#COVID19 Teknolojia ya 5G na Chanzo cha Covid-19: Nadharia Njama (Conspiracy Theory) yenye maswali mengi

#COVID19 Teknolojia ya 5G na Chanzo cha Covid-19: Nadharia Njama (Conspiracy Theory) yenye maswali mengi

Binafsi sikubaliani na wewe kwa kiwango kikubwa juu ya argument yako hii...

Umeshindwa kuwataja hao unaowaita "manabii wa uongo" kwa majina. Lakini kwa hakika kabisa mmojawapo uliyemlenga ni Bishop Dr Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima...

Huyu ameshajitokeza hadharani na wa wazi na kumzungumzia mdudu - kirusi huyu aitwaye Korona kwa mantiki uliyoeleza hapa...

Katika maelezo ya Mch. Gwajima, sijaona mahali anapokataa kuwa janga la COVID-19 halipo....

Sijaona mahali ambapo Mch. Gwajima anawahimiza wafuasi wakristo wenzake wadharau na wasijikinge na virusi vya Corona....

Wala sijaona ktk maelezo yake yote iwapo Mch. Gwajima anapingana na maendeleo ya teknoljia ya mawasiliano ya 5G yenye nia njema kumwendeleza na kumsaidia binadamu katika utendaji wa shughuli zake za kila siku....

Maudhui ya maelezo ya Mch. Dr Gwajima yamejikita zaidi ktk kuwaelemisha wakristo juu ya ujanja wa binadamu wanaotumikia ulimwengu wa uovu kutumia mambo mazuri (mfano teknolojia ya mawasiliano ya 5G) tunayopewa na Mungu kwa ajili ya manufaa yetu ili kutekeleza ajenda zao ovu...za kuangamiza kizazi cha binadamu....

Lakini watu hawa waovu ambao tunaweza kuwaita mawakala wa shetani - baba wa uovu wanageuza kusudi jema la Mungu na kilipa sura ya ubaya ili tu wao waweze kutekeleza malengo na nia yao ovu dhidi ya uumbaji wa Mungu na kumwangamiza binadamu....

Hii mbinu ndugu zangu kwa sisi watu wa imani tunaelewa kuwa haijaanza ktk majira haya ya mlipuko wa COVID-19 tu.....

Imeanzia tangu enzi zile mara baada ya uumbaji wa Mungu kukamilika. Baada ya hapo Mungu akamuumba mtu (Adamu) ili atawale UUMBAJI huu. Kwa hiyo kusudi la Mungu kutuumba kwa "mfano wake" lilikuwa ni kumiliki na kutawala uumbaji wake kwa niaba yake.....

Wakati huohuo alikuwepo malaika aliyeasi enzi yake huko mbinguni na Mungu hakuwa na option nyingine isipokuwa kumwadhibu kwa kumtupa chini akiwa amenyang'anywa kila kitu kwa maana ya mamlaka ya umiliki na utawala wa uumbaji wa Mungu. Huyu ndiye shetani kwa tafsiri ya "mdanganyifu".....

Mamlaka ya umiliki na utawala ya uumbaji wa Mungu yakakabidhiwa kwetu binadamu....

Huyu muasi (Shetani) vita yake na Mungu inaendelea hadi leo na binadamu ndiye uwanja wa vita hii...

Ndiyo maana Mara baada ya Adamu na Hawa kukabidhiwa mamlaka ya utawala wa uumbaji wa Mungu pale Eden, shetani akiwa katika sura ya nyoka na kwa udanganyifu wa hali ya juu kwa kumtumia Hawa (Eva) mke wa Adam alifanikiwa kuupotosha UKWELI wa Mungu kuwa UONGO naye akauamini UONGO badala ya UKWELI .....

KWA mara ya kwanza binadamu akaasi maagizo ya muumba wake. Akawa chini ya utawala wa Shetani wa KIFO na MAUTI hadi miaka zaidi ya 2000 iliyopita alipokuja Yesu Kristo - Mungu mwenyewe ktk umbo la binadamu kuturejeshea tena mamlaka na utawala wetu binadamu dhidi ya uumbaji wa Mungu tulionyang'anywa na shetani pale Eden...

Hata hivyo vita hii si kwamba imeisha, bado inaendelea na walio upande wa Yesu Kristo wanaishinda kwa ukamilifu wake....

Hira na mbinu za shetani kuupumbaza ulimwengu (watu wa dunia) ni za hali ya juu sana kwa kutumia haya haya tunayoita maendeleo ya kisayansi na teknoljia....

Mungu wetu mwaminifu anatutia moyo kwa kutuambia

".....hamtakosa kuzitambua hila na fikra (mbinu na mikakati) zake (shetani)....."

Angalia historia ya matukio ya Kibiblia utagundua kuwa binadamu siku zote ni mgumu kuamini maelezo na maagizo rahisi kabisa ya wokovu wake toka kwa Mungu dhidi ya majanga mbalimbali yanayomnyemelea kumwangamiza ...

Mara zote binadamu huyu huyu hung'ang'ana na maarifa na akili zake kutaka kujiokoa na mwisho wake huangamia kabisa....

Hata nyakati za gharika, watumishi WA KWELI wa Mungu i.e Nuhu alipata changamoto hii hii alipokuwa anawaambia watu kujiandaa na wokovu kwa sababu dunia ilikuwa inakwenda kuangamizwa/kufutiliwa mbali kwa maji...

Nuhu alidharauliwa, alioonekana kama nabii tapeli aliyewataka watu kuchangia sadaka za ujenzi wa Safina ili ajipatie fedha tu....

Alionekana ni mtu asiyeweza kuthibitisha unabii/maelezo yake aliyoyapokea toka kwa Mungu kwa misingi ya sayansi ama maarifa ya kibinadamu.....

NB: Hata hivyo nakubaliana na wewe kwa kitu kimoja kuwa, ni kweli kabisa wapo manabii wa uongo ambao hutumia fursa kama hizi kupotosha watu

Lakini Mungu yuko kazini, akiwatumia watu (watumishi) wake waaminifu kuokoa watu wake kutoka katika hila za uangamivu za shetani

Mimi naaamini. Kwa Mungu ni KUAMINI TU. Hatutumii maarifa na akili na ujuzi wetu binafsi kujiokoa isipokuwa kwa NEEMA YAKE KRISTO...!!
 
Mkuu hii dunia ina mambo ya siri sana yanayoratibiwa na waabudu shetani, tutumie akili zetu kung'amua namna mchezo unavyoenda. Hii teknolojia ya 5G na hili gonjwa la korona inaweza kuwa turning point ya matukio makubwa zaidi duniani mengine yakawa ya kuogofya na kutia mashaka zaidi ya hili tunaloshuhudia kwa sasa la korona. Inawezekana ikawa mwanzo wa matukio ya kinabii yaliyoandikwa kuhusu mwisho wa hii sayari ya dunia.....
 
Ni kweli kabisa afrika tupo katika mkwamo mzito sana, tunaishi dunia ya copy and paste halafu wakati mwingine tunajifanya kujua kuliko wajuaji halisi.

Kuna Shekhe mmoja jirani yangu, yeye anasema COVID 19 ni matokeo ya dhambi za wakristo ndio kisa cha Italia na nchi za kikristo kuwa na vifo vingi, lakini akili ya kawaida tu ni kwamba MECCA mwaka huu hakuna waliokwenda kuhiji.

Israel imezifunga zile sehemu takatifu ambazo ni sehemu muhimu kwao katika kuingiza fedha za utalii, hili ni janga zito, halipaswi kuunganishwa na imani za kidini, kule Ujerumani wanakufa wapagani wengine tu.

Kuna nchi hazimwamini Mungu wa Biblia na Quran na hazina idadi kubwa ya wagonjwa wa Corona.
 
Binafsi sikubaliani na wewe kwa kiwango kikubwa juu ya argument yako hii...

Umeshindwa kuwataja hao unaowaita "manabii wa uongo" kwa majina. Lakini kwa hakika kabisa mmojawapo uliyemlenga ni Bishop Dr Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima...

Huyu ameshajitokeza hadharani na wa wazi na kumzungumzia mdudu - kirusi huyu aitwaye Korona kwa mantiki uliyoeleza hapa...

Katika maelezo ya Mch. Gwajima, sijaona mahali anapokataa kuwa janga la COVID-19 halipo....

Sijaona mahali ambapo Mch. Gwajima anawahimiza wafuasi wakristo wenzake wadharau na wasijikinge na virusi vya Corona....

Wala sijaona ktk maelezo yake yote iwapo Mch. Gwajima anapingana na maendeleo ya teknoljia ya mawasiliano ya 5G yenye nia njema kumwendeleza na kumsaidia binadamu katika utendaji wa shughuli zake za kila siku....

Maudhui ya maelezo ya Mch. Dr Gwajima yamejikita zaidi ktk kuwaelemisha wakristo juu ya ujanja wa binadamu wanaotumikia ulimwengu wa uovu kutumia mambo mazuri (mfano teknolojia ya mawasiliano ya 5G) tunayopewa na Mungu kwa ajili ya manufaa yetu ili kutekeleza ajenda zao ovu...za kuangamiza kizazi cha binadamu....

Lakini watu hawa waovu ambao tunaweza kuwaita mawakala wa shetani - baba wa uovu wanageuza kusudi jema la Mungu na kilipa sura ya ubaya ili tu wao waweze kutekeleza malengo na nia yao ovu dhidi ya uumbaji wa Mungu na kumwangamiza binadamu....

Hii mbinu ndugu zangu kwa sisi watu wa imani tunaelewa kuwa haijaanza ktk majira haya ya mlipuko wa COVID-19 tu.....

Imeanzia tangu enzi zile mara baada ya uumbaji wa Mungu kukamilika. Baada ya hapo Mungu akamuumba mtu (Adamu) ili atawale UUMBAJI huu. Kwa hiyo kusudi la Mungu kutuumba kwa "mfano wake" lilikuwa ni kumiliki na kutawala uumbaji wake kwa niaba yake.....

Wakati huohuo alikuwepo malaika aliyeasi enzi yake huko mbinguni na Mungu hakuwa na option nyingine isipokuwa kumwadhibu kwa kumtupa chini akiwa amenyang'anywa kila kitu kwa maana ya mamlaka ya umiliki na utawala wa uumbaji wa Mungu. Huyu ndiye shetani kwa tafsiri ya "mdanganyifu".....

Mamlaka ya umiliki na utawala ya uumbaji wa Mungu yakakabidhiwa kwetu binadamu....

Huyu muasi (Shetani) vita yake na Mungu inaendelea hadi leo na binadamu ndiye uwanja wa vita hii...

Ndiyo maana Mara baada ya Adamu na Hawa kukabidhiwa mamlaka ya utawala wa uumbaji wa Mungu pale Eden, shetani akiwa katika sura ya nyoka na kwa udanganyifu wa hali ya juu kwa kumtumia Hawa (Eva) mke wa Adam alifanikiwa kuupotosha UKWELI wa Mungu kuwa UONGO naye akauamini UONGO badala ya UKWELI .....

KWA mara ya kwanza binadamu akaasi maagizo ya muumba wake. Akawa chini ya utawala wa Shetani wa KIFO na MAUTI hadi miaka zaidi ya 2000 iliyopita alipokuja Yesu Kristo - Mungu mwenyewe ktk umbo la binadamu kuturejeshea tena mamlaka na utawala wetu binadamu dhidi ya uumbaji wa Mungu tulionyang'anywa na shetani pale Eden...

Hata hivyo vita hii si kwamba imeisha, bado inaendelea na walio upande wa Yesu Kristo wanaishinda kwa ukamilifu wake....

Hira na mbinu za shetani kuupumbaza ulimwengu (watu wa dunia) ni za hali ya juu sana kwa kutumia haya haya tunayoita maendeleo ya kisayansi na teknoljia....

Mungu wetu mwaminifu anatutia moyo kwa kutuambia

".....hamtakosa kuzitambua hila na fikra (mbinu na mikakati) zake (shetani)....."

Angalia historia ya matukio ya Kibiblia utagundua kuwa binadamu siku zote ni mgumu kuamini maelezo na maagizo rahisi kabisa ya wokovu wake toka kwa Mungu dhidi ya majanga mbalimbali yanayomnyemelea kumwangamiza ...

Mara zote binadamu huyu huyu hung'ang'ana na maarifa na akili zake kutaka kujiokoa na mwisho wake huangamia kabisa....

Hata nyakati za gharika, watumishi WA KWELI wa Mungu i.e Nuhu alipata changamoto hii hii alipokuwa anawaambia watu kujiandaa na wokovu kwa sababu dunia ilikuwa inakwenda kuangamizwa/kufutiliwa mbali kwa maji...

Nuhu alidharauliwa, alioonekana kama nabii tapeli aliyewataka watu kuchangia sadaka za ujenzi wa Safina ili ajipatie fedha tu....

Alionekana ni mtu asiyeweza kuthibitisha unabii/maelezo yake aliyoyapokea toka kwa Mungu kwa misingi ya sayansi ama maarifa ya kibinadamu.....

NB: Hata hivyo nakubaliana na wewe kwa kitu kimoja kuwa, ni kweli kabisa wapo manabii wa uongo ambao hutumia fursa kama hizi kupotosha watu

Lakini Mungu yuko kazini, akiwatumia watu (watumishi) wake waaminifu kuokoa watu wake kutoka katika hila za uangamivu za shetani

Mimi naaamini. Kwa Mungu ni KUAMINI TU. Hatutumii maarifa na akili na ujuzi wetu binafsi kujiokoa isipokuwa kwa NEEMA YAKE KRISTO...!!

Mpendwa Kitaturu, kwa kuwa umeongea kwa uzito sana na kumtaja mtu/mtumishi kwenye maelezo yako, naomba nikujibu ili kuweka rekodi sawa na tusipotoshe mada.

Moja, nashukuru sana kwa mawazo yako na kutupa summary ya kazi ya ukombozi. Kwa bahati nzuri kwangu, huwa najitahidi sana kutojadili watu kwenye umma (public) kama sio lazima kufanya hivyo. Naweza kujadili hoja zao bila hata kurejea majina yao lakini sio kuwajadili wao. Ndio mana unaona sijataja jina la mtu hata mmoja katika uchambuzi wangu.

Pili, ni bahati mbaya sana kwamba umesoma nilichoandika ukiwa na mtu wako kichwani na umetafsiri kila nilichoandika kwa kumlenga yeye. Kama unafuatilia yanayoendelea duniani, utafahamu kwamba nadharia njama ya 5G imeongelewa na watu wengi sana na miongoni mwao wako "watumishi wenye majina" kama nilivyosema. Hivyo, ninahofia sitajibu chochote kinachomlenga yeye moja kwa moja au mwingine kama wewe ulivyofanya. Ninamfahamu na ninamweshimu.

Tatu, sina hakika kama kuna mahali nimetumia neno "manabii wa uongo" katika uchambuzi wangu. Kama pako ni makosa. Ni bahati mbaya kwamba wewe umeyachukulia maneno kama manabii, wainjilisti na wahubiri katika muktadha wa kikristo pekee . Maneno haya yana maana pana. Mtu anaweza akawa mwinjilisti au muhubiri wa kilimo, wa viwanda, wa teknolojia, nk. Pia mtu yoyote anaweza kuwa nabii wa pombe, sigara, uongo, uovu, 5G, nk. Popote nilipotumia neno manabii au wahubiri katika uchambuzi wangu sijayatumia katika muktadha wa kikristo bali katika upana wake nikimaanisha manabii/wahubiri/wainjilisti wa nadharia njama ya 5G. Nilipolenga imani nimetumia neno "watumishi".

Nne, uko sahihi sana kuhusu njama za wanadamu katika kuasi kusudi la Mungu. Ila sina hakika kama Mungu tunayemuamini, anahitaji sisi kutumia habari za kupikapika, kuungaunga au za uongo na za kutisha watu ili kuonesha kwamba kuna mbinu na njama ovu duniani. Yeye ni mkweli na anakaa katika kweli. Haitaji kusaidiwa na uongo au uzushi au mambo ya kubuni kutusaidia kuijua kweli yake.

Tano, nimesikitika sana kusoma hoja yako kwamba wanaomwamini Mungu hawahitaji kutumia akili, maarifa wala ujuzi binafsi bali wanatakiwa kuamini tu. Hii ni hatari kubwa sana na inaelezea kwa nini imani inatumika sana kupotosha watu. Ninatamani jukwaa hili lingekua la kiimani tujadili huu mtazamo kibiblia kwa reference (maana ndiyo uliyoirejea kwenye maelezo yako). Ninataka kukuhakikishia kwamba Biblia inapingana wewe sana kwenye fikra hizi. Kama hatuhitaji akili, maarifa, elimu, sayansi, na ujuzi biinafsi kama nyenzo za kutusaidia kumjua Mungu zaidi, sasa alitupa vya kazi gani na kutumia wapi? Kwa nini anataka tutafute elimu na maarifa?

Naomba nikomee hapa na nikuombe sana tujadili mada bila kujadili majina ya watu au watumishi kama mimi nilivyofanya. Kama kuna mtumishi ameongea kitu na kinaangukia kwenye mada niliyoandika, basi tujikite tu kwenye hiyo hoja bila kumtaja na kama kuna maswali yanayomhusu yatajijibu. Usichukue comments za watu wengine wanaotaja watu kuwa ndio mtizamo wangu.

MM Togolani
 
Manabii wa UONGO, yu mkini haya walio wateule wa Bwana watakengeuka.

Ukienda kanisani ukasikia au ukaona mtumishi anaanza mambo ya NIMEONESHWA, NIMEOTESHWA ogopa na hasa kama ni mambo ya kuogopesha maana hawa wanaooteshwa na kuoneshwa huonyeshwa mambo ya kuogopesha.

Wamelaaniwa maana Bible inasema ULAANIWE MGUU UPELEKAO HABARI MBAYA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tusiwajumuishe wote kwa namna hii. Tupambane na tatizo tu. Tatizo sio kuoneshwa au kuoteshwa (mambo haya yako kiimani), tatizo ni matumizi ya mabaya ya dhana ya kuoteshwa au kuoneshwa huko.
 
Mlipuko wa Covid-19 unasambaa ukiambatana na taarifa nyingi zisizo sahihi au za kupotosha. Taarifa hizi zinatengenezwa, ama kwa watu kukosa uelewa sahihi wa jambo wanalolizungumzia au kwa makusudi, kama “Nadharia Njama” (
Umewasha taa kila mtu anaweza kuona.

Hatahivyo, sio wote wanaweza kutambua kama hiyo ni taa na huo ni mwanga wa taa ; unawaka.

Licha ya ujumbe kufaa hivi kwamba umechukua mwelekeo unaokubalika, lakini umechukua masuala msingi kiujumla.

Ni bayana kuna tatizo la elimu na uelewa wa mambo ya imani na sayansi. Katika hili jamii ya kiafrika inaongoza.

Kuhusu imani kwa kweli hakuna mtu anayeweza kuishi bila imani.

Licha ya ukweli huu ni hakika kwamba imani haiwezi kusemwa bila kutaja au kuhusishwa na dini.

Hapa kwenye dini ndipo tunaona kuna dini ya kikristo, kiislamu na kadhalika.

Dini zote katika wingi wake nazo zimegawanyika katika makundi kadhaa na hayo makundi kadhaa nayo yamegawanyika. Hapa ndipo kwenye tatizo. Tatizo hili ni kubwa sana hasa Afrika.

Kutokana na kukosa au kutokuwepo elimu na uelewa wa mambo, Afrika haijui dini ya kweli ni ipi ; imani ya kweli. Hapa ndipo yalipo makosa.

Hakuna mtu au jamii inayoweza kuishi bila imani ; dini. Haipo.

Kosa wanalofanya watu wengi ni kushindwa kuelewa kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine kujibu swali hili: imani ni nini ; dini ni nini ? Hapa ndipo makosa yalipo.

Karibu Afrika yote inashikilia na kuishi imani potofu ; dini za uongo. Makosa ya Afrika yako hapa.

Kuhusu teknolojia kama kilivyo kitu kingine chochote haiwezekani isiwe na kasoro ambazo kimsingi haiwezekani kuzifafanua bila kutazama uhuru wa mtu.

Utafiti ambao ndiyo njia inayopaswa kushikiliwa wakati wote katika mambo yote, Afrika hisia (opinions) ndiyo zinatawala mambo.

Kwa jamii za Afrika ugonjwa unahusishwa na mambo mengi (subjective). Kwa kweli Afrika swali la ugonjwa ni nini halijulikani.

Sayansi ambayo inajaribu kufafanua kwa lugha rahisi mambo ya imani, Afrika inakataliwa.

Kwa upande wa Marekani na Uchina katika mambo yote ya uchumi, utawala na teknolojia kuna upotoshaji mkubwa.
 
UOMGO mtupu
kwanza hiyo siyo maana ya 5 Generation kila mtu anaingiza kivyake
5G - Wikipedia
halafu kuingiza Dini ndipo ulipoharibu kabisa
jinsi Generation inavyoendelea ndio tunagundua mengi na magonjwa yaliyopo yataonekana sasa
mwishowe mtatuambia 6G ndio mwisho wa Dunia
Ooopsss!!! Du !!! Sasa sijui tatizo ni Mimi ndio sjaelewa au?

Nimejaribu kwenda kwenye link ya wikipedia uliyoiweka kusupport hoja yako lakini sijaona tofauti ya tafsri ya 5G iliyopo kule na kwenye uzi huu

Zaidi nimeona mhemuko kupitia dirisha la imani ya dini katika mtazamo uleule alioongelea mleta mada

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeshindwa kuwataja hao unaowaita "manabii wa uongo" kwa majina. Lakini kwa hakika kabisa mmojawapo uliyemlenga ni Bishop Dr Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima...

Kitaturu

Umeiona clip ya pili ya Gwajima kuhusu Corona, Bill Gates na chanjo yenye chip? Mtizamo wako kwa muktadha wa hii mada ni upi?
 
Ni kweli kabisa afrika tupo katika mkwamo mzito sana, tunaishi dunia ya copy and paste halafu wakati mwingine tunajifanya kujua kuliko wajuaji halisi.

Kuna Shekhe mmoja jirani yangu, yeye anasema COVID 19 ni matokeo ya dhambi za wakristo ndio kisa cha Italia na nchi za kikristo kuwa na vifo vingi, lakini akili ya kawaida tu ni kwamba MECCA mwaka huu hakuna waliokwenda kuhiji.

Israel imezifunga zile sehemu takatifu ambazo ni sehemu muhimu kwao katika kuingiza fedha za utalii, hili ni janga zito, halipaswi kuunganishwa na imani za kidini, kule Ujerumani wanakufa wapagani wengine tu.

Kuna nchi hazimwamini Mungu wa Biblia na Quran na hazina idadi kubwa ya wagonjwa wa Corona.
Hivi mpaka sasa huyo shekhe hamjampeleka milembe mnasubiri nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitaturu

Umeiona clip ya pili ya Gwajima kuhusu Corona, Bill Gates na chanjo yenye chip? Mtizamo wako kwa muktadha wa hii mada ni upi?
Ndugu John E. Luyangi, ninadhani ndugu Kitaturu ni member wa kwa Bishop (kutokana na maelezo yake). Kwa kuwa sikua nimesikiliza alichokirejea toka kwa Bishop, nimelazimika nitafute hiyo clip ili nielewe kwa nini Kitaturu alinivaa. Nimetamani ningekua nimemsikiliza kabla ya kuandika uchambuzi huu maana nadhani kuna points ningekua nimeziongeza au kuzipanua zaidi.

Niseme tu mtu anayetaka kuelewa nini nilichokijadili kwenye mada hii, basi asikilize vema alichoongea Bishop na atafute kujua taarifa sahihi ya alichokiongelea na ukweli wa kisayansi ulio nyuma ya jambo hilo. Ni hatari sana kumshutumu Bill Gates kwa wazi namna hii na kwa jambo ambalo ukweli wake ni rahisi sana kupatikana. Gates amesaidia sana nchi za Afrika pamoja na Congo kupitia taasisi yake. Pamoja na mambo mengine, anafadhili miradi mingi sana ya kupambana na malaria duniani na Congo amekuwepo tangu 2011 na mradi wa chanjo ya pnemonia inayokua inaongoza kwa vifo vya watoto (tazama hapa).

Kuhusu kinachodaiwa ni chanjo, bado hakuna kinga ya Covid-19 na itachukua muda mrefu (sio chini ya mwaka) kwa majaribio yanayofanyika sasa (clinical trials) kukamilika na kuwa kinga inayofaa kutumika. Hakuna kinga watu wanayopewa DR Congo kwa sasa. Kilichotokea ni serikali ya Congo ilisema majuzi kwamba wao wako tayari kuwa sehemu ya clinical trials kwenye process ya kutafuta kinga (Fungua hapa usome). Na majaribio yenyewe kasema kabisa kama yataanza basi ni mwezi wa 7 au wa 8 na nchi zinahusika ni China, Canada na US. Majaribia haya yanafanyika hata nchi zilizoendelea na hayana uhusiano na Bill Gates. Wanasayansi kwenye nchi nyingi wanahangaika maabara kutafuta kutengeneza kinga. Clinical trials hizi sio swala la nchi moja na wengine wamenza kufanya clinical trials ambazo ni hatua ya lazima katika kutengeneza kinga au dawa. Kuna mambo mengi sana ya kufanyiwa tafiti kabla ya chanjo kuanza kutumika na sio ktu cha muda mfupi. Ukiwasiliza hata wale madaktari wawili wajinga wa Ufaransa waliopendekeza kufanyike majaribio Afrika, utaona kwamba tayari kuna trials zinafanyika Australia na kwingine.

Sikua nimemsikiliza Bishop lakini mengi ya aliyoongea yamo kwenye uchambuzi wangu. Sasa nimeelewa kwa ninindugu Kitaturu alidhani uchambuzi wangu umemlenga yeye.

MM Togolani
 
Mathew Togolani Mndeme

Asante sana. kwa ruhusa yako, naomba nitumie bandiko mabandiko yako namba 1 na 57 kama rejea. Naamini kupitia kwa maandishi yako, kuna jamii itasaidika hata kwenye mapambano dhidi ya Corona.

Kaka John,

I put here for public consumption. Ni ruhusa kutumia kwa malengo yaliyokusudiwa (kuelimisha na kuchochea mjadala wa kutafuta ukweli).

MM Togolani
 
Unawaaminisha watu kuwa 5G ni hatari au ni shetani huku mfukoni una simu ya 4/5G na hotuba au mahubiri unayotoa unayarusha live kwa Youtube inayotumia teknolojia ya 5G kuweza kustahimili wingi wa watu wanayoitumia. Pia una accounts za mitandao ya kijamii ambayo kwa sehemu kubwa zinategemea teknolojia unayopambana nayo. Sasa tukuamini kwa lipi?


ASANTE MKUU TOGOLANI.
 
Back
Top Bottom