'The Economist' Takes Gloves off on Kikwete...

'The Economist' Takes Gloves off on Kikwete...

This article is about home, TZ. Hayo ya nchi zingine hayatuhusu. Inawezekana they are doing worse than us. This article is about Tanzania. Whether the writter is Kenyan or is echoing Kenyans sentiments about tz does not make sense.

The truth of the matter is assesment of the perfomance of the government. In which areas has the government done a good/bad job? Unfortunately it seems the mess is everywhere and the mess is increasing not improving.

This assesment trully says that the government is corrupt, inneficient, weak, etc.... Who can thrive under such leadership?? Only the corrupt! Should we all be corrupt to succeed? No corruption has limits. If we all go the corrupt way, we sink the country.
 
Mwandishi huyu wa hii article ya Economist kwa kweli ana mambwana anaotaka kuwaridhisha angali hii sentensi "Yet those who set up shop in the country are often disappointed. Tanzania, many complain, is a “slow” or even “terrible” place to do business—and “ungrateful” for foreign aid or investment."
Hawa wawekezaji wanatarajia kupata faida... Je pia wanataka kupigiwa magoti.

I think you are miss-interpreting the use of "ungrateful". I am assuming the ungratefullness being refered to is the bureaucracy, corruption, slowness of doing business in Tanzania. the policies and services that are rendered in a way that makes an investor feel like he is being punished not welcomed. You know things like...

Why does take it so long to get a business license.
Why does it take so long to get anything done "rudi kesho"seems to be Tanzanians favourite phrase.
Why is it when i go to a government office the person who is supposed to handle X is never there or if he is he wants a bribe to do his job.
...

If i am a serious investor i would also be these people are jokers and are wasting my time and money. If everywhere you turn all you get is red tape, bureacracy, corruption, incompetence and you're about to pour millions of dollars into the country.

You've gotta ask yourself are these people really serious
 
1. Katika sote tunaobonyeza keyboard na kukubaliana na gazeti la economist..ni wangapi tunapiga kura? kuibadilisha hiyo hali?

2. Kwa kiasi kikubwa tunakubali kwamba democracy ina madudu mengi...lakini vile vile any alternative is worse. Sasa jamani hizo changes zitapatikana vipi..kama tumeamua kuwaachia babu zetu na shangazi zetu-ambao hata mlango wa darasa hawakuuona..ndo watuwakilishe kwenye sanduku la kupiga kura?

3. CCM ina wanachama wangapi? na Tanzania ina wapiga kura wangapi? ukweli ni kwamba wengi hapa tunapiga kelele..lakini kikifika kipindi cha kupiga kura tunawapigia CCM..either kwa sababu wagombea ni marafiki zetu au tunawafahamu..maslahi ya nchi yanakuja baada ya urafiki. We just vote kama kutimiza wajibu bila kuangalia implications za maamuzi yetu. Bado tunawapigia kura watu kwa sababu wote ni wapenzi wa Yanga..tunakunywa nao bia Blake point..au ni washkaji tulisoma nao... Kikwete is such an example ya kura za urafiki na ushkaji. Na mataokeo siyo sisi tuu..hata The Economist wameyaona...

4. Sehemu ambayo unategemea kwamba watu wana uelewa at least..ni Bongo DSM..ambako wamejaa wasomi na wafanyakazi..wanaopata hata access ya magazeti na kuona "real life"..lakini ni sehemu kama DSM-tena Kinondoni..utakuta wamechagua mbunge kama Idd Azzan ambaye ni primary seven graduate! Kisa..Azzan ni "mtoto wa mjini". Sasa you wonder huyu msomi anayekaa Kinondoni..leo ndo anakuja kukuhubiria ubaya wa CCM...what is he/she upto!

5. Wakuu..to be a Tanzanian nowadays is increasingly becoming a liability. Morally and materially... Kwa kweli umasikini umetuandama mno. Anayebisha anaishi kwenye sayari ya Pluto au kwenye ndoto za kusadikika..We should be collectively ashamed..kuanzia kwa mama yangu Migiro New York to my grand father in the village. Haiwezekani kama taifa tukashindwa kusimama na kulinda hadhi ya UTAIFA wetu. Umasikini umekuwa badge of honour kwetu. Ni aibu..hata wewe unayeandika hapa ukiwa Japan au Atlanta..just push back your chair and ask yourself! Wewe kama ni diplomat..hata ukienda kutoa keynote address..hakuna "anayekusikiliza" wanajua ni wale wale...It is a collective shame kwetu sote! Tulifikaje hapa na tutatokaje hapa? Ndo swala la kujiuliza...

6. Tunajua fika kabisa viongozi wetu hawana interests na maisha yetu..sasa tufanye nini? Kikwete..akishinda kwa 80% hapo ni nani mwenye tatizo? ni sisi kama taifa. Mpaka tutakapojua umuhimu wa kila Mtanzania katika harakati za kuijenga Tanzania..tutazidi kupiga marktime hapa tulipo.

I always say and I say again: Stupidity is the art of doing something over and over again expecting different results.

7. Naomba watu tuache longo longo..ambao mko majuu...anzeni kufanya mpango wa kurudi home next year kupiga kura. Its the ONLY we way we can influence changes. CCM has proved hawawezi kutupeleka popote. Kama ukiona kwamba kura yako moja haiwezi kuleta mabadiliko..na wengine wataona hivyo hivyo..na tutaishia kwenye mzunguko wa umasikini. Kama hujui umuhimu wa kura moja..uliza umuhimu wa "absentee ballots" huko unyamwezini.

8. Please come and vote next year and we should be real kuchagua viongozi kwa kuangalia records zao na si urafiki. KAMA Kigoma na Karatu waliweza ..kwa nini wengine washindwe?

9. From now on..nataka hapa JF watu tuanze kufikiria kwa vitendo..na mwaka kesho is our golden opportunity..tuone wasomi wetu wanaolalamika on behalf of the oppressed watafanya nini. Maana hata tukiandika tons and tons..bila vitendo..we are doomed to fail.

Hope people can make a decision kuanza kutafuta tiketi next year waje home hata kwa siku chache..WAPIGE KURA. IT will make a difference.
 
SteveD said:
... isn't the term 'dictator' loosely used here?

... why are we letting this 'dictator' join forces in the making of EA federation?

steveD,

..the Presidents of the founding nations of EAC allowed Rwanda to join the community.

..most Tanzanians who expressed their views before Prof.Wangwe's commission objected to the idea of Rwanda being a member of EAC.
 
Well the EAC agenda is irrelevant at this point. Tanzania needs no markets, it hasnt even reached its elasticity point internally.. We have the labour force, 20 million strong, we have the reosources, water, natural gas, uranium, arable land 880,000 sq kms of it... we have ports tht are not even well developed (to their potential).. Sasa matatizo yetu ni self-inflicted.. Hatuna elimu wala afya tunayostahili... We dont need a political federation with politically unstable states.. This EAC thing should happen 30 years from now.. Kwanza tuwasomeshe watanzania.. tuwawezeshe pia.. Ilitakiwa Rais katika siku 30 za mwezi siku mbili au tatu akalime na wananchi... The man is pure mediocrity.. That is the problem..... "kilimo ni uti wamgongo" lakini hawa punda hawana akili yakufikiria self-reliance at least katika chakula.. How can we go hungry in the 21st century? That is a shame.. Alafu tunataka kuwaita wasaudia waje walime in our land.. Sasa kama sio matope akilini ni nini.. alafu itatokea njaa.. watatutumia mchele kutoka morogoro as MISAADA alafu tutawashukuru...
 
Labda Nyani Ngabu ndivyo lilivyo. Kama unaamini ulivyo ndivyo ulivyo na huwezi kubadilika usitujumuishe wote humo. Wengine tumeona mapungufu na tunapiga kelele watu wabadilike. Na hilo linawezekana kabisa.

Mapungufu tumeyaona tokea tupate Uhuru. Kipi kipya ambacho tunakiona sasa ambacho hatukukiona zamani?

Pigeni tu makelele yenu. Hata kulia lieni na msage meno kabisa. Lakini kaeni mkijua kuwa kulia lia na kupiga makelele hakutabadilisha chochote.
 
Kikojozi,

Kuna maelfu ya watanzania weusi wenye entreprising mind na wanahangaika huku na kule. Lakini serikali yao ndo inawarudisha nyuma kupitia mzigo wa kodi zisizolipika. Hao wasomali na wahindi unaowasifia ni watu walio-toka nchi zilizooza zaidi kwa rushwa na corruption. Wengi wao hutumia njia chafu na zisizo halali kupata hicho unachoita mafanikio. They are defended by corrupt officials na wako tayari kulipa anything to keep going.

Watanzania wa kawaida ambao hawajaoza kihivyo hawawezi kuhonga ovyo. Ndo maana incentives za biashara hutolewa kwa hao wenye corruption. Kwa nini incentives zisitolewe kwa locals? Unadaiwa income tax wakati unaomba lesseni ya biashara.

Muajiriwa wa kibongo wa leo ndo mfanyabiashara wa kesho (at least some percentage). Ikiwa waajiriwa hawa wamebebeshwa mzigo wa kodi ambazo hao wageni hawalipi (through corruption) huoni kuwa uwanja umepinduliwa against them? This is where the government is needed. Watanzania hawataki serikali iwagawie hela, ndio wanaipa hela. Serikali inatakiwa iwape mazingira badala ya kushirikiana na watu ambao wamebomoa kwao kuboma na Tanzania.

Watanzania wanataka bandari iendeshwe kitaalam ili na wao biashara zao ziwe competitive. Watanzania wanataka mfumo bora wa umeme ili biashara zao ziwe competitive. Kusifia hao unaowaita wasomali na waasia eti hawalalamiki wakati unaona wageni wanaokuja kuwekeza wakilalamika kilio kile kile cha watanzania ni kusifia upuuzi na kutoelewa tatizo.

Hao unaosema hawalalamiki ndio virusi vinavyofanya serikali izidi kubomoka na kutopea kwenye rushwa. Wengi wao wanachuma kupitia njia ambazo locals hawaziwezi kwa sababu huko walikotoka njia hizo hizo zimebomoa nchi zao.

Mkuu,

Kuna vitu viwili nataka tutafakari:

1. Kama hawa minorities wanaweza ku-overcome hizi changamoto zilizopo nchini kwetu, hata sisi weusi tunaweza. Admittedly, sio weusi wote hawajafanikiwa kibiashara. Pia sio minorities wote ni wahalifu.

2. Tuwe watengenezaji wa vitu (makers of things). Hatuwezi kutegemea tu primary products za kilimo, utalii na madini. We need to add value to our resources, export finished goods and earn foreign exchange. Tanzania tunatengeneza kitu gani ambacho wakenya, wamarekani, waingereza, wajapani, wachina watataka kununua kutoka kwetu kwa wingi?
 
Kaka NN, je unadhani ni nini kifanyike ili tusiwarudishe hawa viongozi madarakani.

Nini kifanyike? Nitajiongelea mwenyewe hapa. I have never voted for and I don't see myself voting for CCM for as long as I am in this world. Why Ngabu, you may ask. Well, I vote for something and with CCM I don't have anything to vote for them for. If I vote for them then I know for sure I'm voting for a bunch of unscrupulous politicians of whom I am diametrically, totally against.
 
Hiyo sababu ya saba, Watanzania, ndio kiini cha tatizo. Si CCM, si Kikwete, si serikali.

ECONOMIST wametutandika fimbo wote, kwamba Watanzania ni watu slow, tusio na mwendo wa kwenda mbele, hatuna "dynamism." Hatuna ujuzi, tumezidiwa na Wakenya na Waganda, tunawaogopa. Tuko slow wanasema mpaka tumeshindwa hata kutumia hela tulizoomba, $ 2.4bil. Ukweli si kejeli, ashakum si matusi.

Kikwete sio dawa, sio ugonjwa. Miundombinu yetu ya reli na bandari imechoka mbaya, "rickety," wanasema. Reli, bandari, ndege, barabara, magari ya usafirishaji yalianza kuchoka toka enzi Nuhu anaibuka kutoka kwenye Gharika ya Kwanza ya Dunia. Kikwete kakikuta hiki kifafa cha miundombinu, na hana dawa.

Wananchi wa Tanzania, sio Kikwete, wote tumejaa uvivu, uchovu, ukilaza, uzembe wa mawazo na kazi. Jumatatu unaingia saa sita, jana ulilala msibani ukihani marehemu Mzee Dau, baba wa shangazi yake mke mdogo wa jirani yako. Jummanne inabidi uombe udhuru kumpeleka Pili hospitali. Jumatano unaenda kwenye mazishi, haupo kazini nusu siku. Alhamisi unaondoka mapema kuwahi lifti ya Mama Tarimo maana ukiikosa hii basi usafiri jioni udhia mtupu, isitoshe yabidi uwahi kwenye send off. Ijumaa unatakiwa harusini, ulitoa mchango. Wiki ijayo huna udhuru, utajitahidi kutulia kazini unasoma "Acha Umbea" na "Alasiri," ukichoka unachomoka kidogo kutafuta supu ya utumbo, ukirudi ni kusogoa na kunywa chai na maandazi. Nusu ya maisha yako ya kazi ni livu, na mshahara utapata wote. Sio wewe tu utapata mshahara mzima, na marehemu Mzee Dau nae atalipwa.

Sasa kama hapo tatizo ni Kikwete basi waandishi wa makala hiyo wametutusi wote maana wamesema Mrisho atachaguliwa tena, wameongea kwa ukomo wa uhakika, atachaguliwa tena, na itakuwa ni kwa kishindo cha mmomonyoko wa ardhi ya uchaguzi, landslide. Kwa nini, kwa sababu Chama cha Mapinduzi kimewachota watu akili, wanasema kimetukuka katika longolongo dufu, "ponderous propaganda."

Na wametuasa kusikiliza wenyenchi ndani ya chama kutaka kuwapeleka tena wananchi kwenye Ujamaa kwa kigezo cha mporomoko wa ubepari duniani. Wachambuzi wa The Econonimist wanasema genda ulole.

Asante Dillunga kwa maelezo ambayo ni ukweli mtupu.
Bishanga nashukuru pia kwa maelezo positive....Ila hizi siasa ni mambo ya mijini na ndio maana politics za JK kushinda zitaendelea tuu.

Nimeamua nigusie posting zote mbili yani hii hapo juu pamoja na ya Bishanga...Ni postings mbili zenye jumbe ambazo zinaufanya mjadala huu kuwa wa maana sana kwa Watanzania especially hao wenye kutuongoza na wenye nafasi za kuchangia kwenye jamii kwa vitendo.

Dillunga uliyosema ni kweli lakini umezungumzia wananchi wenye kufanya kazi maofisini,na ni wazi umezungumzia tatizo hilo kama ni utamaduni wa mtanzania,na hivyo basi mtanzania kama mtanzania bila ya kujali kama ni wa ofisini huko mijini ama wakulima huko vijijini,wote tayari wako kundi moja.

Kwa upande mwingine Bishanga ametolea mifano mizuri sana tu based on points zilizoko kwenye makala hii....Kwamba tunaweza tukawekeza kwenye kilimo cha irrigation,na akatolea mfano wa bonde la mto Rufiji,tulishasema sana na wengi waliotutangulia walishasema sana,bila Kilimo hatwendi mahali.

Kilimo pekee ndio kinachoweza kumwondoa hata asiye na elimu kutoka kwenye umasikini na baada ya hapo akaweza kusomesha watoto na hence maendeleo
Maendeleo na elimu vinategemeana lakini utajiri unaweza kuleta vyote kama ukitumiwa vizuri.

Angalia ukweli mtupu kuhusu sisi kuwa na "Tiny middle class" kwenye East African population...Huku tukiwa na tatizo kama hilo bado tunatembeza bakuli,halafu kwasababu ya ukweli kwamba tuna viongozi ambao wanatoa maamuzi kwa niaba yetu wananchi,huwa ninashangazwa pale tunapotumia dhana ile ile ya kuwalaumu wananchi kwa kujifananisha na viongozi kwamba hatuna cha kufanya simply kwasababu wote sisi mpaka Kikwete ni wavivu,na umetoa mifano ya maofisini ya wananchi sambamba na Kikwete ambaye kiukweli naye hakai ofisini...Yani ukweli mtupu,ila nini cha kufanya?

Tuatauzungumzia vipi uchumi wa Tanzania bila kuhusisha kilimo? Kama mawazo yetu yamebakia kwenye kazi za maofisini na uongozi na siasa,vitu ambavyo hata hivyo hupatikana kimatabaka,je siyo sababu kubwa kuwa Taifa limekwama? Hakuna nidhamu ya kazi kwasababu hata taratibu za uajiri ni za kujuana nk.

Nchi nyingi sana ziliwapatia wananchi wao maendeleo na elimu kwa kuzitumia rasilimali zake,kwa mfano hapa USA ni miji mingi sana ilijengwa mara baada ya ugunduzi wa either madini ya shaba,gold,mafuta na hata makaa ya mawe,chumvi nk,wananchi ambao hata hawakusoma walipata maendeleo na kuwasomesha wanao na kutengeneza jamii ya na kuboresha miundo yao ya kijamii,nimetembelea miji ambayo ilijengwa na kilimo na bado Kilimo ndio kinaiendesha,pia miji ambayo rasilimali walizonazo zimeijenga na baada ya hapo kujijengea misingi ambayo ndiyo baadaye unaona kuna wasomi na wafanyabiashara wakubwa wanaoibuka na kuuendeleza utajiri ule ama kuinvest smartly...Mambo hayaanzii juu,huanzia chini,huu ni ukweli usioipingika.

Na hivyo basi kama alivyosema Bishanga na pia kama walivyosema watanzania wengine,we can kama tukibadilisha mentality yetu....Alipotupitisha mwalimu ni tofauti na walikopita wananchi wa mataifa yetu ya jirani,lakini mimi naamini kama tungepata viongozi wa maana,basi tungekuwa matawi ya juu,hatuwezi kabisa kuwa na utajiri wote tulio nao halafu bado turidhike na kiongozi mwenye kusafiri kila kukicha kuomba eti kwasababu watanzania ni wavivu wanakunywa supu tu,huo ni utamaduni wa watanzani walio wengi wenye kukaa mijini ambako hawakuzoe kuwa na kazi na hata kazi zenyewe pia hazitolewi kimaadili ya kazi nk. Na hao ni asilimia ndogo sana ya watanzani na ndio hao tunaoendelea kuwachambua kuanzia kwenye the ecomomist hadi hapa JF

Mkuu Dillunga sijui umetokea maeneno gani,lakini nakuhakikishia hao watanzania unaowaona huko maofisini wanakokunywa supu ya utumbo,maandazi na chai,huko vijijini kwenye asilimia kubwa ya watanzania si hivyo dugu yangu....Kama kweli kilimo kikipewa kipaumbele basi ungekuja na stori ya jinsi mkulima huyu ama yule alivyofanya bidii na kupata mazo bora nk.
Product karibia zote zinazotumika kwa wingi zimetokea mashambani,hata hapa USA, na miji mingi tu,hao wanaowaita blue color workers,hawajasoma,ila wako well trained kwenye shughuli flani flani za maendeleo ya kiuchumi...Something minor as packaging kinatukwamisha watanzania. Unakuta tuna uwezo wa ku export product flani lets say food product,packaging tu ambayo hata mtoto aliyemaliza lasaba anaweza kuwa trained na kurun machine,lakini hakuna mipango wala taratibu za kuelekea huko,badala yake eti tuendelee kuomba hadi hapo tutakapotengemaa,sasa sijui kutengemaa kwa namna gani maana si wanasema hata misaada mingine hatutumii? Sasa kama ni hivyo si ina maana mafisadi wanatufundisha kuitumia? Watanzania wenye kuombewa misaada ni wachache na ndio wanaopiga kura na kunywa chai na maandazi,lakini si wa vijijini....Politics hovyo sanaa!

Kuna watu wanashika jembe na wana uchungu vibaya mnoo! Hawana nafasi kwenye siasa zetu maana maisha yao hayaandikwi wala hayagusiwi kwenye mijadala ya macritic kama sisi.

Cha msingi ni sisi kuanza kufikiria kama watanzania wenye kuelewa tulikotoka na kujuwa kuwa hatuwezi kuendelea kama tutataka kujipatia maendeleo kwa kujaribu kujenga middle class bila ya kuzingatia kuwa majority ya watanzania wako rural areas...Na huku siasa zikiwa mijini huko kwenye supu na nyama choma na bia tukisubiri next campaign.

Mkuu kwa kumalizia,ni kweli uliyoyasema hapo juu lakini hukuwataja wakulima na watu wa vijijini ambapo kama kweli tunataka tujishindanishe na majirani zetu,basi ni lazima wawe included kwenye jedwali.

Bishanga pia nashukuru kwa maneno mazuri yenye kutia moyo ambayo yanaweka mtizamo mwingine chanya wakati mjadala huu ukiendelea.
Tumekikimbia kilimo kila mtu ni mjini na siasa,kweli hapo tulitegemea nini?
 
Nchi inapokosa dira na mwelekeo wa kueleweka kimaendeleo basi hakuna chochote cha maana tunachoweza kufanya. Leo hii kama ukimuuliza kiongozi yoyote kwa nini nchi ni masikini na tufanyeje kujiondoa sidhani kama utapata jibu la kueleweka na mbaya zaidi kila kiongozi atakuwa na jibu lake tofauti. Tunahitaji kuwa na uwezo wa kujibu kwa sauti moja kwamba tumetoka wapi, tuko wapi na tunataka kwenda wapi kama taifa ikiwa tunataka maendeleo.
 
wewe loser watu kibao wanakimbia tz wanakwenda rwanda kudaka mishiko minene.....madokta,engineers na wengineo wamelundikana Kigali wanakula happy....hata wewe kama una qualificatio za maana toka huko kwenye box nenda kigali kwa watoto wazuri ule maisha

Hapo ndio ninapozumgumzia,je unafikiri ni kwanini wanakwenda huko? Wananchi waliowengi wako vijijini na ni masikini,wakati wa mwalimu walikuwa wachache tu na waliajiriwa na serikali. Sasa ni juu ya nani kutransform mfumo wetu wa kiuchumi ili kuweza kukabiliana na changamoto?

Tukibaki kupiga domo na kuingiza siasa kwenye issue za kitaalam ama kiuchumi ndio matokeo yake hayo,ukada wa ccm ni priveledge kuliko qualification yoyote ile kamuulize Rostam.

Hao tiny middle class tulionayo hapo bongo can only take a bit,na wengineo wanaoendelea kugradutae hawawezi kuwafuta the rest "Majority" walioko vijijini,sasa nini kitawawezesha hao zaidi ya kilimo na labda matumizi bora a rasilimali zao?
Is BAKULI THE ONLY SOLUTION?
 
Kuna Hii Kanuni Inaitwa "Hypnosis" .

Inaweza kutumika vizuri kabisa na ku brain wash mtu na akili zake akafanya mambo ya kijinga na yasiyo na msingi kabisa.

Nimejaribu kutafuta sababu za kunifanya Kumuondoa J.kikwete kuwa kafanyiwa hypnosis against kuamini na kufia kuomba misaada kwa moyo wake wote.

I tend to beliave He is brain washed to just do it again and again and again... Ametengenezwa Kukana Uwezo wake yeye mwenyewe wa kujitegemea hata katika ngazi ya UTU huru n abinafsi. wachilia mbali kifamilia.

Nimetafuta kwa makini ni wapi imeonyesha kuwa anaamini hata kiasi kidogo dhana ya Kujitegemea sijapaona.... Au kama kuna mtu ambaye ameona kokote kuwa hata harufu ya kujitegemea anayo.... pls help.

Ndio maana yeye ni key problem of the Nation and its development!!! Ndio watanzania wote tunachangia lakini yeye kuwa kiogozi anachangia zaidi na zaidi.

Hata kijana mdogo haamini kuwa rafiki wake wa kike atakuwa anapata msaada toka kwa wanume wengine na bado akabakaia mwanaume halisi mbele ya Mkewe.

Katika hatua ndogo kama hiyo ndipo tunapata dhana nzima ya kujitegemea kifamilia mpaka Kitaifa. Ni hitaji la msingi kwa binaadamu yeyote mwenye akili timamu. Taifa gani linaogozwa na Mtu asiye jali hata chembe ya Hitaji muhimu la kibinaadamu la "Kujitegemea?"

Inakera!!!!
 
Zakumi,Nyani Ngabu,...

..yaani huyu Kagame alivyokunywa damu ya mamilioni ya wa-Congo leo ni kati ya viongozi "influencial" toka Afrika?

..nimeuliza mara nyingi lakini sipewi majibu. Msumbiji waliathirika kiuchumi[kilimo,miundombinu,elimu,nguvu kazi yenye elimu] kutokana na vita kwa kiwango kikubwa kuliko Rwanda. sasa kwanini Msumbiji hawasifiwi kwa kujikwamua anasifiwa huyu muuaji-mnyonya damu Kagame?

NB:

..wa-Tanzania mara nyingine wananishangaza sana jinsi wanavyofikiri.

..yaani hii kero ya viongozi mafisadi haitoshi, sasa tunatamani madikteta na wauaji kama Kagame.

Jokakuu:

Huwa napingana sana na watu wanaotaka viongozi visionary na madikteta. Uchumi wa leo ni very fluid, dynamic na chaotic. Anatakiwa mtu pragmatic tu kama mcheza chess.

Mcheza chess au bao ana strategies nyingi. Na strategies zake zinategemea na mpinzani wake.

Matatizo ya kuwa na madikteta na visionaries ni kutumia nguvu na wao kuwa static.

Tunachoshindwa kuelewa ni kuwa vitu ambavyo havifanyi kazi na kupitwa na wakati, hata kama vitasimamiwa na dikteta bado vitakuwa havifanyi kazi na kupitwa na wakati.
 
Nchi inapokosa dira na mwelekeo wa kueleweka kimaendeleo basi hakuna chochote cha maana tunachoweza kufanya. Leo hii kama ukimuuliza kiongozi yoyote kwa nini nchi ni masikini na tufanyeje kujiondoa sidhani kama utapata jibu la kueleweka na mbaya zaidi kila kiongozi atakuwa na jibu lake tofauti. Tunahitaji kuwa na uwezo wa kujibu kwa sauti moja kwamba tumetoka wapi, tuko wapi na tunataka kwenda wapi kama taifa ikiwa tunataka maendeleo.

Tanzania ina consumers ambao ni wachache walioko mijini,na hao wanaweza kukonsume kiasi flani tu,wengi wenye utajiri mkubwa wamewekeza kwenye siasa,na ukiwekeza kwenye siasa lazima uwe na media nk,ni kama trend flan hivi,tumeona kwa wenzetu chini ya mfumo wa ubepari.
La msingi ni kwamba ili uweze kuinua idadi ya consumers especially middle class,ni lazima uinvest mahali ambapo asilimia kubwa ya wananchi ipo,kwasababu kuwainua kiuchumi utawapa uwezo wa kuspend.
Tuna rasilimali,hazisimamiwi vizuri,tuna ardhi nzuri haiwi utilized,kile kinachopatikana pamoja na kile kinachoombwa kinaishia kwa politicians,kutoa hongo ili washinde na kujijengea utajiri.
Siyo politics kabisa kusema kwamba viongozi wetu wametulet down,inakuwa vipi tuwe na viongozi wanosema sisi ni masikini halafu wanauza rsilimali zetu na huku wakidai kuwa majirani zetu wanataka wanufaike na utajiri wetu wa ardhi,hayo mabilioni waliinvest kwenye mashangingi,mishahara mionono ambayo bado wanadai haiwatoshi,mabilioni wanayoyaita vijisenti kwenye akaunti ya nje,hawakuinvest kwenye ardhi,na huko ndipo asilimia kubwa ya wananchi ilipo,sasa si kukaribishautumwa kwa ufinyu wa fikra?
 
Mkitaka kujua nini kimeidekeza na hatimaye kudumaza Tanzania tayari mnakijua. Foreign aid.. Mkitaka CCM wacharuke pigeni kelele wasitishe misaada ya kigeni. Kwa sababu ikisitishwa ndiyo kwa mara ya kwanza ile urgency ya kusimamia fedha zetu wenyewe vizuri itaonekana, ndipo wananchi wataanza kuona impact ya ufisadi (sasa hivi hakuna anayeiona kwani pale cha kitu kiliponyakuliwa wajomba wakajaza vya kwao)..

Naamini adui mkubwa wa uhuru wetu ni misaada ya kigeni!! Ni kama toto kubwa ambalo halitaki kuachia nyonyo!
 
Naamini adui mkubwa wa uhuru wetu ni misaada ya kigeni!! Ni kama toto kubwa ambalo halitaki kuachia nyonyo!

Kweli kabisa, linataka nyonyo na pia kwa kudekezwa linaona misaada ni haki yake. Sijui nasi lini tutakuwa kama Kenya, Zambia ama Malawi tuiondoe CCM madarakani.
 
I needed to know the origin of the article before, for assessing the authenticity and intended impact of the article. I don’t want be trapped into political castigation instead of the really argument.

The sentiment of the whole article is even translated by the title? It mocks Nyerere’s famous quotation when he assured Tanzanian of running while our fellows are walking.

It is even dangerous as we are encouraged to embrace Kenya as our partner in EAC development. Kenya is our competitor. She is and will never be a partner.

But off course, our Ocean road Tenant is at no compass.
 
Mkitaka kujua nini kimeidekeza na hatimaye kudumaza Tanzania tayari mnakijua. Foreign aid.. Mkitaka CCM wacharuke pigeni kelele wasitishe misaada ya kigeni. Kwa sababu ikisitishwa ndiyo kwa mara ya kwanza ile urgency ya kusimamia fedha zetu wenyewe vizuri itaonekana, ndipo wananchi wataanza kuona impact ya ufisadi (sasa hivi hakuna anayeiona kwani pale cha kitu kiliponyakuliwa wajomba wakajaza vya kwao)..

Naamini adui mkubwa wa uhuru wetu ni misaada ya kigeni!! Ni kama toto kubwa ambalo halitaki kuachia nyonyo!

Kwa upande wa foreign aid, kwa mara ya kwanza tutakula sahani moja hapa JF.
 
Mkitaka kujua nini kimeidekeza na hatimaye kudumaza Tanzania tayari mnakijua. Foreign aid.. Mkitaka CCM wacharuke pigeni kelele wasitishe misaada ya kigeni. Kwa sababu ikisitishwa ndiyo kwa mara ya kwanza ile urgency ya kusimamia fedha zetu wenyewe vizuri itaonekana, ndipo wananchi wataanza kuona impact ya ufisadi (sasa hivi hakuna anayeiona kwani pale cha kitu kiliponyakuliwa wajomba wakajaza vya kwao)..

Naamini adui mkubwa wa uhuru wetu ni misaada ya kigeni!! Ni kama toto kubwa ambalo halitaki kuachia nyonyo!

Mwanakijiji hata hivyo kwani hiyo misaada inamwendea nani? Mimi nafikiri ni uongozi,wafadhili wao wanasema wanausikiliza uongozi ulioko madarakani madhali umechaguliwa na wananchi kwenye free elections. Hilo ni tatizo kubwa sana ambalo tulikumbana nalo hata wakati wa sakata lile la Balali.

Kama kuna watanzania wenye mawazo ya tofauti kabisa na haya wa kuomba omba,halafu wakawa wanapata hiyo misaada,basi watahakikisha inafanya kazi penny by penny,ni usimamizi,viongozi hawajawahi kuwa na nia ya kweli ya kuwasaidia wananchi,hilo liko wazi,either ni kwa makusudi ama kwa kutokujua hapo ndipo sifahamu.
Ila swali la msingi ni hilo,je kuna namna yoyote tunaweza kufuatilia kuona misaada hiyo inavyokuwa spent?

Huwa pia najiuliza,kwani na hao wafadhili hawafuatilii kama zinatumika kwa niaba ya wananchi? Ama na wao wana manufaa makubwa zaidi wanayoapata kuliko kile wanachotoa? Kwenye Capitalism is there anything as such as a free lunch?
 
Wana JF, naomba msaada nini def. ya "middle class" kama ilivyotumiwa hapa kwenye hii makala ya Economist "
...country’s tiny middle class fears being swamped in a common market by better-qualified Kenyans and Ugandans..."

na waTZ kitakwimu wanagawanywa vipi kwenye hizo classes?
 
Back
Top Bottom