Tenzi za rohoni

Tenzi za rohoni

 
Mkuu hili sio swala la ufahamu wa mtu ni swala ambalo ni kanuni ya kawaida tu kwenye Ulimwengu wa roho watu wengi bado hawajajua bado ulimwengu wa Roho unavyo tenda kazi,
Ufahamu hawana wengi hata viongozi wetu wa kiimani pia,
Sisemi kwa ubaya au kujitukuza ila hua naumia sana kuona watu wengi sana bado wapo gizani
mambo madogo tu bado hawajayajua Bado inahitaji Neema ya MUNGU na kweli Ya Kristo iwafikie watoke huko maana Yesu alisema enendeni Ulimwenguni pote mkawafanye watu wawe Wanafunzi Ila ajabu sasa hao wanafunzi sasa wamekaa makanisani miaka Tele na bado hawaja hitimu still waMeshikiliwa na taratibu,Kanuni na Mapokeo ya kanisa still bado watumwa na hata Neno na Mambo ya msingi ni Zero kwao MUNGU ni kama Foreigner Na sio BABA tena
nakubaliana na wewe Ndugu ROHO MTAKATIFU atuongoze tujitambue na tUtambue Mamlaka tuliyopewa Katika jina La YESU!
Usijihesabie kufahamu kuliko wengine ndugu na kuona wengine hawajui kuomba, kusifu na kuabudu, kumbuka akili ya Mungu haichunguziki!! Mwache mtu aombe Kwa kadri anavyoongozwa na Roho Mtakatifu maana pekee ndie anaweza kutusaidia kuomba! Kwa akili zetu hatuwezi tutaishia kujiona sisi ni bora kuliko wengine. Warumi 8:26-27, omba kadri unavyoongozwa ili mradi usimkufuru Roho wa Bwana.

Sent from my itel A662L using JamiiForums mobile app
 
Usijihesabie kufahamu kuliko wengine ndugu na kuona wengine hawajui kuomba, kusifu na kuabudu, kumbuka akili ya Mungu haichunguziki!! Mwache mtu aombe Kwa kadri anavyoongozwa na Roho Mtakatifu maana pekee ndie anaweza kutusaidia kuomba! Kwa akili zetu hatuwezi tutaishia kujiona sisi ni bora kuliko wengine. Warumi 8:26-27, omba kadri unavyoongozwa ili mradi usimkufuru Roho wa Bwana.

Sent from my itel A662L using JamiiForums mobile app
Acha ulokole ndugu nani kajihesabia kujua tatizo lenu hampendi kuambiwa ukweli na kuchukua hatua

hapo juu nimetoa namna bora ya kushirikiana na Roho mtakaitifu na namna ya kumwimbia MUNGU
Na nimetoa mifano ya nyimbo zinaopaswa kuimbwa ndugu huwezi kumwimbia MUNGU kama huna connection na Roho Mtakatifu hivi unaimba usinipite mwokozi na unategemea roho mtakatifu akuhudumie?
hivi hujui kwenye Ulimwengu wa Roho lazima kitu uamini upo nacho ndipo unapata udhihilisho?
Mungu anakaa ndani yako yaani BABA MWANA NA ROHO MTAKATIFU wapo ndani yako halafu unaimba asikupite akili zako zinakua timamu kweli?
kumbuka imani ni kuchukua hatua ya kile unachokiamini gues what
unaamini yupo mbali au Mbinguni na Maandiko yanasema yupo ndani yako unategemea
udhihilisho gani?
angalieni muimbavyo MUNGU ni MFALME na mwimbieni kwa akili!
mpendwa usiponielewa naomba Roho Mtakatifu akufunulie namna bora ya kushirikiana na ufalme wa MUNGU
SHALOM!
 
Hizi za chini ndio zangu dahh, Hiyo nasikia kuitwa wakati nahangaika na uzinzi na ujana ilikuwa inasema nami sana Moyoni Mwangu. Uliyewaita dah, hiyo ninlazima nitoe machozi nikiisikia na huwa najitahidi sana nisiisikilize mbele za watu.

Nilikuta mtu anasikiliza hiyo tenzi huwa naondoka kwani huwa nataka sana machozi. Naipenda sana na Marehemu mzee wangu alikuwa anaipenda sana. Kwenye msiba wake, watoto tuliomba tuombe huo wimbo kama kumbukumbu yake.
Pole kwa kuondokewa na mzee wako, mimi hizo zote zikiimbwa machozi huja bila kuitwa yaani
 
Kaa nami

Mwamba wenye imara

Salama rohoni

Bwana u sehemu yangu

Kijito cha utakaso

Hizi tenzi zinanifanya nahisi kuwa karibu zaidi na Mungu pindi ninapokosa msaada wa kibinadamu [emoji120]
 
Mwenyezi Mungu awabariki wote walioshiriki kutunga nyimbo hizi za TENZI ZA ROHONI.

Hizi ni baadhi tu ya nyimbo hizo zinazogusa moyo (Heart touching songs)
1.Mungu ni Pendo
2.Usinipite Mwokozi
3.Salama Rohoni
4.Yesu unipendaye
5.Mwamba wenye imara
6.Nataka nimjue Yesu
7.Bwana u sehemu yangu
8.Ni tabibu
9.Kumtegemea Mwokozi
10.Kaa nami
11.Bwana Mungu nashangaa kabisa.

Wakati mwingi unatembea au uko busy na shughuli zako unajikuta unaimba tu peke yako, unahisi amani ya ajabu ndani ya moyo wako.

Muwe na siku njema wana wa Mungu.
🙏🙏🙏🙏🙏🙏
Tenzi za rohoni,zinampa mtu utulivu na amani.
 
Kwa ufupi hizi tenzi za Rohoni zina mguso wa Roho Mtakatifu...ndiyo maana ukizisikiliza unapata mguso wa kiroho.

Kuna nyimbo ukisiliza unahisi kama umefika heaven...kumbe uko hapa hapa. Hizi ni baadhi tu ya tenzi zinazonibariki sana.

1. Mlango wazi.
Mlango uko wa wema, mlango wazi Huo.
Yesu ameufungua na hakuna kufunga.

2. Bubujiko/There is a fountain
Damu imebubujika, ni ya Imanueli.
Wakioga wenye taka, husafishwa kweli.

3. Ninaye Rafiki.
Ninaye Rafiki naye alinipenda mbele
Kwa kamba za pendo lake nimefungwa milele.
Aukaza moyo wangu niache ugeuzi
Ninakaa ndani yake, yeye kwangu milele.

4. My Jesus I love thee
5. Rock of ages cleft for me
6. Nionapo amani kama shwari/It is well(Horatio Spafford story)
7. Abide with me/kaa nami.

The list is long....simply put, every note and every toned voice be to the glory and honor of God.
 
Back
Top Bottom