ili waongeze mapato ,Kama laini ziko 500,000 na wao wakaamua kuchukua 1,000@ kila mwezi tayari watakuwa wameteneza mpunga wa kutoka 500,000,000 (Milioni mia tano kila mwezi)
 
Mimi naona mauzauza tu, alama ya vidole imemaliza kilakitu hapo niliwaunga mkono lakini hii ya line 1 kiukweli wamekurupuka inabd wafkrie tena
 
Wapuuzi sana sasa mbona kwenye sheria yenyewe hawajasema kama unatakiwa laini nyingine utolee ufafanuzi wa matumizi? Wakitaka kutunga visheria vyao vya hovyo wangekusanya maoni kutoka kada mbali mbali sio wanakurupuka kama "TAJIRI WA KIGOMA BROTHER K".
Sasa kama mpeleka sheria ni yule mama Jenista Mhagama mnadhani kuna kitu hapo au utopolo tu? Hili limama litakufa mdomo wazi.
 
Sheria ya umiliki wa laini moja ya simu kwa kila mtandao imeanza kutumika leo Julai Mosi 2020 ambapo ndio siku ya kwanza ya mwaka wa fedha wa serikali.

Hata hivyo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuwa sheria hiyo haimzuii mtu kumiliki laini zaidi ya moja kwa mtandao mmoja, isipokuwa atalazimika kutolea ufafanuzi laini ya ziada, na kwamba lengo la sheria hiyo ni kudhibiti umiliki holela wa laini za simu na kudhibiti uhalifu.

“Kuna wengine wanasajili [laini zaidi ya moja] kwa ajili ya matumizi ya biashara au majumbani, hivyo huwezi kuwafunga kwa kuwaambia wamiliki laini moja,” amenukuliwa Msemaji wa TCRA, Semu Mwakyanjala wakati akizungumza na Gazeti la Mwananchi.

Kifungu cha 18 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, sheria ya usajili wa laini za simu ya mwaka 2020 inaeleza kuwa mtu anatakiwa kumiliki laini moja ya simu kwa mtandao kwa ajili ya matumizi ya kupiga, kutuma jumbe na huduma za intaneti.

Sheria hiyo inaeleza kuwa mtu atakayemiliki laini zaidi ya moja kwa mtandao kinyume cha sheria atatozwa faini ya TZS 5 milioni au kifungo jela kwa miezi 12 au vyote kwa pamoja.

Na katika kila siku ambayo laini ya ziada ilitumika mhusika atalipa faini ya TZS 75,000 kwa siku.

Aidha, sheria hairuhusu kampuni kumiliki laini zaidi ya 30 ambazo zitatumika katika kupiga, kutuma jumba au huduma ya intaneti. Endapo kampuni itakiuka sheria hiyo, itatozwa faini isiyopungua TZS 50 milioni pamoja na TZS 175,000 kwa kila siku ambayo laini za/ya ziada ilitumika.

Wananchi kupitia mitandao ya kijamii wameonekana kuilalamikia sheria hiyo ambayo baadhi wamedai kuwa inaminya uhuru wao.

View attachment 1494501
View attachment 1494502

Pia soma > Ukimiliki laini zaidi ya moja ya mtandao mmoja utalipa faini Tsh 5M au kufungwa gerezani kwa miezi 12 au vyote kwa pamoja kuanzia 1 Julai, 2020
Mimi nina laini tatu za voda na zote zinatumika na hiyo milioni tano ya faini sina wakianza kukamata wambieni waanze na mimi maana hata mtaani huku maisha ni tait nikale vya bure
 
mi nnazo mashine kibao zipo site, zinatumia sim card, kuwasha/kuzima vifaa kwa sms
not to mention mita smart za maji, zinatumia sim card for internet access

Tuviorodheshe maana inaelekea wataalamu wa TCRA hawajui uwepo wa vifaa kama hivyo hata kushindwa kuwashauri wabunge wetu wakapitisha sheria hii ambayo inapitwa na wakati kabla haijaanza kutumika.
 
Tuviorodheshe maana inaelekea wataalamu wa TCRA hawajui uwepo wa vifaa kama hivyo hata kushindwa kuwashauri wabunge wetu wakapitisha sheria hii ambayo inapitwa na wakati kabla haijaanza kutumika.
wanajua fika, wametoa mwongozo hapo juu, kama unataka izo zengine ziwe online rasmi, ni kuwaandikia 'barua/ombi'
 
wanajua fika, wametoa mwongozo hapo juu, kama unataka izo zengine ziwe online rasmi, ni kuwaandikia 'barua/ombi'

Je kumiliki simu ya ziada kwa ajili kuwasiliana na nyumbani (makazi) kwangu nayo itahitaji barua/ombi ?
 
Sheria ya umiliki wa laini moja ya simu kwa kila mtandao imeanza kutumika leo Julai Mosi 2020 ambapo ndio siku ya kwanza ya mwaka wa fedha wa serikali.

Hata hivyo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuwa sheria hiyo haimzuii mtu kumiliki laini zaidi ya moja kwa mtandao mmoja, isipokuwa atalazimika kutolea ufafanuzi laini ya ziada, na kwamba lengo la sheria hiyo ni kudhibiti umiliki holela wa laini za simu na kudhibiti uhalifu.

“Kuna wengine wanasajili [laini zaidi ya moja] kwa ajili ya matumizi ya biashara au majumbani, hivyo huwezi kuwafunga kwa kuwaambia wamiliki laini moja,” amenukuliwa Msemaji wa TCRA, Semu Mwakyanjala wakati akizungumza na Gazeti la Mwananchi.

Kifungu cha 18 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, sheria ya usajili wa laini za simu ya mwaka 2020 inaeleza kuwa mtu anatakiwa kumiliki laini moja ya simu kwa mtandao kwa ajili ya matumizi ya kupiga, kutuma jumbe na huduma za intaneti.

Sheria hiyo inaeleza kuwa mtu atakayemiliki laini zaidi ya moja kwa mtandao kinyume cha sheria atatozwa faini ya TZS 5 milioni au kifungo jela kwa miezi 12 au vyote kwa pamoja.

Na katika kila siku ambayo laini ya ziada ilitumika mhusika atalipa faini ya TZS 75,000 kwa siku.

Aidha, sheria hairuhusu kampuni kumiliki laini zaidi ya 30 ambazo zitatumika katika kupiga, kutuma jumba au huduma ya intaneti. Endapo kampuni itakiuka sheria hiyo, itatozwa faini isiyopungua TZS 50 milioni pamoja na TZS 175,000 kwa kila siku ambayo laini za/ya ziada ilitumika.

Wananchi kupitia mitandao ya kijamii wameonekana kuilalamikia sheria hiyo ambayo baadhi wamedai kuwa inaminya uhuru wao.

View attachment 1494501
View attachment 1494502

Pia soma > Ukimiliki laini zaidi ya moja ya mtandao mmoja utalipa faini Tsh 5M au kufungwa gerezani kwa miezi 12 au vyote kwa pamoja kuanzia 1 Julai, 2020
Wakati tunaanza usajili hawakututangazi hilo la kutoa ufafanuzi na kwanani, anyway sheria hii ilipitishwa na wabunge wa CCM bila kuhoji.
 
Back
Top Bottom