Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ndio mkuuWw ni mzao wa kwanza.?
Najitahidi sana mkuu nijaribu kuongezea mengine lakini mainly ata ile situation ya kwanza nliokutumia inahusika piaNakuandalia uzi mkuu. Ila mbaya hujanieleza hasa yanayokusibu
Pole sana mkuu kwa unayopitia..Najitahidi sana mkuu nijaribu kuongezea mengine lakini mainly ata ile situation ya kwanza nliokutumia inahusika pia
Lakini ntajitahidi niweze kufanya ivo mkuu maana ni sababu zilizo nje ya uwezo wangu kutokufanikisha mpaka mda huu
Usijali mkuu tuko pamoja soon tu utaona ujumbe au ngoja nijaribu kukutumia mda huuPole sana mkuu kwa unayopitia..
Unieleze ili nijue nakusaidia vipi
Tayari mkuu pitia tu jumbe utaikutaPole sana mkuu kwa unayopitia..
Unieleze ili nijue nakusaidia vipi
Ahsante sana mkuuMkuu asante kwa hii Elimu ambayo haifundishwi shule hata katika familia zetu.
Kuna jiran yangu juzi nilikuwa napiga nae story nikamwambia huwa najiuliza hili swali je? Unamajibu yake au ulishawahi jiuliza mwenzangu kuwa hiv MAISHA ndio HIVI HIVI? AU KUNA KINGINE CHA ZIADA ? yaan
NMEZALIWA
NIMESOMA NIMEMALIZA
NIMEPATA AJIRA
NEXT NMEOA NINA FAMILIA
NEXT NI KUSUBIR USTAFU KAZI.
Sikupata majibu na yeye hakunielewaa [emoji3][emoji3][emoji3]lakin Binafsi piaa naona bado kuna kitu sijafanya na najiona nadaiwa.
Asante kwa uzi kaka ila naomba tuwe marafik mkuu tubadilishane mawazo Asante
Ahsante sana mkuu
Karibu sana mkuu. Access granted
mose tia neno hapa..
Be blessed kiongoziVisa hivi vinapendeza hapa.
Sura ya 26
Yesu akiwa Kataki. Gari la kukokotwa la Jaganati. Yesu awafunulia kwa watu wazi utupu wa matendo ya kiimani ya Kibrahmu, na jinsi ya kumuona Mungu katika Mtu. Awafundisha kanuni manani ya kufanya dhabihu.
KATIKA miji yote ya Orisa Yesu alifundisha. Huko Kataki, kando ya mto, alifundisha, na maelfu ya watu walimfuata yeye. 2 Siku moja gari la Jaganati lilikuwa likisindikizwa na kubebwa na watu wengi waliokuwa na hali ya fujo fujo, na Yesu akasema, 3 Tazamani, namna ya umbo lisilokuwa na roho lapita karibu; mwili usiyokuwa na roho nafsi; helalu lisilokuwa na moto wa altare. 4 Gari hili la Krishna ni kitu kitupu, kwa kuwa Krishna hayumo pale. 5 Hili gari ni sanamu la watu waliolewa mvinyo wa vitu vya mwili wa nyama. 6 Mungu haishi katika makelele ya ndimi; hakuna njia kuelekea kwake tokea kwenye dhabahu la sanamu. 7 Kutaniko la Mungu na mtu lipo ni moyoni, na katika sauti iliyosimama tuli azungumza; na yeye mwenye kusikia ni aliyesimama tuli. 8 Na watu wote wakasema, tufundishe kumjua Mtakatifu Mmoja mwenye kuzungumza ndani ya moyo, na katika sauti ndogo iliyosimama tuli. 9 Na Yesu akasema, Pumzi Takatifu haiwezi kuonekana kwa macho ya mwili wenye kufa; na wala watu kuona roho za Mtakatifu; 10 Lakini katika mfano wa sura yao mwanadamu alifanywa, na yeye mwenye kuangalia katika uso wa mtu, auangalia mfano wa uso wa Mungu, na kile ambacho mtu anachokitendea kwa mtu, akitendea kwa Mungu. 12 Na yawapasa mtie akilini ya kwamba mtu akidhuru kwa mawazo, au kwa neno ama kwa matendo mtu mwingine, amtendea makosa Mungu. 13 Ikiwa ungali ukimtumikia Mungu mwenye kuzungumza ndani ya moyo, basi watumikie tu ndugu zako wa karibu, na wale wasio ndugu wa karibu, wageni katika malango yako, adui mwenye kutafuta kukufanyia madhara; 14 Wape msaada maskini, na wasaidie walio dhaifu; usimfanyie madaa yeyote, na usitamanie kisicho chako kuwa chako; 15 Halafu, kwa ulimi wako Mtakatifu Mmoja atazungumza; na atatabasamu nyuma ya machozi yako, ataitia nuru sura ya uso wako kwa furaha, na kuujaza moyo wako kwa amani. 16 Na halafu watu wakauliza, kwa nani tutalitoa zawadi? Ni wapi tutalitoa dhabihu? 17 Na Yesu akasema, Baba-Mungu wetu haombi kwa upotezaji wa mimea, nafaka, au njiwa, au mwanakondoo. 18 Kile mkichomacho katika madhabahu yoyote ni mwakitupa zake. hakuna baraka yenye kumnyeshea mmoja mwenye kuchukua chakula kutoka midomoni mwa wenye njaa kuharibiwa kwa moto. 19 Wakati ungalipo ukitoa dhabihu kwa Mugnu, chukua tu zawadi yako yanafaka, au nyama na kuilaza juu ya meza ya maskini. 20 Kutoka kwa hiyo uvumba utainukia juu, ambao utakurudia na ubarikio. 21 Vunjulieni chini sanamu zetu; haziwezi kuwasikia; pindueni altare zenu za dhabihu katika makaa ya makolozeo ya moto. 22 Fanyeni mioyo yenu ni Hekalu moyo wa mwanadamu ni altare , na chomeni dhabihu zenu kwa moto wa upendo. 23 Na watu wote wakaingiwa na furaha ya kuchangamsha moyo, na wangeliweza kumabudu Yesu kama Mungu; lakini Yesu akasema, 24 Miye mtu-kaka yenu niliyekuja kuoneshea njia kuelekea kwa Mungu; msije kumuabudu mtu; mtukuzeni Mungu, Mtakatifu Mmoja.
===
Sura 44
Yesu azuru Ugiriki na kukaribishwa na Waathenia. Akuatana na Apollo. Ahutubia Wakuu wa Kigiriki kwenye Uwanja wa Jukwaa la Maonesho. hutuba.
Filosofia ya Ugiriki ilijaa kwa kweli zilizo na ukali, na Yesu alitamania kusoma na pamoja na wakuu katika shule za ugiriki. 2 Na hivyo aliondoka nyumbani Nazareti na kuikatisha vilima vya Karmeli, na bandarini alipanda meli, na baada ya muda mfupi alikuwa makao makuu ya ugiriki. 3 Sasa, Waathensi alipata kumsikia kama ni mwalimu na mfilisofia, na walikuwa ni wenye furaha kuwa yeye amekuja kwao ili kuwa waweze kupata kusikia maneno yake ya kweli. 4 Miongoni mwa wakuu wa wagiriki kulikuwapo na mmoja, Apolo, ambaye aliitwa, mlinzi wa Orako, na alitambulika katika nchi nyingi kama mwenyebusara wa kigiriki. 5 Apolo alimfungulia Yesu milango yote ya mafundisho ya kimapokeo ya wagiriki, na katika Areopagusi alisikia wakuu wenyebusara kabisa kuliko wote wazungumza. 6 Lakini Yesu alileta kwao hekima iliyo kubwa mbali kuliko ya kwao; na hivyo alifundisha. 7 Wakati akiwa Amphitheata alisimama, na Apolo alipomtaka kuzungumza yeye alisema, 8 Wakuu wa Kiatheni, sikilizeni! Katika zama za zamani kupita, watu, wenyehekima juu ya kanuni za mazingira ya asili yote, waliitafuta na kuipata nchi ambayo juu yake mji wenu mkuu wasimama. 9 Mwajua vyema kabisa ya kwamba kuna sehemu katika dunia ambapo moyo wake mkubwa hurushia juu mawimbi ya kietha ambayo hukutana na etha za kutoka juu: 10 Ambako mwangaza-kiroho na uelewa, kama nyota za usiku, hung'aa kumulika. 11 Ya zote sehemu za dunia hakuna pahala palipo na kugusishwa hisia, zaidi kurehemiwa-kiroho, kuliko pale ambako Athensi yasimama. 12 Naam, Ugiriki yote imerehemiwa. Hakuna nchi ingine imekuwa ni nchi-nyumbani ya watu wakubwa wa fikara kama vile sura ya mvuto ya mikunjo maarufu ya maandishi. 13 Wenyeji wa wakubwa na imara wa filosofia, wa ushairi, wa sayansi, na wa sanaa, walizaliwa katika ardhi ya ugiriki, na kubembea mwendo hadi kuwa watu wazima katika kitanda chenu cha mtoto cha fikra safi. 14 Sijaja hapa kuzungumzia ya sayansi, ya filosofia, ya sanaa, ya haya ninyi ni mlio bora kabisa duniani sasa. 15 Lakini mafanikisho yenu yote makubwa ni ila tu mawe yakukanyagia kuelekea alimwengu za mbali kuzidi alamu za fahamu za mwili; ni ila tu kimvuli cha sura isiyo na ukweli kamili juu ya ukuta wa wakati. 16 Lakini nitaliwaambia ninyi ya maisha ya kuzidi mbali ndani; maisha ya kiukweli ambayo hayawezi kupita zake. 17 Katika sayansi na filosofia hakuna nguvu iliyo imara vya kutosha kufaa kukaba nafasi yote nafsi roho ijitambue yenyewe, ama ikomunike na Mungu. 18 Sitaliuacha ulivyo mtiririko wa mkondo yenu mikubwa ya fikara; ila nitaigeuza kuwa matawi ya mikondo ya nafsi roho. 19 Bila kusaidiwa na Roho-Pumzi, kazi ya uakilishi huwa ikitatua tu mafumbo ya vitu tuvionavyo, na si zaidi ya hapo. 20 Fahamu za mwili zilitofanyika kuleta katika uakili picha picha tu za vitu vyenye kupita zake; hazijihusishi na vitu vya kiukweli halisi; hazimaizi kanuni ya hali ya milele yote. 21 Lakini mwanadamu anachokitu katika nafsi roho yake, kitu ambacho kitararua kutenganisha pazia ili kwamba yeye aweze kuja kuona ulimwengu wa vitu vya kiukweli halisi. 22 Tunakiita kitu hiki, ufahamu roho; wenyewe umelala katika kila nafsi roho, na hauwezi kuamshwa mpaka Pumzi Takatifu kuja kuwa mgeni mkaribishwa. 23 Pumzi Mtakatifu huyu hubisha hodi katika kila nafsi roho, lakini hawezi kuingia mpaka nia ya mtu ifungue wazi mlango. 24 Hakuna nguvu katika akili kuzungusha funguo; filosofia na sayansi vyote viwili vimechacharika kazi kupata kiashirio cha namna kuona sura halisi nyuma ya pazia; lakini ni vyenyekushindwa. 25 Springi ya siri ambayo hulegeza wazi kidogo mlango wa nafsi roho huguswa na si kingine chochote ila usafi wa maisha, kwa sala na fikara takatifu. 26 Rudini, Eh mikondo ya kisikirifu* ya fikara za Kigiriki, na kuchanganyika pamoja maji meupe na furiko tiririkaji la Roho-maisha; na tena ufahamu roho hautolala tena, na mwanadamu atajua, na Mungu atabariki. 27 Yesu alikwisha kusema hivyo akasimama kando. Wakuu wa kigiriki wakastaajabishwa na hekima ya maneno yake; nao hawakujibu.
===
Sura 52
Yesu atumia siku arobaini katika bustani za hekalu. Afaulu jaribio la tano la ubruda na kupokea shahada ya tano, USHUJAA.
BUSTANI takatifu za hekalu zilikuwa zimejaa kwa sanamu, minara ya kuinukia juu ya alama za kumbukumbu na madhabahu; hapa Yesu alipenda kutembea na kutafakari. 2 Na baada ya kuishinda mapigano nafsi yake alizungumza na mazingira ya asili katika bustani hizi kwa siku arobaini. 3 Na halafu muongozeaji njia alichukua minyororo na kumfunga yeye mkono na mguu; na halafu kumtupa kumtelekeza katika tundu la wanyama wenye njaa, ndege wasio safi, na vitu vitambaavyo. 4 Tundu lilikuwa ni lenye kiza kama usiku; wanyama mwitu walikuwa wakilia sauti; na ndege katika makelele ya hasira; namna za mijusi zikitoa mlio wao mwembamba. 5 Na Yesu akasema, ni mwenyekuwa ni kitu gani aliyenifunga mimi hivi? Ni kwanini nilikaa tu kukubali tu kufungwa kwa minyororo? 6 Nakwambia, hakuna mtu mwenye nguvu ya kuifunga nafsi roho ya binadamu. Ni kwa kitu gani pingu zimetengenezwa? 7 Na kwa nguvu zake kuu akasimama, na kile alichofikiri ni minyororo zilikuwa ni tu kamba zisizo lolote zilizoachanika kwa mguso wake. 8 Na halafu akacheka na kusema, minyororo yenye kuwafunga watu na na mizoga ya dunia imekandamizwa kuundwa katika karakana ya vitu vya bandia; vilivyofanywa kwa hewa, na kuchomelewa kwa moto usio wa kikweli. 9 Ikiwa mtu atasimama wima, na kutumia nguvu zake za nia, minyororo yake itaanguka, kama kipande cha karatasi; kwani nia na imani ni vilivyoimara kabisa kuliko minyororo iliyomigumu kabisa ambayo mwanadamu amepata kutengeneza. 10 Na Yesu akasimama wima kati ya wanyama wenye njaa, na ndege, na kusema, nini ni hili giza lenye kunifunika kote miye? 11 Ni ila tu utowepo wa nuru, na nuru ni nini? Ni ila tu pulizo la pumzi ya Mungu itetemayo katika mwenendo wa kupanda na kushuka uliokasi wa fikara. 12 Na halafu akasema, kuwe na nuru; na kwa nia kubwa sana aliimsha kuikoroga etha zaidi, na mitetemo yake itafikia wanda ya nuru; na kukawa na nuru. 13 Ukiza wa tundu la giza ukaja kuwa mwangaza wa asubuhi ya siku. 14 Na halafu aliaangalia kuona wanyama, na ndege, na vitu vitambaavyo; lo, havikuwa ndivyo. 15 Na Yesu akasema, nafsi roho huogopa nini? Hofu ni mkokoteni ambao mwanadamu huupanda kuuendesha kuelekea mauti; 16 Na anapojikuta katika chimbo la wafu, hujifunza ya kwamba amelaghaiwa; mkokoteni wake ulikuwa ni hadithi, na mauti mtoto wa bandia. 17 Lakini siku moja masomo yote ya mwanadamu yatakuwa yameshafundishwa, na kutoka katika tundu la wanyama wasio wasafi,na ndege, na vitu vitamaavyo atainuka kutembea katika nuru. 18 Na Yesu aliiona ngazi iliyotengenezwa kwa dhahabu, ambayo aliikwea juu, na juu yake kabisa kuhani aliyevaa vazi jeupe alikuwa anamngojea. 19 Na tena alisimama mbele za kiambaza cha baraza; na tena hakuna neno lililosemwa; tena hirofanti aliifikia kuubariki mkono wake. 20 Aliweka mikononi mwa Yesu kitabu kingine cha mkunjo, na katika huu mmoja kulikuwa kumeandikwa, USHUJAA. 21 Logosi alikabiliana uso kwa uso na hofu na namna za maruwe ruwe yake yote, na katika mgongano alifanikiwa Ushindi.
===
Sura 53
Yesu afaulu jaribio la sita la ubruda na kupokea shahada ya sita, UPENDO AGAPE(Pia kusemwa Pendo Manani).
KATIKA nchi yote hakuna mahala palipopambizwa kuliko vyumba urembo vya makaribisho vya hekalu la jua. 2 Wanafunzi wachache waliingia katika vyumba hivi vya kitajiri; makuhani walivitazama kwa furahiko, na kuviita majukwaa ya siri za maajabu. 3 Yesu alipopata ushindi juu ya hofu, alipata haki ya kuingia hapa. 4 Muongozeaji njia akamuongoza njia, na baada ya kuvipita vyumba vingi vilivyopambwa kwa thamani walilifikia Jukwaa la Utulivu; na hapa Yesu aliachwa peke yake. 5 Miongoni mwa vyombo vya muziki kulikuwa na Kinubi, na Yesu aliketi katika hali ya kufikiri sana akikagua kwa karibu hicho, wakati ambapo, katika hali ya ukimya, mwanamwali wa uzuri wa kupendeza sana aliingia ndani ya Jukwaa. 6 Hakuonekana kumtia machoni Yesu kadri alivyoketi na kuzama ndani, kushikwa sana na mawazo. 7 Alijipatia nafasi yake kando ya kinubi; alizigusa nyuzi zake kwa upole sana, na kuimba nyimbo za Israeli. 8 Na Yesu akapendezwa; uzuri kama huo hajapata kuuona; muziki kama huo hajapata kusikia. 9 Mwanamwali aliimba nyimbo zake; hakuonekana kana kwamba kujua kulikuwa na mtu karibu; alikwenda njia yake. 10 Na Yesu, akijisemea mwenyewe, akasema, nini ni maana ya tukio hili? Sikujua ya kwamba uzuri wa kupendeza sana kama huo na ukama-malkia wenyekuvutia machoni ulikuwa ukipatika hata mara moja katika wana za wanadamu. 11 Sikujua ya kwamba sauti ile ya malaika yenye sura hasa ya kibinadamu ya kuvutia mno, au ule muziki wa kiserafi kata siku moja kuja kutokea kwenye mdomo wa mwanadamu. 12 Kwa siku kadhaa aliketi katika hali ya kuvutiwa; mkondo wa mawazo yake ulibadilishwa; hakufikiria kitu ila mwimbaji na nyimbo zake. 13 Alitamania kumuona yeye tena; na baada ya siku kadhaa alikuja; alizungumza na kuilaza mikono yake juu ya kichwa chake. 14 Mguso wake ulimsisimua nafsi roho yake, na kwa muda, ilisahaulika kazi aliyoagizwa kuinfanya. 15 Machache yalikuwa ni maneno ambayo aliyoyazungumza mwanamwali; alienda njia yake; lakini moyo wa Yesu alikuwa umeguswa. 16 Mwali-upendo ulikuwa umewashwa katika nafsi roho yake, na aliletwa kukutana uso kwa uso na jaribio lenye kuumiza la maisha yake. 17 Hakuweza kulala na wala kula. Mawazo ya mwanamwali yalikuja; na hayakuenda zake. Asili yake ya kimwili wa nyama iliita kwa sauti ukaribu wake na yeye. 18 Na halafu akasema, lo, nimemshinda kila adui ambaye nimekutana naye, je sasa nijekushindwa na penzi hili la limwili? 19 Baba yangu amenituma hapa kuonesha nguvu ya upendo agape, ule upendo wenye kufikia kila chenye kuishi. 20 Je, huu msafi, upendo katika vyote usharabiwe ndani kwa upendo wa kimwili wa nyama? Je, nitashahau viumbe vyote, na kupoteza maisha yangu katika mwanamwali huyu mzuri, ingawaje yeye ni wa uzuri wa hali ya juu ya urembo, usafi na pendo? 21 Ndani kabisa kuzama kwenye nafsi roho yake alikuwa amekorogwa, na kwa muda mrefu alipigana mweleka na sanamu-malaika ya moyo wake. 22 Lakini siku ilipokuwa karibu kupotea, nafsi mimi yake ya juu iliinukia katika ukubwa; akajipata yeye mwenyewe tena, na halafu tena akasema, 23 Ingawa moyo wangu utavunjika sitaanguka katika azimio la shughuli yangu iliyongumu kabisa; Na nitakuwa ni mshindi juu ya pendo la kimwili. 24 Na mwanamwali alipokuja tena, na kumpa mkono na moyo, yeye akasema, 25 Mpendevu, uwepo wako wanisisimua kwa furaha ya moyo; sauti yako ni mbaraka kwa nafsi-roho yangu; nafsi yangu ya kibinadamu yangaliweza kuruka na wewe, na kuwa imeridhishwa kwa pendo lako; 26 Lakini ulimwengu wote watamania kupata pendo ambalo nimekuja kulidhahirisha. 27 Yanilazimu, basi, kukutaka wewe uende; lakini tutakutana tena; njia zetu juu ya dunia lazima zipishane mwelekeo. 28 Ninakuona katika makundi ya watu wa dunia yenye kwenda haraka kama mtumishi mfundishi wa pendo; Nasikia sauti yako katika wimbo, ambayo yaishinda mioyo ya wanaume kwa vitu vilivyo bora zaidi. 29 Na tena kwa huzuni na machozi mwanamwali akaenda zake, na Yesu alikuwa pekee yake tena. 30 Na mara moja kengele kubwa za hekalu zikalia; na waimbaji wakaimba mpya, wimbo mpya, giroto* ikawashwa mwanga, 31 Na hirofanti mwenyewe akatokea, na kusema, Wote salamu! Logosi aliyeibuka ni mshindi, salamu! Mwenyekulishinda pendo la kimwili asimama katika vima vya juu. 32 Na halafu akaweka mikononi mwa Yesu kitabu cha mkunjo ambacho kilikuwa kimeandikwa, UPENDO AGAPE. 33 Kwa pamoja walikwenda na kupitia katika giroto* ya urembo, na katika jukwaa la maakuli walihudumiwa, na Yesu alikuwa ni mgeni mwenye kuheshimiwa.
***