TCRA yawafungia Wasafi FM kwa kutumia lugha za matusi

TCRA yawafungia Wasafi FM kwa kutumia lugha za matusi

TCRA imekifungia kituo cha utangazaji cha Wasafi Fm baada ya watangazaji wake na mgeni wao baba Levo kutumia lugha za matusi na zinazoudhi mbele ya jamii.

Mfano neno " msambwanda" linakarahisha

Kituo cha Wasafi hakitakuwa hewani kwa muda wa siku 7 kwa mujibu wa adhabu waliyopewa.


Maendeleo hayana vyama!
TCRA YAKIFUNGIA KITUO CHA WASAFI FM KWA SIKU 7
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekifungia kutoa huduma za utangazaji Kituo cha Redio cha Wasafi FM kwa muda wa siku saba kuanzia Septemba 12 hadi Septemba 18 mwaka huu
-
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kilaba amesema uamuzi huo umechukuliwa kutokana na kituo hicho kukiuka kanuni namba 11 ya Kanuni za Mawasiliano ya kielektroniki na Posta ya mwaka 2018 katika vipindi vya The Switch na Mashamsham
-
Aidha, Mkurugenzi huyo ametoa rai kwa Vyombo vya Habari kuzingatia kanuni za utangazaji wa maudhui yenye lugha ya staha kwa Watanzania huku akiitaka Wasafi FM kuomba radhi kwa Umma
 
Ila niliitazama kile kipindi kiukweli TCRA wanakahaki ya kufungia stesheni. Yaani kipindi kimekosa maudhui hadi basi.....

Baba levo aliulizwa swali kuwa kati ya mwanamke mnene mwenye shepu na wembamba ni yupi anapendelea....

Baba levo akajibu yeye wanawake wembamba asichowapendea ni wanachoka haraka kitandani halafu wanakuharakisha na wewe ukojoe haraka haraka, so yeye huwa anachofanya anawakojolea mkojo wa kawaida na sio bao lile la utamu.....




Katika hali ya kawaida mazungumzo ya namna hii hayana hadhi ya kurushwa hewani as if ni jambo la kawaida na wakati ni kinyume na maadili yetu ya kitanzania na kiafrika lakini mbaya zaidi inachochea maswala ya ngono.
Kama ni hivyo tcra wapo sawa, tena hiyo adhabu ya wiki 1 ni ndogo sana, shwain zao.
 
TCRA imekifungia kituo cha utangazaji cha Wasafi Fm baada ya watangazaji wake na mgeni wao baba Levo kutumia lugha za matusi na zinazoudhi mbele ya jamii.

Mfano neno " msambwanda" linakarahisha

Kituo cha Wasafi hakitakuwa hewani kwa muda wa siku 7 kwa mujibu wa adhabu waliyopewa.


Maendeleo hayana vyama!
Wanazuga tu ili ionekane kuna haki....laanaturahi
 
View attachment 1566500
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesitisha utoaji huduma za utangazaji kwa Wasafi FM kwa muda wa siku saba kuanzia Septemba 12 hadi Septemba 18 mwaka huu.

Uamuzi huo umetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kilaba jijini Dar es Salaam ambapo amesema hatua hiyo ni kutokana na kituo hicho kukiuka kanuni namba 11 ya Kanuni za Mawasiliano ya kielektroniki na Posta ya mwaka 2018.

Mhandisi Kilaba amesema kuwa ukiukwaji huo wa kanuni ulifanyika katika vipindi vya The Switch na Mashamsham.

Aidha, ametoa rai kwa vyombo vya habari kuzingatia kanuni za utangazaji wa maudhui yenye lugha ya staha kwa Watanzania huku akiitaka Wasafi FM kuomba radhi kwa umma wa Watanzania.
Mwendo wa kabali.
 
Kwa hili TCRA wanastahili pongezi,kumekuwa na lugha za kuudhi zisizo na staha ambazo zinatolewa baadhi ya watangazaji.Napendekeza adhabu iwe kubwa zaidi,swala la maadili lazima kuwa wakali zaidi.
 
IS JAMII FORUMS STILL WHERE WE DARE TO TALK OPENLY???
 
Ila kweli hapa wamezingua, Serious

WCB Mnaleta waongeaji ongeaji tu wasiofuata weledi wa kazi
Mnaambiwa muajiri watangazaji wasomi nyie mnasemaa oooh haina haja

Huyu baba levo kazingua big time, anafikiri studio hapo wanapiga soga kama za vijiweni...kuna maneno yanatakiwa yasiende On Air, wayaongee Off mic
Baba Levo nae anaropokaga ropokaga hovyo tu, siridhishwi na aina yake ya utangazaji hasa ya kuropoka bila kupangilia maneno

Katuponza sisi wasikilizaji wa vipindi vya michezo #SportsArena na #SportsCourt


[emoji35][emoji35][emoji35][emoji35]

Mondi na Dabiliyusibii wajitafakari hiii aina ya watangazaji wanaowaleta.. Sio kila mzungumzaji au anayeongea ongea tu na kwa kuwa ni maarufu basi ana kipaji cha kutangaza...Mambo ya kufosi vipaji tuyaacheni twendeni kwenye Weledi wa kazi...

Uandishi wa habari na utangazaji una ethics zake
 
Kwa hili TCRA wanastahili pongezi,kumekuwa na lugha za kuudhi zisizo na staha ambazo zinatolewa baadhi ya watangazaji.Napendekeza adhabu iwe kubwa zaidi,swala la maadili lazima kuwa wakali zaidi.
Kuna maneno fulanifulani ya Kisukuma ni matusi ya nguoni kwa lugha yetu kwa hiyo Rais wetu mpendwa anapohutubia kilugha tukiwepo au kwenye vyombo vya Habari tunadhalilika sana na kumwona hana maadili. TCRA waangalie hili.
 
Ila kweli hapa wamezingua, Serious

WCB Mnaleta waongeaji ongeaji tu wasiofuata weledi wa kazi
Mnaambiwa muajiri watangazaji wasomi nyie mnasemaa oooh haina haja

Huyu baba levo kazingua big time, anafikiri studio hapo wanapiga soga kama za vijiweni...kuna maneno yanatakiwa yasiende On Air, wayaongee Off mic
Baba Levo nae anaropokaga ropokaga hovyo tu

Katuponza wasikilizaji wa vipindi vya michezo #SportsArena na #SportsCourt


[emoji35][emoji35][emoji35][emoji35]

Mondi na Dabiliyusibii wajitafakari hiii aina ya watangazaji wanaowaleta.. Sio kila mzungumzaji au anayeongea ongea tu na kwa kuwa ni maarufu basi ana kipaji cha kutangaza...Mambo ya kufosi vipaji tuyaacheni twendeni kwenye Weledi wa kazi...

Uandishi wa habari na utangazaji una ethics zake
Jose tafuta mabilioni na wewe ufungue chako!
 
Back
Top Bottom