TFF hakikisheni Simba inakuwa ya pili ili iungane na Yanga kuiletea nchi heshima. Sio Azam

TFF hakikisheni Simba inakuwa ya pili ili iungane na Yanga kuiletea nchi heshima. Sio Azam

Ni kweli sheria ilibadilishwa na waliobadilisha ni UEFA wenyewe hivyo ni sahihi kuwa Liverpool alienda kushiriki CL kwa ticket ya bingwa mtetezi wa CL.
Na hilo tukio la bingwa wa UCL kushindwa kufuzu kwa ticket ya msimamo wa ligi kuu ndio lilitokea kwa mara ya kwanza tangu hayo mashindano yaanzishwe mwaka 1956, hapo kabla haikuwahi kutokea bingwa wa UCL kushindwa kufuzu kucheza CL kwa tiketi ya ligi kuu. Hivyo Liverpool ndio ilikuwa ni timu ya kwanza kubeba ubingwa wa UCL huku kwenye msimamo wa ligi kuu akiwa hana vigezo vya kushiriki UCL msimu unaofuata. Hivyo waliobadilisha ni wenyewe UEFA na ikabidilishwa ili kuipa favour timu yeyote ile itakayobeba ubingwa wa UCL kuutetea ubingwa wake.

Ingekuwa hicho mnawaza nyie ndio ipo hivyo, kwanini Liverpool ambaye anauzoefu wa UCL hakupewa favour msimu huu na shirikisho la soka la Uingereza kwa maslahi ya taifa lao na ili Newcastle ambayo haina uzoefu wasishiriki?
Upo sawa Mkuu ila kwa maslahi mapana ya mpira wetu tunaomba Azam atupishe endapo atakuwa namba 2.
 
Jibu lake wenzetu hawana team 2 tu kushabikiwa nchi nzima, team zote zina washabiki wake na wanajaza uwanja kila wiki iwe league sijui kikombe mpaka mechi za kirafiki. Nchi haikugawanyika na team 2. EPL ni kampuni na team zote zina share na wote wana vote sawa. Sasa sio sawa kufananisha wenzetu na sisi, sisi nchi nzima ni team 2 tu hao Azam wenyewe majumbani kwao wanavaa uyanga na usimba sasa hawa ndio wakatuwakilishe sisi?
Halafu hata Mchezaji wao Prince Dube alisema akifunga dhidi ya Simba Maboss wake wanamnunia.
 
hizi ndizo akili za watanzania kwenye swala la Simba na Yanga....leo hii miaka nenda miaka rudi timu pinzani ni mbili kwenye taifa lenye watu milioni 60,hamtaki mabadiliko hadi mnaomba kupangiwa matokeo.....maana ya kuwepo ligi ni nini sasa,ndio maana soka letu halikuwi kwa ujinga kama huu.
Siku zote watanzania hawapendi mabadiliko ndio maana mpaka leo ccm ipo madarakani na vyakula vikuu bado wali na ugali.


Na ukitaka kuwaletea kitu kipya watakipinga kwa nguvu zote bila sababu zozote za maana.
 
Hapana wanaenda timu zilizochukua ubingwa na timu zinazoshika nafasi ya pili endapo shirikisho la soka husika wamekidhi vigezo vya kuingiza timu mbili klabu bingwa. Timu zitakazoshika nafasi ya tatu na nne zitaenda CAFCC kwa mashirikisho yenye vigezo vya kuingiza timu nne
CafCC imefutwa mkuu
 
Back
Top Bottom