The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

Kikwete apokewa kwa mabango Buzwagi
*Yeye awaambia matatizo yao yatashughulikiwa na mkoa
*Barrick wasema Karamagi aliwaita kusaini mkataba London

Na Mwandishi Wetu, Kahama

WANANCHI wa vijiji vya Kakola na Tegete wilayani hapa, jana walizuia kwa muda msafara wa Rais Jakaya Kikwete kwa mabango wakati akielekea katika mgodi mpya wa madini wa Buzwagi jana. Rais Kikwete yupo katika ziara ya siku nane kutembelea na kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo mkoani Shinyanga.

Wananchi wenye mambango na wasio na mabango, walijipanga katikati ya barabara na hivyo kuzuia msafara wa Rais ambao ulikuwa ukielekea katika mgodi mpya wa Buzwagi ambao ulizua mjadala mkubwa baada ya Mbunge wa Kigoma Kasikazini, Zitto Kabwe, kuwasilisha hoja binafsi akitaka kuundwe Kamati Teule kwa ajili ya kuchunguza mazingira ya utiwaji saini wa mkataba wa mgodi huo uliofanyika jijini London Februari mwaka huu na waziri wa nishati na madini, Nazir Karamagi.

Wananchi hao waliokuwa wamejipanga barabarani, walikuwa na mabango mbalimbali yakionyesha shida wanazokumbana nazo kila siku na kumtaka Rais Kikwete kutoa tamko kuhusiana na kero zao. Katika mabango hayo kulikuwa na ujumbe kama "Tunataka huduma za maji na umeme, tunataka barabara ya lami, asilimia 70 ya dhahabu inakwenda sisi tunaachiwa 30, tunakwenda wapi?

Baada ya kusimama, Rais Kikwete aliwaambia kwamba matatizo ambayo wanakumbana nayo kila siku yatashugulikiwa na serikali ya mkoa na kwamba huduma za maji zitakamilika baada ya mradi wa maji kutoka katika Ziwa Victoria kuhitimishwa.

Hata hivyo, Rais Kikwete, wakati akihutubia wananchi katika mgodi wa Buzwagi, hakuongelea mjadala unaondelea sasa dhidi ya mazingira ya utiwaji saini wa mkataba wa mgodi huo huko London, Uingereza. Badala yake, Rais alishukuru kampuni ya Barrick kwa kukubali kutoa fungu katika mapato yake na kuzipa halmashauri za wilaya zinazozunguka migodi hiyo. Pia alishukuru kampuni hiyo kwa kujenga nyumba za wanakijiji ambao walikuwa katika maeneo ya machimbo ya migodi ya dhahabu.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Barrick, Deo Mwanyika, alisema ni kweli mkataba wa mgodi wa Buzwagi ulisainiwa nchini Uingereza. "Ni kweli kabisa mkataba wa Buzwagi ulitiwa saini nchini Uingereza baada ya kuambiwa kufanya hivyo na Wizara ya Nishati na Madini," alisema Mwanyika.

Alisema ulipowadia wakati wa kusaini mkataba wa mgodi huo, alimpigia simu Waziri Karamagi, lakini yeye alimwambia aende wizarani kwa ajili ya kupata maelekezo. Mwanyika alipokwenda wizarani, aliambiwa waziri alikuwa Uingereza na Rais Kikwete hivyo, wampekekee huko akausaini.

Pia Mwanyika alisema ni kweli walisaini mkataba huo hotelini kwa kuwa Barrick hawana ofisi London bali ofisi yao ipo Canada. Hata hivyo, hakueleza kwa nini hawakusaini mkataba huo katika Ubalozi wa Tanzania ulioko London Uingereza. Mwanyika alisema walilazimika kumfuata Waziri kwa kuwa muda wa kusaini mkataba ulikuwa unaelekea ukingoni.

Mapema Rais Kikwete aliwahakikishia wananchi wa Kakola kuwa hawatahamishwa kutoka katika kijiji hicho ili kutoa nafasi ya kupanua mradi wa machimbo ya dhahabu ya Bulyanhulu. Rais Kikwete aliwahakikishia wananchi hao akiwa njiani kuelekea Kahama ambako alifungua shule ya sekondari na nyumba za wananchi wa Buzwagi zilizojengwa na kampuni ya Barrick kama fidia ili kupisha mgodi mpya wa Buzwagi unaomilikiwa na kampuni hiyo.

"Hamtahama na matatizo yenu mengine mtaendelea kuyazungumza ili mpatiwe ufumbuzi," alisema Rais Kikwete. Vilevile, aliwahakikishia wananchi hao wa Kahama kuwa ahadi zote alizotoa wakati wa kampeni zitatimizwa kama vile kuleta maji kutoka Ziwa Victoria ambapo vijiji kumi vitarajia kufaidika.

Alisema majaribio ya maji yanatarajiwa kufanyaika Septemba na baadaye mradi kukamika Desemba mwaka huu. Ahadi ambayo Rais alitoa ni ujenzi wa shule ambapo awamu yake ilikuta shule 78 na sasa ziko shule 265 yaani shule mpya 187.

Kuhusu ahadi ya barabara Rais Kikwete alisema tayari tathimini imeanza na ahadi zote zilizotolewa wakati wa kampeni za mwaka 2005 ziko katika hatua mbalimbali za utekelezaji.
 
sasa huu ni uchafuzi. wenzio wameshaanzisha mada na hili uliloposti limeshapostiwa,lakini wewe mwenzetu ahah! unaamua kupost nyingine ili kusukuma mada muhimu chini. Hivi huwa husomagi walikoandika wenzako? wewe unaboa! Kabla hujaposti kitu kile kile angalia basi kama mwenzako ameshatangulia siyo unaposti tu, inakuwa kama "kiziwi ataka kusikia" unisamehe kama nimekuudhi.

Asante.
 
Mh. Zitto

Tunashukuru sana kwa viambatanisho...............kwa kweli kama kuna mtu hajaelewa hili saga la Karamagi et al na asome hivyo viambatanisho. ktk nukuu za Bunge soma sehemu za Mh Zitto.

The most interesting ni kile kiambatanisho cha pili toka gazeti la the Citizen......hawa akina Lisu Tundu ni watu muhimu sana ktk jamii yetu Tanzania..............hebu angalieni hiki kipande

Executive Director of the Lawyers Environmental Action Team (LEAT) and well-known critic of the mining industry, Tundu Lissu, told Sunday Citizen on Friday that he is not surprised that the government has actually failed to do away with the controversial Clause, which they claim to have done, even though it is detrimental to the country.

This, he said, is because the Investment Act of 1997 makes it difficult for the government to execute such changes.

Section 19 (1G) of the Investment Act of 1997 states: "A business enterprise in respect of which a certificate is granted under this Act shall be entitled to the benefits which are applicable to that enterprise under the provisions of the Income Tax Act, 1973, the Customs Tariff Act 1976, the Sales Tax Act, 1976, or of any other written law for the time being in force."

Section 19 (2) goes on: "For the purposes of creating a predictable investment climate, the benefits referred to under sub-section (1) shall not be amended or modified to the detriment of the investors enjoying those benefits."

Lissu said that while the government is making loud noises about having removed the said Clause, presenting evidence to the Parliament, they have quietly reinstated the Clause that provides too much benefit to mining companies.

He added that because many Tanzanians, including parliamentarians, are not well versed in law, and do not bother to read and investigate, government officials get away with blindfolding the nation.

Confirming to the Sunday Citizen that the Clause does exist in the Income Tax Act (1973), amended in 2002, Lissu said: "You are absolutely right. Here is my copy of the Income Tax 1973, amended in 2002 and the 15 % clause is here."

 
Taarifa zilizoingia muda mfupi ulipita ni kuwa Rais Kikwete amezuiwa na wananchi kuingia Buzwagi, na msafara wake umegeuza njia kurudi Bulyanhulu (ambako tayari alishatembelea)...

Kwa mliosikiliza VOA...ni kweli msafara ulilazimika kurudi bulyanhulu?

Tanzanianjema
 
subirini magazeti mengine ya kesho. Miye source zangu zilikuwa kwenye msafara, na nimeona hata mwananchi wametone down kilichojiri hasa.
 
Defu Gazati La Mwananchi Linamilikiwa Na National Media Ya Kenya Lakini Kwa Hapa Tanzania Mmoja Wa Wanahisa Ni Ali Mafuruki Kama Unamjua Huyu Jamaa .
 
Kama Watu Wanatumiana Mikataba Na Tenda Nyeti Za Serikali Kwa Njia Ya Email Sioni Sababu Ya Kumlaumu Karamagi Kwa Hili
 
Kama Watu Wanatumiana Mikataba Na Tenda Nyeti Za Serikali Kwa Njia Ya Email Sioni Sababu Ya Kumlaumu Karamagi Kwa Hili

Mikataba na tenda nyeti zipi hizo?

Tanzanianjema
 
Ziko Nyingi Tu Watu Wanatumiana Kwa Njia Ya Mtandao Na Saidi Zimeshakuwa Attached Mtu Ana Print Kwahiyo Hii Ya Karamagi Sio Mpya Hapa Nchini
 
Defu Gazati La Mwananchi Linamilikiwa Na National Media Ya Kenya Lakini Kwa Hapa Tanzania Mmoja Wa Wanahisa Ni Ali Mafuruki Kama Unamjua Huyu Jamaa .

Hujui hisa za duguyo Rostam ama unakwepesha hilo?

Tanzanianjema
 
Bubu,

Magazeti ya Tz yameripoti kinidhamu nidhamu; VOA Kiswahili jana jioni wanaema Rais alizuiwa na Wananchi waliojipanga barabarani na hivyo msafara wake kulazimika kusimama (alisimamishwa).

VOA wanaripoti kuwa pamoja na Rais kuwa anajibu malalamiko yao bado wananchi walikuwa wakinong'ona-nongona kuonyesha kutoridhishwa na majibu ya Mh. Rais. Wananchi walimueleza Rais kuwa umasikini wao ni mkubwa sana pamoja na kuwa wanao dhahabu.
 
Bi Centi umeniacha hoi kidogo kwa neno lako la kusema wamwache Rais.Kwa nini unatka wamwache ? Ujinga wa Karamagi can only be stopped by JK na si zaid ya hapo . Tumempa dhamana JK na yeye kampa mamlaka mshikaji wake Karamagi. Now wana demand maelezo toka kwa Mbunge wao ambaye ni Kilaza na yes man na mtiifu kwa Chama what will he say ? Kumbuka jimbo lina wananchi wa Vyama vyote , na yeye ni Mbunge wa CCM. Kumbuka pia kwamba dhahabu yao inaenda Serikali kuu moja kwa moja na huko ndipo alipo JK .Bi Centi nakuuliza kitu hapa. Leo unasema Buzwagi waende kwa Mbunge wao mtiifu kwa CCM je richmond sisi twende jimbo gani ?
 
Defu Gazati La Mwananchi Linamilikiwa Na National Media Ya Kenya Lakini Kwa Hapa Tanzania Mmoja Wa Wanahisa Ni Ali Mafuruki Kama Unamjua Huyu Jamaa .
Huyu Mfuruki ni mwenyekiti wa bodi kutokea upande wa Nation ya Kenya, nafikiri ndio waliomnunua Balozi Ruhinda (I stand to be corrected). Rostam bado ana hisa kama zamani lakini siyo majority shareholder isipokuwa ana influence kwa vile timu yote ilyopo ni ya kwake.
 
Sijui wananchi wataendelea kukumbuka adha hizi hadi siku ya uchaguzi?


Viongozi wa CCM wanatafuta furaha ya kweli kwa kujirimbikizia Fedha haramu.

Madilu,

Napenda kukwambia kuwa wakati wa uchaguzi ukifika watsahaulishwa kwa kupewa Tshirts, Kofia na Khanga pamoja na kilo chache za sukari,pamoja na burudani ya TOT then ghadhabu zao zitatulia na CCM itaendelea kuwa nambari Wani!

Viongozi wa CCM wanatafuta furaha ya kweli kwa kujirimbikizia Fedha haramu.

Tutazifuata hukohuko Uswisi! Hata kama watazificha kuzimu tutamwamuru Shetani azirudishe!
 
Kutoka Tanzania Daima:

Jinamizi la Zitto lamfuata Kikwete
Wananchi wenye mabango waandamana


na Mwandishi Wetu



KIWINGU cha hoja ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini aliyesimamishwa, Kabwe Zubeir Zitto (Chadema), ya kupinga utiaji saini wa mkataba wa uchimbaji madini kati ya Kampuni ya Barrick Gold Mine na Waziri wa Nishati na Madini, sasa linaonekana kupanda juu na kumfikia Rais Jakaya Kikwete.
Hali hiyo ilijionyesha jana wakati Rais Kikwete alipokuwa ndiyo kwanza ameanza ziara yake ya kikazi mkoani hapa, kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo, zikiwamo zile za madini.

Akizungumza mbele ya Rais Kikwete, Mkurugenzi wa Barrick, Deo Mnyika, alisema kampuni yake ilikuwa imesikitishwa na hoja hiyo ya Zitto ambayo mbali ya kumuelekeza Waziri Nazir Karamagi, ilikuwa ikigusa moja kwa moja maslahi yao pia.

Kikwete alikutana na ujumbe huo wa Barrick wakati alipotembelea mgodi wa Bulyanhulu, ambao ni moja kati ya miradi minne ya uchimbaji wa madini inayoendeshwa na kampuni hiyo, mbali ya ule wa Buzwagi ambao ndiyo uliozaa hoja ya Zitto, hata kusababisha Bunge lifikie hatua ya kumsimamisha kwa miezi mitano.

Mnyika, alisema utiaji saini wa mkataba huo ulizingatia taratibu zote, na kwamba ulilazimika kusainiwa Uingereza kwa kuwa muda wa kufunga mkataba ulikuwa umewadia.

Alisema wao ndio waliomfuata Waziri Karamagi nchini Uingereza ambaye alikuwa katika ziara na Rais Kikwete.

Mnyika alisema wao hawana ofisi nchini Uingereza, bali makao makuu ya kampuni hiyo ya Barrick yapo Toronto, nchini Canada.

Kuhusu kulipwa fidia kwa wananchi wanaoishi jirani na eneo la mgodi wa Buzwagi, mkurugenzi huyo, alisema kuna makundi mawili ya wananchi (kundi la watu 25 na 12), ambao wamegoma kuhama kwa madai kuwa kiwango cha fidia hakilingani na thamani ya mali zao zilizopo.

Aidha, katika Kijiji cha Kakula, kilicho jirani na mgodi wa Bulyanhulu, Rais Kikwete alikutana na mabango ya wananchi waliokuwa wamebeba mabango mbalimbali wakiomba wasihamishwe katika eneo hilo.

Pia wananachi hao katika mabango yao hayo, walieleza matatizo yanayowakabili ambayo ni tatizo la umeme, ajira na barabara.

Akijibu ujumbe wa mabango hayo, alipowahutubia jana, Rais Kikwete, aliwahakikishia wananchi hao kwamba hawatahamishwa.

Kuhusu suala la ajira, alisema kampuni hiyo imeshatoa ajira 1,500 na kwamba itaendelea kutoa ajira kulingana na mahitaji yao.

Ingawa rais alipopata fursa ya kuhutubia katika eneo hilo, hakugusia kuhusu malalamiko hayo ya Barrick kuhusu hoja ya Zitto, aliishukuru kampuni hiyo kwa kuboresha huduma za kijamii, ikiwamo kuwajengea nyumba bora wananchi wa Bulyanhulu.

Rais aliwataka wawekezaji wengine nchini, kuhakikisha wanaiga mfano wa Barrick katika kuwajali wananchi kwa kuwapatia huduma bora wanazohitaji.

Kwa mara ya kwanza, hoja ya Zitto kuhusu mkataba wa Buzwagi, ambao kwa wiki moja sasa imekuwa ndiyo ajenda kuu katika vyombo vya habari, ilianza Julai 17, mwaka huu, siku Waziri Karamagi alipowasilisha makadirio na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka 2007/08.

Zitto katika hoja yake hiyo, aliahidi kuwasilisha hoja ya maandishi akilitaka Bunge kuunda kamati teule ya kuchunguza uamuzi wa Karamagi wa kusaini mkataba huo London, Uingereza na tena baada ya rais kutangaza kuwa, serikali ilikuwa imesitisha mikataba mipya ya madini hadi baada ya kamati aliyoiunda kuhusu utata uliopo katika mikataba hiyo kumaliza kazi yake.

Zitto, mbunge mdogo kuliko wote wa kuchaguliwa, alitoa rai hiyo muda mfupi baada ya Bunge kupitisha bajeti ya wizara hiyo, jioni ya siku hiyo hiyo.

Kikubwa kilichomfanya mbunge huyo afikie uamuzi huo wa kutaka kuchunguzwa kwa Karamagi, kilikuwa ni majibu ya waziri huyo kuhusu uamuzi wake wa kusaini mkataba wa madini kati ya serikali na kampuni ya madini ya Barrick nje ya nchi.

Zitto aliielezea hatua hiyo ya Karamagi kuwa inayokwenda kinyume na maelekezo ya Rais Kikwete ya kutosainiwa kwa mkataba wowote mpya kabla ya kazi ya kuhakiki mikataba ya zamani haijakamilishwa na ripoti kuwasilishwa na kamati maalum.

Aidha, mbali ya hilo, Zitto, mmoja wa wabunge machachari wa upinzani, aliliambia Bunge kuhusu kutoridhishwa kwake na majibu ya waziri huyo, juu ya uamuzi wake wa kusaini mkataba huo wa madini, Uingereza badala ya Dar es Salaam.

Alisema kuwa, sababu alizozitoa Karamagi kuhalalisha kuusaini mkataba huo nje ya nchi, bado hazijitoshelezi, hivyo upo umuhimu mkubwa wa suala hilo kuchunguzwa kwa kina na Bunge kama chombo huru kinachoisimamia serikali.

"Majibu kuhusu mkataba huo si sahihi. Waziri amedanganya katika majibu yake, napenda kulitaarifu Bunge lako tukufu, kwamba nitawasilisha hoja ya kimaandishi kutaka hoja hiyo iundiwe kamati teule ya kuchunguza," alisema mbunge huyo Julai 17.

Akijibu hoja hizo za Zitto kwa mara ya kwanza hiyo Julai, Karamagi alikiri kusaini mkataba huo huko London, akisema alifanya hivyo kwa nia njema, akirejea historia yake ya kutokea katika sekta binafsi ambayo inamfanya aone suala la muda kuwa ni jambo muhimu.

Hata hivyo, alisema wakati akisaini mkataba huo, tayari ulikuwa umeshapitiwa na kuhakikiwa na timu ya wataalamu wa wizara yake, Mwanasheria Mkuu na Kamati ya Ushauri wa Madini kama taratibu zinavyotaka.

Jumanne iliyopita, baada ya kupata baraka za Spika wa Bunge, Zitto aliwasilisha hoja yake binafsi ya kutaka kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza utiaji saini huo.

Hata hivyo, baada ya Karamagi kupata fursa ya kuandaa majibu ya serikali kuhusu madai hayo, mjadala kuhusu hoja hiyo ya Zitto ulimalizika kwa Bunge kufikia uamuzi wa kumsimamisha ubunge kwa miezi mitano, akituhumiwa kusema uongo bungeni.

Uamuzi huo wa Bunge umepokelewa kwa malalamiko mengi kutoka kwa wanasiasa, hususan wale wa upinzani, wanaharakati na wanasheria mbalimbali ambao wanaiona hatua hiyo ya Bunge kuwa iliyochukuliwa kisiasa zaidi badala ya kikanuni na kisheria.

Tangu Bunge lipitishe uamuzi wake huo, umaarufu wa Zitto umepanda kwa haraka hadi kufikia hatua ya kumfanya awe ndiye gumzo kuu la kisiasa kwa kipindi chote hicho.
 
nasikia msafara wake umekwamishwa kuingia Buzwagi wananchi wanataka wapewe maelezo... mbona mbunge wao hakuambiwa kuwa mkataba umesainiwa?

Mwanakijiji,

Hii uliitoa wapi? Kwenye vyombo vyote hakuna sehemu niliposoma au kusikia kwamba wananchi walikuwa wanahoji kusainiwa kwa mkataba.
 
Mtanzania what a question you are bringing here ? Wote tumesoma habari hii jana na mtu akaleta habari toka Mwananchi leo unasemaje?The chance of the media not to tell the people about what happened jana is obvious.JK na kundi hawataki challenge wala kuambiwa ukweli.Sasa Channel 10 walikuwepo na wamesema walichoweza wewe unakataa nini ?Ama kwa vile IPP na This Day hawajaseme ?
 
Mwanakijiji,

Hii uliitoa wapi? Kwenye vyombo vyote hakuna sehemu niliposoma au kusikia kwamba wananchi walikuwa wanahoji kusainiwa kwa mkataba.


Ulitaka Mwanakijiji aitoe wapi? Wacha fujo!
 
Lunyungu,

Nimesoma makala ya Mwananchi, nimesoma Tanzania Daima na nimesikiliza VOA. Sijaona mahali popote walipoandika wananchi walikuwa wanalalamikia kuhusu mkataba wa madini uliosainiwa London.

Nitashukuru ukitoa links hizo unazo ongelea.

Labda nimepitiwa lakini mimi sijaona hicho mnachoongelea cha wananchi kupinga mambo ya mkataba.
 
Back
Top Bottom