'The Economist' Takes Gloves off on Kikwete...

'The Economist' Takes Gloves off on Kikwete...

Huwezi kunitoa Tanzania na kunipeleka eti Kenya au Rwanda kwa sababu huko kuna fursa bwelele za mimi kufanikiwa.
wewe loser watu kibao wanakimbia tz wanakwenda rwanda kudaka mishiko minene.....madokta,engineers na wengineo wamelundikana Kigali wanakula happy....hata wewe kama una qualificatio za maana toka huko kwenye box nenda kigali kwa watoto wazuri ule maisha
 
SteveD:

Ukweli wa mambo ni kuwa watanzania hatutaki kuukubali ukweli. Shughuli zote ambazo zingefanya kipindi hiki cha JK kiwe na maendeleo zilitakiwa kuwa na misingi ya miaka zaidi ya 30 iliyopita.

Technocrats waliopo Kenya au Uganda hawakwenda shule jana. Ni watu wenye zaidi ya miaka 45.

Hivi miaka yote toka tumepata uhuru tunafanya nini ???

..Tumelazwa usingizi wa pono na kuufurahia.

..Tumezinduka walau kwa dakika chache kupiga chabo. Je, tubakie katika usingizi huo mzito au tuamke kamili kamili na kupata stimulant ya kuanza nayo (upinzani)?
 
Maisha ya watu wa vijijini SSA kama anavyosema NN hayana tofauti kubwa..almost the same: hatuna tofauti kubwa!

Hata Angola, Nigeria na Guinea ya Ikweta ni tajiri sana kwa mafuta: watu wao vijijini hawana tofauti kubwa na Tz vijijini!

Exception ipo Mauritius tu: wengine wote tuko tu sawa!
 
wewe loser watu kibao wanakimbia tz wanakwenda rwanda kudaka mishiko minene.....madokta,engineers na wengineo wamelundikana Kigali wanakula happy....hata wewe kama una qualificatio za maana toka huko kwenye box nenda kigali kwa watoto wazuri ule maisha

Mkuu, Mambo ya "loser" mbona yataharibu hii thread.. please!
 
wewe loser watu kibao wanakimbia tz wanakwenda rwanda kudaka mishiko minene.....madokta,engineers na wengineo wamelundikana Kigali wanakula happy....hata wewe kama una qualificatio za maana toka huko kwenye box nenda kigali kwa watoto wazuri ule maisha

Kwa taarifa yako sibebi boksi mimi. I've got it good and I'm happy. Rwanda mnayoizungumzia nyinyi ni ile mnayoilinganisha na Rwanda ya 1994,1995,1996 na kuendelea. They hit rock bottom and nopw they are on the come up. Soon they will hit a plateau and y'all will be like what happened...they were supposed to be the next Africa's success story...

Mnakumbuka Uganda walivyokuwa touted kuwa wao ndio Africa's success story miaka ile ya 98 na 99? Where are they now? What happened? Hatuzisikii tena hizo sifa...

Hii ni kwa sababu walikokuwa wametoka kulikuwa chini mno na sasa ndio wamefikia plateau na hawaendi mbele wala nyuma.
 
Kwa taarifa yako sibebi boksi mimi. I've got it good and I'm happy. Rwanda mnayoizungumzia nyinyi ni ile mnayoilinganisha na Rwanda ya 1994,1995,1996 na kuendelea. They hit rock bottom and nopw they are on the come up. Soon they will hit a plateau and y'all will be like what happened...they were supposed to be the next Africa's success story...

Mnakumbuka Uganda walivyokuwa touted kuwa wao ndio Africa's success story miaka ile ya 98 na 99? Where are they now? What happened? Hatuzisikii tena hizo sifa...

Hii ni kwa sababu walikokuwa wametoka kulikuwa chini mno na sasa ndio wamefikia plateau na hawaendi mbele wala nyuma.
mkuu tz haiwezi kulingana na Rwanda kwa lolote wako mbele zaidi yenu watz....

....kuanzia miundo mbinu,elimu,huduma ya afya hatuwafikii ng'o watz mmerogwa.....leo raisi wenu anatalii uzunguni na kuacha wananchi wanakufa na njaa hawana chakula,malumbani yasiokuwa na msingi yanaendelea yeye kauchuna tu....

.....hivi unafikiria tz itakuja kuifikia rwanda kimaendeleo? haipo....

Ngoja niitishe press conference nikujibu vizuri...
 
Last edited:
Hiyo article ya Economist haijasema chochote kipya.

Funny thing, kwenye hii hii nchi ambayo tunaona inadhiki sana, minorities (wahindi, waarabu, wasomali, wazungu) wanaonekana mambo yao yanawanyookea na si rahisi kusikia wanalalamika ovyo kila saa. Hata wageni wanatoka nchi fukara na kuja kuneemeka hapa. Kuna kitu gani hawa watu wanaona/wanafanya sisi waafrika weusi hatuwezi? Kwanini ni sisi tu waafrika weusi tunalalamika Kikwete, CCM, serikali, viongozi, Mungu,..nk? Mpaka hata wasomi. Aibu.

Jibu, hatutengenezi vitu vya thamani. Hao minorities hapo juu wanajishugulisha na uzalishaji mali, biashara na utoaji huduma kwa ufanisi. Wengi wetu sisi waafrika weusi kazi ni utegemezi: kutegemea ajira, Rais, CCM, serikali, miujiza, ushirikina, neema za Mungu na misaada.

Sasa tuanze kuzalisha mali, kufanya biashara na kutoa huduma kwa ufanisi. Tuuze kwenye soko ndani na nje ndo "tutatoka". Mapharmasia wetu kweli hawawezi kutengeneza dawa yoyote ya kisasa? Ma-engineer wetu kweli hawawezi kutengeneza mashine yoyote? Au kifaa chochote cha umeme. Nini kinawatoa wahindi na wachina?

Haya mambo ya kulalamika uongozi mbovu hayana msingi. Nchi kama Italy inaendeshwa kimafia na kifisadi kama sisi lakini kwasababu watu wa kawaida wanatengeneza vitu na kuuza, mambo yao ni mazuri.

Miafrika mieusi mienzangu, tujishugulishe na tuzalishe. Tukiweza hayo mengine yatafuata.
 
Kwa taarifa yako sibebi boksi mimi. I've got it good and I'm happy. Rwanda mnayoizungumzia nyinyi ni ile mnayoilinganisha na Rwanda ya 1994,1995,1996 na kuendelea. They hit rock bottom and nopw they are on the come up. Soon they will hit a plateau and y'all will be like what happened...they were supposed to be the next Africa's success story...

Mnakumbuka Uganda walivyokuwa touted kuwa wao ndio Africa's success story miaka ile ya 98 na 99? Where are they now? What happened? Hatuzisikii tena hizo sifa...

Hii ni kwa sababu walikokuwa wametoka kulikuwa chini mno na sasa ndio wamefikia plateau na hawaendi mbele wala nyuma.

...okay, so that glass ceiling is genetic per se'
 
Maisha ya watu wa vijijini SSA kama anavyosema NN hayana tofauti kubwa..almost the same: hatuna tofauti kubwa!

Hata Angola, Nigeria na Guinea ya Ikweta ni tajiri sana kwa mafuta: watu wao vijijini hawana tofauti kubwa na Tz vijijini!

Exception ipo Mauritius tu: wengine wote tuko tu sawa!

MH:

Nakubaliana na wewe kuwa mambo ya vijijini ni sawa kwa nchi zote. Na vilevile msimamo wa NN ni statistical. Viongozi wetu ni reflection yetu. Hawakutulazimisha wao kuwa viongozi, na kuna wanaopiga kampeni warudi madarakani.

Pamoja na hayo ninakuwa mgumu kutumia maisha ya vijijini kama indicator. Kufanya hivyo ni sawa na mtu kulinganisha na maisha ya Ghetto Marekani na slums za Manzese na kusema kuwa Tanzania na Marekani ziko sawa.
 
Maendeleo yanahitaji suffering jamani na sacrifice.. I'm not an agro-economist lakini embu tujiulize.. How can we improve Agriculture in Tanzania.. Kiukweli... Is our technology that bad... and our brains too.. Tunamaji, tujenge ma trekta yetu wenyewe.. Serikali iiache kununua ma limousine itrain engineer, iweke hela ijenge hizi trekta.. It cant be that hard.. Wallah ntaenda kusoma engineering sasa niache kazi yangu ya sheria.. This is ubsurd. Hii article imeniudhi kweli kweli.. We need vision..


even this we cant do as a nation.. basi sisi mbuzi..

http://www.green-trust.org/junkyardprojects/FreeTractorPlans/FarmTractor#3.pdf

Serikali imejaa punda.. We need people with brains.. We create a market for ourselves
Can we not design engines tht can use alternative fuel kama bio diesel.. build tractors and then create a massive market for bio diesel.. Tuache kulima na hand-hoe.

Inamaana inashindikana kuimport the technology from China or any other country ambayo wamemaster hili tatizo...

Tumezungukwa na maji kila kona.. Irrigation... tunashindwa wakati warumi walijenga aquaducts over 2000 years ago.. Its a shame sana.. sisi hatutaki kufikiri..

Mimi ntadedicate my life to changing this.. Haiwezekani.. Labda nife... Watu wanakuwa resolved kuwa maskini (mapenzi ya Mungu)..lol its just stupid.
 
Jamani tunaposoma hizi taarifa tunatakiwa kuwa "analytical na critical" inanisikitisha sana kuona mambo ya unazi yanavyotumiwa kuposha. Mwandishi huyu wa hii article ya Economist kwa kweli ana mambwana anaotaka kuwaridhisha angali hii sentensi "Yet those who set up shop in the country are often disappointed. Tanzania, many complain, is a “slow” or even “terrible” place to do business—and “ungrateful” for foreign aid or investment."
Hawa wawekezaji wanatarajia kupata faida... Je pia wanataka kupigiwa magoti.

Matatizo ya uchumi sasa hivi niya dunia nzima JK, Godon Brown, Obama, Hu, Angela Mekel na Sakocozy wote wanaogelea kwenye dimbwi moja iweje JK apate lawama za ziada??
Jibu la matatizo ya uchumi dunia nzima ni kumwaga mapesa kwenye uchumi, Obama na G20 wanakopa China, JK anaongoza nchi isiyo kopesheka bali kupitia Benki ya Dunia njia nyingine aliyonayo ni misaada tu!!(Siyokuwa naipenda sana)

Ila kwa suala la Umeme, Bandari na Reli kwa kweli hakuna kisingizio wanastahili lawama zote. Hizi zingekuwa mkombozi wa uchumi wa TZ.
 
Nitataja kwa kifupi kwa nini Tanzania inashindwa kujitegemea na inategemea misaada na hivyo kauli za Viongozi siku zote ni kuomba omba na kung'ang'ania kuwa misaada ni muhimu na si kuimarisha uzalishaji wa mali na matumizi mazuri ya rasilimali zetu ndani ya nchi.


6. Udhaifu wa mipango na mikataba, ni moja ya mambo ambayo yanasababisha Taifa kupoteza mapato na kuishia kutumia fedha nyingi na kuombaomba badala ya kuwa makini na kujiongezea mapato na kuhakiki mipango kwa kutoa kipaumbele kwa mipango na matumizi ya lazima na yenye manufaa.
7. Hujuma. Iwe ni ufisadi, uvivu, uzembe, wizi au kukosekana kwa mwamko, Watanzania tunajihujumu wenyewe na hata kama leo tutadai Rostam, Somaiya, Manji, Mengi na Patel ni mafisadi, bado sisi wenyewe kama wananchi tunachangia kwa sehemu kubwa sana kuimarika kwa ufisadi.

Ukisoma habari hii hapa chini, inabidi ujiulize, je ni lini tutaamka na kubadilisha mwenendo wetu?

Unatafuta laana mkuu?
 
Kwa taarifa yako sibebi boksi mimi. I've got it good and I'm happy. Rwanda mnayoizungumzia nyinyi ni ile mnayoilinganisha na Rwanda ya 1994,1995,1996 na kuendelea. They hit rock bottom and nopw they are on the come up. Soon they will hit a plateau and y'all will be like what happened...they were supposed to be the next Africa's success story...

Mnakumbuka Uganda walivyokuwa touted kuwa wao ndio Africa's success story miaka ile ya 98 na 99? Where are they now? What happened? Hatuzisikii tena hizo sifa...

Hii ni kwa sababu walikokuwa wametoka kulikuwa chini mno na sasa ndio wamefikia plateau na hawaendi mbele wala nyuma.

NN:

Wewe kweli umejiandaa kuwa pariah na outcast hapa JF. JF inilishawishi kuamini kuwa Rwanda wanafanya vizuri. Lakini kuna jamaa nimekutana naye kutoka Rwanda anasema kwa mara ya kwanza nchi hiyo ndio imefikia bajeti ya kutegemea misaada kwa 50%. Hiyo ni bajeti ya mwaka jana.

Usemi wako Hatuzisikii tena hizo sifa... unakaribia ukweli wa utabiri wa kitume.
 
Zakumi,Nyani Ngabu,...

..yaani huyu Kagame alivyokunywa damu ya mamilioni ya wa-Congo leo ni kati ya viongozi "influencial" toka Afrika?

..nimeuliza mara nyingi lakini sipewi majibu. Msumbiji waliathirika kiuchumi[kilimo,miundombinu,elimu,nguvu kazi yenye elimu] kutokana na vita kwa kiwango kikubwa kuliko Rwanda. sasa kwanini Msumbiji hawasifiwi kwa kujikwamua anasifiwa huyu muuaji-mnyonya damu Kagame?

NB:

..wa-Tanzania mara nyingine wananishangaza sana jinsi wanavyofikiri.

..yaani hii kero ya viongozi mafisadi haitoshi, sasa tunatamani madikteta na wauaji kama Kagame.
 
Kwa taarifa yako, hao Kenya, Uganda, Botswana, Rwanda hawajatuzidi kihivyo. Nymba za udongo kila kona. Lishe duni. Rushwa kama kawa. Ukabila na mengineyo mengi. Kwa ujumla hali za nchi nyingi za Kiafrika kusini mwa jangwa la Sahara ziko similar. Kwa hiyo kujibu swali lako, hao iliowataja na wenyewe Ndivyo Walivyo

Labda Nyani Ngabu ndivyo lilivyo. Kama unaamini ulivyo ndivyo ulivyo na huwezi kubadilika usitujumuishe wote humo. Wengine tumeona mapungufu na tunapiga kelele watu wabadilike. Na hilo linawezekana kabisa.
 
Hiyo article ya Economist haijasema chochote kipya.

Funny thing, kwenye hii hii nchi ambayo tunaona inadhiki sana, minorities (wahindi, waarabu, wasomali, wazungu) wanaonekana mambo yao yanawanyookea na si rahisi kusikia wanalalamika ovyo kila saa. Hata wageni wanatoka nchi fukara na kuja kuneemeka hapa. Kuna kitu gani hawa watu wanaona/wanafanya sisi waafrika weusi hatuwezi? Kwanini ni sisi tu waafrika weusi tunalalamika Kikwete, CCM, serikali, viongozi, Mungu,..nk? Mpaka hata wasomi. Aibu.

Jibu, hatutengenezi vitu vya thamani. Hao minorities hapo juu wanajishugulisha na uzalishaji mali, biashara na utoaji huduma kwa ufanisi. Wengi wetu sisi waafrika weusi kazi ni utegemezi: kutegemea ajira, Rais, CCM, serikali, miujiza, ushirikina, neema za Mungu na misaada.

Sasa tuanze kuzalisha mali, kufanya biashara na kutoa huduma kwa ufanisi. Tuuze kwenye soko ndani na nje ndo "tutatoka". Mapharmasia wetu kweli hawawezi kutengeneza dawa yoyote ya kisasa? Ma-engineer wetu kweli hawawezi kutengeneza mashine yoyote? Au kifaa chochote cha umeme. Nini kinawatoa wahindi na wachina?

Haya mambo ya kulalamika uongozi mbovu hayana msingi. Nchi kama Italy inaendeshwa kimafia na kifisadi kama sisi lakini kwasababu watu wa kawaida wanatengeneza vitu na kuuza, mambo yao ni mazuri.

Miafrika mieusi mienzangu, tujishugulishe na tuzalishe. Tukiweza hayo mengine yatafuata.

Kikojozi,

Kuna maelfu ya watanzania weusi wenye entreprising mind na wanahangaika huku na kule. Lakini serikali yao ndo inawarudisha nyuma kupitia mzigo wa kodi zisizolipika. Hao wasomali na wahindi unaowasifia ni watu walio-toka nchi zilizooza zaidi kwa rushwa na corruption. Wengi wao hutumia njia chafu na zisizo halali kupata hicho unachoita mafanikio. They are defended by corrupt officials na wako tayari kulipa anything to keep going.

Watanzania wa kawaida ambao hawajaoza kihivyo hawawezi kuhonga ovyo. Ndo maana incentives za biashara hutolewa kwa hao wenye corruption. Kwa nini incentives zisitolewe kwa locals? Unadaiwa income tax wakati unaomba lesseni ya biashara.

Muajiriwa wa kibongo wa leo ndo mfanyabiashara wa kesho (at least some percentage). Ikiwa waajiriwa hawa wamebebeshwa mzigo wa kodi ambazo hao wageni hawalipi (through corruption) huoni kuwa uwanja umepinduliwa against them? This is where the government is needed. Watanzania hawataki serikali iwagawie hela, ndio wanaipa hela. Serikali inatakiwa iwape mazingira badala ya kushirikiana na watu ambao wamebomoa kwao kuboma na Tanzania.

Watanzania wanataka bandari iendeshwe kitaalam ili na wao biashara zao ziwe competitive. Watanzania wanataka mfumo bora wa umeme ili biashara zao ziwe competitive. Kusifia hao unaowaita wasomali na waasia eti hawalalamiki wakati unaona wageni wanaokuja kuwekeza wakilalamika kilio kile kile cha watanzania ni kusifia upuuzi na kutoelewa tatizo.

Hao unaosema hawalalamiki ndio virusi vinavyofanya serikali izidi kubomoka na kutopea kwenye rushwa. Wengi wao wanachuma kupitia njia ambazo locals hawaziwezi kwa sababu huko walikotoka njia hizo hizo zimebomoa nchi zao.
 
Niliposoma ile article ya kwanza ya "The Economist" nilijua hawajamjua vizuri Kikwete.

Sasa naona wamem-Shwaziniga vizuri tu, sawa sawa.
 
I suspect the article originates from a Kenyan. There are indication of forceful demand for the land to be within the EAC treaty and then there is a word “Wabenzi” a colloquial language used by Kenyan. Dar never use the term.

However, it is always good to get somebody’s weakness from his/her enemies.

I can see some challenges. We Tanzanian have failed to task this human in the house to tell us the benefits of his unscheduled trips abroad.

This is a guy who had no time to be in Musoma for May Day celebrations. He was in Dar attending the mabomu business. Then fast he can leave the mabomu chaos to Copenhagen!

The article is now telling us he never harvested anything from china, something the ‘governement’ out to brief us before releasing the man for another trip which may be fruitless too.

Now we are in danger! IF he wins the next election as presumed while the bigs are realizing his flaws, then TZ is down to hell. Wait!!
 
Zakumi,Nyani Ngabu,...

..yaani huyu Kagame alivyokunywa damu ya mamilioni ya wa-Congo leo ni kati ya viongozi "influencial" toka Afrika?

..nimeuliza mara nyingi lakini sipewi majibu. Msumbiji waliathirika kiuchumi[kilimo,miundombinu,elimu,nguvu kazi yenye elimu] kutokana na vita kwa kiwango kikubwa kuliko Rwanda. sasa kwanini Msumbiji hawasifiwi kwa kujikwamua anasifiwa huyu muuaji-mnyonya damu Kagame?

NB:

..wa-Tanzania mara nyingine wananishangaza sana jinsi wanavyofikiri.

..yaani hii kero ya viongozi mafisadi haitoshi, sasa tunatamani madikteta na wauaji kama Kagame.

... isn't the term 'dictator' loosely used here?

... why are we letting this 'dictator' join forces in the making of EA federation?
 
Tusiwalaumu viongozi. Tujilaumu wenyewe kwa kuwarudisha madarakani kila chaguzi.

Wewe huoni hata huyo mwandishi wa hiyo makala kasema karibu kwa uhakika kuwa Kikwete atachaguliwa tena kuwa raisi? Viongozi wetu ni reflection yetu sisi wenyewe wananchi.

Kaka NN, je unadhani ni nini kifanyike ili tusiwarudishe hawa viongozi madarakani. Tatizo ni jinsi wananchi wengi wanaopiga kula ni kutoka vijijini na kwa kweli tayari hali yao ya maisha ni duni sana, kwa hiyo akija Jk na smile yake na mafuta kilo ya sukari, mambo yamekwisha. Labda kungekuwa na elimu kidogo juu ya long time impact ya wao kuchagua viongozi wasio bora, labda ingeleta maendeleo. Lakini kuwaelimisha watu mpaka waelewe kwamba viongozi waliopo sasa hawajaleta maendeleo ni kazi. Ni watanzania wangapi wanaweza kuchambua hali ya uchumi na kuoanisha na maisha yao. Kwa kweli tungeweza kuwaelimisha wananchi wavijijini, labda tusingeweza kurudi makosa. Bostswana kwa kweli wako angalau mbele kidogo. Sera zao ni kwa manufaa ya wananchi. Nyumba za udongo si kipimo cha maendeleo, kuendeleza utamaduni.
 
Back
Top Bottom