TCU rudisheni mfumo wa kudahili wanafunzi vyuoni kwa njia ya mtandao (CAS)

TCU rudisheni mfumo wa kudahili wanafunzi vyuoni kwa njia ya mtandao (CAS)

Kwanza unawatengenezea hao watoto tatizo ambalo hawana na hawajaliona kama ni kero kwao.
Alafu unaishia kusema kuna Udini, ukabila na Rushwa bila kusema wazi ni wapi hapo kwenye hayo mambo.
Hiyo ni Kazi ya TCU kufanya evaluation ya uhahiri kwenye vyuo vyake. Ifanye utafiti wa kupata idadi ya watoto wote walioomba kudahiriwa kwenye kila chuo Na ufaulu wao Na wale waliodahiriwa Na ufaulu wao ili kujua kama kulikuwa Na walioachwa wenye ufaulu mkubwa kuliko ule wa waliodahiriwa katika kila kozi kila chuo. Mimi ni whistle blower tu kaka unanionea kuniomba nikwambie nani kafanya nini.
 
Mtoa mada unauumiza moyo wangu katika jambo alilolifanya mwendazake la maaana ni pamoja.na hili mimi huo mfumo ulinipeleka IFM na niliweka last option na nichuo ambacho nilikua sikipendi imesababisha mpaka nisimalize degree yangu yan huu mfumo mpya mzuri sanaaa najutaaa yan bora huu mfumo mpya ningeenda kusoma chuo cha ndoto yangu UDSM
Mkuu hapa tatizo sio CAS bali ni wewe mwenyewe, umejaza option ambayo huipendi. Wao wanajua umeipenda na wamekupa. Hili ni tatizo la wengi waolalamika hawajui nini wanataka.
 
Hiyo ni Kazi ya TCU kufanya evaluation ya uhahiri kwenye vyuo vyake. Ifanye utafiti wa kupata idadi ya watoto wote walioomba kudahiriwa kwenye kila chuo Na ufaulu wao Na wale waliodahiriwa Na ufaulu wao ili kujua kama kulikuwa Na walioachwa wenye ufaulu mkubwa kuliko ule wa waliodahiriwa katika kila kozi kila chuo. Mimi ni whistle blower tu kaka unanionea kuniomba nikwambie nani kafanya nini.
Vyuo vikisha fanya selection hupeleka majina ya waliomba wote na tcu hupitia kuona kama waliochaguliwa wastahili na kama waloachwa kweli wameachwa kihalali.
 
Wale wa zamani watakuwa wanakumbuka, yaani unaomba chuo zaidi ya kimoja, na majibu yanakuja "Multiple Selection", una confirm chuo kimoja maisha yanaendelea, na HESLB wanakufuata huko huko ulipo-confirm.

Kule kwenye chuo kingine, nafasi inajazwa kwa second selection.

Tuache ujanja ujanja wa kutaka kuwahonga TCU ili chuo kipate wanafunzi wengi.

Napinga kwa nguvu zote mwanafunzi kupangiwa chuo na TCU.

Pamoja na mapungufu ya jiwe, ila kwenye hili ntaendelea kumuunga mkono.
Ki ukweli CAS haipangii mtu chuo. Kilicho kuwa kinatokea kuna wanafunzi ambao kutokana na ufaulu wao na chaguzi zao walikosa nafasi kabisa. Badala ya kuwaacha kabisa tcu iliwa nafasi waliko ona ufaulu wao unaendana nako, lakini kama mtu hapendi ana acha.
Jambo lingine CAS ni automated na haina multiple selections hakuna nafasi inayopotea.
 
Vyuo vikisha fanya selection hupeleka majina ya waliomba wote na tcu hupitia kuona kama waliochaguliwa wastahili na kama waloachwa kweli wameachwa kihalali.
We jamaa hiyo sio kweli, TCU wanahakiki kama waliochaguliwa wana at least the MINIMUM pass kwaajili ya kozi walizochaguliwa, lakini haingalii kwanini kwenye BBB kaachwa na kuchukuliwa mwenye CCD.
 
Mimi nilichaguliwa kulinga na hyo system ya CAS naona ilikuwa nzuri kuliko ya Sasa unaomba vyuo vitano na kila chuo na ada ya kuomba Mara kufanya ma verification plus usumbufu mwingi na gharama
 
"Sasa hivi wanafunzi lazima waombe wenyewe kwenye vyuo husika kwa gharama zao, hivyo mwanafuzi atalazimika kuomba vyuo zaidi ya kimoja kwa gharama za uombaji za kila chuo na chuo ndicho kinanachochagua wanafunzi wa kusoma kwenye chuo chao na kutuma majina TCU kwa uhakiki."

Tusidanganyane, mwanafunzi aombe chuo anachotaka na akasome huko huko.

Suala la kusema eti elimu za vyuo vikuu vinafanana huo ni uongo mkubwa! Elimu zinatofautiana kabisaa.

Je, kuna mzazi yoyote aliyelalamikia gharama kubwa za kuomba vyuo vingi?

Kila mhitimu ana vigezo vyake vya kuomba chuo, mwingine anataka aishi mkoa fulani kutokana na sababu zake, sasa akipangiwa mkoa mwingine na CAS si ni shida!

Ipo wazi, baada ya kufuta mfumo wa CAS, vyuo fulani vya ujanja ujanja vilianza kukosa wanafunzi, kw sababu wanafunzi walikuwa hawavitaki.

Baadhi ya vyuo vilitumia hila kupata idadi kubwa ya wanafunzi, na kuzima ndoto za wahitimu. CAS inampeleka kwenye kozi na chuo ambavyo hana interest nazo!

Toa elimu bora, matangazo kwa sana, utapata tu wanafunzi, usitegemee CAS ikubebe baada ya kuhonga TCU!
Hata Sasa hivi ka hauna cut off point za udsm hawakuchukui kabisa mzee licha ya kuomba vyuo vingi. So CAS ilikuwa system nzuri na rahisi
 
Mfumo wa CAS sii mzuri, ni wa kizamani. Hata ulaya hawafanyi ujinga huu.
TCU ni taasisi inayodhibiti ubora wa elimu ya juu. Inakagua, inashauri, inaruhusu Na kusimamisha au kufuta vyuo visivyokidhi vigezo vya ubora. Hivyo, vyuo vyote ambavyo vinatoa mafunzo vimefikia vigezo (minimum) vya ubora wa kumudu kutoa mafuzo yaliyokusudiwa. Ingawa ni kweli vyuo vinatofautiana kwa ubora.

TCU ndiyo yenye takwimu za vyuo vikuu vyote kuhusu kozi, ubora na idadi ya wanafunzi wanaoweza kudahiriwa kwenye kila chuo pamoja na ada inayotozwa kwa kila chuo.

Kabla ya kufutwa na Rais JPM wanafuzi walikuwa wanatuma maombi ya kujiunga vyuo vikuu kwa kutumia CAS kuchagua kozi na vyuo na mfumo huo wa udahiri ulikuwa na uwezo wa kumpangia mwanafuzi kozi aliyoomba kwenye chuo alichoomba kulingana na ufaulu wake na idadi ya walioomba kozi hiyo kwenye chuo hicho. Na kama nafasi kwenye chuo hicho imejaa mfumo ulikuwa ukimpeleka kwenye chuo kingine chenye nafasi bila usumbufu na gharama ya ziada kwa mwanafunzi.

Sasa hivi wanafunzi lazima waombe wenyewe kwenye vyuo husika kwa gharama zao, hivyo mwanafuzi atalazimika kuomba vyuo zaidi ya kimoja kwa gharama za uombaji za kila chuo na chuo ndicho kinanachochagua wanafunzi wa kusoma kwenye chuo chao na kutuma majina TCU kwa uhakiki.

Kufanya hivi kuna hasara zifuatazo:
1. Mwanafunzi anatumia hela nyingi kwenye maombi ya nafasi vyuoni.
2. Wanafuzi wanarundikana kwenye chuo kimoja wakati kuna nafasi kwenye vyuo vingine.
3. Unatoa nafasi ya wazazi kutoa rushwa kubwa vyuoni ili watoto wao wachaguliwe kozi fulani kwenye chuo fulani.
4. Baadhi ya vyuo vimepata nafasi ya kuwabagua wanafunzi wanaotoka kaya maskini wenye hela za kudunduliza kulipia karo kubwa za vyuo vyao.
5. Utaratibu unatoa mwanya kwa watendaji wa vyuo kuchagua ndugu zao, kabila na rafiki zao kupata nafasi ya kusoma chuoni kwao na kuwaacha watoto wengine wenye ufaulu mkubwa kuliko walioingizwa chuoni.
6. Mfumo unatoa mwanya wa UDINI kwenye selection. Anaechagua nani achaguliwe anaweza kusukumwa na vionjo vya udini na dhehebu lake kupatia nafasi kwanza watoto wa dini na dhehebu lake hata kama walioachwa wana ufaulu mkubwa kuliko waliopendelewa.

7. Vyuo vinadahiri kupita uwezo wao waliokadiriwa.

Faida zilizokusudiwa za utaratibu huu wa sasa ni moja tu, kuwa mwanafunzi atachagua chuo anachokitaka yeye. Lakini uzoefu unaonyesha kuwa hata kwenye utaratibu huu sio kweli kuwa wanafunzi wote wanachaguliwa kwenye vyuo walivyovitaka, bado wanaendelea kudahiriwa kwenye vyuo vyenye nafasi kama zamani baada ya kukosa nafasi kwenye vyuo wanavyovipenda.

Wanafunzi na wazazi wanadanganywa na majina ya vyuo kumbe elimu ni ileile hata kwa vyuo vingine.

Kudhibitisha ukweli huu TCU ipitie ufaulu wa wanafunzi wote walioomba kwenye vyuo ilinganishe na ufaulu wa wanafunzi wote waliodahiriwa kwenye vyuo wataogundua dhambi hii ya ubaguzi.
 
Mimi nilichaguliwa kulinga na hyo system ya CAS naona ilikuwa nzuri kuliko ya Sasa unaomba vyuo vitano na kila chuo na ada ya kuomba Mara kufanya ma verification plus usumbufu mwingi na gharama
Mfumo wa CAS sio mzuri hata kidogo. Sikudanganyi hata ulaya hawafanyi hivyo.
 
Mimi chagua langu la kwanza lilikuwa Hilo hilo
Sasa chuo kikuu sio sekondari kuanza kuchaguana tunaingia form one au five. Duniani kote mtu anachagua vyuo vyote anavyovipenda, kisha anafanya, maamuzi ya mwisho mwenyewe na sio kufanyiwa maamuzi ya kozi ya kusoma.
 
Sasa chuo kikuu sio sekondari kuanza kuchaguana tunaingia form one au five. Duniani kote mtu anachagua vyuo vyote anavyovipenda, kisha anafanya, maamuzi ya mwisho mwenyewe na sio kufanyiwa maamuzi ya kozi ya kusoma.
Ufaulu wako ndo muamuzi mkuu..hujipangii tu wewe na three yako ya PCB isiyokuwa na kichwa wala miguu kutaka kwenda kusoma MD Muhas.
 
Sasa chuo kikuu sio sekondari kuanza kuchaguana tunaingia form one au five. Duniani kote mtu anachagua vyuo vyote anavyovipenda, kisha anafanya, maamuzi ya mwisho mwenyewe na sio kufanyiwa maamuzi ya kozi ya kusoma.
Hata hyo system unachagua course unazoxitaka kulingana na ufaulu, cut off point na competition Sasa umepata three mbovu wataka kwenda udsm competition inakutupa kupeleka kwenye choice zako nyingine. TCU ilikuwa haikupangii course ambayo haujaomba.
 
Mfumo wa kuomba direct ni mzuri saana kwa 7bu
1... gharama ni uniform (10000) tu na kwingine free kabisa.
2... fursa ya kuomba course nyingi zaidi kuanziw 3 hadi 15 (udsm).
3... uhuru wa kuombaa vyuo upendavyoo.
4... kuondoa nentality ya chuo fulani ndio bora zaidi angali vyote viko under TCU guidelines, requlations
Kama unavifahamu vyuo vya Diploma Afya, Uhandisi au Ualimu ambavyo n bure. Nitajie plz
 
Back
Top Bottom