Tetemeko kubwa lazikumba Uturuki na Syria. Watu zaidi ya 36,257 Wafariki Dunia

Tetemeko kubwa lazikumba Uturuki na Syria. Watu zaidi ya 36,257 Wafariki Dunia

Syria hali itakuwa mbaya maana hadi muda huu mpaka pekee umefungwa, hivyo misaada imeshindwa wafikia.
Pia hakuna nchi inaruhusiwa kwenda huko
Doooh
Sasa si waruhusu watu waingie wakawaokoe
 
Vifo vimevuka 9,000

Watu zaidi ya 100,000 hawajulikani walipo

Bado watu wamefukiwa

Misaada mbali mbali inaendelea kutua
yani watu afu9
na laki1 hawajulikani walipo aiseee [emoji114] Mungu atuepushe..
majanga ya asili mabaya sana maana yanasafisha vizazi
 
Huyu mzee kwenye picha ameshikilia mkono wa binti yake wa miaka 15 ambaye bado amefunikwa kifusi lakini tiyari amesha fariki nadhani huyu mzee hataki kuamini anacho kiona.
FB_IMG_16758311032488756.jpg
 
Vifo vimefikia 11,000.
Zoezi la uokozi litachukua muda mrefu
Hadi leo watu zaidi ya 17000 waondolewa ndani ya vifusi
 
Vifo vimefikia 11,000.
Zoezi la uokozi litachukua muda mrefu
Hadi leo watu zaidi ya 17000 waondolewa ndani ya vifusi

Wapo watanzania wanaosoma na wanaoishi sehemu hizo ?? Kuna habari yoyote kuhusu wao ??
 
Watoto ni malaika
Watoto kuna favor ya pekeyao wanayo aisee


Nakumbuka Kuna kipindi tulipata msiba,
Ule muda alifariki marehemu mtoto Aliangua sana kilio kikali.
Tukawa tunamnyamazisha.

Baadaye kuja kufatilia taarifa,kumbe ule muda mtoto Analia,ndio muda ambao kule alikuwa anakata moto.
 
Maafisa wa Uturuki wanasema watu 8,574 wamefariki nchini humo huku idadi ya vifo vilivyothibitishwa nchini Syria hadi sasa ni 2,662

Aidha, kufuatia malalamiko kuwa Mamlaka za Turkey zilichelewa kufika katika baadhi ya maeneo yaliyoathiriwa, Rais Recep Tayyip Erdogan amesema kuwa Serikali inashughulikia miundombinu ya ndege na barabara, ili kurahisisha jitihada za uokozi
UPDATE: VIFO VYA TETEMEKO VYAZIDI 8,700

Kwa mujibu wa Shirika la Maafa nchini Turkey, idadi ya Vifo imeongezeka hadi 6,234, huku takriban watu 37,011 wakijeruhiwa

Vyombo vya Habari vya Serikali nchini Syria vimesema takriban watu 2,500 wameuawa huku idadi ya majeruhi ikishindikana kujulikana mara moja
Vikosi vya Uokoaji vinazidi kutafuta manusura waliofukiwa na vifusi, Kusini mwa Turkiyë na Kaskazini mwa Syria baada ya matetemeko makubwa mawili ya ardhi kuyakumba maeneo hayo Februari 06, 2023

Huku jitihada za uokoaji zikiendelea, mamlaka zimeonya kuwa idadi ya vifo inaendelea kuongezeka kutokana na kusuasua kwa zoezi la uokoaji, linaloathiriwa na baridi kali pamoja na uharibifu mkubwa wa Miundombinu
Tetemeko kubwa la ardhi la kipimo cha 7.9 limepiga katikati mwa Uturuki na Kaskazini-Magharibi mwa Syria siku ya Jumatatu, na kuua maelfu ya watu na kujeruhi mamia wakati majengo yakiporomoka


Uokoaji wa walionusurika kwenye vifusi katika eneo hilo lenye theluji unaendelea.

Shirika la maafa la Uturuki limesema watu 76 wameuawa, na 440 wamejeruhiwa, wakati mamlaka ilipotawanya timu za uokoaji na kusambaza ndege katika eneo karibu na mji wa Kahramanmaras, huku ikitangaza "kiwango cha 4 ya uokoaji" inayotaka usaidizi wa kimataifa.

Vyombo vya habari vya serikali ya Syria vimesema kuwa idadi kubwa ya majengo yameporomoka katika jimbo la Aleppo, huku chanzo cha habari katika utumishi wa umma cha Hama kikisema kuwa majengo pia yameporomoka huko.

UPDATES
Vifo zaidi ya 100 upande wa Uturuki, 39 Upande wa Syria huku watu wengi wakiwa bado chini ya vifusi.

Italia yaonya kuwa tsunami yaweza tokea kutokana na tetemeko hilo

UPDATE: WALIOFARIKI KWA TETEMEKO LA ARDHI UTURUKI NA SYRIA WAFIKIA 1500

Wakati shughuli za Uokoaji zikiendelea baada ya kutokea Tetemeko lenye kipimo cha Richa 7.8, zoezi hilo linaanza kukabiliwa na ugumu kutokana na Mamia ya Watu kunaswa kwenye vifusi

Zaidi ya watu 5000 wamejeruhiwa na wengine bado hawajulikani walipo na wana hali gani. Nchi za Cyprus, Misri na maeneo ya Lebanon yamepata Mtikisiko kutokana na Tetemeko hilo.

---
UPDATE: IDADI YA WALIOFARIKI KWA TETEMEKO LA ARDHI UTURUKI YAFIKIA WATU 1,800

Vifo zaidi vinazidi kuripotiwa kufuatia Tetemeko la ukubwa wa Richa 7.8 kuzipiga Uturuki na Syria usiku wa kuamkia Februari 6, 2023 na kuporomosha mamia ya Majengo wakati watu wakiwa wamelala

Idara ya Dharula Nchini Uturuki imeomba msaada kwa Jumuiya za Kimataifa baada ya kutokea Matetemeko mengine mawili yenye kipimo cha 7.5. Uingereza tayari imetuma Wataalamu 76 wa Utafutaji na Uokoaji.


UPDATE: Zaidi ya watu 2,300 wamepoteza maisha huku waokoaji wakiendelea kutafuta manusura
Zaidi ya watu 2,300 wamepoteza maisha huku waokoaji wakiendelea kutafuta manusura kutoka chini ya vifusi vya majengo yaliyoporomoka kutokana na Tetemeko kubwa la ardhi lililozikumba Uturuki na Syria leo Februari 6, 2023 na kuacha majeruhi zaidi ya 10,000 na wengine wakiwa hawana makazi.

UPDATE: Staa wa zamani wa Chelsea Christian Atsu akwama kwenye kifusi

View attachment 2508725
Staa wa zamani wa Chelsea na Newcastle za England Christian Atsu (31) Raia wa Ghana ambaye kwa sasa anacheza Hatayspor ya Uturuki amekwama kwenye kifusi cha jengo lililoanguka baada ya tetemeko la ardhi.

Harakati za kumuokoa Atsu zinaendelea lakini kwenye tetemeko hilo lililotokea leo nchini Uturuki mitandao mbalimbali imeripoti kuwa watu zaidi ya 1400 wamefariki Dunia.

Atsu ambaye alijiunga na Chelsea 2013 na kuishia kutolewa kwa mkopo Newcastle na Everton, alikuwa sehemu ya mchezo wa Ligi Kuu Uturuki jana kati ya timu yake ya Hatayspor dhidi ya Kasimpasa ambapo aliisaidia kupata ushindi wa 1-0 akifunga goli dakika ya 90+

UPDATE: Matetemeko mengi madogo 100 yatokea baada ya lile kubwa
Takriban matetemeko 100 yenye ukubwa wa 4.0 au zaidi yametokea tangu tetemeko la ardhi lenye kipimo cha 7.8 lilipotokea Kusini mwa Uturuki Jumatatu asubuhi saa za huko, kulingana na Utafiti wa Jiolojia wa Kituo cha Marekani.

Kadiri muda kutoka kwa tetemeko la ardhi la asili unavyoongezeka, frequency na ukubwa wa matetemeko ya baadaye hupungua.

Hata hivyo, matetemeko ya kipimo cha 5.0 hadi 6.0 bado inaweza kutokea nchini humo na kuleta hatari ya uharibifu zaidi. Hii inaleta tishio kwa zoezi la uokozi linaloendelea na kwa timu za uokoaji na manusura.

UPDATE: WALIOFARIKI KWA TETEMEKO LA ARDHI UTURUKI, SYRIA NI ZAIDI YA WATU 4,300
Ripoti za idadi ya waliofariki inaendelea kuongezeka kufuatia Tetemeko la Ardhi la ukubwa wa 7.8 kwa kipimo cha Richa, kuzipiga Uturuki na Syria usiku wa kuamkia Februari 6, 2023.

Watu 2,921 wameripotiwa kufariki Nchini Uturuki huku zaidi ya 15,000 wakijeruhiwa, upande wa Syria imeripotiwa waliofariki ni watu 1,444; ikifanya jumla ya vifo kufikia 4,365, inaelezwa idadi inatarajiwa kuongezeka.

Rais wa Korea Kusini, Yoon Suk-yeol amesema Nchi yake itatuma timu ya waokoaji na vifaa vya matibabu ya dharura Nchini Uturuki ili kusaidia uokoaji unaoendelea.

UPDATE: VIFO VYAFIKIA 8,700
Kwa mujibu wa Shirika la Maafa Nchini Turkey, idadi ya Vifo imefikia 6,234, huku takriban Watu 37,011 wakijeruhiwa

Vyombo vya Habari vya Serikali Nchini Syria vimesema takriban Watu 2,500 wameuawa huku idadi ya Majeruhi ikishindikana kujulikana mara moja.

UPDATE: VIFO VYA #TURKEYEARTHQUAKE VYAFIKIA ZAIDI YA 11,200
Maafisa wa Uturuki wanasema Watu 8,574 wamefariki Nchini humo huku idadi ya vifo vilivyothibitishwa Nchini #Syria hadi sasa ni 2,662

Rais wa #Turkey, Recep Tayyip Erdogan, amesema Serikali inashughulikia Miundombinu ya Ndege na Barabara, ili kurahisisha jitihada za uokozi
watu 11,200 hiyo si sawa na bom la nuclear? Mungu atusaidie haswa!
 
Ungejua uturuki wakristo ni wengi wa kutosha usingesema, na sababu ya tetemeko huwa ni kuzidi madhambi kuunganisha tukio la sweden na na tetemeko la uturuki naona ni kupoteza muda.
Wewe mfia dini kayafa mpuuzi,nani alikudanya kuwa chanzo au sababu za tetemeko ni kuzidi kwa madhambi,huko makanisani na misikitini kumbe mnajifunza upuuzi namna hii!!?
 
Back
Top Bottom