Matokeo ya kidato cha nne hayatangazwi na wizara yanatangazwa na NECTAjaman vp mbona jana nimesikia kwamba matokeo yametangazwa na wizara ilikuwa inashughulika kuweka kwa mtandao bt hamna ki2 mpaka sasa!!vp jaman?
hahaa acha woga wewe!
jaman vp mbona jana nimesikia kwamba matokeo yametangazwa na wizara ilikuwa inashughulika kuweka kwa mtandao bt hamna ki2 mpaka sasa!!vp jaman?
Habari wana JF,
kwa tetesi nilizopata matokeo yatakuwa displayed tar 08/02.
UPDATE:
Jan 08, 2013
BARAZA LA MITIHANI LAIKANA PAGE YA FACEBOOK INAYOTUMIA JINA LAKE
Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limesema matokeo ya kidato cha nne bado hayajakamilika na kuwa habari zilizozagaa wiki hii kuwa yapo tayari si za kweli.
Hata hivyo Baraza hilo limebainisha kuwa licha ya kutokamilika, matokeo hayo yanakaribia kutoka kwa mujibu wa ratiba za baraza hilo ambapo hutakiwa kutoa matokeo hayo mwezi Februari.
Akizungumza na mwandishi jana, Ofisa Habari na Mawasiliano wa NECTA, John Nchimbi alisema uvumi wa kwamba matokeo hayo yako tayari ulitokana na kuzushwa kupitia mtandao wa kijamii (Facebook).
Alifafanua kwamba habari kuwa matokeo hayo yameanza kutoka kisirisiri kabla hayajatangazwa rasmi na kwamba hatua hiyo inalenga kuyachakachua, siyo taarifa sahihi.
Aliwataka wananchi kuwa makini na uvumi huo kwa vile endapo matokeo hayo yatakuwa tayari yatatangazwa na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo na pia kuwekwa kwenye tovuti ya Baraza pamoja na wananchi kuweza kuyapata kupitia simu zao za mkononi.
Uvumi huu umetokana na mtu asiyejulikana kufungua akaunti ya facebook yenye jina la Baraza na kuanza kuweka taarifa hizo zisizo sahihi. Napenda kuwajulisha wananchi kuwa Baraza letu halina mtandao kama huo hivyo taarifa hizo si sahihi.
Nchimbi alibainisha kuwa matokeo hayo si siri hivyo yakiwa tayari Katibu Mtendaji atayatangaza kupitia vyombo vya habari na baadaye yataanza kusambazwa kwa kutumia mtandao.
Aliwataka wananchi kuwa makini ili wasitapeliwe na wanaojifanya kuwa wanaweza kupata matokeo ya mwanafunzi kabla hayajatangazwa rasmi kwa vile suala hilo haliwezekani.
Habari wana JF,
kwa tetesi nilizopata matokeo yatakuwa displayed tar 08/02.
UPDATE:
Jan 08, 2013
Nipo hapa katika ukumbi na katibu ndo anatueleza hayo matokeo so nimeamua kuwapasha japo kidogo,asilimia 50.02 ya watahiniwa wamefaulu, shule za binafsi zang'ara na za vipaji maalumu.
Top ten ina shule za St. Francis, Marian, Feza boys, St. Joseph Millenium, Abbey, St.Mary Goreth, Kandoto girls, Mzumbe, Kibaha, Ilboru na wanafunzi bora ni Mary A . Ndona(St. Francis), Rebecca Nsingwe (Marian), Joseph Ulapi(Mzumbe), Ismail Kandeya(Arusha day), Martin Kaimbo(Kibaha)
...ntazid kuwajuza
Tulia kijana acha papara. Yakitoka utayaona.Kwahiyo matokeo yanatarajiwa kuwa display tarehe ngapi?