Thamani ya maneno POLE na SAMAHANI katika Mahusiano

Mi unafikiri hata napata nae shida mkuu waaala sipati nae tabu,,Hutu wangu anaomba radhi kwa ishara tu na anakubali kosa kwa kukaa kimya huwa hajibu kitu kama amekosea baas,,na akishajua amekosea chochote unachoomba utapewa hata usichoomba
 
Inategemea unaongea nae vipi akikukosea
Ukija juu km kifuu hatosema samahani

Ila onyesha alivokukera kwa njia isiyomkera yeye
Mfano;kakukatia simu labda kwny maongezi muhimu au kasema neno baya kwako

Legeza sauti na tone iwe neutral, mwambie kitu km; mfano Dady kweli we ndo wa kunikatia simu mimi..ts not fair jmn ,unanionea....tone iwe chini usiwe km unamfokea bali km unalalamika mana for real kafanya kitu cha kukuumiza

Au Bby umeisoma msg yangu jmn afu ukanchunia tu...nk

Rejea hvo kuendana na matukio..akikukera mweleze huku unadeka hivii..afu nuna kdg ...km anakupenda utaona tuu
Noo Mpenzi sio hivo m sorry...au samahani mama nlikua tite sijasoma msg yako vzur nk

Napo yategemea na mood yake na we pia ukikasirika sio rahisi kudeka bt ukijifunza utaweza

all in all 'neno la upole hugeuza hasira'
 
Kuna kuomba msamaha alafu kuna kumfanya mwombaji msamaha mtumwaa. Kama mimi ni mwepesi tu kuomba msamaha ila kosa lisiwe fimbo ya kuninyanyasa
 
Asante kwa kutuelewesha,tutajitahidi kufanyia kazi,ila tukiharibu kazini tunapiga mpaka magoti ila huku nyumbani ndio inakuwa shida,lakini moyoni huwa tunajutia kweli,mi nadhani ni kwasababu wanaume wengi tuna aibu...
 
Nina mke na watoto wanne na Niko na BA yangu bila kuomba msamaha sijuagi huwa napendaga kusema YAMEISHA ,TUYAMALIZE ,TUACHANE NAYO,YAMESHAPITA TUGANGE YAJAYO sasa sijui hayo
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Jf bwana!
 
mwenye huu uzi atakua ashaolewa asaiv anatupenda wanaume hatatunanga tena, tuombee atulie huko aliko asije achwa
 
Sio hatujui
Mimi kwa mfano ,najua kuomba msamaha lakini sipendi
 
Mimi huwa naomba msamaha na sjawahi kuona kama ni weakness, isipokuwa nione kabisa dhahiri makosa yangu. kuomba msamaha hakunifanyi a lesser man. Bali kuna nifanya a responsible man
Thats right. Tatizo wengi wa dad zetu wanataka kuwa macho man. Muhuni, anae watreat vibaya. Wenyew wanaita bad boy.

Ikitokea mwanaume alie tulia akiomba msamaha kama wewe bas wanaanza kuwa bored. Wabadilike tu
 
Nikuombe msamaha kwani papuchi unayo wewe pekee yako hapa Duniani??
 

Sema li mume langu/Li boy friend langu la Kitanzania halijui kuomba Msamaha, wewe unaanaza mahusiano na watu wa Chato halafu unategemea uombwe msamaha? then unajumuisha watu wote kama tumezaliwa chato?
 
Katika maisha pole huonesha kuguswa na kujali. Kutoa au kuomba msamaha ni kwa kundi fulani, la kwenye akili za kati. Wenye akili ndogo wao ni kulipiza. Kwenye akili kubwa wao ni kupuuza.
 
Sijui ni mimi tu ninaye experience hiki tu ila kwa mtazamo wangu wanaume tupo tayari kujishusha na kuomba msamaha, hata kama hakuna kosa ulilotenda. Trust me hakuna mwanaume anayependa nyumba ambayo haina amani.
 
Wengi hutumia maneno haya kama funika kombe mwanaharamu apite, lakini huwa hayatoki moyoni kabisa.
Kifalsafa muundo wa mahusiano hujengwa kwa maneno haya mawili yaani pole na samahani.
Ili kukamilisha mafiga matatu ne no ASANTE lazima litumike ili litengeneze pembe tatu zilizoungana na kufanya umbo moja,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…