TEUZI: Rais Samia amteua Jaji Mustapha Siyani kuwa Jaji Kiongozi, Sophia Mjema kuwa RC Shinyanga

TEUZI: Rais Samia amteua Jaji Mustapha Siyani kuwa Jaji Kiongozi, Sophia Mjema kuwa RC Shinyanga

Miaka mingi nyuma, majina ya viongozi wengi yalikuwa maarufu kwa wananchi, siku hizi mimi kuwajua hata mawaziri tu ni shida, yaani mpaka afanye mambo ya kiki ndo nimjue, sijui kama ndo ilivyo kwa wengine!
Ni vile watu tumeipuza siasa na kwenda kwenye Mambo ya msingi baada ya kuona siasa ni Mambo ya kipumbavu!
 


Kauli alizowahi kuzitoa Mh. Jaji Mustapher Mohamed Siyani kusisitiza haki na weledi ili Mahakama zijijengee imani kwa umma mpana.

Jaji Mfawidhi M.M. Siyani asisitiza mahakimu wafawidhi kusikiliza mashauri kwa kuzingatia weledi na kutenda haki ili wasiathiri Imani ya wananchi kwa Mhimili wa Mahakama.
Jaji Mfawidhi Mustapher Mohames Siyani alisema Mahakama haiwezi kujitenga na mchakato wa kidemokrasia wa nchi yetu,hivyo ushiriki wa muhimili uko katika hatua zote ikiwemo kabla ya kuanza kwa uchaguzi na hata baada ya matokeo kutangazwa.

Jumatatu, 31 Agosti 2020​

MASHAURI YA UCHAGUZI YASIATHIRI IMANI YA WANANCHI KWA MAHAKAMA – JAJI SIYANI​

Na Innocent Kansha – Mahakama Dodoma.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dodoma Mhe. Mustapher Siyani amewataka Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Mahakama ya Tanzania kusikiliza mashauri uchaguzi kwa kuzingatia weledi na kutenda haki ili wasiathiri Imani ya wananchi kwa Mhimili wa Mahakama.

Akifungua awamu ya tatu ya mafunzo ya namna bora ya uendeshaji wa Mashauri ya uchanguzi kwa Waheshimiwa Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi Tanzania, Jaji Siyani amewataka Mahakimu hao wafawidhi kusimamia masjala kwa karibu zaidi, ili mashauri yanayofunguliwa yaweze kushughulikiwa ndani ya muda stahiki.

Jaji Mfawidhi aliwakumbusha Mahakimu hao kutilia mkazo matumizi ya Teknologia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili mashauri yanayofunguliwa kwa njia ya mtandao (E-Filing) yaweze kusikilizwa na kumalizika kwa wakati.

“Mafunzo haya ni muhimu kwenu binafsi na Mahakama kama taasisi, umuhimu wake hauelezeki kwa maneno mepesi, kwa wale ambao wamewahi kusikiliza mashauri ya uchaguzi wanaelewa nini ninachozungumzia hapa”, alisistiza Jaji Siyani.

Alisema, katika kuyashughulikia mashauri yatokanayo na uchaguzi, suala la muda ni jambo la muhimu kwani viongozi wa ngazi za juu wa Mahakama pia wameelekeza mashauri hayo kutodumu Mahakamani kwa zaidi ya miezi minne tu na si vinginevyo, hivyo amewataka Mahakimu hao kujiandaa kutekeleza majukumu maelekezo hayo muhimu.

Jaji Mfawidhi alisema Mahakama haiwezi kujitenga na mchakato wa kidemokrasia wa nchi yetu,hivyo ushiriki wa muhimili uko katika hatua zote ikiwemo kabla ya kuanza kwa uchaguzi na hata baada ya matokeo kutangazwa. Aliongeza kuwa Ibara ya 107 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka dhahiri kuwa Mahakama ndicho chombo chenye kauli ya mwisho katika kutoa haki. Source : MASHAURI YA UCHAGUZI YASIATHIRI IMANI YA WANANCHI KWA MAHAKAMA – JAJI SIYANI
 
Miaka mingi nyuma, majina ya viongozi wengi yalikuwa maarufu kwa wananchi, siku hizi mimi kuwajua hata mawaziri tu ni shida, yaani mpaka afanye mambo ya kiki ndo nimjue, sijui kama ndo ilivyo kwa wengine!
Siku hizi viongozi hawaendi kwa wananchi,muda mwingi wanawalaumu wataalamu na watendaji kwa kushindwa kutatua matatizo ya wananchi.
 
It seems, Jaji Siyani hakuwa onboard kwenye njama za kumfunga Mbowe. Sasa imewabidi walete Jaji mpya ambaye hajasikiliza ushahidi yeye binafsi, ambaye itakuwa rahisi kwao kumpa maelekezo ya kufanya kwenye hii kesi.

HII NI AIBU KUBWA SANA.
This is a molestation of justice!
 
Nina wasiwasi kwamba huu ni mkakati maalum wa kuchelewesha kesi hiyo na kuzidi kumdhalilisha Mbowe na si ajabu hata kumfunga.

Huu uteuzi wa Siyani umekuja kimkakati au ni mpango uliokuwepo?

Hasa wakati huu ambao hukumu ya kesi ndogo ilikuwa inasubiriwa tar 19.10.2021, napata mashaka.

Nilimkubali sana alivyosikiliza kesi ndogo ya Mbowe, alikuwa kama refarii haswa, upande mmoja ukiweka objection anauliza upande wa pili wanaonaje, then wakijibu anarudi kwa upande wa waliotoa objection kama wanakubaliana na hoja ya upande wa pili, wakikataa, jaji anaangalia sheria inasemaje, then anaupa haki upande unaostahili kesi inaendelea kusikilizwa.

Sijui kama wataipangia kesi jaji mwingine, if yes, napata ukakasi na huu uteuzi kama sio wa kimkakati, kumuondoa huyu aliekuwa anaenda na sheria halafu wamrudishe kama yule wa mwanzo kuwafundisha jamhuri nini cha kufanya, fingers crossed.
 
Jaji Siyani ni Mfano mzuri kwa Majaji wengine.
ni mtu mtenda haki na mpenda haki, ni mtu asiye penda uonevu, asiye penda majungu wala fitina ni mtu mwenye maono,
mchapa kazi asiye choka.
bado kijana ana nguvu ya kuleta mabadiliko.
Hakika akishirikiana na Mtendaji Mkuu wa Mahakama Prof: Elisante wataisafisha mahakama na itaboreka zaidi.
 
Hii ya Jaji Makungu imekaeje,amepanda cheo au kashushwa.au maandalizi ya kuwa jaji mkuu
Amepanda. Kutoka Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu, hadi Jaji wa Mahakama ya Rufaa, (Justice of Appeal).

Mahakama ya Rufaa ndiyo Mahakama ya mwisho kimaamuzi ndani ya Muungano. Ipo juu ya Mahakama zote ikiwemo za Zanzibar.

Hata Marehemu A.S. Ramadhan aliwahi kuwa CJ Zanzibar na CJ Tanzania.

NB: Kuwa CJ Tanzania, ni lazima muhusika awe Jaji wa Mahakama ya Rufaa, (Justice of Appeal)
 
Back
Top Bottom