Temitope Balogun Joshua, (TB Joshua) afariki Dunia

Temitope Balogun Joshua, (TB Joshua) afariki Dunia

1623022262413.png

Wanangu wana jamvi,
Kifo cha tapeli mkubwa mwenye roho mtakakitu TB Joshua si habari mpya tena. Hata hivyo, kina funzo hasa kwa matapeli wanaomuuza Yesu wasijue kuna mwisho. Jamaa alijirundikia ukwasi asijue atakufa kijana hata kabla ya kuufaidi.

Sijui akina Gamanywa, Gwajima, Kakobe, Mzee wa Upako, Mwingila na wengine wengi wanajifunza nini? Je wachovu na wajinga wataendelea kuwatajirisha matapeli wakijidanganya kuwa sala na si kuchapa kazi vinaweza kuwakomboa?

Je wapumbavu wanaoamini manabii wa uongo watapata somo hapa? Naomba kuleta hoja tekenyeshi wanangu.
 
Mkuu mbona kama umeandika kwa hasira sana?

Sema pia maswala ya kumjaji mtu nayo hayafai!
 
Mkuu mbona kama umeandika kwa hasira sana??
Sema pia maswala ya kumjaji mtu nayo hayafai!
Mwanangu sijaandika kwa hasira. Ni ukweli mtupu. Yesu alipowaafufua wafu, aliweza kufufuka mwenyewe (kama wanaoamini hivyo wanavyodai). Huyu tapeli ngoja uone kama atafufuka zaidi ya kutokomea kama akina Rwakatare aliyewaibia akina mama angewapatia waume wakati yeye hakuwa naye hata wa chembe zaidi ya ushugamami mwanangu. Nina hasira na matapeli hawa kusema ule ukweli.
 
Mwanangu sijaandika kwa hasira. Ni ukweli mtupu. Yesu alipowaafufua wafu, aliweza kufufuka mwenyewe (kama wanaoamini hivyo wanavyodai). Huyu tapeli ngoja uone kama atafufuka zaidi ya kutokomea kama akina Rwakatare aliyewaibia akina mama angewapatia waume wakati yeye hakuwa naye hata wa chembe zaidi ya ushugamami mwanangu. Nina hasira na matapeli hawa kusema ule ukweli.
Tatizo ni kwamba hizo stori za kufufuka mi siziamini☹
 
Mwanangu sijaandika kwa hasira. Ni ukweli mtupu. Yesu alipowaafufua wafu, aliweza kufufuka mwenyewe (kama wanaoamini hivyo wanavyodai). Huyu tapeli ngoja uone kama atafufuka zaidi ya kutokomea kama akina Rwakatare aliyewaibia akina mama angewapatia waume wakati yeye hakuwa naye hata wa chembe zaidi ya ushugamami mwanangu. Nina hasira na matapeli hawa kusema ule ukweli.
Sio kila anaehubiri neno la Mungu ni tapeli Wengine ni wapakwa mafuta wa Bwana
 
Huo ni mtazamo wako Hasi kwa TBJoshua, Mimi nimemjua Kama muhubiri mwenye upako na kibali Cha Mungu, pia alijitahidi kufuata misingi ya bibilia kwa kuwajali wajane,mayatima na wahitaji.

Ninakushauri tenga muda fuatilia historia yake utamwelewa. Mbali ya elimu yake ndogo ya kidunia alikuwa na uwezo wa kipee kutoa elimu ya kiroho na kidunia hata kwa wasomi wakubwa.
 
Sio kila anaehubiri neno la Mungu ni tapeli Wengine ni wapakwa mafuta wa Bwana

Hicho hicho kitabu wanachotakiwa kukihubiri kinasema kuwa siku za mwisho za dunia watakuja manabii wa uongo!!! Ndio hao wanaotumia bibilia kujitajirisha na kutumia unyonge wa watu masikini kupata fedha za kujenga majumba na magari ya kifahari na vitu vingine vya anasa huku waumini wao wakizidi kuwa mafukara. Ndio maana ni sahihi kuwaita matapeli wa dini.
 
Lusekelo,Gwajima,Mwamposa na Mwingira kwangu mm taa nyekundu inawaka
Kwavile haya mambo watu hufanya kwa kupenda kwao mi sioni shida yoyote!

Mtu unajua kabisa kuwa kitu ni uongo ila unaamua kuamini kwa sababu zako binafsi, sasa hapo unakuta wamekusanyana masikini 2000 kumchangia mtu mmoja kwanini asitajirike?
 
Sio kila anaehubiri neno la Mungu ni tapeli Wengine ni wapakwa mafuta wa Bwana
Hebu tuache utani. Nani anawapaka mafuta hayo kama siyo utapeli kama wa anayeitwa mtume paulo aliyewaua wanafunzi wa Yesu ila baada ya kugundua kuwa janja yake ilikuwa imekwisha wangemsulubisha, akasingizia alikutana na Yesu na kuona mwanga. Hakuna cha kupakwa mafuta wala nini bali ukihiyo na usasi wa ngawira na uchumia tumbo,
 
Back
Top Bottom