TFF na Bodi ya Ligi wapo kimkakati zaidi katika upangaji wa ratiba

TFF na Bodi ya Ligi wapo kimkakati zaidi katika upangaji wa ratiba

Huu uzi hausiani na mapungufu ya waamuzi. Bali ni uzi unahusu chombo kinachosimamia ligi na kinachosimamia mpira wa miguu Tanzania kwa kuifanya timu moja iwege nyuma kwa idadi ya mechi na huku aliyejuu yake waendeleege tu kucheza mechi.
Na mimi naweka malalamiko yangu hapa ili wahusika wafanyie kazi
Hii nayo ni offside
1000027124.jpg
 
Karia anajulikana ni mnazi wa simba na coastal union
Tujue wasifu wa makamu waje , katibu na ceo .
 
Tangu Yanga iaanze kuchukua ubingwa misimu miwili mfululizo viingereza vya kizaramo vimeongezeka hapa jukwaani.Halafu MASHABIKI wa YANGA mna muda wa kujitafutia hata mkate wenu wa kila siku kila siku Yanga Yanga au wengi wenu mnalelewa na dada zenu waliokwapuliwa na minjemba fulani hivi
We ni thimba kolowizard og. Maana hata iweje kolo ni mbishi grade one! Ananyolewa na Ambangula ila bado yumo tu anashupaza tu shingo! Ambangula kaharibu kabisa mfumo wa kufikiri wa makolo! Hasira za makolo Sasa zipo kwenye mataulo ya makipa wa timu pinzani!

Sasa msumari wa mwisho na mazishi ya huu ujinga wa kuibeba thimba kwa viporo ni mechi yetu ya derby, tutawakanda na kufikisha lile gepu tunalopenda la points kumi!

Angalau sasa kidogo afadhali marefa wamepunguza kuibeba kolowizard maana ilikuwa inachefua kucheki mechi za Simba wanaopewa penati kama pipi
 
Mechi mliyopoteza 2-1 mlipoteza kwa ujinga na uzembe wenu kilichowafanys mpeleke mechi Jamuhuri Morogoro ni kipi na kuacha uwanja wa Chamazi, nyie ndio mlikuwa mpo nyumbani na mechi tatu mlikuwa mpo nyumbani sasa wajinga ni nani kama sio nyie wenyewe mliopeleka mechi Morogoro kisha mkaona mambo magumu mkarudi Dar Chamazi
Ukiwa unajua mpira utaona ukichoandika ni ujinga.

Hivi kati ya Jamuhuri na Manungu kipi kiwanja kibovu?

Simba imecheza Manungu na kupata alama 3 kwenye kiwanja kibovu kwanini sababu ya kupoteza mechi iwe ni uwanja?

Nakukumbusha kwamba mechi ya juzi tumecheza na JKT kwenye uwanja wao mpya ambao sio mzuri na bado tulipata matokeo

Katika mechi ambazo Simba amecheza mkoani asilimia 90 zote ameshinda.

Pointi alizodondisha nyingi zote kazipotezea nyumbani

Sare na Namungo ilikuwa ni Uhuru pale tayari tumepoteza pointi 2

Sare na KMC tena kwenye uwanja wa Chamazi unaoutaja taja.

Ungekuwa umeangalia mechi usingetaja sababu ya uwanja.

Makosa personal ya wachezaji hayawezi kufanya sababu iwe ni uwanja.

Nafasi ngapi tulitengeneza za kufunga lakini poor marking za forward yetu ndio iliyokuja kutuhukumu.

Plus Manura anakosaje lawama kwenye yale magoli? Au ulitaka lawama iende kwa uwanja?

Jifunze kuujua mpira na sometimes kukubali kushindwa ni moja ya fairness ya kumheshimu mpinzani.
 
Hiyo gap ya muda ilikuwa kote kote sio kwa Simba pekee hata kwa Yanga ilikuwa wanacheza kila baada ya siku mbili Yanga imecheza tarehe 8 kisha 11 kisha 14 kisha tarehe 17.
Na kwenye ratiba ni mechi moja pekee Simba ndio alikuwa away dhidi ya Coastal union sasa wapi Simba ilipoonewa hapo? Mmejionea wenyewe kwa upuzi wenu kupeleka mechi ya nyumbani Morogoro.

Hoja Yangu ipo hapa, kuna ulazima gani Azam na Yanga wacheze tarehe 17 wakati timu zote mbili hizo zina michezo mingi kuliko Simba.

Swala la kuongoza ligi sio hoja, kwahiyo ukiongoza ligi ndio hauna haki ya kukosoa makosa ya upendeleo wa upangaji wa michezo. Hiki kiporo cha Simba ni tokea mwaka jana lakini cha ajabu mpaka leo hakichezeki.

Hoja Yangu sio ratiba ngumu, kwanini Simba amalizi hiko kiporo chake, badala yake waliojuu yake wanaendelezewa tu kupangiwa michezo?
Azam amecheza michezo 20 wewe umecheza michezo 19

Unaelewa maana yake?

Maana yake Azam angekuwa ni mtu wakutafuta huruma angeanza kulia kuwa wewe unapendelewa.

Unakumbuka ule muda ambao Azam alikuwa anaongoza ligi kutokana na kucheza michezo mingi?

Lini uliwahi kujitokeza hadharani kukemea TFF kwa kitendo cha kuiachia Yanga na Simba viporo?

Gape la mechi ambalo lipo kati yako na mimi ni mechi moja tu na hiyo ilitokana na AFL kuingilia ratiba ndio maana unaona gape hilo.

Sasa niambie wewe gape lako na Azam kwenye utofauti wa mechi moja limetokana na nini?

Hoja ni kwamba kuna ugumu gani unaofanya Yanga ishindwe kushinda hiyo mechi kisa tu Simba ina kiporo?


Kwasababu hata wakati juzi mnacheza na Ihefu bado ratiba ilikuwa ni ileile ya Simba kuwa na kiporo, na bado mkashinda na hakukuwa na kelele za Simba kwanini ana kiporo.

Leo umeona unacheza na Azam ambao ni wagumu umeanza kulia lia kutafuta sababu, ni uoga tu.
 
Hujaelewa na hutaelewa kwasababu uko kishabiki zaidi.
Kwa nini koporo cha Yanga vs JKT na Simba vs Mtibwa kisimalizwe kwanza Machi 17 na 18 mtawalia?
Je hapo pana sababu ya kuvitunza viporo vya namna hiyo?
Unaelewa JKT na Mtibwa wakicheza hizo mechi watakuwa wamecheza mzunguko wangapi?

Unaelewa sababu yako ya kutafuta fairness kwa Yanga inaenda kuzikandamiza timu zingine kwa sababu zile zile ulizokuwa unazilalalmikia wewe?
 
This is well known . Time table ya league 23/24 ipo designed to favor SIMBA in all aspect . Sijui lini this non sense will stop [emoji706] . Allow AZAM or coastal to be favorable . Not the big 2
Akili za viazi mbatata hizi!
 
Ukiwa unajua mpira utaona ukichoandika ni ujinga.

Hivi kati ya Jamuhuri na Manungu kipi kiwanja kibovu?

Simba imecheza Manungu na kupata alama 3 kwenye kiwanja kibovu kwanini sababu ya kupoteza mechi iwe ni uwanja?

Nakukumbusha kwamba mechi ya juzi tumecheza na JKT kwenye uwanja wao mpya ambao sio mzuri na bado tulipata matokeo

Katika mechi ambazo Simba amecheza mkoani asilimia 90 zote ameshinda.

Pointi alizodondisha nyingi zote kazipotezea nyumbani

Sare na Namungo ilikuwa ni Uhuru pale tayari tumepoteza pointi 2

Sare na KMC tena kwenye uwanja wa Chamazi unaoutaja taja.

Ungekuwa umeangalia mechi usingetaja sababu ya uwanja.

Makosa personal ya wachezaji hayawezi kufanya sababu iwe ni uwanja.

Nafasi ngapi tulitengeneza za kufunga lakini poor marking za forward yetu ndio iliyokuja kutuhukumu.

Plus Manura anakosaje lawama kwenye yale magoli? Au ulitaka lawama iende kwa uwanja?

Jifunze kuujua mpira na sometimes kukubali kushindwa ni moja ya fairness ya kumheshimu mpinzani.
Kumbe mlifungwa kwa makosa ya personal, kwanini hapo juu ulilalamikia fixture mgumu ndio iliyochangia kwa timu ya Simba kupoteza mechi. Tusimame na fixture au tusimame na makosa personal?
 
Mwaka jana wakati mko shirikisho viporo vilidandiana hampigi kelele,mkiona simba wana viporo mnaanza kupiga kelele kama manesi wa zamu
 
U
Azam amecheza michezo 20 wewe umecheza michezo 19

Unaelewa maana yake?

Maana yake Azam angekuwa ni mtu wakutafuta huruma angeanza kulia kuwa wewe unapendelewa.

Unakumbuka ule muda ambao Azam alikuwa anaongoza ligi kutokana na kucheza michezo mingi?

Lini uliwahi kujitokeza hadharani kukemea TFF kwa kitendo cha kuiachia Yanga na Simba viporo?

Gape la mechi ambalo lipo kati yako na mimi ni mechi moja tu na hiyo ilitokana na AFL kuingilia ratiba ndio maana unaona gape hilo.

Sasa niambie wewe gape lako na Azam kwenye utofauti wa mechi moja limetokana na nini?

Hoja ni kwamba kuna ugumu gani unaofanya Yanga ishindwe kushinda hiyo mechi kisa tu Simba ina kiporo?


Kwasababu hata wakati juzi mnacheza na Ihefu bado ratiba ilikuwa ni ileile ya Simba kuwa na kiporo, na bado mkashinda na hakukuwa na kelele za Simba kwanini ana kiporo.

Leo umeona unacheza na Azam ambao ni wagumu umeanza kulia lia kutafuta sababu, ni uoga tu.
Upo kishabiki sana, kwahiyo hapa kinacholalamikiwa hakimjumuishi na uonevu anaofanyiwa Azam? Kwanini Azam unamtoa wakati ni mmoja wa waathirika katika hili ambapo mimi nipo kumuongelea pia? Kwanini umekaa kiusimba na uyanga pekee badala ya kukaa kiunamichezo?
Unazungumzia AFL je imeisha lini au bado inaendelea? Kwanini baada ya kuisha mechi za AFCON kwanini Simba na Yanga wacheze idadi sawa ya mechi ilihali mmoja kamzidi mwenzie michezo?
Kwanini baada ya kuisha michezo ya klabu bingwa ipangwe ratiba kwa kurudia kosa hilo hilo la kuwapa idadi sawa ya mechi Simba na Yanga wakati Simba ndiye aliyekuwa nyuma kwa mechi moja.
 
Kumbe mlifungwa kwa makosa ya personal, kwanini hapo juu ulilalamikia fixture mgumu ndio iliyochangia kwa timu ya Simba kupoteza mechi. Tusimame na fixture au tusimame na makosa personal?
Mechi ngumu kwa sababu mechi za Simba zilifululiza na bado hapo ilitakiwa kuwe na kiporo ili kupunzisha wachezaji
 
Wazee wa kulialia tulijua hii tabia mmeiacha.

Mnaongoza ligi kwa gape la point 7 bado mnalia lia kudai TFF inaipendelea Simba?

Unasema ratiba inaibana Yanga, umeangalia Simba mpaka sasa imecheza mechi ngapi ndani ya siku ngapi?

Tarehe 6 tumecheza na Prisons tukapoteza kwa kufungwa 2-1

Kumbuka hiyo ni mechi tuliyocheza mkoani wachezaji wanabidi wasafiri kurudi Dar na pia wapate muda wa kupumzika.

Lakini walikuwa wana siku mbili tu, ndani ya siku hizi mbili walitakiwa wapumzike na pia waingie kwenye mazoezi kwa ajili ya mechi inayofuata ambayo ilikuwa ni tarehe 9 dhidi ya Coastal ambayo nayo inawalazimu wasafiri kwenda mkoani.

Kesho yake tarehe 10 timu inatoka Tanga inaelekea Dar hapo tayari unakuwa na siku 1 ya kujiandaa kwa ajili ya mechi ya tarehe 12 dhidi ya Singida.

Timu inaenda kukutana na Singida ambayo imepumzika kwa muda wa siku 10 bila mechi yeyote.

Kwa hapo mnajijua wenyewe mna balance vipi muda ili muweze kupata muda wa kupumzika na uchovu wa safari, lakini vile vile kwenye muda huo huo unabidi uutumie na kufanya mazoezi kwa ajili ya kucheza mechi hiyo dhidi ya Sangida.

Baada ya kumaliza mechi dhidi ya Singida unakaa siku mbili tena kwa ajili ya kujiandaa na mechi nyingine. At least round hii mechi ya Singida imechezwa Dar hivyo wachezaji watakuwa wameepuka uchovu wa safari.

Jana tarehe 15 Simba kaingia tena dimbani kumenyana na Mashujaa ambao mechi yao ya mwisho walicheza tarehe 6. Mashujaa wamekaa almost siku 9 bila kucheza mechi yeyote.

Ebu eleza tena kwa ratiba hii ya Simba TFF inaibebaje Simba?

Simba inanufaika vipi na ratiba hii?
Mbona hiyo ratiba unayoongelea ilikuwa ni sawa kwa Yanga mzee,
Wote wanapumzika siku sawa sawa. Simba tarehe 6 yanga tarehe 8 baada ya hapo tarehe 9 Simba na tarehe 11 Yanga. Wote wamekuwa wakipumzika siku mbili ya tatu mechi. Au point yako ni ipi hapo?
 
U

Upo kishabiki sana, kwahiyo hapa kinacholalamikiwa hakimjumuishi na uonevu anaofanyiwa Azam? Kwanini Azam unamtoa wakati ni mmoja wa waathirika katika hili ambapo mimi nipo kumuongelea pia? Kwanini umekaa kiusimba na uyanga pekee badala ya kukaa kiunamichezo?
Unazungumzia AFL je imeisha lini au bado inaendelea? Kwanini baada ya kuisha mechi za AFCON kwanini Simba na Yanga wacheze idadi sawa ya mechi ilihali mmoja kamzidi mwenzie michezo?
Kwanini baada ya kuisha michezo ya klabu bingwa ipangwe ratiba kwa kurudia kosa hilo hilo la kuwapa idadi sawa ya mechi Simba na Yanga wakati Simba ndiye aliyekuwa nyuma kwa mechi moja.
Wewe unaongelea Yanga siyo Azam ndo maana mada haina jina la Azam, hata Simba angekuwa mbele mchezo mmoja bado ungelalamika tu maana ni nature ya utopolo
 
Mechi ngumu kwa sababu mechi za Simba zilifululiza na bado hapo ilitakiwa kuwe na kiporo ili kupunzisha wachezaji
Wote wamefululiza.
Ratiba ya Simba ilikuwa tarehe 6, 9, 12,15
Huku Yanga ilikuwa ni tarehe 8,11,14,17 sasa kuna tofauti gani hapo katika kufululiza mechi kwa Yanga?
Hoja ya msingi mnaikwepa, kwanini Azam acheze na Yanga tarehe 17 wakati kwanza ligi inasimama kwenda mapumziko na kalenda ya FIFA?
2) kwanini wakati Simba atakuwa anaendelezewa mzigo wa viporo?
 
Wewe unaongelea Yanga siyo Azam ndo maana mada haina jina la Azam, hata Simba angekuwa mbele mchezo mmoja bado ungelalamika tu maana ni nature ya utopolo
Je umeona mada ina jina la Yanga?
 
Unaelewa JKT na Mtibwa wakicheza hizo mechi watakuwa wamecheza mzunguko wangapi?

Unaelewa sababu yako ya kutafuta fairness kwa Yanga inaenda kuzikandamiza timu zingine kwa sababu zile zile ulizokuwa unazilalalmikia wewe?

Hivyo ni viporo haijalishi watakuwa na mzunguko wa ngapi lakini lazima viporo vichezwe.
 
Back
Top Bottom