TFF yafungua shauri dhidi ya Ofisa wa Yanga, Haji Manara baada ya kudaiwa kuzozana na Rais Karia

Manara anajua anachokifanya na anatafuta anachokitaka kwake coz pale alipo kuna shauri lake TFF yeye na Barbra halijatolewa ufafanuzi,halafu bila uwoga anamjibu as if anamuweza sana Karia, sio kwamba hana akili ila anajua kitakachotokea

Labda niwape za ndaani kabisa Mkataba Wa Haji Manara na GSM ktk kurejesha hamasa ndani ya klabu ya Yanga ulikuwa ni Wa Mwaka mmoja tu

Eng.Hersi akishachaguliwa kuwa Rais na makamu wake Arafat Haji pamoja na wajumbe Wa bodi,Yanga inaenda kubadilisha uongozi mzima pale Yanga na hawa watu Bumbuli na Manara hawapo kwenye tena kwenye mipango ya kuwa kwenye safu ya kitengo cha habari pale Yanga

Manara anaijua future yake ktk Mpira haipo tena,kwahyo yupo katika kutafuta sababu ya kutojihusisha na Maisha ya Mpira kabisa

Source: Trust Me Bro
 
Alipigwa faini mwakalebela kwa jambo jepesi kabisa, lakini huyu ambaye daily haishiwi kashfa na tena zenye ushahidi wa wazi ambao kila mtu anaona lakini bado wanafuga ubovu kwa kumlea lea
tatizo la manara mlililea nyinyi makolo . alipokuwa akiwakashifu yanga na kuwatukana hamkuwa kunyanyua midomo yenu kumkanya. Leo ndo mmejua kuwa jamaa ni mlopokaji?
 
Wa Tz tuacheni unafiki Tuangalie Msingi wa Mabishano tusimuhukumu Msemaji wa kumtukuza Karia
 
Acha kutupiga fix, Manara ameleta hamasa gani Yanga? Miaka minne bila kombe uliona Yanga hamasa imekufa?

Yeye ni pesa za GSM ndio zimemfanya kula matapishi yake, hata swala la haya mataji wana Yanga kwa kauli moja tunakubaliana ni pesa za GSM ndio zimeleta faraha jangwani na si vinginevyo.

Hizi kama ni za ndani basi ni ndani kwako siyo ndani ya Yanga wala GSM.
 
Mwana kulitafuta mwana kulipata na ikiwezekana apigwe ban la kukanyaga au kuongelea football na kuiongelea simba popote pale. Mtu mmoja mjinga saana
 
OK.......sina muda wa kuargue na Mpumbavu
 
Acha uchawi kushabikia kwa ubaya Rizki ya mwezako
 
Punguza upimbi, nani anamtukuza Karia? Kwahiyo tuseme na wewe unamtukuza huyo punguwani Manara?
Kukbe hata wew hujui nini kinaendelea ushapitisha hukumu 😀😀Pimbi plus
 
Mi naona kuna sintofahamu inayoendelea kimya kimya baina ya manara na bumbuli

Nafasi ya bumbuli ni kama inasahaulika yani since manara kaja Yanga taratibu naanza kuona uwepo wa bumbuli pale yanga umeanza kufifia.

Yanga imeweza kudumu na bumbuli kwasababu ya busara lakini manara amekuwa kipenzi zaidi cha mashabiki kwasababu ya mtindo wake wa ku attack timu au uongozi mzima wa Simba.

Siku ambayo Yanga imechukua kombe sikuona sehemu yeyote ambayo bumbuli alipostiwa picha na club yake akiwa ameshika hilo kombe

Lakini manara ambaye ni mdogo kicheo ndio amekuwa karibu kwenye kila kitu ambacho Yanga inaratibu.

Kuhusu nkataba wa manara kuisha mwaka mmoja sioni kama itakuwa ni kigezo cha kumtimua, inawezekana akaongezwa mkataba na ukakuta amepewa cheo kikubwa zaidi ya hicho.

Ila ukiniambia bumbuli life span yake imefikia ukingoni siwezi kubisha.
 
Gsm ni wafanyabiashara wanamapungufu tunayajua mengi tu. I
Illa wakimgangania Manara kupata wanachotaka watamkimbia hata wao Manara kwa sasa hayupo sawa kuoa kuoa tena bila kificho kujigamba hii ni tabia za malimbukeni - unaona kabisa ataporomoka.
 
Shafii dauda akikuwa mjumbe wao
 
tatizo la manara mlililea nyinyi makolo . alipokuwa akiwakashifu yanga na kuwatukana hamkuwa kunyanyua midomo yenu kumkanya. Leo ndo mmejua kuwa jamaa ni mlopokaji?
Manara hata wakati yupo simba mimi nilitofautiana naye kwa mambo mengi husuani yale ambayo yalikuwa rahisi ku reason kwa akili ya kawaida tu

Mfano kuna lile tukio la yeye kuongea mbele ya camera kuwa ametumwa na familia ya MO kuongelea swala la upoteaji wa MO

Alikuwa na kawaida ya kuwasema yanga kwa dhana ya utani na hapo mimi sikuwa na noma as long as hatukani, ila hili la kusema familia mmemtuma ilikuwa ni extreme.

Manara anapiga vijembe kwa simba kuanzia viongozi hadi na mashabiki, lakini bado nam treat kama utani wa soka

Ila akiongelea mambo personal hapo lazima nitofautiane, au malalamiko yake ya watu wanao respond back michambo yake kwa kudai kuwa wana wivu naye kwasababu ana followers wengi au kwakua anapata deals nyingi za ubalozi mi nitamuona mjinga tu.
 
Nimekumbuka alikuwa na bifu kali na Kitenge hadi wazazi wakaingilia kati kuweka mambo sawa.

Alifikia kusema Kitenge alidondosha hirizi ITV, ila Jamaa ana shida isiyovumilika.
 
umebaki Yanga na akili zako. Tunaweza kuleta ushabiki lakini kwenye mambo ya msingi tuwe serious kama hivi
 
kwa hiyo kwako wewe manara akiwa simba mamho mengi aliyokuwa akiiongelea yanga wewe ulikuwa unachukulia ni utani wa jadi . manara aliwahi sema ukiwatoa Baba yake na Mzee Kikwete mashabiki wote wa Yanga hawana akili . kwako wewe na huo nao ulikuwa utani ? Kama ni utani kwanini amtoe baba yake na mzee JK?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…