Japo kuwa
STUNTER hajakuuliza maswali ya maana saana hasa deep kwa mtu wa level yako, watu kama nyie mna maswali yenu bwaanaaa, mambo ya kiungo sijui usichokipenda sijui mbuzi kwenye gunia hayo ni ya kina mond na wema, BTW amejitahidi kukuvuta hapa kwakuwa bold alikuwa anaonekana katika makala au andishi lake tu, Leo kujumuika hapa aiseee mungu mkubwa, ni sawa na diamond akafanye show ya bure uwanja wa taifa,
Ok labda mm niulize maswali yangu matatu tu ambayo sijaridhika nayo.
1. Ningependa kujua elimu yako stage kwa stage kama fundi wa tanesco anavopanda ngazi zake kumfungia mteja mpya umeme, [emoji3][emoji3][emoji3] from vidudu- ------++
2. Umesema umeanza kutumikia taifa tangu upo shule, JE KIVIPI? Kuna ukakasi nauona hapa ukizingatia na umri wako sio kivileee hadi tukuweke katka list ya waliosoma kipindi cha mwalimu....
Tungependa utuambie ni kazi gani hiyo najua unaendelea nayo, kazi gani kwa serikali gani ya kukufanya ulale hadi saa 3/4 asubuhi?
3. Hili linaweza tegemeana na swali la pili kiasi fulani, kuhusu kibiti umesema kuwa wahusika walikufuata kukuomba ushauri how? Waache mawaziri wastaafu, wabunge wa upinzani mbali na kufuatwa hawaruhisiwi hata kuzungumzia hiyo kitu. Kwanini wew?
Inatosha kwa sasa nikikumbuka jambo nitauliza tena
Cc
The bold