THE MODERN WAR: Simulizi ya kijasusi mapenzi na upelelezi

THE MODERN WAR: Simulizi ya kijasusi mapenzi na upelelezi

THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya........55
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

Ni siku chache sana zilikuwa zimepita tangu Dokta Gondwe kuzikwa, Najma bado alikuwa katika hali ya maumivu makubwa. Hakuna kitu kiliwahi kumuumiza hapa Duniani kama kuondokewa na baba yake mzazi. Tena kifo cha baba yake kinakuwa ni cha kikatili sana huku muuaji wa baba yake akiwa ni mwanaume ambaye tayari alishaanza kumpenda.

Leo Najma binti mrembo alitoka nyumbani akiwa amevalia mavazi meusi akiwa bado kwenye maombolezo ya kifo cha baba yake. Alielekea makaburini ambako mafundi walikuwa wakiendelea na zoezi la kulijenga kaburi la baba yake kama alivyoagiza.
Hakuwa na muda wakutulia kabisa bado akili yake ilitamani kufanya kitu kwa ajili ya marehemu baba yake. Alishuka kwenye gari yake akatembea akivuka makaburi kadhaa kuelekea lilipo kaburi la baba yake. Mara mbele yake alimuona mwanaume mmoja akiwa amempa mgongo anasali mbele ya kaburi moja kubwa. Najma hakujali sana aliendelea na safari yake lakini alipomkaribia yule mtu naye ndio alikuwa anamaliza sara yake baadae akageuka tayari kuondoka. Uso kwa uso mtu huyo akagonganisha macho yake na macho ya Najma.
Bado lilikuwa ni tukio la kawaida kwa Najma kwani hakuiona sura ya mtu huyo kutokana na namna alivyokuwa amevaa. Alivaa barakoa nyeusi na kofia nyeusi aliyoishusha sana chini kiasi cha kufanya sura yake isionekane bali macho pekee. Kilichomsangaza Najma ni baada ya mtu huyo kushtuka sana mara baada ya kumuona. Mtu huyu alikuwa ni Inspekta Aron ambaye watu wote wanaamini amekufa isipokuwa Osward pekee ndiye anayeijua siri ya Aron kuwa hai.

Inspekta Aron alitazamana na Najma kwa sekunde kadhaa baada ya hapo akainamisha kichwa chake chini akapiga hatua kuondoka. Wakati wanapishana Najma aligeuza shingo yake kumuangalia mtu huyo lakini bado hakuweza kumfahamu ila alijikuta anapata msukumo wakuendelea kumtazama zaidi akageuka kumuangalia hadi alipofika barabarani akapanda pikipiki na kuondoka.

"Vipi unaangalia nini Najma" ilikuwa ni sauti ya kiume iliyomshtua Najma kutokea mbele yake kule alikokuwa akielekea awali akageuka haraka. Alikuwa ni Osward
"Mbona hujaniambia kama unakuja?" Aliuliza Osward huku akihema kwa nguvu mikono yake ikiwa imechafuka kwa udongo.
"Sikujua kama utakuwa hapa"
"Ahh! Sawa niliifanya ile kazi mapema tu nimeshakutumia picha WhatsApp nikaona nije huku kusaidia saidia mafundi wanaojenga kaburi kazi ikae vizuri"
"Sasa kwani wewe ni fundi si ungewapa maelezo tu halafu uendelee na mambo mengine" alisema Najma huku akichukua simu yake na kufungua mtandao wa WhatsApp.
"Tatizo na wewe unakuwa mkali sana, kwani kuna ubaya gani mimi kushiriki kila hatua kwenye mazishi ya baba mkwe wangu!?"
Najma akawa kimya anaangalia zile picha alizotumiwa na Osward ambaye naye alisogea upande wake wakawa wanaangalia wote.

"Hii ya pili ndio nzuri zaidi tukilijenga hivi kaburi la mzee itapendeza sana"
Alisema Osward
"Na hii ya tatu mbona kama nyumba?"
"Eeh! Yani kaburi fulani hivi la kishua linajengwa vizuri kwa marumaru halafu juu inakuwa kama msauzi flani hivi siku mkija kutembea panapambwa vizuri mnaweza kula hata chakula hapo" alieleza Osward
"Ahh! Hizi picha zote ulizotuma hakuna niliyopeinda, nataka kaburi liwe simple tu ila zuri kama hili" Alisema Najma huku akinyoosha kidole kwenye kaburi la baba yake Aron.
Osward akawa kimya huku akimuangalia Najma usoni.
"Vipi?"
"Unajua hili kaburi la nani?"
"Noo, nitajuaje sasa"
"Ndio maana"
"Ndio maana nini?"
"Unataka kaburi la babako lifanane na kaburi la baba wa muuaji wa baba yako"
"Una maana gani?"
"Hili ni kaburi la baba yake Aron jenerali Phillipo Kasebele"
Alisema Osward kauli iliyomshtua Najma kiasi, akawa anawaza jambo. Ni dakika chache tu zimepita amepishana na kijana wa kiume aliyekuwa akisali kwenye kaburi hilo
"Vipi unawaza nini?"
"Hivi huyu mzee ana watoto wangapi wa kiume? Si ni Tino na Aron pekee?"
"Ndio kwani vipi, alafu achana na hao watu tayari walishatuvurugia maisha kwa nini kila mda Aron, Aron yaani ni wewe na Aron uniboa kwa kweli"
"Wewe kinachokuumiza ni nini?"
"Unaudhi bana, ni kama hajamuua baba yako vile"
"Ni kweli siamini mpaka sasa kama Aron ndiye aliyemuua baba, Mungu kamchukua mapema nilitaka nithibitishe mwenyewe kama alihusika, na kama nikweli ningemuua pia"
Aliongea Najma.
"Kwa hiyo unataka kusema uliyaamini maneno ya yule mpuuzi alivyosema hajamuua baba yako?"
"Usijali bado nafuatilia sio muda nitajua ni yeye au ni mwingine" kauli hii ya Najma ilimtisha sana Osward.
"Ameshakufa achana na hayo mambo Najma"
"Siwezi kuachana nayo Osward tayari nimeshakwambia na unalijua hilo, kifo cha baba yangu bado kina fumbo kubwa, hivi kama Inspekta Aron angekuwa kweli muuaji kwa nini naye amekufa au unafikiri amekufa kwa bahati mbaya kule rumande? Alafu nasikia mwili wake umepotelea kwenye maji kirahisi rahisi tu yani watu wanafuta ushahidi, siwezi kukubali Osward siwezi"

"Sasa utafanya nini wewe mwanamke jamani"
"Kuwa mwanamke sio shida kwanza nipo na wewe hapo mwanaume suruali utanisaidia upende usipende la sivyo ndoa hamna"
"Eti nini? Mbona nimeshaongea na mama yako tumepanga kila kitu, mwezi ujao tunaanza vikao vya ndoa"
"Msivyo na haya mnapanga mipango ya ndoa msibani Shame on you!! Hebu nisikilize vizuri Osward" alisema Najma kisha akamgeukia vizuri Osward wakawa wanatazamana.
"Kwanza kabisa nitakuwa sijatenda haki kama nitaacha kifo cha baba yangu kipite bure wakati naona kabisa kuna mambo hayako sawa. Pili ni kuhusu vimelea vya V-COBOS sijasahau hata kidogo, sijasahau kuwa kuna wapuuzi wachache wanataka kutuletea janga lingine kama Korona kwa tamaa zao bila kujali maisha ya watu wengine. Nitapigana kwa nafasi yangu ingawa ulinitisha lakini kamwe siwezi kuruhusu hili litokee wakati ninao uwezo wa kufanya kitu, siwezi elewa hivyo" Najma aliongea kisha akaanza kupiga hatua kuondoka zake, Osward alijikuta anachoka akili na mwili alimjua vizuri Najma alikuwa ni mwanamke wa kumaanisha kila analoliongea. Shida ilikuwa si kumdhibiti hapana shida ilikuwa ni mapenzi ya dhati aliyonayo Osward kwa mwanamke huyo aliyemteka haswa. Osward anampenda sana Najma laiti kama angekuwa ni mtu mwingine anaongea maneno kama yale kifo cha haraka kilikuwa ni haki yake.
Osward alitamani sana Najma aachane na yote akubali tu kufunga naye ndoa waishi kama mke na mume lakini haikuwa rahisi. Endapo Najma akifuatilia akagundua kuwa kumbe Osward ndiye muuaji wa baba yake mambo yatakuwa ni magumu zaidi lakini pia akifuatilia sana kuhusu vimelea vya V-COBOS bado maisha yake yatakuwa hatarini zaidi, kichwa kilimuuma Osward.

Wakati akiwa amesimama anawaza cha kufanya mara mbele yake ilipo barabara aliona watu watatu kila mmoja na pikipiki yake wakiwa wamesimama pembeni ya barabara hiyo, wakawa wanamuonyesha ishara fulani kuwa asogee walipo. Osward aliweza kuwatambua watu hao walikuwa ni kikosi hatari cha wanawake watatu wanaojiita malaika weusi yaani Asia, Erica na Elina.
Osward akaangalia huku na kule kwa mbali akamuona Najma yuko bize akiongea na mafundi wanaojenga kaburi, haraka akapiga hatua kuwafuata Malaki weusi.

"Vipi mko poa?"
"Poa tu" Elina Erica na Asia wote waliitikia kwa pamoja
Osward aliwatazama mapacha Erica na Elina kwa zamu kisha akageuka kwa Asia
"Wameachiwa lini hawa?"
"Jana jioni lakini hilo sio la muhimu, hivi wewe Osward ni nini unafanya huku, umetufanya tunakutafuta kutwa nzima"
"Unanitafutaje si nilikwambia namna ya kunipata?"
"Simu yako hupatikani, sema kakangu na wewe mapenzi mengi yaani mnabebishana hadi makaburini"
"Acha dharau basi sipatikani ndio si nilikwambia nimeipoteza simu kule mochwari"
"Hivi Osward ulikuwa serious kweli na yale maelezo yako ya mochwari au ni wenge tu? Ni kweli Aron yuko hai?"
"Asia nilikuwa namaanisha kabisa Aron hajafa kama wengi mnavyodhani, nilishuhudia mwenyewe kwa macho yangu akifumbua macho na kuinuka" Alieleza Osward kwa vitendo.
"Sasa kwa nini mpaka sasa hujamwambia Mheshimiwa"
"Kama wewe tu umeshindwa kuniamini huyo Rais Cosmas ataniamini, acha nipambane mwenyewe kwanza sitaki ajue huu uzembe niliifanya hadi nikafungiwa mochwari"
"Kwa hiyo tunafanyaje umeshapata simu mpya nipe namba yako"
"Ndio hii hapa andika" Alisema Osward huku akimpa simu yake Asia.
"Kwa hiyo unafanyaje kuhusu Aron?" Aliuliza Elina
"Cha kufanya nitaendelea kupambana na mzimu wa Aron kimya kimya ila kuna muda nitahitaji msaada wenu, yaani kama huyu mwamba anaendelea kuishi mimi maisha yangu nakosa amani kabisa"
"Usijali tumekuja hapa kukuambia mkuu anakikao na sisi leo jioni saa 11" alisema Asia huku akirudisha simu ya Osward
"Poa nitafika ni ishu gani kwanza?"
"Anasema kuna watu atatuunganisha nao tunakazi ya kufanya kwa yule mama yake Aron aliyelazwa hospitali yule wanamwita nani.. yes Madam Sultana" Alieleza Asia
"Mh! Basi sawa"
"Mbona umeguna?" Aliuliza Erica
"Naona unaongea simple simple tu hivi hujui kazi za Mheshimiwa Cosmas Kulolwa zinavyowaga ngumu na hatari"
"Hahaha ngumu kuliko tuliyofanya juzi juzi kukuchomoa gerezani, kumuua Dokta Gondwe na kumkamata Aron?"
"Hiyo cha mtoto mbona, hivi mlishawahi kusikia au kuona hiki kitu V-COBOS!?"
"Ndio nini?"aliuliza Elina
"Nawauliza mlishawahi sikia au kuona?"
Asia Erica na Elina walitazamana kisha wakanyanyua mabega kila mmoja akionyesha hajui kitu.
"Basi subiri mda ufike, ukisikia VITA YA KISASA ndio tunaenda kuingia rasmi" Alisema Osward huku akitabasamu.
"Acha kututisha basi, kwamba umesahau show zetu za kibabe... Poa baadae"
Alisema Asia kisha wote watatu wakawasha pikipiki na kuondoka kwa kasi. Osward aliwasindikiza kwa macho hadi alipopotea.

"Hivi vi dada vinafikiri natania, ngoja hiyo saa 11 ifike" Aliwaza Osward

"Ni akina nani hao?" ilikuwa ni sauti ya kike iliyomshtua Osward kutokea nyuma yake haraka akageuka, alikuwa ni Najma.

"Vi..vipi Najma tayari unaondoka?" Osward aliuliza swali badala ya kujibu swali.
"Hapana kuna kazi nataka unisaidie"
"Kazi gani?"
"Naomba unikutanishe na Tino kaka yake marehemu Inspekta Aron"
"Whaat! Tino wa nini?"
"He is one who was very close with my Dad, i wanna talk to him"(Ni mmoja kati ya watu waliokuwa karibu sana na baba yangu, nataka kuongea naye)
"To talk about what Najma..!!?"(kuongea kuhusu nini Najma?)
"I want to ask him about V-COBOS"( Nataka kumuliza kuhusu V-COBOS)
"Oh! my God"(Mungu wangu)

[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili Jasusi Shadow alifumbua macho taratibu na kujikuta amelala ndani ya chumba cha ajabu sana sehemu ambayo hakuelewa ni wapi. Kulikuwa na mwanga hafifu uliomuwezesha kuona makorokoro mengi yaliyokuwa ndani ya chumba hicho. Alisimama kwa taabu sana akiwa bado anahisi kizunguzungu, ile sindano aliyochomwa wakati ule ilikuwa bado inafanya kazi mwilini mwake.

Alisogea mlangoni akachungulia kupitia vitundu vidogo vidogo vya mlango hapo akaweza kuona msitu mkubwa uliozunguuka ngome hiyo huku watu mbalimbali wakizunguuka huku na kule ndani ya ngome hiyo. Mmoja kati ya watu aliowafahamu alikuwa ni Jesca mwanadada mashuhuri mke wa Tino ambaye anafanya kazi kwa ukaribu na Madam Sultana. Sasa alikuwa anaandaa vikosi tayari kuifuata chupa ya kijivu yenye kinga na tiba dhidi ya vimelea vya V-COBOS kama alivyoagizwa.

"Oo shit! Nipo Ngome ya Ambross ya Madam Sultana!"
Alisema Jajusi Shadow huku akitazama saa yake mkononi, ndio tumaini pekee alilobaki nalo.
ITAENDELEA...

Simulizi hii ni Tsh 1000 tu lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina Saul au Airtel money namba 0788967317 jina Saul
Kisha njoo WhatsApp namba hzo hzo[emoji120]
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya ............56
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ENDELEA...
[emoji294][emoji294][emoji294]
Fungo alizidi kukanyaga mafuta na kuifanya gari iende kwa kasi sana, Sandra alikaa pembeni yake akitamani kasi ya gari iwe kubwa zaidi ya ilivyo hivi sasa, ilikuwa ni lazima wawahi kumsaidia Jajusi Shadow kwani hadi dakika hiyo hawakujua amepatwa na tatizo gani.
Nyuma ya gari hiyo alionekana Inspekta Aron naye akiwa kasi na pikipiki akiwafuata. Tayari walishampata na kumueleza kila kitu kuhusu mwenzao Jajusi Shadow kuwa hatarini hivyo wote kwa pamoja wakakubaliana kwenda kumsaidia.
Dakika 6 baadae walifika nje ya jengo kubwa la ghorofa ambayo ni hospitali ya kimataifa Mountenia. Fungo aliendesha gari akazunguuka upande wa pili tofauti na ule ulio na geti kuu la kuingia hospitalini hapo.
Baada ya gari kusimama Sandra alishuka upesi kisha akamuonyesha ishara fulani Inspekta Aron ambaye naye aliegesha pikipiki pembeni ya barabara akaanza kumfuata nyuma, wakawa wanatembea kwa tahadhali wakikatisha njia mbalimbali za hospitali hiyo hadi zile zilizokuwa zimekatazwa, mwisho wakaufikia mlango wa nyuma ya hospitali wakaingia pasipo kuonekana.

"Chukua hii vaa sikioni kwa ajili ya mawasiliano" alisema Sandra kwa sauti ya chini akimkabidhi Aron kifaa fulani kidogo cha mawasiliano kilichounganishwa na wote watatu. Wakaendelea kutembea kuingia ndani zaidi ya hospitali.
"Hizi njia umezijuaje mbona kama wewe ni mwenyeji humu ndani?" Aliuliza Aron
"Yes! Ila Jasusi Shadow ndio mwenyeji zaidi huwa anapita humu kila anapokuja kukutana na Sultana mama yako" Alieleza Sandra wakati wakizidi kwenda mbele. Mara sauti ya Fumbo ikasikika ikiongea kupitia vile vifaa walivyovyaa sikioni.

"Jamani naona kama mwanga unafifia hapa kwenye kompyuta yangu haujakolea sana kama mwanzo nahisia huenda Jasusi Shadow akawa hayupo hapa"
Alieleza Fungo.
"Sasa ndio nini mda wote ulikuwa wapi kutuambia?" Sandra aliongea kwa ukali kiasi.
"Jesus Christ! Huo mda wa kuchungulia kompyuta ningepata wapi na unajua nilikuwa naendesha gari"
"Sawa basi angalia yuko wapi"
"Dakika zero"
Alijibu Fungo kisha akaendelea kupekuwa pekuwa kwenye kompyuta yake huku Sandra na Aron wakiwa na shauku ya kusikia ni wapi alipo Jajusi Shadow muda huo.
"Jesus Christ!"
"Nini?"
"Ni kweli hayupo hapo, location yake imehama"
"Iko wapi tena?"
"Hebu njooni kwenye gari kwanza"

Sandra na Aron walitazamana kisha wakaanza kupiga hatua kurudi walikotoka lakini kabla hawajafika mbali mara walisita ghafula na kurudi nyuma.
"Kuna mtu anakuja" Alisema Aron
"Ndio nimemuona atakuwa nani mbona huku chini ni adimu sana watu kupita" alisema Sandra kisha wote wawili wakajificha nyuma ya pambo moja la ua kubwa wakawa wameinama na kulizunguuka ua hilo huku wakipishana na yule mtu asiwaone.

Alikuwa ni mwanamke wa makamo mrefu na mnene, kichwani alivaa hijabu na barakoa nyeusi, baada ya kupiga hatua kadhaa alivua ile barakoa na kuiweka kwenye mkoba wake. Hapo ndipo sura yake iliweza kuonekana wazi wazi licha ya kwamba kulikuwa na mwanga hafifu eneo hilo lakini Inspekta Aron alijikuta anatoa macho kwa mashangao mara baada ya kumuona mwanamke huyo.

"Mama...!! " aliita Inspekta Aron kwa sauti ya chini iliyoambatana na mshangao. Ndiyo mtu huyo hakuwa mwingine bali mama yake yaani Madam Sultana.
"Nini! mama yako?" Sandra aliuliza ili kujihakikishia alichosema Aron, lakini Aron hakujibu kitu bali alipiga hatua kutaka kumfuata Sultana.
"Unafanya nini Aron hebu subiri"
"Niache Sandra" Aron aliongea kwa ukali hali akilengwa na machozi. Likuwa ni tukio lingine lenye kuuvunja moyo wa Inspekta Aron kwa kiasi kikubwa siku hiyo, licha ya kwamba tayari alikuwa ameambiwa kila kitu na Mheshimiwa Rais kuwa mama yake ni mzima ila anaigiza kujifanya mgonjwa lakini kitendo cha kumuona kwa macho yake kilimuumiza mno.
"Jitulize Aron jitulizee...."
"Haloo! Ninyi vipi mbona kama mnapapasana huko, hebu twendeni basi aliko Jasusi Shadow" Fungo Alisikika akiongea kupita vile vinasa sauti masikioni mwao.
"Nenda Sandra"
"I can't go without you Aron"( siwezi kwenda bila wewe Aron)
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili...
Sharma Khumar yule dada mwenye asili ya kihindi ambaye amewasili nchini akiwa pamoja na wale wazungu kutoka Mexico. Majira haya ya mchana alionekana akiwa maeneo ya uswahilini pembeni kidogo ya mji, alishuka kwenye gari huku nyuma yake akiwa ameongozana na mlizi wake.
Sharma alikuwa amevaa mavazi ya kujificha sana uso wake, kichwani alijitanda hijabu pamoja na miwani mikubwa ya jua. Aliongoza njia na kuingia kwenye mgahawa mmoja wenye hadhi ya chini sana.
Siku hiyo Sharma Khumar alipanga kukutana na mtu mmoja kwa siri mahali hapo. Hata wale wenzake kutoka Mexico hawakujua lolote kuhusu mkutano huo.
Akiwa ndio kwanza anaingia mgahawani hapo mara alikutana na varangati la aina yake, Mwanaume mmoja ambaye ni kati ya wahudumu wa mgahawa huo alikuwa akigombana vikali na mteja wake wa kike. Sababu ilikuwa ni kwamba mwanamke huyo anataka kuondoka pasipo kulipa hela ya chakula alichokula.

"Huwezi kuondoka humu bila kulipa dada, unasemaje umelipa wakati hela yako mimi sina..." Aliongea kwa sauti kubwa yule muhudumu huku wateja wachache waliokuwepo mgahawani wakishuhudia kinachoendelea.

Yule dada mteja alibaki ametulia kimya huku akionekana kukelwa mno na maneno ya shombo kutoka kwa yule mhudumu. Nywele za dada huyo zilikuwa ni ndefu sana zinazofika mgongoni lakini zilionekana kukosa huduma kwa muda mrefu, zilikuwa zimevurugika hovyo mithiri ya kichaa.

"Mademu wengine mnaleta umalaya hadi kwenye kazi za watu..." Alisema yule muhudumu.
Kufika hapo uvumilivu ulishinda yule dada, ghafula kama umeme aliruka na kwenda kumvaa yule muhudumu akamkaba shingoni kisha kumvuta kwa nguvu huku wakipalamia vyombo na meza zilizoanguka chini, lakini hakujali. Akaendelea kumkaba shingoni na mwisho akambamiza kwenye ukuta uliojengwa kwa mabanzi.

Akiwa bado amemkaba muhudumu shingoni kwa nguvu yule dada alichomoa kisu kutoka mfukoni kwa kutumia mkono wake wa kushoto kisha akakiinua na kukizamisha kwenye ukuta wa mabanzi pembeni ya shingo ya yule muhudumu. Watu walipiga kelele kwa hofu huku wengine wakiziba macho yao wakiamini yule dada anakizamisha kisu kwenye shingo ya muhudumu.
Baada ya kufanya hivyo yule dada alimsukuma muhudumu pembeni akaanguka huku akikohoa kwa nguvu na kushika shingo yake akawa anahangaika kuvuta pumzi baada ya kuikosa kwa dakika kadhaa.

Mara wakati huo aliingia muhudumu mwingine wa kike akiwa na mfuko wa viazi begani, alishangaa kukuta hali asiyoielewa mle ndani vitu vilikuwa vimevurugwa vurugwa hovyo huku watu wote wakiwa kwenye hali ya hataruki.

"Jamani kuna nini, eti Sam nini shida" Aliuliza yule mhudumu akimsogelea mwezake aliyekuwa bado amekaa pale chini.

"Hu..huyu..dada...ha...ha...hajalipa" Alisema yule mhudumu wa kiume huku akimnyoshea kidole yule dada aliyemkaba almanusura amuue.
"Ahh! Mbona huyu dada alilipa hata kabla hajaanza kula jamani, alishanipa hela tayari kwani imekuwaje?"

Kauli hii iliwashangaza watu wote walikuwa mle ndani. Baada ya kusema hivyo yule dada alichomoa kisu chake ukutani akakirudisha kwenye mfuko wa suruali yake kisha akawa anaondoka zake taratibu huku akiziweka nywele zake vizuri ambazo zilikuwa zimelala kwa mbele na kuufunika uso wake wakati wa varangati lile.
Alipozirudisha nyuma kuziweka sawa hapo ndipo sura yake iliweza kuonekana dhahiri shahiri. Amini usiamini ndugu msomaji huyu hakuwa mwingine bali ANNAH.
Ndiyo ni Annah yule yule ambaye kwa mara ya mwisho alipotelea kusiko julikana baada ya kushindwa kesi mahakamani. Haya ndio maisha yake mapya anayoyaishi tangu siku hiyo, ni kama akili zake hazikuwa vizuri, si Annah yule tunayemfahamu, hata sura yake ya kirembo kwa sasa ilifichwa kutokana na ugumu wa maisha anayoyaishi hivi sasa.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Yule dada wa kihindi Sharma Khumar alilishuhudia tukio lote hili kuanzia mwanzo hadi mwisho. Wakati wote Sharma alikuwa akitabasamu kila alipokuwa akiangalia mapigo ya Annah, alivutiwa naye haswaa.
Wakati Annah anaondoka Sharma alimgeukia mlinzi wake na kumwambia.

"I need her" (namuhitaji huyu mwanamke)
Alisema Sharma Khumar kisha yeye akaingia mgahawani na kwenda kukaa chumba cha pili cha mgahawa huo chumba chenye utulivu ambako huko ndiko alipanga kukutana na mgeni wake, bado alikuwa hajafika.
Wakati huo mlinzi wa Sharma Khumar alianza kupiga hatua kumfuata Annah.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande mwingine Sandra na Inspekta Aron walionekana wanatoka hospitali ya Mountenia kupitia mlango wa nyuma wakatembea hadi lilipo gari lao wakufungua milango na kuingia kila mmoja upande wake.
"Vipi mbona kinyonge hivyo kwema?"Aliuliza Fungo huku akiwatazama Aron na Sandra kwa zamu.
"Kamuona mama yake" Sandra alijibu kwa kifupi
"Jesus Christ! Sultana huyu huyu?"
"Ndiyo"
Kimya kikatawala kwa sekunde kadhaa
"So Shadow yuko wapi sasa?" Aliuliza Sandra, Fungo akainua kompyuta yake akageuza kuwaonyesha. Kwenye uso wa kompyuta hiyo waliona ramani kisha kukawa na kidoti chekundu kinachoonyesha hapo ndipo alipo Shadow wakati huo.
"Umejua ni wapi?" Aliuliza Fungo.
"Nafikiri hii ni Ngome ya Ambross ya Sultana ambayo huwa nasikia Jasusi Shadow anaitaja mara kwa mara akiwa anaongea na Mheshimiwa Rais" Alieleza Sandra.
"Jesus Christ"
"No way inabidi twende haraka. Vipi Aron tunaenda wote au tukuache ukatulize akili yako kwanza maana huku tunakokwenda ni ngome iliyopo chini ya mama yako, ngome ya Ambross. Sio ajabu kukatokea vita ya risasi sasa kama hauko sawa naona bora tukuache" Aliongea Sandra
Bila kujibu Aron alifungua mlango kisha akashuka.

"Let's go to work" (Twendeni kazini) alijibu Aron kisha akaufunga mlango kwa nguvu na kuanza kuelekea alikopaki pikipiki. Sandra na Fungo walitazamana kisha wakatabasamu.
"Huo ndio uanaume"
Alisema Sandra
"Acha kumsifia sana ana mke huyo" alijibu Fungo
"Mke yupi zaidi yangu"
"Jesus Christ"
ITAENDELEA...
.Simulizi hii ni Tsh 1000 tu lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina Saul au Airtel money namba 0788967317 jina Saul
Kisha njoo WhatsApp namba hzo hzo[emoji120]
 
Simulizi hii ni Tsh 1000 tu lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina Saul au Airtel money namba 0788967317 jina Saul
Kisha njoo WhatsApp namba hzo hzo[emoji120]
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya............57
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Sandra,Fungo na Inspekta Aron wako njiani kwenda kumsaidia Jajusi Shadow ambaye ametekwa na Madam Sultana.
Wakati huo huo upande wa pili Mwanadada Sharma Khumar anaonekana kuvutiwa na binti Annah, anamuagiza mlizi wake amfuate

Je, nini kitafuata?

SASA ENDELEA...
Haukupita muda aliingia mwanaume mmoja ndani ya mgahawa huo akiwa amevaa kofia kubwa ya duara pamoja na miwani ya jua. Alijipenyeza ndani ya mgahawa huo akatembea hadi upande wa pili kule alipokaa mwanadada Sharma Khumar. Huyu ndiye alikuwa mtu aliyepanga kukutana naye eneo hilo aliitwa Bwana Andiwelo katabi mkemia mkuu wa serikali. Andiwelo katabi ni mshirika kati ya watu wanaoifahamu siri ya kuwepo kwa vimelea vya V-COBOS nchini ukiacha marehemu Dokta Gondwe na Mheshimiwa Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa, Andiwelo alikuwa mmoja wao pia. Hata kile kikao cha mwisho kilichofanyika katika nyumba ya Mheshimiwa Cosmas Kulolwa wote wawili yaani mwanadada Sharma Khumar na Andiwelo katabi walikuwepo lakini leo wanaamua kukutana pembeni ya mji wakiwa wawili tu kwa ajili ya mazungumzo yao ya siri.

"Nambie Miss Sharma simu yako imenitisha sana, vipi kwema?" Andiwelo alianzisha mazungumzo.
"Kwema, kwa nini utishike mbona nilishakweleza kila kitu Andiwelo"
"Ni sawa lakini muda mrefu umepita nikajua ulishahairisha huu mpango wako hatari"
"Hapana siwezi, unajua kabla Profesa Fernando Arturo hajatuzunguuka ni vema tukawahi kuchukua kilicho chetu mapema"
"Lakini wewe umejuaje kama atatuzunguuka?"
"Andiwelo mimi nimefanya kazi na hawa wamexico kwa muda mrefu sana naelewa mipango yao yote, wakishapata wanachokitaka watatuua sisi wote kisha watarudi kwao kufufua upya maabara yao ya ZMLST huku wakiendelea kupiga pesa za ugonjwa wa V-COBOS, sisi tunatumika tu rafiki yangu"
Alieleza Miss Sharma Khumar

Mkemia mkuu wa serikali Andiwelo katabi alitulia kwa muda huku akijaribu kuyatafakari maelezo ya Miss Sharma kisha akaongea.
"Hili jambo tunalotaka kulifanya ni hatari sana Miss Sharma, ona marehemu Dokta Gondwe alijaribu kwenda kinyume na Profesa Fernando kama hivyo unavyotaka tufanye haikuchukua muda akawa ameuawa mchana kweupe, huyu jamaa ana watu kila kona mbaya zaidi yupo pamoja na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa naye anawatu kila kona huoni kama ni hatari, atatuchinja kama kuku"
"Kuhusu hilo usijali ndio maana nilitangulia kuja hapa nchini kabla ya wao kufika nimeshaweka mipango yangu sawa hakuna kitakacho haribika"
"Mipango ipi Sharma?" Aliuliza Andiwelo lakini kabla hajajibiwa yule mlinzi wa Miss Sharma alifika.
"Mkuu yule binti nimemleta yule pale" alisema mlinzi huku akinyoosha kidole pale alipokaa Annah.
"Umeshaongea naye?" Aliuliza Miss Sharma
"Hapana"
"Ongea naye mwambie nataka kufanya kazi na yeye"
"Sawa bosi" alijibu mlinzi kisha akapiga hatua kumfuata Annah huku akiacha mazungumzo ya bosi wake na Andiwelo yakiendelea.
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Sikia binti bosi wangu amekupenda anataka kufanya kazi na wewe kama uko tayari akuajili niambie, ni hilo tu" alieleza kwa kifupi yule mlinzi mara baada ya kurudi pale alipomuacha Annah.

Annah ambaye muonekano wake ulikuwa tofauti kabisa na tulivyomzoea kipindi kile akiwa karibu na Inspekta Aron, aliinua uso wake uliofubaa na kumtazama yule mlinzi.
"Yaani umeniita kwa sababu ya hilo au kuna lingine?" Annah aliuliza kibabe
"Ni hilo tu, tunataka kuyatengeneza maisha yako. Nakuona kabisa wewe ni mrembo ila maisha unayoishi yanakufanya uonekane kama kichaa fulani hivi" Alisema yule mlinzi kauli iliyomfanya Annah amkate jicho kali sana. Mlinzi akawa makini akijipanga kwa lolote kwani alikumbuka vizuri dakika chache zilizopita Annah alitoka kumkung'uta muhudumu mmoja wa mgahawa huo.
"Siwezi naondoka"alisema Annah huku akiinuka tayari kuondoka.
"Aah.. subiri... Subiri kwanza kwani wewe unatakaje eeh!?" Aliuliza yule mlinzi.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati huo mazungumzo ya Miss Sharma na Mkemia mkuu Bwana Andiwelo yaliendelea. Mara akaja tena mlinzi.
"Boss yule dada amekataa anataka kuondoka"
"Umempa pesa?"aliuliza Sharma
"Hapana nimemwambia tu tutampa pesa nyingi"
"Muonyeshe pesa, maneno matupu huwezi kumshawishi mtu wa aina ile au unataka na wewe akupige?" Alisema Sharma, bila kupoteza muda yule mlinzi aliondoka hadi pale alipomuacha Annah.

"Dada usiondoke kaa kwanza nakuja dakika 1 tu" alisema Mlinzi huku akipiga hatua ndefu ndefu akatoka nje ya mgahawa akawa anaelekea waliposimamisha gari yao.
Annah alitulia huku akimtazama mwanamke aliyetaka kumuajili kwa macho ya kuibia ibia, akatega sikio akitamani kusikia kile walichokuwa wakizungumza watu hao wawili, kwa bahati nzuri safari hii waliongea kwa sauti kubwa kiasi, walijisajau.
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Miss Sharma sijakuelewa vizuri hebu nifafanulie mpango wako nikuelewe" Alisema Andiwelo.
"Tatizo lako ni uoga, unafikiri watakuua kama walivyomuua Dokta Gondwe hapana niamini mimi nitakulinda"
"Hamna sio kwamba naogopa ila nachukua tahadhari"
"Sawa, nimekwambia tutaendelea kuwa karibu nao na kufanya kazi kwa pamoja kama kawaida lakini tutakuwa tukiwazunguuka kwa siri sana" alieleza Miss Sharma
"Kivipi?"
"Tutamtumia kijana mmoja ambaye naye malengo yake ni kama yetu"
"Nani huyo?"
"Anaitwa Tino, mtoto wa marehemu jenerali Phillipo Kasebele na ni kaka wa marehemu Inspekta Aron pia"
"Mnh wewe umewajuaje wote hao?"
"Nilikwambia nilitangulia kuja hapa nchini sio kushangaa magari, nilikuja kufanya kazi"
"Sawa sasa nimeanza kukuelewa ila huyo Tino utamtumia vipi wakati na yeye anataka kitu tunachokitaka sisi"
"Baada ya kifo cha Dokta Gondwe Tino amepoteza muelekeo hana kwa kuanzia, anahangaika anataka kumteka Osward lakini pia anawaza kukuteka hata wewe ili tu apate pa kuanzia sasa kama tutamuweka karibu na kumpa mwanga atatuamini na kuanza kufanya kazi na sisi"
"Kivipi?"
"Sisi tuna taarifa ya wapi vilipo vimelea vya V-COBOS na jinsi ya kuvipata lakini hatuwezi kwa sababu hatuna nguvu kazi, Tino anayo nguvu kazi vikosi imara sana avilivyoachwa na Dokta Gondwe lakini hana taarifa muhimu kama tulizonazo sisi"
Alieleza Miss Sharma akijaribu kuufungua ubongo wa Andiwelo.
"Anha! Nimeanza kukuelewa kwamba sisi tutaendelea kubaki huku tuliko upande wa Profesa Fernando lakini tutakuwa tukivujisha siri kwa Tino"
"Yes! Hiyo ndio maana yangu kubwa"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Annah akiwa amejikausha huku masikio yake yakiwa yamesimama kama sungura alishtushwa na burungutu la pesa zilizomwagwa juu ya meza. Zilikuwa ni pesa nyingi sana kutoka kwa yule mlinzi wa Miss Sharma Khumar.

Annah alibaki ameduwaa huku akizitazama zile pesa lakini amini usiamini mawazo ya Annah hayakuwa kwenye zile pesa bali yalikuwa mbali akijaribu kuyatafakari maneno kadhaa aliyoyasikia kutoka kwa Sharma Khumar na mgeni wake Andiwelo.

"Kumtumia Tino....kifo cha Dokta Gondwe...kifo cha Aron...Rais mstaafu..kumteka Osward...." Haya ndio maneno yaliyokuwa yakipitapita kwenye kichwa cha Annah wakati huo. Kwa kuwa lengo la Annah siku zote ilikuwa ni kulipa kisasi kwa Tino na wenzake waliohusika na mauaji ya baba yake, kisasi kwa wote waliohusika kumuweka mwanaume ampendae hatiani yaani Inspekta Aron hadi kusababisha kifo chake, kisasi kwa wote waliohusika kupindisha ukweli hadi Osward akaachiwa huru, Annah aliona kabisa ni kama miujiza imemfuata pale alipo. Pesa zilizokuwa mezani si kitu bali kufanya kazi na Miss Sharma Khumar ndilo lilikuwa jambo la msingi zaidi kwani aliamini moja kwa moja kuwa atamsogeza karibu na wabaya wake.

"Vipi mbona umeduwaa unazitaka hizi pesa, basi kubali kufanya kazi na bosi wangu"
"Sawa nimekubali" Annah alijibu upesi huku akizichukua zile pesa kuzirudisha kwenye mfuko. Yule mlinzi akawa anatabasamu akiamini kuwa pesa ndio kitu kilichomnasa Annah, la asha.

Dakika 10 baadae Annah alionekana akiwa ameongozana na Sharma Khumar wakitoka nje ya ule mgahawa yule mlinzi akiwa nyuma yao, wakaingia ndani ya gari na kuondoka.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Inspekta Aron, Sandra na Fungo tayari walishafika msituni ilipo ngome ya Madam Sultana na sasa walikuwa wamejificha msituni pembeni kidogo ya ngome hiyo wakawa wanapiga hesabu za kikomandoo namna ya kuingia kumsaidia mwenzao Jajusi Shadow.
Kwa mbali waliweza kuona watu waliokuwa kwenye ngome hiyo wakiwa bize kupakia mizigo ndani ya gari tatu zilizokuwa zimewekwa tayari kuondoka.

"Ni kama wanataka kwenda sehemu" alisema Fungo huku akitazama kupitia darubini.
"Ndio, zile ni siraha sijui wanakwenda wapi!" Alijibu Sandra kisha akageuka kumtazama Inspekta Aron pembeni yake.
"Vipi Aron mbona uko kimya, au bado unamuwaza mama yako?"
"Hapana, Dunia ina siri nzito sana unaweza ukawa unaishi ilimdradi ukiamini watu wote wako hivyo kumbe wenzako unaoishi nao wamebeba vitu vizito mno na hujui"
"Una maana gani Aron?"
"Unamuona huyo dada anayewaongoza watu kupakia mizigo kwenye gari"
"Ndiyo namuona"
"Huyo ni shemeji yangu anaitwa Jesca ni mke wa kaka yangu Tino nilikuwa namuona wa kawaida sana na siku zote alikuwa ananitaka kimapenzi, nilimuona malaya malaya tu mwanamke asiyejitambua kumbe na yeye ni hatari kama alivyo kaka yangu Tino"
"Mmh! Kweli kifo chako kimekufanyaa uyajue mengi, kwa hiyo huyu dada anafanya kazi na mama mkwe wake huku akimzunguuka mume wake Tino si ndio hivyo"
"Hata sina majibu inafikirisha sana hadi kichwa kinaniuma, hebu tuachane na hayo tuingie kazini tumchomoe ndugu yetu"
"Subiri..subiri wanaondoka"alisema Fungo
"Haya gari zote tatu zimeondoka vipi Jajusi Shadow anaonekana wapi yupo ndani au wameondoka naye?"
"Yupo ndani"
"Haya twende kazi wanaume" alisema Sandra huku akisimama, akatoa kibanio cha nywele zake kisha akaziachia na kuzilaza kwa nyuma, akachomoa bastola mbili moja akaishika mkono wa kulia na nyingine mkono wa kushoto, akaanza kupiga hatua kuelekea mbele ilipo ngome ya Ambross.
Inspekta Arone yeye akavaa barakoa yake vizuri kama ilivyo kwa Sandra naye akachomoa bastola mbili alizokishwa zisindilia risasi za kutosha kisha akaanza kumfuata nyuma. Fungo yeye alikuwa na bunduki aina ya AK47, akachomeka magazine iliyojaa siraha kisha akaanza kumfuata Inspekta Aron nyuma.
Hazikupita dakika Tano milindimo ya risasi ilianza kushika kasi na kusikika karibu kila kona ya msitu huo. Walinzi wachache waliokuwa wamesalia kwenye ngome ya Ambross inayomilikiwa na Madam Sultana walikuwa kwenye shughuli nzito kuwakabiri Sandra,Fungo na Inspekta Aron.

Je, nini kitafuata?
Annah kwenye himaya ya Sharma Khumar...
Najma bado anatamani kuuchimba ukweli wa kifo cha baba yake....
Jesca anakwenda kuchukua chupa ya kijivu yenye kinga na tiba dhidi ya vimelea vya V-COBOS....
Inspekta Aron ndani ya kundi la kikomandoo na leo anaifanya kazi yake kwa mara ya kwanza kumuokoa Jasusi Shadow....

Mambo ni mengi, muda ni mchache USIKUBALI KUPITWA...!!
ITAENDELEA...
 
KUPATA SIMULIZI NYINGINE YA SAUL DAVID, BONYEZA HAPA[emoji116][emoji116]
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya............58
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Hazikupita dakika Tano milindimo ya risasi ilianza kushika kasi na kusikika karibu kila kona ya msitu huo. Walinzi wachache waliokuwa wamesalia kwenye ngome ya Ambross inayomilikiwa na Madam Sultana walikuwa kwenye shughuli nzito kuwakabili Sandra,Fungo na Inspekta Aron

SASA ENDELEA...
Kelele hizo za milio ya risasi vilimshitua Jasusi Shadow ambaye alikuwa amekaa na kujiinamia kwa zaidi ya nusu saa. Alikurupuka na kusimama kisha akaenda kuchungulia kupitia vile vitundu vidogo mlangoni.
Jasusi Shadow aliachia tabasamu baada ya kuwashuhudia wenzake yaani Fungo, mwanadada Sandra na Inspekta Aron wakiwa wamepeana mgongo na kutengeneza duara huku wakimimina risasi zisizo na hesabu.

Wote walikuwa wamevaa sura ya kazi, si Sandra si Fungo wala si Aron kila mmoja alikuwa ameishikilia siraha yake sawasawa akiwatwanga risasi walinzi wa ngome hiyo bila huruma. Walinzi walijikuta kwenye wakati mgumu mno kila walipojaribu kuwavizia watu hao watatu wenye ujuzi mkubwa wa kutumia siraha walijikuta wanaambulia patupu. Mfumo wa mashambulizi walioingia nao ulikuwa madhubuti sana kiasi cha kuwafanya ndani ya dakika nane pekee tayari walikuwa wanakaribia kuiangusha ngome hiyo ya Ambross.

Dakika 15 baadae Sandra alitoa ishara fulani wanayoielewa wao haraka kila mmoja alitoka kwa kasi na kuelekea upande wake. Sasa ikawa ni kazi ya kuwamalizia wale walinzi wengine waliokuwa wamejificha.

Jasusi Shadow akiwa na matumaini ya asilimia zote za kuokolewa alianza kujiweka tayari kuondoka. Mara mlango ulifunguliwa alipotazama mbele alimuona Inspekta Aron ambaye alinyoosha mkono wake wa kulia akimtaka Jajusi Shadow atoke.
Shadow aliachia tabasamu kwa mara nyingine huku akimtazama Inspekta Aron usoni. Alivuta kumbukumbu zake akajikuta anamkumbuka marehemu jenerali Phillipo Kasebele ambaye ni baba wa Aron. Kiasi alikuwa anafanana sana na kijana wake hata tabia pia.

"Twende shadoooow" Aron aliongea kwa msisitizo baada ya kuono shadow amemkodolea macho tu badala ya kutoka. Hapo Shadow alipiga hatua kumfuata, bado hali yake ya kiafya alikuwa haijatengamaa hakuwa na nguvu za kutosha.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili kabla ya Jesca kuondoka na kikosi chake aliomba kuonana na mumewe Tino nyumbani kwa lengo la kumuaga. Hakutaka kuondoka kimya kimya kwa sababu alipokuwa anakwenda kuchukua ile chupa ya kijivu yenye kinga dhidi ya vimelea vya V-COBOS ni mbali ingemlazimu kutumia siku kadhaa hivyo aliona ni vema amuage mumewe.

"Sijaelewa wiki mbili zote utakuwa unafanya nini nyumbani kwenu?" Aliuliza Tino
"Mume wangu si nimekwambia mama anaumwa, hakuna mtu wa kumuangalia zaidi yangu wadogo zangu wote hawapo wako shule" Jesca alidanganya.
"Unajua mimi na wewe tumefunga ndoa ya kiserikali hao ndugu zako simjui hata mmoja kila wakati nikikwambia twende kwenu huwa unanikwepa, kwa nini lakini wewe mwanamke"
"Osward jamani, nimekwambia mama anaumwa hayo mambo yanatoka wapi tena mume wangu?"
"Sawa lakini wiki mbili ni nyingi sana Jesca" Tino aliongea kinyonge sana, pamoja na ubabe wake wote lakini alikuwa ni dhaifu sana mbele ya mkewe, huwezi kuamini mpaka leo hii Tino hajawahi kuongea lolote kuhusu ile picha ya ngono kati ya mkewe Jesca na marehemu Dokta Gondwe bado aliifanya kuwa siri hasa baada ya Dokta Gondwe kufa hakuona haja ya kuongea lolote ingawa bado roho yake ilikuwa ikimuuma sana.
"Nitaona naweza kurudi mapema kama hali ya mama itakuwa nzuri" Alisema Jesca mwisho wakaagana wakati huo simu ya Tino ilikuwa inaita. Baada ya kuhakikisha Jesca amepiga hatua yuko mbali Tino aliipokea.

"Nambie Bosco"
"Ee! Bosi mbona hurudi?" Bosco Alisikika upande wa pili wa simu ile
"Nakuja niliitwa na wife mara moja hapa ndio natoka"
"Sawa vikosi viko tayari vinasubiri amri yako mkuu, tunaenda kumteka nani ni Osward au Mkemia mkuu Andiwelo katabi?"
"Mmh! Hapo Osward ndio atafaa zaidi yeye ndio atatupa mwanga namna ya kujipanga kuvipata vimelea vya V-COBOS"
"Sio utakuwa mzunguuko mkubwa bosi, kwa nini tusimteke moja kwa moja Mkemia mkuu wa serikali Andiwelo nahisi yeye ndiye anajua moja kwa moja ni wapi vilipo vimelea...hallo.. hallo bosi...mbona kimya...hallo" Bosco alikuwa akiita upande wa pili baada ya kuona bosi wake Tino amekaa kimya. Macho ya Tino wakati huu alikuwa ameyalekeza getini kuna jambo aliliona lililomshtua kiasi.
"Kata simu Bosco nakupigia" Alisema Tino huku akiirudisha simu yake mfukoni.

Wakati Jesca anatoka akiwa getini alikutana na wageni ambao nao ndio walikuwa wakiingia, wageni hawa alikuwa ni Najma akiwa ameongozana na Osward.
Ulikuwa ni ugeni ambao hata Jesca mwenyewe hakuwa ameutegemea.

"Karibuni"
"Asante" Osward na Najma waliitikia kwa pamoja, baada ya salamu Osward aliuliza.
"Tuna shida na Bwana ako Tino sijui tumemkuta?"
Jesca alisita kidogo kujibu swali hilo lakini kwa bahati nzuri Tino naye akawa anakuja tayari alishawaona.
Ilikuwa ni tukio la kushangaza sana mtu ambaye alikuwa anajadili kumteka sekunde chache zilizopita kaja mwenyewe nyumbani kwake.

"Karibuni, niwasaidie nini?" Tino aliongea kwa sauti iliyojaa kiburi. Badala ya kujibu Osward alipiga hatua kuingia ndani Najma naye akafuata nyuma.

Jesca aliwatazama watu hao kwa zamu pamoja na mumewe kisha akaamua kuondoka zake. Alijua wazi hali si shwari lakini hakutaka kuendelea kupoteza muda tayari alishamuaga mumewe kwa kudanganya na sasa rasmi alikuwa tayari kuelekea kule ilipo chupa ya kijivu akiwa na kikosi chake cha kazi. Hakujua lolote kuhusu kile kilichotokea Ngome ya Ambross dakika chache tu mara baada ya wao kuondoka.

"Nina mazungumzo na wewe Tino kama hutojali" Alisema Najma kauli iliyowafanya Tino na Osward watazamane.
"Sawa karibu" alijibu Tino huku akimuonyesha ishara waelekee kwenye viti vilivyokuwa kwenye bustani nzuri ya maua nje ya nyuma hiyo.
"Najma mimi niko hapa nje kwenye gari nakusubiri" alisema Osward
"Hapana wewe pia njoo tuzungumze wote" Alijibu Najma.

Dakika tatu baadae wote watatu walikuwa wamekaa kwenye vitu huku Tino na Osward wakionekana kuwa na shauku ya kujua ni jambo gani Najma anataka kuzungumza.

"Unaweza kuzungumza haraka haraka Najma niko bize kidogo samahani" alisema Tino baada ya kuona Najma yupo kimya kwa muda mrefu.
"Usijali, kwanza pole kwa kifo cha mdogo wako Inspekta Aron"
"Asante pole pia kwa kufiwa na baba yako lakini pia na mpenzi wako Aron" alijibu Tino kauli iliyomfanya Osward amkate jicho baya.
"Nashukuru, nitaenda haraka kama ulivyosema. Najua ninyi wote wawili mmefanya kazi na marehemu baba yangu Dokta Gondwe. Tino ulikuwa mtu wake wa karibu sana pamoja na Osward pia. Nakumbuka mara ya Mwisho Tino pamoja na baba yangu mlikuwa mnapambana sana kutaka kumsaidia Osward atoke gerezani kwa hiyo bila shaka ninyi wote wawili mnamajibu ya swali langu" Alisema Najma wakati huo Osward akimeza fundo kubwa la mate.

"Niko hapa kutaka kujua sababu hasa iliyopelekea kifo cha baba yangu. Kwa kuanza nataka kujua ni nani muhusika mkuu wa mchakato mzima wa virusi vya V-COBOS kutoka Mexico kuja hapa nchini?" Najma aliuliza swali moja kwa moja kuhusu vimelea vya V-COBOS swali lilowafanya Tino na Osward kutoa macho kwa mshangao.

"Umeniambia niende haraka na ndio mana sijataka tuzunguuke sana, natumaini hili neno sio geni kwenu hata kidogo na ndio kitu mlichokuwa mkikipambania sana mkiwa pamoja na marehemu baba yangu. Hiki hapa ni kitabu cha kumbukumbu yaani diary ya baba yangu ameandika kila kitu hukusu hao vimelea, sasa nahitaji kujua ni nani mkubwa wenu ni nani kiongozi wa opareshini hii" Najma alikuwa akiongea kirahisi sana tena kwa kujiamini mno, aliwaonyesha kile kitabu cha kutunza kumbukumbu cha marehemu Dokta Gondwe kisha akakirudisha kwenye begi.

"Najma unajaribu kufanya nini?"
Aliuliza Osward
"Kaa kimya Osward nitapenda kumsikiliza Tino kabla yako"
Najma alimkatisha.
"Sijui unaongea nini Najma" alijibu Tino.
"Sawa, kama hujui basi nitakwenda kueleza yale nayoyajua Polisi nitaweka wazi kila nachokijua na kuwapa hiki kitabu cha kumbukumbu za baba, nafikiri huko nitapata msaada ule ambao nimeukosa kwenu" alisema Najma kauli iliyozidi kuichanganya akili ya Osward na Tino.
Osward alihofia sana usalama wa Najma kile alichokuwa anakifanya ilikuwa ni hatari kupita maelezo japo yeye alichukulia rahisi, na kama angeenda kutoa taarifa polisi basi angeharibu mpango wa bosi wake mpya yaani Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa na watu wake kutoka Mexico. Vivyo hivyo kwa Tino naye alihofu kama Najma anajua siri hiyo na anataka kueleza mbele ya vyombo vya sheria basi ataharibu mpango wake wa kuvitaka vimelea vya V-COBOS alioanza nao miaka mingi ikiyopita kiasi cha kumfanya hadi amuue baba yake mzazi.

"Sikiliza Najma mi nilijua umekuja hapa kutaka kujua ni kwa nini mdogo wangu Aron alimpiga baba yako risasi na kumuua lakini kumbe umekuja na mada tofauti kabisa, nashindwa kuelewa"
"Tino sikutaka kuanzia huko kote kwa ajili ya kuokoa muda wako kama ulivyosema. Nina imani Aron hakumuua baba yangu na hata kama alimuua yeye basi alifanya hivyo kwa ajili ya hiki nachokisema sasa V-COBOS" Najma aliongea kwa msisitizo, wakati huo kijasho chembamba kilikuwa kikimtililika Osward, alitamani Najma aache kufanya anachokifanya mara moja.

"Naomba niwe muwazi kwako Najma sina jibu ya swali unalouliza, it's over"
"Okay fine, tutaonana" Najma alijibu kisha akasimama na kuanza kuondoka, Osward na Tino nao wakasimama huku wakimsindikiza kwa macho mdada huyo mrembo mwenye umbo la kuvutia.

""Ni wakati wa kuchukua maamuzi magumu Osward, huyu kiumbe ni bomu hatakiwi kabisa kuishi, najua unajua nini cha kufanya kumziba mdomo mchumba wako, ama umuue wewe au umuache tukusaidie" Alisema Tino kwa sauti ya kunong'ona kisha akachukufua funguo ya gari mezani akaweka koti lake sawa na kuondoka akimuacha Osward ameduwaa"
Je, hiki anachokifanya Najma ni salama?
Kama si salama nini kitatokea?
Vipi kuhusu safari ya Jesca?
Jasusi Shadow ameokolewa?
ITAENDELEA....
 
Back
Top Bottom