TFF kilichoshindikana kwa Tuisila Kisinda kiliwezekana kwa Perfect Chikwende (double standard)

TFF kilichoshindikana kwa Tuisila Kisinda kiliwezekana kwa Perfect Chikwende (double standard)

Yanga walifanya sub kwa mikupuo 4 badala ya 3.

Msimu jana wachezaji wao mhimu hawakucheza match za kimataifa kwa sababu ya upuuzi wa viongozi wao.

Yanga ni Yanga tu!!!!😂😂

Halafu utasikia "tff wanatuonea"
 
Kwa hiyo huyo Kisinda atakuwa anakula posho ya Bure?!
 
Kuna swali najiuliza, hivi team ikisajili mchezaji na kabla ya deadline huyo mchezaji huyu akawa mgonjwa, inamaana hairuhusiwi tena kusajili mchezaji mwingine kabla ya hiyo deadline?

Kama ni ndio basi kuna mahala kanuni zetu hazipo vizuri.

Sipo hapa kusema nani yupo sahihi nan ani hayupo sahihi ila kwa namna hii team ya Yanga ninaweza kuipongeza kwa kuibua mapungufu katika kanuni zetu. Kwanini?

Haiwezekani mchezaji amesajiliwa katika muda sahihi na kufuata taratibu zote halafu iwepo kanuni ya kumzuia mchezaji huyo. Hiyo kanuni itakuwa na mapungufu makubwa sana au itakuwa imewekwa kimtego kwajili ya ‘’watu flani’’ na kwa bahati mbaya watu hao wameingia kwenye kumi na nane za ‘’watawala’’ ambao kwa siku za hivi karibuni wanasema wanaongoza kwa mawazo yao na si kanuni. Kanuni hutumika tu pale “unapoonekana kushindana na mamlaka.”

Kwanini?

Ni vile tu tumekuwa wasahaulifu sana hasa hawa ndugu wa TFF wamekuwa wasahaulifu mno kupindukia,

Mwaka jana 2021, katika usajili wa dirisha dogo, SIMBA SC ilimsajili Perfect Chikwende na kufanya idadi ya wachezaji wa kigeni kufikia wachezaji 13. Kilichofanyika Francis Kahata akatolewa kwenye usajili wa ligi ya ndani halafu Perfect Chikwende jina lake likaingizwa. Francis Kahata akasajiliwa kwenye mashindano ya kimataifa tu. Kitu ambacho this time around Yanga wamefanya hivyo hivyo.

Lakini wakati huo hatukusikia TFF ikikataa usajili huo.

Wachambuzi wenye ‘mbambamba’ nyingi kama akina Juma Ayo, Jemedari Said na Wilsom Oruma hatukuwasikia pia katika uchambuzi wa kujifanya wanajua kutetea sheria kama wanavyotetea sasa.

Hivyo hapa inaonekana kuna ‘ajenda’ ya siri kama ‘mungu mtu wa mpira’ alivyosema ukishindana na mamlaka wewe ndio utakaye umia. Ni wazi kuna watu wameanza kupata maumivu kwasasabu sheria ileile inayoibana team B sasa haikumbana team A.

Swali la msingi ni kujiuliza tu hizi sheria ni kwa team zote au kwajili ya team flani flani?
Umeashuka vizuri ila naomba nikurekebishe huyo JUMA AYO naomba umtoe maana % kubwa ya mashabiki hatumuelewi
 
Kipindi kile caf walitoa sheria maalumu ya kusajili wachezaji wa ziada kwa timu ziluzoingia hatua ya makundi kwa sababu za covid...ilikue ni sheria ya mpito tu na simba ilisajili waxhezaji zaidi ya 13 wengine hawakucheza hata mechi koja lakini waliosajoliwa kwenye ligi walikua ni 10 tu kama sheria ya tff ilivyotaka..kwa hiyo kuchikulia ishu ya chikwende nankahata kamq mfano haipo hiyo tafuteni pa kujitetea
 
Kipindi kile caf walitoa sheria maalumu ya kusajili wachezaji wa ziada kwa timu ziluzoingia hatua ya makundi kwa sababu za covid...ilikue ni sheria ya mpito tu na simba ilisajili waxhezaji zaidi ya 13 wengine hawakucheza hata mechi koja lakini waliosajoliwa kwenye ligi walikua ni 10 tu kama sheria ya tff ilivyotaka..kwa hiyo kuchikulia ishu ya chikwende nankahata kamq mfano haipo hiyo tafuteni pa kujitetea
simple logic ni kwamba basi wangemsajili chikwende hata kwenye mashindano ya CAF, sasa kwanini hawakumsajili kucheza mashindano ya kimataifa it means kuna sheria iliwabana.
 
Elewa concept ya mleta mada. Mfano wake hauhusiani na Covid na hata 2021 haikuhusiana na Covid. Anachoongelea ni Chikwende kuruhusiwa kucheza ndani na kumtoa Kahata kubaki na mashindano ya nje pekee. Hiki ndo Yanga walichokifanya kwa sasa kumtoa Kambole ndani na kumbakiza nje pekee kisha kumleta Kisinda ndani na nje badala yake. Tofauti unaiona wapi hapo?
Kambole atabakije nje pekee ikiwa hana leseni ya tff!? Kumbuka ili upate leseni ya caf ni lzm uambatanishe (kwenye maombi ya leseni hiyo) leseni ya tff!? Tff wanatoa leseni kwa wachezaji 12 tu wa kigeni kwa kila timu sasa huoni kuna mmoja hapo (aliyezidi) awe kisinda au kambole atakosa kupewa leseni ya tff na hivyo kupelekea kukosa leseni ya caf!?

Au mimi ndio haya mambo sijayaelewa vizuri!?

Tff haijawahi kuwa neutral
 
Kahata ilikuwa hivyo, usiseme haiwezekani. Alicheza ya kimataifa ila ndani alikuwa hachezi
Kumbuka ilikuwa wakati wa usajili wa dirisha dogo. Chikwende alishacheza michuano ya CAF akiwa na timu yake ya Platnum hivyo Simba wakamsajili kwa ajili ya ligi Kuu tu.
 
Swali linakuja kwanini Kahata jina lake lilikatwa kwenye ligi ya ndani!? Au kwanini Chikwende hakusajiliwa kucheza mechi za kimataifa!?
Sina uhakika sanaa ila alitolewa kwa mkopo..kanuni inaelekeza kama unampunguza mchezaj asiendelee kusalia kweny club husika...nikosolewe kama sipo sahih
 
Tuvute pumzi kidogo tuache mihemko.
Mimi nilivyoelewa kulingana na press release ya Ndimbo, Hoja ya TFF ni kuwa " Yanga Wamesjili wachezaji wa kigeni zaidi ya 12 walioruhusiwa na TFF msimu huu". Swali ni jee ikiwa CAF wanaruhusu wachezaji hata 40 na TFF 12 pekee, kanuni zinaku-applied vipi hapa?
Caf inaruhusu wachezaji 40 lkn hao wachezaji ni lazima wawe na leseni ya shirikisho husika. Sasa hapa kwetu tff hawatoi leseni kwa wachezaji wakigeni zaidi ya 12 kwa tim moja. Maana yake ni kwamba simba inaruhusiwa na caf kupeleka wachezaji 40 bila kujali mataifa yao lkn kwanza ni lazima wasajiliwe na wapewe leseni ya tff ndipo wapewe leseni ya caf. Kama simba itakuwa na wachezaji 13 wa kigeni na 27 wa ndani jumla 40 ina maana kwa kanuni za tff mchezaji mmoja wa kigeni kati ya hao 13 hatopewa leseni na tff na hivyo hatopata leseni ya caf! Kwa jumla ya wataopata leseni za tff ni 39 na ndio watakaopata leseni za caf mmoja atakosa ambaye ni wa kigeni. Na atakosa licha ya ukweli kwamba timu haijazidi kiwango cha wachezaji wanaoruhusiwa na caf (40)

Issue ilivyo kwa yanga. Inasemeka yanga walitoa maelekezo kwa tff wakate jina la kambole waweke jina la kisinda. Tatizo ni kwamba tff walikuwa washatunza usajili wa kambole kwa hiyo kambole ndio mwenye leseni ya tff na ndie atayepata leseni ya caf. Kisinda mlichelewa
 
Ilishawahi kutungwa kanuni ya bench la timu kuto vaa vipensi, Hii ikitokea baada ya aliyekua kocha wa Yanga kuwa ana vaa pensi akiwa uwanjani, Tff hii hii ya Karia, Baada ya Zahera kuondoka Yanga kwasasa kanuni iyo haifanyikazi, Matola kocha wa Simba anavaa pensi na abugudhiwi.
Karia yupo kwa masrahi ya Simba
 
kwenye dirisha dogo timu zinaruhusiwa kusajili wachezaji wakigeni zaidi ya inavyoruhusiwa kikanuni? tuelimishe hapo mkuu
Wakati ule kilichotokea ni kuwa CAF waliongeza idadi ya wachezaji ili kukabiliana na UVIKO 19, hivyo Kahata alitolewa kwenye idadi ya wachezaji wa kigeni watakaocheza ligi kuu na akabakia kucheza michuano ya CAF tu, Chikwende akacheza ligi kuu kwa vile alishachezea michuano husika (ya CAF) akiwa na Platnum. hapo Simba ikawa na wachezaji 13 wa Kigeni.
 
Yanga walifanya sub kwa mikupuo 4 badala ya 3.

Msimu jana wachezaji wao mhimu hawakucheza match za kimataifa kwa sababu ya upuuzi wa viongozi wao.

Yanga ni Yanga tu!!!![emoji23][emoji23]

Halafu utasikia "tff wanatuonea"
Kufanya Sub kwa mikupuo minne ni Uzembe wa Refarii wa Mezani.
 
Ndugu, hoja ya TFF ni kwamba hata kama CAF wanaruhusu wachezaji wa kigeni zaidi ya 12 kwenye michuano yao; wao TFF hawataki wazidi 12!.

Issue ni kanuni hii ya TTF inaweza override kanuni ya CAF kwenye michuano ya CA?

Naomba nijibiwe hapa.
Hakuna swala la kuoverride

Ili mchezaji apewe leseni na caf ya kumruhusu kucheza michuano ya caf ni lzm kwanza awe na leseni ya shirikisho husika ambayo ataitumia kuombea leseni ya caf.

Tff haitoi leseni kwa wachezaji wa kigeni zaidi ya 12 ukileta 13 mmoja atakosa leseni ya tff na hvyo atakosa kigezo cha kupata leseni ya caf.
 
Yanga walifanya sub kwa mikupuo 4 badala ya 3.

Msimu jana wachezaji wao mhimu hawakucheza match za kimataifa kwa sababu ya upuuzi wa viongozi wao.

Yanga ni Yanga tu!!!!😂😂

Halafu utasikia "tff wanatuonea"
Ni sahihi lakini waliadhibiwa na TFF na kwakuwa walifanya makosa hakuna hata mtu wa Yanga aliyelalamika
 
simple logic ni kwamba basi wangemsajili chikwende hata kwenye mashindano ya CAF, sasa kwanini hawakumsajili kucheza mashindano ya kimataifa it means kuna sheria iliwabana.
Kwani waliingia dirisha moja? Chikwende aliingia january
 
Back
Top Bottom