THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya............54
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA....
Jasusi Shadow alitulia kwa muda kisha akafanya kama alivyo amrishwa. Baada ya hapo aliwaona watu watatu kila mmoja akiwa na bunduki mkononi huku sura zao zikiwa zimefunikwa na vinyago vyenye muundo wa kichwa cha simba wakipita na kusimama mbele yake.
SONGA NAYO....
Jasusi Shadow aliwakagua mmoja baada ya mwingine akagundua kuwa wote watatu walikuwa ni wanawake. Hakujua ni nini kimetokea hasa kwenye chumba cha bosi wake Madam Sultana. Akiwa katika hali ya kufikiri mara akasikia vishindo vya watu zaidi ya wawili wakiingia kutokea nyuma yake, walitembea taratibu na kusimama mbele yake.
Jasusi Shadow alipowatazama moyo wake ulipiga Paaa!! Kutokana na mshituko mkubwa alioupata, alikuwa ni Jesca yule mke wa Tino akiwa na Madam Sultana pamoja na Daktari wa hospitali hiyo ambaye ndio mtu pekee hospitalini hapo anayeijua siri ya Sultana.
"Unashangaa nini hukutegemea kutuona? Unafikiri ungeendelea kutuchezea akili mpaka lini Shadow?" Aliongea Madam Sultana huku akiwa anamtazama Jasusi Shadow kwa macho makali.
"Nini shida bosi?" Aliuliza Jasusi Shadow akitaka kujua ni nini hasa kilichomfanya Sultana amuweke chini ya ulinzi, alihisi mambo tayari yameharibika akataka kujihakikishia.
"Shadow najua umekuwa mwaminifu kwetu tangu enzi za marehemu mume wangu ila tangu ujue mipango yangu ni wazi umeanza kwenda kinyume na mimi, unanisaliti" Alieleza Sultana.
"Kivipi bosi mbona sielewi?"
"Ahh! Usijifanye hujui kitu najua unanielewa vizuri, tulikubaliana na marehemu kuwa utakuwa bega kwa bega na mimi ukinilinda nyakati zote haijarishi nini kitatokea sasa mbona unakwenda kinyume? Unaweza kuniambia kuanzia tulipoachana hapa kwa mara ya mwisho ulikuwa wapi?"
"Bosi ulitakiwa kuniuliza kwanza na sio kuni...."
Alisema Jasusi Shadow lakini kabla hajamalizia kuongea Sultana alichomoa bastola iliyokuwa ndani ya baibui lake akaikoki na kufyatua risasi ambayo ilipiga sakafuni katikati ya miguu ya Jajusi Shadow.
"Unafikiri natania Shadow, now tell me everything...!! ni nani unaeshirikiana naye na mnapanga kufanya nini usiponiambia ukweli nakuhakikishia leo ndio utakuwa mwisho wako" Sultana aliongea kwa kumaanisha huku akisogea karibu kabisa na alipo Shadow.
Ni kweli Sultana alikuwa amedhamiria kufanya kile anachokisema tayari alishagundua kuwa kijana wake wa muda mrefu Shadow alikuwa anamzunguuka kwa namna moja au nyingine.
"Haukwenda kule tulikopanga, haujaenda kuleta chupa ya kijani tuliyokubaliana, hiyo ndio sababu haukutaka nikupe watu wa kukusaidia kumbe unamambo yako ya siri unayafanya, haya unaweza kuniambia ulikuwa wapi? na nani? mnafanya nini?"
Aliuliza Sultana.
Wakati wote huo Jajusi Shadow alikuwa kimya huku akiwaza nini afanye. Alishaona kabisa tayari mambo yameharibika Sultana kamshitukia.
Uwezo wa kupambana na kutoka kwenye balaa hilo alikuwa nao, kwa namna Sultana alivyomsogelea angeweza kumvaa na kumteka kisha kutoka akiwa salama lakini aliwaza kama atakuwa mbali na Sultana basi ni ngumu kujua ilipo chupa ya kijivu yenye kinga na tiba dhidi ya vimelea vya V-COBOS, hakuna mtu mwingine anayefahamu chupa hiyo ilipo zaidi ya Sultana mwenyewe.
"Huna cha kujibu au unafikiri unàweza kutoka hapa ukiwa salama Shadow ukweli nakuua leo" aliongea Madam Sultana kisha akatoa ishara fulani wale wanawake waliweka bunduki zao sawa na kuzielekeza alipo Jajusi Shadow, Jesca na Sultana nao walimnyoshea bastola zao zilizofungwa kifaa maalumu kinachozuia mlio wa risasi kusikika 'silencer'
"Haya Jajusi endelea kuwaza namna ya kutoroka mimi sina muda wa kupoteza nahesabu mpaka kumi kama hujaongea ukweli basi nakuondoa duniani, Kumi...tisa....nane....saba.....sita....tano...nne...tatu....mbi...."
"Nitaongea! nitaongea! nitaongea ukweli bosi Sultana.." Jajusi Shadow alidakia kabla Sultana hajamaliza hesabu yake na kufyatua risasi.
"Ongea nakusikiliza.."
"Ukweli sikwenda kuvamia maabara Madam" Alisema Shadow huku akiwaza namna gani ataweza kujiokoa mwenyewe
"Najua.. eleza mtu unaeshirikiana naye kunizunguuka na usijaribu kudanganya nitakuua"
"Hakuna ninayeshirikiana naye madam ila wakati najiandaa kwenda maabara kuu ya serikali nilitekwa na watu nisio wafahamu sijui waliwezaje kunipata, baadae nikagundua ni wale wazungu kutoka Mexico namaanisha wale wamiliki halali wa virusi vya V-COBOS. Sultana hawa watu tayari wapo hapa nchini na tayari wameshachukua vimelea kutoka maabara kuu ya serikali na sasa wanaitafuta ile chupa ya kijivu niliwasikia wakiongea kuwa tayari wameshajua ilipo na jioni ya leo wataenda kuichukua" Shadow alidanganya.
Sultana alitulia kwa muda akijaribu kutafakari maelezo hayo ambayo kwa kiasi yalimuingia. Habari za wamexico kuwepo nchini ndio zilizomchanganya zaidi, kusikia virusi vimetolewa maabara na sasa wanavyo wao ilikuwa ni habari mbaya mno kwa Sultana. Ndoto aliyoihangaikia kwa muda mrefu sasa ilikuwa mbioni kuzimwa kama mshumaa uliopulizwa na upepo.
"Wewe uliwezaje kutoka?" Aliuliza Sultana huku safari hii sauti yake ikiwa ndogo
"Niliwatoroka"Alijibu Shadow. Kukawa na ukimya tena, mwisho Sultana akaongea.
"Jesca andaa kikosi kazi muondoke kuifuata chupa yangu ya kijivu" Alisema Sultana lakini kauli hii ilimshtua sana Jesca
"Madam tutawezaje kwenda bila wewe, kumbuka chupa ilikabiziwa kwa chifu wa kabila hawawezi kuitoa bila wewe kuwepo"
"Tumieni nguvu ikibidi hata kuua"
"Sultana lile kabila sio rahisi kupambana nalo mbona uki..."
"Jescaaaaa! Umeanza lini kunipa ushauri, fanya kama nilivyosema nendeni mkailete chupa hapa mimi nina kazi ya kufanya au hujasikia kama wazungu wamechukua vimelea vyao, unafikiri kama wote tukienda huko hivi vimelea tutavipataje, kumbuka tunahama kutoka plan A kuja plan B"Sultana alifoka, kisha akageuka na kumuangalia Shadow.
"Na wewe nikigundua kuwa unatudanganya nitakuua kifo kibaya sana. Haya mhamisheni hapa mpelekeni kwenye ngome hakikisheni mnamlinda na msisahau kwamba huyu ni mtu hatari sana kosa moja linaweza kuwaghalimu. Siwezi kumwamini kwa sasa mpaka mambo yatakapokaa sawa"
Baada ya Sultana kusema hivyo, Daktari wake aliingiza mikono kwenye mifuko ya koti lake akatoa kichupa kidogo na bomba la sindano akavuta ile dawa kisha akasogea karibu na Jajusi Shadow.
Wakati huo wote Shadow alikuwa ametulia kimya kabisa tayari uongo wake ulikuwa umefanya kazi kwa asilimia kadhaa alipata akachokitafuta. Tayari alishajua mazingira ambayo chupa ya kijivu inaweza kuwepo japo hakujua ni wapi. Maneno aliyoyazingatia katikati majadiliano ya Sultana na Jesca ni haya...
,,,,Chupa ilikabidhiwa kwa chifu wa kabila,,,,,,
,,,Lile kabila sio rahisi kupambana nalo,,,,,,
Haya ndio maelezo muhimu shadow aliyoyapata, angalau alikuwa na kwa kuanzia. Wakati daktari akiwa amefika karibu yake Shadow alitazama saa ya ukutani akaona ilikuwa ni saa nane na nusu mchana kisha akaminya kitufe furani kilichokuwa kwenye saa yake ya mkononi. Shadow alijua nini anafanya.
Yule daktari alifika na bila kusita iliinua mkono wake kwa nguvu kisha akaizamisha ile sindano kwenye shingo ya Shadow na kusukuma ile dawa. Hazikupita sekunde 30 Shadow alianguka chini na kupoteza fahamu.
"Mbebeni mpelekeni kwenye ngome, nasisitiza tena kuweni makini"
"Sawa bosi"
Walijibu wale wanawake walioshika bunduki.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati ule Jajusi Shadow amebonyeza kitufe cha saa yake ya mkononi upande wa pili saa aliyokuwa amevaa Sandra ilitoa mtikisiko na kisha kuanza kuwaka mwanga mwekundu. Akiwa nje ya ile nyumba msituni alikimbia hadi kwenye gari moja iliyokuwa imeegeshwa pembeni kidogo na nyumba akafika na kumuamsha mtu mmoja ambaye alikuwa amepumzika ndani ya gari hiyo.
"Fungo Fungo" Sandra aliita huku akigonga gonga kioo cha gari hiyo.
Fungo ni kijana mmoja mtaalamu wa kompyuta na mtandao ambaye ni kati ya wale watu watatu wanaofanya kazi chini ya Mheshimiwa Rais Dkt Alfredo Zumo kwa siri. Ndio huyu aliyeweza kuliendesha gari la Tino akiwa nje ya gari na mwisho akalitupa darajani ndani ya maji.
"Nini Sandra"
"Hivi hujaona saa yako"
"Kwani vipi?" Aliuliza Fungo huku akivaa miwani yake mikubwa na kuangalia saa yake ya mkononi. Kama ilivyokuwa kwa Sandra saa ya Fungo pia ilikuwa ikitoa mwanga mwekundu.
"Nini kinaendelea?"
"Ni Jajusi Shadow atakuwa kwenye matatizo"
"Jesus Christ..!!"
"Angalia haraka ni wapi alipo ngoja nimshtue Aron"
"Aron alitoka.." Alijibu Fungo huku akifungua kompyuta yake na kuanza kucharaza vidole vyake kwa kasi ya ajabu.
"Nini! Aron kaenda wapi?"
"Aliniaga kaenda kwenye kaburi la baba yake"
"Sasa kwa nini ulimruhusu?"
"Jesus Christ! Sandra unanichanganya hebu acha kwanza nimtrace Jajusi Shadow... Ningeanzaje kumkatalia asiende kwenye kaburi la baba yake na unajua kapewa historia nzito hayuko sawa. Usijali nilimpa mavazi mazuri hawezi kujulikana, ila kaondoka na pikipiki yako"
Alijibu Fungo huku akiendelea kucharaza kompyuta yake ndogo kwa kasi sana.
"Huyu hapa nimempata, yuko Hospitali ya Mountenia" Alisema Fungo
"Mh! Hospitali, yupo kwa Madam Sultana sasa kuna shida gani hadi aombe msaada au kashitukiwa"
"Jesus Christ! Mungu aepushie mbali"
"Washa gari twende pitia makaburini tumchukue Aron pia"
"Jesus Christ! Makaburini tena huoni kama tutachelewa"
"We twende bwana"
[emoji294][emoji294][emoji294]
Inspekta Aron alionekana maeneo ya makaburini mbele ya kaburi la baba yake marehemu jenerali Phillipo Kasebele. Alikuwa amevaa nguo nyeusi kofia na barakoa nyeusi pia, kofia yake aliishusha chini sana kiasi cha kufanya macho yake pekee ndio yawe wazi, haikuwa rahisi kwa mtu yeyote kumtambua.
Mambo aliyokuwa ameelezwa na Mheshimiwa Rais yalikuwa ni mazito mno kwa Aron. Kilichomuumiza sana ni kuambiwa mtu aliyemuua baba yake ni kaka yake Tino tena mbaya zaidi kwa ajili ya tamaa ya kuvitaka vimelea vya V-COBOS ambavyo mpaka sasa wanagombania yeye na mama yake Sultana. Habari hizi hazikuwa njema hata kidogo kwa Inspekta Aron.
Alimaliza kuomboleza akageuka tayari kuondoka lakini uso kwa uso anakutana na mwanamke anayemfahamu akiwa amesamama nyuma yake. Alikuwa ni Najma. Inspekta Aron aliduwaa kwa muda
"Au naota" Aliwaza Aron
Je, nini kimetokea? Imekuwaje? Kwa nini Najma yuko hapa? Vipi kuhusu Sultana na Jesca?
Jasusi Shadow atakuwa salama?
ITAENDELEA....