Da'Vinci
JF-Expert Member
- Dec 1, 2016
- 35,812
- 107,628
- Thread starter
- #201
Mkuu haya ya kuhusu kuwadahrau watoto weusi umeyatoa wapi??Sawa Mkuu umejitahidi ,
Lakini!!!! Hao watoto Maskini, kwenye Utangulizi wa Bandiko lako! wanadhihirisha nini?
Kwa nini wapo hapo? na hawana uhusiano na ulicho kiandika. au unamaanisha wazazi wao weusi (waafrica) hawakujua kusudi la kuwazaa?
Kwa nini umetuonyeshea watoto maskini kwenye akili zetu? tena wana masikitiko?
Wana dalili zote za uyatima hawa, Mkubwa kambeba mdogo! anakovu takoni tena yu uchi, wachafu, wako peku, kigodoro kichafu, wanamikamasi, wamekata tamaa, wanakula kutumia mkopo mbaya km wa kuchambia chooni, wana huzuni, je Mr Mzungu unaifurahia hii picha ya watoto wenye hali hii? kwa nini africa weusi? unaamini tunafurahia?
Umepataje ridhaa yao? au ya wazazi wao? Mbaya zaidi ni waafrica- weusi km tulivo wengi humu, ina maana gani kwa sisi wazazi wa ki-Africa, tuseme Kwa sababu labda Yesu ni Mzungu, basi hukutaka kudhalilisha rangi yake?,
Ila Nyani weusi, ( siyo maneno yangu, ndivo mnavotuita sometimes mnaturushia ndizi) watumwa wenu Rukhsa! unaweka utakavyo bila kujali itawaliza wangapi. hata chembe ya huzuni huna Mkuu?
Kwa nini hukuweka ya watoto wazungu km wewe mwenyewe? nijuavyo mimi wewe ni Mzungu- Pure, japo sijui ni wa Ulaya nchi gani, ila jina -Da' Vinci linasadifu wewe ni mzungu, Avatar yako pia ni ya Mzungu.
Siyo kama African's avatar ya Tata Nyarusare Ruya Nyamtibhita!. Nyie wazungu bana sijui tuliwakosea nini, kwa ubaguzi na madharau mmekubuhu tena, kukomesha hii ubaguzi Duniani ni kama udongo na chuma kamwe havichangamani. ki ukweli nimeumia sana,
Mkuu Jipimie mwenyewe wewe ni nani!!! au tukuiteje, na Naomba ufafanuzi.
lakini pia wapi nimesema kwamba mimi ni mzungu???????