THE MODERN WAR: Simulizi ya kijasusi mapenzi na upelelezi

THE MODERN WAR: Simulizi ya kijasusi mapenzi na upelelezi

THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya...............39
Mtunzi: Saul David
Email: saulstewarty@gmail.com
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Kwa kuwa nguo alizokuwa amevaa Osward zilikuwa ni sawa kabisa na nguo alizovaa Inspekta Aron kuanzia juu mpaka chini walinzi waliamini moja kwa moja kuwa huyo ndio yule yule mtu waliyekuwa wakimuandama tangu awali mtu aliyempiga risasi ya kifua Waziri wa afya Dokta Gondwe, hakuna aliyejua mabadilishano yaliyotokea ndani ya sekunde chache kabla ya wao kufika.

Je nini kitafuata?

SASA ENDELEA...

"Wanataka kuniuzia kesi" Aliwaza Inspekta Aron ni kama aliweza kuelewa kwa haraka ni nini kinaendelea hadi dakika hiyo. Kitendo cha akina Osward kumtupa maeneo yale kisha kuondoka na kumuacha tayari kilimfanya aielewe mbinu hiyo hasa baada ya kuwaona wale walinzi wanakuja nyuma yake kwa kasi sana.

"Kwani Osward kafanya tukio gani? hapana siwezi kukubali" aliwaza Aron huku akisimama haraka.

"Usijaribu tena kuendelea kukimbia tutakumwaga ubongo wako, simama na ujisalimishe mwenyewe" alisema mlinzi mmoja ambaye yeye alikuwa na mbio kuwazidi wenzake tayari alikuwa amefika jirani kabisa na alipokuwa Inspekta Aron.

"Hapana siwezi kuwa na mwisho wa kizembe namna hii, haiwezekani kabisa" Aron aliwaza na hapo akaanza kukimbia kwa kasi lakini kabla hajapiga hatua hata tano mara alihisi kitu cha moto kimezama kwenye paja lake la kushoto ikifuatiwa na maumivu makali.
Inspekta Aron hakuweza tena kuunyanyua mguu wake alishika sehemu ile yenye maumivu kwa mkono wake wa kulia, alipoutazama mkono wake ulikuwa umelowa damu. Naam Inspekta Aron alikuwa amepigwa risasi.
Kufumba na kufumbua polisi wengine wa mtaa pamoja na trafiki wa barabarani wakatokea mbele yake wakija kwa kasi huku siraha zao zikiwa mbele.
"Nimekwishaa..." Alijisemea Inspekta Aron huku akilegea mwili na akili.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Dakika tano tu mara baada ya Dokta Gondwe kupigwa risasi gari la wagonjwa liliwasili kwa kasi eneo hilo, upesi wahuduma wa afya walifika na kuanza kutoa huduma ya kwanza kabla ya kumuingiza kwenye gari. Kwanza walijaribu kuzuia damu nyingi iliyokuwa ikimtoka Dokta Gondwe na baadae kujaribu kuunganisha mfumo wake wa upumuaji na mtungi wa gesi waliokuja nao.

Wakati jitihada hizi zikiendelea Najma alikuwa pembeni akilia kwa uchungu huku akiwa ameshikiliwa na baadhi ya watu wakijaribu kumzuia ili awaache madaktari wafanye kazi yao. Hofu ilikuwa ni kubwa si kwa Najma tu bali kwa kila mtu aliyekuwepo eneo hilo kila mtu aliyekuwa akishuhudia au kuliona na kulisikia tukio hili kupitia vyombo vya habari.

Baada ya kupambana sana kuyaokoa maisha ya mtu mkubwa serikalini Dokta Isaack Gondwe hatimaye jitihada zao zilionekana kugonga mwamba kwani risasi ilikuwa imepenya sehemu mbaya mno haikuwa rahisi hata kidogo Dokta Gondwe kusalimika.
Naam, Waziri wa afya Mheshimiwa dokta Gondwe aliaga Dunia pale pale kabla hata jahaingizwa kwenye gari kupelekwa hospitali.

Wataalamu wa afya waliokuwa wamemzunguuka Dokta Gondwe wakipambania maisha yake walianza kutoka mmoja baada ya mwingine na kurudi kwenye gari, sura zao zilitoa tafsiri harisi ya kile kilichokuwa kikiendelea. Hakukuwa hata na sababu ya kuuliza kwani walio salia waliufunika mwili wa Dokta Gondwe na shuka la kijani kuanzia juu mpaka chini na kisha kuubeba kwenye machela hii ilionyesha wazi kuwa tayari Roho ya Waziri wa afya imekwisha kuacha mwili.

"Baaabaaaaaaaa!!" Najma alipiga kelele huku safari hii akiwazidi nguvu watu waliokuwa wamemshika, akakimbia na kwenda kusimama mbele ya wataalamu wa afya walioubeba mwili wa baba yake. Najma alianza kuutikisa mwili wa baba yake huku akilia kwa uchungu, baadhi wa watu walifika na kushika tena kwa mara nyingine huku wakijaribu kumtuliza binti huyo ambaye alimpenda mno baba yake.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati sekeseke hilo likiendelea mheshimiwa Profesa Cosmas Kulolwa Rais mstaafu alikuwa bado yuko juu kabisa ghorofani katika nyumba yake ya kifahari. Alikuwa akifuatilia kwa kila hatua juu ya mambo yaliyokuwa yakiendelea wakati huo. Kila kitu kilikuwa kinaenda kama alivyopanga, yote yaliyokuwa yakiendelea wakati huo ilikuwa ni ndani ya mpango madhubuti wa mzee huyu Profesa Cosmas Kulolwa. Tayari alishapata taarifa ya kifo cha rafiki yake kipenzi Dokta Gondwe, sasa alikuwa akisubiri taarifa mbili muhimu wakati huu. Ya kwanza ilikuwa ni kukamatwa kwa Inspekta Aron akiwa kama mtuhumiwa namba moja wa kesi ya mauaji ya Dokta Gondwe na taarifa ya mwisho ilikuwa ni hukumu ya kijana wake Osward mahakamani muda mfupi ujao.
Wakati akiwaza hayo mara simu yake iliingia ujumbe wa maandishi katika mtandao wa WhatsApp ujumbe uliombatana na picha. Ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Profesa Fernando wa mexico mkurugenzi mtendaji wa maabara ya ZMLST. Picha iliwaonyesha wazungu wawili ambao sura zao hazikuwa ngeni kwake lakini nyuma yao wakiwa wamesindikizwa na watu weusi watatu waliojazia misuli huku wakiwa na vipara vilivyong'aa sana kichwani. Profesa Kulolwa aliitazama ile picha kisha akasoma ujumbe uliopo chini.
,,,,,,,,,,as we talked before, we have already started an official trip to your country to come and find our gray bottle and then spread the COBOS virus, you have definitely done your job,,,,,,,,,,,
(kama tulivyoongea kabla, tayari tumeanza safari rasmi kuja nchini kwako kwa ajili ya kuja kutafuta chupa yetu ya kijivu na kisha kusambaza ugonjwa wa virusi vya COBOS bila shaka umeshafanya kazi yako)
Baada ya kuusoma ujumbe huu Profesa Cosmas Kulolwa alivuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu.
"Kumekucha" Alisema Profesa Kulolwa.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili ile gari aina ya Noah ilizidi kuchanja buga kwa kasi huku binti mrembo Asia akiwa ndio dereva, wakati huo Osward alikuwa bize kubadilisha nguo zake akavaa nguo za magereza zile alizotoroka nazo usiku wa jana kisha akamalizia na koti kubwa jeusi kwa juu.
Dakika chache baadae gari ilifika na kuingia hadi ndani kabisa ya lile jengo chakavu walilokuwepo mwanzo.
Asia aliingiza gari ndani na kufungua breki kali, bila kupoteza muda mlango wa gari ukafunguliwa Osward na wale malaika weusi wakashuka kwa haraka.
"Sasa warembo mimi narudi gerezani kisha nitapelekwa mahakamani alafu baada ya hapo nitarudi uraiani tutakuwa pamoja sawa" alisema Osward huku akisogea kwenye moja kati ya pikipiki nne zilizokuwa zimeegeshwa katika mstari mmoja ndani ya jengo hilo.

"Sawa kila la kheri Osward sisi tunarudi eneo la tukio kuangalia kinachoendelea kama ilivyopangwa, jukumu letu la mwisho ni kuhakikisha unashinda kesi bila pingamizi lolote" alijibu Elina huku yeye na wenzake wakivua zile baibui sasa wakabaki na nguo nyingine walizovaa ndani. Vipensi vya jeans vilivyoacha mapaja yao nje, kitopu na kijikoti cha mikono mifupi kwa juu. Waliongeza kwa kuvaa miwani ya jua na mwisho kabisa walichukua siraha kama visu na bastola wakazichomeka kwenye mifuko ya ndani ya koti. Wakati huo Osward alishawasha pikipiki na kuondoka kwa kasi sana.
Baada ya kukamilisha kila kitu Erica Elina na Asia kila mmoja akiwa na pikipiki yake walitoka kwa mwendo wa taratibu nje kabisa ya jengo hilo baada ya kufika umbali wa mita kadhaa wakasimama.

Erica alivua miwani yake na kuwatazama wenzake, wote wakaonyesha ishara kuwa afanye alichokusudiia kufanya. Haraka Erica alitoa rimoti fulani ndogo kwenye mfuko wa pensi yake akabinya kitufe chenye rangi nyekundu hapo mlipuko mkubwa ukatokea kwenye kile jengo walilokuwepo. Kila kitu kikasambaratika na kuteketea kwa moto ikiwa ni pamoja na lile gari Noah nyeusi vyote vilikuwa vikiungua kwa moto wakati huo Erica Elina na Asia wakawa wanaondoka eneo hilo kwa mwendo wa taratibu sana kila mmoja akiwa na pikipiki yake.

ITAENDELEA....
Simulizi ni shillingi 1,000/= lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina saul au Airtel money namba 0788967317 jina saul kisha njoo WhatsApp inbox namba hizo hizo
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.............40
Mtunzi: Saul David
Email: saulstewarty@gmail.com
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Kila kitu kikasambaratika na kuteketea kwa moto ikiwa ni pamoja na lile gari Noah nyeusi vyote vilikuwa vikiungua kwa moto wakati huo Erica Elina na Asia wakawa wanaondoka eneo hilo kwa mwendo wa taratibu sana kila mmoja akiwa na pikipiki yake

SASA ENDELEA....
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati mwili wa aliyekuwa Waziri wa afya marehemu Dokta Isaack Gondwe ukiingizwa kwenye gari ya wagonjwa ghafula tukio lingine la kustaajabisha likatokea. Walinzi wa jengo la Maendeleo CFC, walinzi wa Dokta Gondwe na askari polisi wengine walioneka wakirudi eneo la tukio wakiambatana na muharifu ambaye ni Inspekta Aron wakiamini ndiye aliyehusika na tukio la mauaji ya Dokta Gondwe.

Inspekta Aron alikuwa akiletwa mkuku mkuku na wale walinzi wakati huo pia gari ya polisi difenda ilifika na kufunga breki kali katika eneo la tukio. Aron alikuwa amejeruhiwa vibaya mara baada ya kupigwa risasi katika mguu wake wa kushoto uso wake ulikuwa wazi mara baada ya kuvuliwa maski na kofia aliyovalishwa na wale malaika weusi.
Macho na kamera za watu ziligeuka kutoka kwenye mwili wa marehemu na sasa habari kubwa ikawa ni kukamatwa kwa muuaji ambaye ni askari mpelelezi kutoka kituo cha kati Morton kilichopo mjini hapo. Sura ya Inspekta Aron haikuwa ngeni sana machoni pa watu tayari alikuwa ameanza kujizolea umaarufu mkubwa kutokana na tabia yake ya uchapakazi. Lakini pia alikuwa ni mtoto wa mtu maarufu nchini marehemu Jenerali Phillipo Kasebele.
Wakati Najma akilia kwa sauti kumlilia baba yake, alisikia kelele za watu wakimlaani na kumsema vibaya mtu aliyehusika na tukio la mauaji ya baba yake. Akiwa na majonzi mazito Najma aligeuka kumtazama muuaji huyo ambaye aliikatisha safari ya maisha ya uhai wa baba yake.
Uso kwa uso Najma akagonganisha macho na inspekta Aron mwanaume ambaye tayari alikuwa ameshauteka moyo wake na alikuwa akimpenda sana.
"Aron!!?" Najma aliita kwa sauti ya chini huku akiwa haamini kile anachokiona, ni kweli Aron kijana aliyemuona kuwa mwaminifu na mwenye moyo wa kipekee sana kumbe ni muuaji. Ndio huyu aliyeyakatisha maisha ya baba yake ambaye alikuwa akimpenda kuliko maelezo.
Upande huu alikuwa Najma akiwa ameshikiliwa na baadhi ya watu waliokuwa wakimfariji upande mwingine alikuwa Inspekta Aron nae akiwa ameshikiliwa na polisi wakawa wanatazamana uso kwa uso na Najma.
Najma aliumia sana kiasi cha kukosa nguvu za kuhimili kusimama, akaanguka chini mzima mzima akawa amepoteza fahamu.
"Najmaa..."Aron aliita huku akijaribu kujitoa kwenye mikono ya wale polisi waliokuwa wakimkokota kumpeleka kwenye gari.
"Hivi hili jamaa lina akili kweli? Yaani umemuua baba yake alafu unajifanya kumuonea huruma" Aliongea askari mmoja kwa rafuzi ya kisukuma huku akimtwanga Inspekta Aron kibao kizito kichwani.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Tukio hili la kutisha lililotokea asubuhi hii liliteka hisia za watu wengi sana nje na ndani ya nchi. Macho na masikio ya kila mtu yalikuwa yameelekezwa katika tukio hili ambalo liliibua simanzi nzito nchini. Tukio la kuuwawa kikatili mtu mkubwa serikali mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe ilikuwa sio jambo la kitoto. Mbaya zaidi iliaminika moja kwa moja kuwa muhusika wa mauaji hayo alikuwa ni Inspekta Aron mtoto wa aliyekuwa Jenerali wa kuheshimika bwana Phillipo Kasebele. Wengi walitamani kuchimba na kujua undani harisi wa tukio hili, kwa nini Aron kijana muadilifu kazini aamue kumuua waziri wa afya?. Kila mmoja alikuwa akiongea lake mtaani, wapo waliosema labda ni kwa sababu ya tamaa za madaraka lakini bado haikuingia akilini. Wengine wakadai labda yule mwanamke kwenye picha chafu za Dokta Gondwe zilizosambaa mtandaoni ni mpenzi wa Inspekta Aron lakini bado hii nayo haikuingia akilini. Kila kitu kikabaki kuwa fumbo tena fumbo kubwa. Hakuna aliyedhani wala kufikiri kuhusu muuaji harisi ambaye ni kijana Osward aliyetoroshwa kutoka gerezani usiku kisha akakamilisha mauaji haya halafu akarudi tena gerezani.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Hizi zilikuwa ni habari mbaya sana kwa Tino kaka yake na inspekta Aron ambaye alizipata akiwa ndani ya ile ofisi yake ya kurekodi na kusambaza picha za utupu. Tino akiwa na kijana wake mwaminifu Bosco walipata taarifa hii wakati walipokuwa wakifuatilia matangazo ya moja kwa moja kutoka katika mkutano wa Dokta Isaack Gondwe na waandishi wa habari. Walishuhudia kila kitu tangu Dokta Gondwe alipopigwa risasi akafariki Duniani na hata kukamatwa kwa Inspekta Aron.

"Aron umefanya nini mdogo wangu? Umefanya nini we kijanaa" Tino alikuwa akiongea kwa masikitiko makubwa.

"Kwa nini kila siku wewe? Kwa nini huwa huachi kuingilia mipango yangu na kuiharibu? Yaani uko hivyo tangu tukiwa wadogo, wewe ndio ulikuwa chanzo cha baba yangu kunichukia ni wewe Aron, leo tena....." Tino alizidi kualalamika hali akizunguuka huku na huku ndani ya kile chumba, alionekana kudata haswa.

"Yalikuwa yamebaki masaa tu masaa machache tu Aron, yaani masaa tu umeshindwa kuvumilia mimi nikabidhiwe vimelea vya V-COBOS masaa machache tu Aron, eti Bosco si masaa tu yalikuwa yamesalia ee.." Alisema Tino akionekana kulaani vikali kitendo cha mdogo wake Tino kumuua Dokta Gondwe, wala saula la kukamatwa kwa mdogo wake halikumuumiza sana kama kifo cha Dokta Gondwe.

"Bosi hebu jaribu kutuliza akili yako tuone ni nini cha kufanya tafadhali" Bosco alijaribu kumtuliza Tino aliyeonekana kuchanganyikiwa.

"Tutafanya nini Bosco? Tutafanya nini? Ona tayari Dokta Gondwe ameshakufa ni wapi tutapata vimelea vya V-COBOS, ni wapiiiii?... Unajua ni kiasi gani nilitamani kumuua huyu mtu mimi mwenyewe? si unajua lakini Bosco kuwa huyu mwanaharamu alilala na mke wangu, alimfanya mke wangu lakini mimi nilikaa kimya sikumuua nilivumilia kila kitu, Sasa inakuwaje mtu anakuja na kumuua kirahisi kwa nini yani? Aron kuanzia leo wewe utakuwa ni adui yangu namba moja. Haijarishi utapewa adhabu gani lakini nakuahidi ni lazima nitakupa machungu zaidi ya haya uliyonisababishia hii leo" Alisema Tino wakati huo macho yake yalibadilika na kuwa mekundu sana.

"Lakini bosi mimi kuna kitu nakiona hapa" Alisema Bosco wakati huo akizidi kufuatilia kila hatua yaliyokuwa yakiendelea nje ya jengo la Maendeleo CFC.

"Nini?" Aliuliza Tino
"Vipi kama huu ukawa ni mtego? Vipi kama ni mbinu ya Dokta Gondwe kutaka kutukwepa kwa mara nyingine?" Aliuliza Bosco
Tino alitulia kwa muda kisha akaongea...
"Ni kweli Dokta Gondwe amekufa Bosco, mtu mkubwa kama huyu serikalini hawezi kudanganya kwa kiwango hichi"
"Ni kweli bosi lakini vipi kuhusu vimelea vya V-COBOS nalo sio jambo dogo ni kubwa, sioni ajabu Dokta Gondwe kujaribu kuigiza kifo" Bosco aliendelea kukazia wazo lake
"Kwa hiyo unataka tufanyaje?"
"Bosi tukiendelea kukaa humu hakuna tutakachokipata, hebu twende tujichanganye mtaani eneo la tukio tutaelewa kila kitu" Bosco alitowa wazo ambalo baada ya kufikiri sana Tino akaunga mkono, haraka alichukua simu yake na kumpigia Godwin maarufu kama sniper G yule mdunguaji.

"Dogo uko wapi?"
"Nipo naelekea jengo la Maendeleo kaka, si umesikia kilichomtokea bosi hatunae tena"
"Nimesikia, ni taarifa mbaya sana ki ukweli. Sasa sikia mimi pia nakuja hapo sio mda naomba fanya kazi ya kuchuguza kwa makini kila kinachoendelea hapo lolote utakalohisi haliko sawa wewe ulifuatilie kwa ukaribu, Najua unajua nini namaanisha Godwin" Alieleza Tino
"Sawa lakini umeshasikia mtu aliemuua bosi"
"Kusikia kivipi?"
"Aaa... Yaani namaanisha unajua kama mdogo wako Inspekta Aron ndio kamuua Dokta Gondwe?"
"Najua hebu fanya kazi niliyokupa"
"Sawa kamanda nimeshafika eneo la tukio" Alijibu Godwin kisha akakata simu.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Inspekta Jada alikuwa miongoni kati ya watu waliofika eneo la tukio haraka sana mara tu baada ya taarifa kuanza kusambaa kwa kasi kwenye vyombo vya habari.
Alifika na kusimamisha gari la Inspekta Aron alilokuja nalo akashuka haraka na kuanza kukimbia kuelekea kwa wale askari ambao ndio kwanza walikuwa wanampandisha Inspekta Aron kwenye difenda tayari kuondoka nae.

"Nipishe nishipe.. sorry..." Alisema Jada wakati akikatisha katikati ya umati mkubwa wa watu waliofurika eneo hilo kushuhudia kila kinachoendelea.
Jada alijipenyeza hadi alipowafikia wale askari haraka akakimbia na kwenda kusimama mbele ya gari kabla Inspekta Aron hajarushwa ndani.

"We dada hebu pisha hapo haraka" Askari mmoja alifoka na kumchimba mkwara mzito Jada ambaye alikuwa ameyagandisha macho yake kumtazama Inspekta Aron.

"Inspekta Jada sogea pembeni tafadhali, tuache tufanye kazi yetu" Askari mwingine ambaye yeye alikuwa akimfahamu Jada alikazia. Lakini Jada hakutaka kuelewa akasogea hadi alipo Inspekta Aron akamshika begani kwa mikono yote miwili.

"Inspekta Aron umefanya nini, sema kitu tafadhali mbona uko kimya" alisema Inspekta Jada huku akimtikisa Inspekta Aron ambaye wakati wote alikuwa kimya akionekana kama mtu aliyedata.

Polisi walitaka kumvaa na kumtoa Inspekta Jada lakini yule mwingine aliyeonekana kumfahamu Jada aliwazuia na kuwataka wampe mda kidogo azungumze na Aron.

"Sema kitu basii"
"Annah.. Annah" alisema Inspekta Aron
"Annah? Annah kafanyaje?"
"Mlinde sana Annah, mimi sijaua, aliyeua ni Osward....Jada tafadhali hakikisha Annah anafika mahakamani sasa hivi, nenda kamchukue muda umefika" Alisema Aron kwa sauti ya chini sana. Baada ya kusema hivyo wale polisi walimsukuma Inspekta Jada pembeni kisha wakamnyanyua Inspekta Aron juu juu na kumrusha ndani ya difenda.

Wakati haya yakiendelea katikati ya umati wa watu waliokuwa wakishuhudia tukio hili malaika weusi yaani Asia, Erica na Elina walikuwa ni miongoni mwao.
Wanawake hawa hatari walikuwa wakifuatilia kwa ukaribu sana kila kilichokuwa kikiendelea. Waliona kila kitu hata wakati Inspekta Aron akizungumza kitu na inspekta Jada.
Bado Malaika weusi walikuwa katika utekelezaji wa mpango kabambe uliosukwa na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa, mpaka sasa tayari walikuwa wamefanikiwa kwa mambo mawili muhimu moja ni kuuwawa kwa Dokta Gondwe pili kukamatwa kwa Inspekta Aron jambo la mwisho ambalo lilikuwa bado ni kuhakikisha Osward anashinda kesi yake mahakamani muda mfupi ujao bila kutokea kizuizi chochote kile.

Je, nini kitatokea?
Annah atawahi kufika mahakamani?
Tino na Bosco wako wapi?
Sultana na Jasusi Shadow wako wapi?
Nini hatima ya Inspekta Aron na Najma,?
Vipi wale wazungu wanaokuja kutoka Mexico?
Nini hatima ya kirusi cha COBOS?

ITAENDELEA....
0756862047
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.............41
Mtunzi: Saul David
Email: saulstewarty@gmail.com
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Bado Malaika weusi walikuwa katika utekelezaji wa mpango kabambe uliosukwa na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa, mpaka sasa tayari walikuwa wamefanikiwa kwa mambo mawili muhimu moja ni kuuawa kwa waziri wa afya Dokta Gondwe pili kukamatwa kwa Inspekta Aron jambo la mwisho ambalo lilikuwa bado ni kuhakikisha Osward anashinda kesi yake mahakamani muda mfupi ujao bila kutokea kizuizi chochote kile.

SASA ENDELEA....
[emoji294][emoji294][emoji294]
Asia, Erica na Elina kikosi cha wanawake watatu maarufu kama malaika weusi walionekana wamesimama pembeni ya barabara nyuma ya gari aina ya Noah alilokuja nalo Najma wakawa wanateta jambo.

"Kila kitu kipo shwari au mnaonaje?" Aliuliza Asia
"Hapana binafsi naona kuna jambo halikosawa kati ya Inspekta Aron na Inspekta Jada kuna kitu wamezungumza na kama mlivyoona Inspekta Jada kaondoka haraka sana baada ya mazungumzo yao" Alieleza Erica
"Kwa hiyo unataka kusemaje sisi jukumu letu la mwisho ni kuhakikisha Osward anashinda kesi kule mahakamani, mtu hatari tuliyetakiwa kumdhibiti ni Inspekta Aron huyu ndio tunatakiwa kuhakikisha haleti madhara yoyote hadi hukumu yake itakaposomwa, tuachane na Jada" Alisema Elina
"Hapana Elina, Erica yuko sahihi kama Inspekta Aron kaongea na Jada basi lazima kunakitu watafanya sasa sikieni Erica na Elina ninyi mfuatilieni Inspekta Jada alafu mimi nitabaki kuendelea kufuatilia hatima ya Inspekta Aron" Asia alitoa wazo ambalo baada ya kufikiri wote waliunga mkono, haraka Erica na Elina walienda hadi pale walipopaki pikipiki zao wakapanda na kuondoka kwa kasi kumfuatilia Inspekta Jada kama walivyokubaliana.

Wakati haya yote yakiendelea Godwin yule kijana anayefanya kazi pamoja na Tino chini ya marehemu Dokta Gondwe alikuwa mahali akitazama harakati za Malaika weusi.
Mara alisikia honi ya gari nyuma yake, Godwin alishtuka na kugeuka haraka. Aliweza kulitambua gari hilo lilikuwa ni la Tino. Godwin alipiga hatua akasogea hadi kwenye dirisha la dereva wa gari hilo, alikuwa ni Tino mwenyewe na pembeni yake alikuwepo Bosco.

"Vipi dogo" Tino alianzisha maongezi huku akishusha zaidi kiio cha dirisha la gari yake.
"Poa mambo ndio kama hivyo unavyoona, hivi sasa ndio watu wanatawanyika"
"So mzee kafa kweli au?"
"Aah! Tino swali gani hilo kamanda wangu ni kweli bosi kakata kamba kapigwa risasi ya moyo hivi ndio wameondoka na mwili wake sio mda"
"Aron je?"
"Wamemkamata, difenda ile wanasepa nae"
"Sawa kuna kitu umepata naona ulikuwa umenibipu hapa?" Aliuliza Tino na hapo Godwin akageuka nyuma kutazama.
"Unamuona yule demu?"
"Yupi yule kwenye pikipiki?"
"Yes! Yule aliyevaa kipesi cheusi cha jeans"
"Yap nimemuona"
"Unamkumbuka?"
"Hapana ni nani?" Aliuliza Tino, Godwin akasita kueleza zaidi huku akimtazama Bosco aliyekaa pembeni ya Tino.
"Usijali huyu ni mtu wangu wa karibu we endelea tu" Tino alimtoa Godwin wasiwasi akaendelea kuzungumza.

"Wako wadada watatu wanajiita Malaika weusi, huwa wanafanya kazi na matajiri wakubwa wakubwa wakiwa na ishu wanawatafuta hata kipindi kile Dokta Gondwe anapambana na marehemu baba yako aliwahi watumia hawa wanawake. Kama utakumbuka kipindi kile mzee wako alijeruhiwa sana akanusurika kifo"

"Aaaa... Sawa Malaika weusi, nimewakumbuka kipindi kile ndio nilikuwa naanza kufanya kazi na Dokta Gondwe"
Baada ya kumbukumbu hiyo Godwin alimueleza Tino kila kitu, nyendo zote za wanawake hao alizoziona tangu anafika eneo hilo.

"Kwa hiyo wawili wamemfuatilia Inspekta Jada?" Tino aliuliza ili kuhakiki maelezo ya Godwin
"Yap huyu mmoja ndio alibaki hapa ila naye naona anaifuata ile difenda iliyombeba Inspekta Aron"
"Powa basi wewe endelea kumfuatilia huyo hadi mwisho sisi ngoja twende na hawa waliomfuata Inspekta Jada"
Alisema Tino huku Bosco akitikisa kichwa kukubaliana naye, mwisho wakawasha gari na kuondoka.
"Unafikiri tukiwafuatilia hawa tunaweza kupata chochote Tino mbona kama tunatoka nje ya lengo?" Aliuliza Bosco wakati gari ikivuka upande wa pili wa mtaa kufuata barabara kuu.
"Lazima kutakuwa na kitu Bosco umeambiwa hawa wanawake walishawahi kufanya kazi na Dokta Gondwe" Tino alijibu kwa kujiamini huku akizidi kuongeza kasi ya gari yake.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Hospitali ya Mountenia ndani ya chumba mahututi (ICU) alipolazwa Madam Sultana alizipokea kwa masikitiko makubwa taarifa alizoletewa na shadow kijana wake kuhusu tukio la kuuawa kwa waziri wa afya Dokta Gondwe na muhusika wa mauaji hayo ni mtoto wake wa kumzaa Inspekta Aron.

"Hapana siwezi kuamini, mwanangu hawezi kufanya hivi namjua vizuri Aron, nimemlea mwenyewe hawezi hawezi hawezi" Sultana aliongea kwa msisitizo hali akipiga hatua kwenda mbele na kurudi.
"Hata mimi imekuwa ngumu kuamini bosi, nahisi kunakitu hakipo sawa hapa"
"Unahisi nini shadow hebu niambie"
"Madam nanvyoona hii ni vita ya vimelea vya V-COBOS, Dokta Gondwe kauawa kwa makusudi ili kulinda vimelea vya V-COBOS visitoke kwenda kwenye mikono ya mtu mwingine na kesi hii ya mauaji kapewa kwa makusudi Inspekta Aron" Jasusi Shadow aliongea akionekana ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa kufikiri na kupambanua mambo, alichowaza ndio ulikuwa uhalisia wenyewe.

"Kwa nini sasa waamue kumpa kesi Aron, kwa sababu zipi yani? Mbona hajui chochote kuhusu vimelea vya V-COBOS"
"Sultana kuna mawili, moja huenda Inspekta Aron anajua au anaukalibia ukweli kuhusu vimelea vya V-COBOS hivyo wanataka kumzuia mapema kwa kumsweka gerezani au walio mpa hii kesi ana uhasama nao" Alieleza Jasusi Shadow
"Pili?" Madam Sultana iliuliza
"Aah kitu cha pili kwanza nikuulize, unahisi ni nani anaweza kuwa anafamu siri ya kwamba wewe unayo chupa ya kijivu yenye kinga na tiba dhidi ya vimelea vya V-COBOS?"
"Unataka kusema nini shadow?"
"Maana yangu ni kwamba kama yupo huyo mtu basi hii ni hatua yake ya kwanza anajaribu kukutisha kwa kumtumia mwanao Aron" Jasusi Shadow aliongea kauli iliyomfikirisha sana madam Sultana. Lakini huu ulikuwa ni mtego kutoka kwa Jasusi Shadow kumbuka kwa sasa yupo karibu na madam Sultana ili tu kuzuia njama zake za kutaka kutumia Virus vya V-COBOS kwa manufaa yake binafsi na kuhatarisha maisha ya mamilioni ya watu.
"Sidhani kama kuna mtu anaelewa chochote kuhusu mimi kuwa na hiyo chupa ya kijivu zaidi ya wewe Jesca na Tino, hebu achana na hilo kwanza elekeza akili na mawazo yako kwenye kazi ya leo kuvamia maabara kuu ya serikali na kuviiba vimelea vya V-COBOS basi suala la Aron niachie mimi nitashughulika nalo" Alisema Sultana.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Annah akiwa amejifungia chumbani kwa Inspekta Jada mara alisikia muungurumo wa gari nje ya nyumba hiyo.
"Aron, atakuwa ni Aron wangu" aliwaza Annah huku akikimbia kutoka chumbani hadi sebureni akasogea dirishani na kufungua pazia taratibu akachungulia nje ndipo alipomuona Inspekta Jada anashuka kutoka kwenye gari ya Aron akawa anapiga hatua ndefu ndefu kuelekea mlangoni.
"Aron hayupo? Inamaana hajampata?" Alijisemea Annah huku hofu yake ikizidi kuongezeka, hakika alimpenda sana Aron. Hakujua wala hakuwa na taarifa yoyote juu ya kukamatwa kwa Aron.

Inspekta Jada akiwa amekaribia ulipo mlango wa kuingia ndani ya nyumba yake mara simu yake iliita haraka akaichukua kutoka mfukoni akaipokea.

"Hallo wakili" Jada alianzisha mazungumzo kwa sauti ya chini sana ilikuwa ni simu kutoka kwa mwanasheria ambaye alikuwa akisimama kama wakili upande wa mashtaka katika kesi ya Osward kule mahakamania, aliitwa Andrea.

"Jada ni nini kinaendelea? Inakuwaje Inspekta Aron kakamatwa? Ni kweli kaua?" Andrea aliuliza maswali mfurulizo
"Sina muda wa kueleza sana bwana wakili nikifika huko tutaongea zaidi ila kwa ufupi aliyefanya haya mauaji sio Inspekta Aron kama wengi wanavyodhani ni Osward"
"Osward? Kivipi yani hii inawezekanaje mbona Osward kaletwa hapa mahakamani hata dakika tano hazijapita" aliuliza Andrea
"Ki ukweli sina majibu sielewi, ila kaniambia Aron mwenyewe"
"Mmh! Aisee mambo ni mengi sana, okay fine! Vipi kuhusu huyo binti shahidi yuko wapi ilitakiwa muwe mmeshafika mpaka sasa"
"Hivi ndio nipo kumchukua tuje huko"
"Mnh! Mtawahi kweli hebu jitahidi bado dakika 11 pekee"
Kabla Jada hajajibu kuhusu suala la kuwahi mara aliona kitu ambacho kilimshtua sana, malango wa nyumba ya Inspekta Jada ulikuwa ni wa kioo hivyo kupitia kile kioo aliweza kumuona mtu mmoja akiwa amesimama na pikipiki yake pembeni ya barabara hatua kadhaa kutoka ilipokuwa nyumba yake, alikuwa ni pacha Erica.
Japo hakuonyesha mshtuko wowote lakini kwa macho ya Jada yenye uzoefu wa kazi ya upelelezi aliweza kugundua moja kwa moja kuna kitu hakipo sawa.

"Hallo Jada mbona kimya..hallo" Andrea alisikika upande wa pili akiongea lakini Jada alikuwa anatazama kupitia kioo cha mlango wake ili kujiridhisha na kile alichohisi, wala hakutaka kugeuka nyuma.

"Andrea" Jada aliita huku akifungua mlango na kuingia ndani taratibu.
"Eee nakusikia mbona kimya, nauliza utawahi kweli kumleta shahidi"
"Nakuahidi nitafanya kila ninaloliweza kuhakikisha namleta Annah mahakamani japo mambo sio rahisi huku"
"Kwa nini?"
"Nafuatiliwa" alijibu Jada
"What! na nani tena"
"Hawa watu wamejipanga sana bwana Andrea lakini nakuahidi nitapambana kwa nguvu zote kuhakikisha Annah anafika hapo kwa wakati na kutoa ushahidi, kwa heri" Jada alisema kisha akakata simu, alivuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu kisha akamtazama Annah ambaye naye alimtazama huku akionyesha mwenye wasiwasi mwingi.
"Jiandae tunaondoka" Alisema Jada, wakati huo nje ya nyumba yake Malaika weusi Erica na Elina walikuwa wakilandalanda.

Je, nini kitafuata?
ITAENDELEA....

Simulizi ni shillingi 1,000/= lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina saul au Airtel money namba 0788967317 jina saul kisha njoo WhatsApp inbox namba hizo hizo
 
fanya kama Roma shusha vipande vingi hta kama ni Kwa kutusotesha wiki nzima.
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.............42
Mtunzi: Saul David
Email: saulstewarty@gmail.com
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Jada alivuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu kisha akamtazama Annah ambaye naye alimtazama huku akionyesha mwenye wasiwasi mwingi.
"Jiandae tunaondoka" Alisema Jada, wakati huo nje ya nyumba yake Malaika weusi Erica na Elina walikuwa wakilandalanda.

Je, nini kitafuata?

SASA ENDELEA....
"Inspekta Aron yuko wapi?" Annah aliuliza huku akimtazama Inspekta Jada aliyeonekana kuwa mwenye wasiwasi kiasi alisogea dirishani akafunua pazia kidogo sana akawa anatazama nje kuwaaangalia wale watu ambao aliamini wapo pale kwa sababu maalum.

"Mbona hunijibu?" Annah aliuliza kwa mara nyingine
"Kuna shida imetokea Annah, Inspekta Aron hayuko sawa kaniagiza nije nikuchukue twende mahakamani haraka kwa sababu muda ndio huu" Jada alieleza kwa ufupi, hakutaka kuweka wazi kila kitu kwa Annah, alijua ni namna gani atamchanganya kama atamwambia habari za kukamatwa kwa Inspekta Aron
"Hayuko sawa kivipi? Kuna tatizo limetokea?"
"Jiandae kwanza nitakuambia"
"Mimi niko tayari sina cha kujiandaa"
"Haya basi nifuate" Alisema Jada, akaongoza njia huku Annah akimfuata nyuma taratibu. Jada alitembea akifuata korido moja ndefu ya nyumba yake, akakata kona kulia na kufungua mlango mmoja wa chuma, akageuka nyuma kumtazama Annah
"Annah kwa sasa ni ngumu kukueleza kila kitu, jambo la msingi ni kuhakikisha nakufikisha mahakamani salama na kwa haraka, hadi dakika hii ninayoongea na wewe mazingira ni magumu sana kutoka hapa kwenda mahakamani"
"Kuna ugumu gani?"
"Kuna watu wanatufuatilia Annah, lakini usijali nitakufikisha salama"
"Eeh! Mungu wangu, kwa nini sasa usiite polisi wengine waje kutusaidia kutupa ulinzi watusindikize hadi mahakamani?"
"Ningefanya hivyo Annah lakini tumechelewa sana hadi wafike hapa kisha tuanze kurudi muda utakuwa umekwenda sana hivi tunavyoongea bila shaka tayari kesi imeishaanza kusikilizwa kule mahakamani"
Alisema Jada huku akifungua malango mwingine ambao ni mlango wa nyuma wa nyuma yake wakatoka upande wa pili.

"Nisubiri hapa kwanza" alisema Jada, akanyata hadi kwenye wigo wa seng'enge uliokuwa umefungwa kuzunguuka nyumba yake.
Alitazama huku na huku kuhakikisha usalama hapo akaona mtu mwingine tena tofauti na yule aliyepo upande wa mbele akizunguuka zunguuka na pikipiki yake.

"Ooh! Shit!! Wapuuzi" Alisema Jada huku akiwa anarudi alikotoka, alipomfikia Annah akamshika mkono wakaanza kurudi ndani.
"Vipi mbona tunarudi tena?" Aliuliza Annah akiwa haelewi kinachoendelea.
Jada hakujibu chochote badala yake akachukua simu yake na kumpigia mwanasheria Andrea kwa mara nyingine. Akapiga mara ya kwanza simu ikaita bila kupokelewa mara ya pili napo hali ilikuwa ni ile ile.

Inspekta Jada alizidi kuumiza kichwa nini afanye ili kuhakikisha anamfikisha Annah mahakamani haraka iwezekanavyo.
Erica na Elina waliendelea kuzunguuka zunguuka na kuzuga nje ya nyumba ya Inspekta Jada wakati huo walikuwa wakiwasiliana na Asia kwa ukaribu ambaye sasa alikuwa mahakamani, aliacha kumfuatilia Inspekta Aron baada ya kuhakikisha amefikishwa kwenye mikono ya sheria mahali ambapo hawezi kufanya chochote. Kesi kubwa ya kumuua waziri wa afya Dokta Gondwe ilikuwa imemkalia kooni hakuwa na namna ya kujinasua kwenye tukio hilo la kutisha ambalo lilianza kushika vichwa vya habari karibu ulimwenguni kote.

"Annah" Inspekta Jada aliita baada ya kufikiri kwa zaidi ya dakika tatu
"Beeh"
"Unajua kuendesha pikipiki?"
"Ndiyo najua sana tuh"
"Wow basi sikia ..." Alisema Inspekta Jada huku akitabasamu, akasogea karibu na kuanza kumuelekeza Annah kitu cha kufanya.
[emoji294][emoji294][emoji294]
MAHAKAMA YA IPANGA MJINI...
Kesi nzito ya mauaji inayomuandama mtoto wa kigogo Osward ilianzaa kuunguruma ndani ya mahakama hiyo ikiwa ni kwa mara nyingine tena na huenda ndio ikawa ni mara ya mwisho kwani ilitangazwa kuwa siku hiyo ndio ingekuwa siku ya hukumu kwa kijana Osward ambaye aliua kwa kukusuida lakini watu wake wanaomzunguua wanajipanga kuhakikisha Osward hafungwi. Tayari wamefanikiwa kufuta na kuua mashahidi wote ambao wangeweza kumfanya Osward aonekane mwenye hatia, hata askari ambaye alikuwa akipigana kwa udi na uvumba yaani Inspekta Aron tayari wameshamdhibiti kwa kumpakazia kesi kubwa ya mauaji ya mtu mkubwa serikalini yaani Dokta Gondwe.
Tumaini la Osward ambaye ndiye muuaji pia wa Dokta Gondwe linazidi kuwa kubwa baada ya kuona kuna kila dalili ya kushinda kesi yake, kitu ambacho yeye na timu yake hawakujua ni kwamba Annah shahidi wa mwisho na wa pekee aliyesalia bado alikuwa hai, hakuwa amekufa kama walivyodhani. Lakini licha ya hayo yote bado kulikuwa na kazi nzito ya Annah kufika mahakamani hapo kwani Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa alikuwa ameweka mipango yake vizuri kuhakikisha hakuna mwanya wowote wa kuendelea kuifanya kesi ya Osward kuwa ngumu. Hivi ndivyo alivyomuahidi kijana huyo kama tu atafanikiwa kumuua Dokta Gondwe.

"Mheshimiwa hakimu, imekuwa ni mazoea sasa kila tukija hapa tunaambiwa kuna mashahidi lakini tangu kesi imeanza hakuna hata shahidi mmoja aliwahi kuja na kusimama mbele yetu akathibitisha kuwa mteja wangu anayo hatia. Hamuoni kuwa mnaendelea kumuweka kwenye mazingira magumu mteja wangu kwa muda mrefu pasipo kuwa na hatia yoyote" Aliongea wakili machachali na maarufu nchini bwana Silinde kagame ambaye ndiye alikuwa upande wa utetezi kwa mtuhumiwa Osward.

"Mheshimiwa hakimu mbele ya mahakama yako tukufu tumekuwa tukileta vielelezo mbali mbali vinavyo ashiria mauaji ya mashahidi wetu, kila shahidi anayetegemewa kuletwa hapa wamekuwa wakiuawa kikatili kabla ya siku husika kufika mheshimiwa hakimu mpaka sasa tumepoteza mashahidi tisa, saba kati yao wameuawa kikatili na wawili wamepotea hawajulikani walipo. Je hamuoni kuwa kuna njama za makusudi zimekuwa zikifanyika kwa kuwaua mashahidi wetu ili tu mtuhumiwa kuonekana hana hatia!? Mheshimiwa hakimu naomba mahakama hii tukufu ilifikilie jambo hili kwa kina" Aliongea Andrea wakili upande wa mashtaka.

"Mheshimiwa hakimu sikubaliani kabisa na maneno ya uongo na visingizio kutoka upande wa mashtaka, ninachoweza kusema hakuna mtu anayejua kama watu hao waliouawa na kupotea kama kweli ni mshahidi au wanachochote wanachoweza kusema kuonyesha mteja wangu anayo hatia. Hizi zinaweza kuwa ni njama tu za kuchelewesha maamuzi ya mwisho ya mahakama yako tukufu mheshimiwa hakimu, jukumu la kumlinda shahidi ni lao wenyewe na sio la mahakama naomba kuwasilisha..."

Mambo yalizidi kuwa ni mengi na mazito ndani ya mahakama ya Ipanga mjini. Wakati huo Asia alikuwa miongoni mwa watu aliohudhuria mahakamani hapo akifuatilia kwa ukaribu kila kinachoendelea. Mara kadhaa alikuwa akitoka na kuwasiliana na wenzake Malaika weusi pamoja na mheshimiwa Profesa Cosmas Kulolwa Rais mstaafu kumjulisha kila kinachoendelea.

"Nikirejea maelezo yako ya tarehe 17 Mei mwaka huu uliahidi kuwa leo ungemleta shahidi mwingine kwetu tafadhali tunaomba shahidi huyo asogee mbele tayari kuhojiwa na mahakama pamoja na mawakili wote wawili" Alisema muendesha mashtaka

Kimya kilitawala kila mtu akageuka na kumtazama wakili bwana Andrea ambaye naye alitulia kwa sekunde kadhaa huku moyo wake ukitamani Inspekta Jada na Annah wajitokeze lakini haikuwa hivyo.

"Ni kweli mheshimiwa hakimu nilisema hivyo. Lakini kama linivyokwisha kusema hapo awali kuwa mashahidi wetu wamekuwa wakiwindwa na pengine hata kuuawa kwa kulizingatia hilo shahidi huyu wa mwisho na wa pekee tulimchukulia umakini wa kutosha jambo linalopelekea achelewe kufikishwa mbele ya mahakama hii, Niombe mheshimiwa hakimu mtupe mda na kuendelea kuvuta subra angalau kwa dakika chache shahidi wangu atafika" alieleza Andrea.

Hapo kukawa na ukimya tena na baada ya dakika kadhaa hakimu alitoa muda wa dakika 25 za mapumziko na kama shahidi atakuwa hajafika ndani ya muda huo basi mahakama itatoa hukumu kwa kuzingatia ushahidi uliokwisha tolewa kwa pande zote mbili.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Inspekta Jada alionekana akitoka ndani ya nyumba yake mkononi akiwa amebeba boksi moja kubwa sana, alitembea na kwenda kulipakia nyuma ya gari ya yake. Baada ya hapo Jada aliingia ndani ya gari na kukaa upande wa dereva akaliwasha na kuanza kutoka taratibu. Wakati huo Erica na Elina walikuwa wakishuhudia kila kitu kutokea mbali.

"Anafanya nini huyu Inspekta?" Aliuliza Erica
"Sijui ni kama anataka kuondoka"
"Lile boksi litakuwa na nini?"
"Sijui tuendelee kumfuatilia au tuachane naye mbona hata haelekei mjini anaenda upande mwingine"
"Hebu tumuache kwanza turudi mahakamani kule"
"Lakini vipi....ooh! Asia anapiga simu"
"Enhe! Pokea pengine tayari Osward kashinda kesi"
Alisema Erica, Elina akapokea simu na kuweka sauti ya juu 'loudspeaker'..
"Mko wapi?" Aliuliza Asia kutoka upande wa pili wa simu ile.
"Tuko hapa nyumbani kwa Inspekta Jada, vipi huko mambo yanaendaje?" Elina alijibu na kuuliza.
"Aloo! Mambo si shwari inaonekana kuna shahidi wanategemea atafika hapa sio mda, mahakama imetoa dakika 25 za kumsubiri tafadhali hakikisheni mnafuatilia kwa ukaribu sana Inspekta Jada nahisi anaweza kuwa pamoja na huyo shahidi ngoja niwasiliane pia na mheshimiwa nijue tunafanyaje" Alieleza Asia na kukata simu, kauli hii iliwafanya Erica na Elina watazamane.
"Boksi.." Erica na Elina walisema kwa pamoja ikionyesha wazi walichokiwaza mapacha hawa kilikuwa kinafanana wote wakalitilia mashaka lile boksi kubwa ambalo Inspekta Jada alilipakia kwenye gari yake wakati ule. Haraka bila kupoteza muda waliwasha pikipiki zao na kuondoka kwa kasi kumfuatilia Inspekta Jada.
Wakati huo huo Tino na Bosco kijana wake walifika na kusimamisha gari lao nje kidogo na nyumba ya Inspekta Jada. Walipishana kidogo sana na Malaika weusi ambao wakiondoka sekunde chache zilizopita.

"Mbona pako kimya kuna watu kweli hapa" Aliuliza Tino huku akishusha kioo cha gari yake
"Nashangaa, hata hao wanawake mnaosema sijui Malaika weusi wako wapi?" Alijibu Bosco lakini wakiwa kwenye maongezi hayo mara kwa mbali waliona mlango wa nyumba ya Inspekta Jada ukifunguliwa taratibu.

Je ni nini kinaendelea?

Dakika 25 zilizosalia zitaamua Osward kufungwa au kuachwa huru...
Vipi kuhusu Inspekta Aron?
Ni hatua ipi itafuata kwa Sultana na jasusi Shadow?

ITAENDELEA...
Simulizi ni shillingi 1,000/= lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina saul au Airtel money namba 0788967317 jina saul kisha njoo WhatsApp inbox namba hizo hizo...
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..............43
Mtunzi: Saul David
Email: saulstewarty@gmail.com
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Mbona pako kimya kuna watu kweli hapa" Aliuliza Tino huku akishusha kioo cha gari yake
"Nashangaa, hata hao wanawake mnaosema sijui Malaika weusi wako wapi?" Alijibu Bosco lakini wakiwa kwenye maongezi hayo mara kwa mbali waliona mlango wa nyumba ya Inspekta Jada ukifunguliwa taratibu

SASA ENDELEA....
Kukawa kimya ghafula huku Tino na Bosco wote wakiwa wameelekeza macho kuelekea mlangoni.

Kwa mbali Annah alionekana akitoka ndani ya nyumba ya Inspekta Jada taratibu akiwa na helmet na ufunguo wa pikipiki mkononi. Aliangaza macho huku na huku kuangalia usalama akaona hakuna mtu akatoka na kuingia ndani ya kibanda kilichokuwa nje ya nyumba hiyo. Baada ya mda alitoka akisukuma pikipiki... Ilikuwa hivi....
DAKIKA 5 ZILIZOPITA....
"Unajua kuendesha pikipiki?" Hili ndio swali Inspekta Jada alimuuliza Annah wakati ule kabla hajaondoka
"Ndiyo najua sana tuh"
"Wow basi sikia ..." Alisema Inspekta Jada huku akitabasamu, akasogea karibu na kuanza kumuelekeza Annah kitu cha kufanya, akasema...

"Kuna watu wanalandalanda hapo nje wako wawili tu kama sikosei. Bila shaka wapo hapa kutuzuia ili tusifike mahakamani. Sasa itabidi niwapoteze ili wewe uende mahakamani haraka kabla hatujachelewa. Tuna dakika 22 tu zimesalia mpaka sasa Annah. Mimi natoka na gari yangu nina uhakika hawa watu watanifuata nyuma ukiona hivyo toka haraka chukua pikipiki iko ndani ya kibanda kidogo hapo nje uondoke" Jada alieleza mpango wake haraka haraka na bila kupoteza muda aliingia chumbani akatoka akiwa na helmet, funguo ya pikipiki, simu ndogo ya batani pamoja na boksi moja kubwaa.

"Chukua hii simu kuna namba yangu nimesave 'My voda' tutawasiliana au utanipigia ukiwa na shida yoyote. hatuna mda wa kupoteza Annah najua umenielewa"
Alisema Inspekta Jada na bila kupoteza muda alinyanyua lile boksi na kutoka nalo nje, Annah naye alisogea dirishani, Alimuona Inspekta Jada wakati akiondoka na gari yake na baada ya muda akawaona wale watu wenye pikipiki (Malaika weusi) wakiondoka tena kwa kasi sana. Bila kupoteza muda Annah naye alitoka na kufanya kama alivyoelekezwa na inspekta Jada....
[emoji294][emoji294][emoji294]
Tino na Bosco waliendelea kumtazama Annah wakati akihangaika kuwasha pikipiki iliyokuwa ikisumbua kuwaka baada ya kukaa muda mrefu bila kutumika.

"Aiseeh! Huyu binti mbona ni Annah!!" Tino aliongea kwa mshangao
"Annah! Annah gani? Yule shahidi wa Inspekta Aron?" Aliuliza Bosco
"Yes! Alikufa, niliambiwa amekufa, Godwin alimuua" Tino aliongea kwa kujiamini akiwa haamini macho yake.
"Sasa inakuwaje yupo hai, au hujaona vizuri ni yeye kweli!?"
"Ni yeye mwenyewe nina uhakika, huyu ni mchawi au roho ya paka nilimpiga risasi mara ya kwanza akapona mara ya pili Sniper G'....aah! Haiwezekani mbona Aron alisema amekufa, lakini.... No" Tino alikuwa akiwaza pasipo kupata majibu yaani kifupi mbili haikai tatu haikai.

Wakati huo Annah alifanikiwa kuwasha pikipiki akavaa helmet kisha akatoka kwa mwendo wa taratibu akatoka nje na kuelekea magharibi tofauti na kule alikoelekea Inspekta Jada wakati ule. Annah alipita pembeni ya gari ya Tino kwa kasi

"Kwa hiyo mkuu nini kinafuata?" Aliuliza Bosco
"Unajua Bosco sijui nipo kwenye Dunia gani mimi. Kila kinachoendelea nakuwa sielewi kabisa, ona mdogo wangu Aron kamuua Dokta Gondwe mbele ya waandishi wa habari, ila nina uhakika Aron hawezi kufanya hivyo kwa akili zake mwenyewe. Annah niliyeamini kuwa amekufa leo namuona huyu hapa tena mzima wa afya kabisaa. Alafu bado kuna hili suala la hawa malaika weusi sijui wametumwa na nani kama Dokta Gondwe amekufa, ki ukweli nachanganyikiwa sana" Tino alikuwa alilalamika punde aligeuza gari yake na kuanza kufuata barabara kule alikoelekea Annah.

"Wapi sasa mkuu!?" Aliuliza Bosco
"Vipi hukusu Malaika weusi?"
"Sasa tutamfuatilia nani tumuache nani?" Tino aliuliza kwa sauti ya akali, ilibidi Bosco awe mpole.
"...najua ninachokifanya mdogo wangu kuwa mpole tu" Alisema Tino huku akikanyaga mafuta kuongeza mwendo wa gari yake, dakika chache baadae walimuona Annah akiwa katika ya barabara akihangaika kunyoosha usukani wa pikipiki yake, hakuwa mzoefu sana kuendesha pikipiki tena kwenye barabara kubwa kama ile.

"Nafanya hayo yote kwa ajili yako Aron wangu, japo sielewi uko wapi kwa sasa" aliwaza Annah na hapo ndipo alipoliona gari likija nyuma yake likampita kwa kasi na funguna breki kali mbele yake likiwa limesimama katika ya barabara
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Inspekta Jada alikuwa ameshikilia usukani wa gari yake vizuri alizidi kwenda kwa kasi mara tu baada ya kugundua kuwa nyuma yake alikuwa akifuatiliwa na wale watu waliokuwa wakilandalanda nyumbani kwake wakati ule.

"Erica hivi unaelewa kweli tunachokifanya" Aliuliza Elina kupitia vifaa maalumu vya mwasiliano walivyokuwa wamevivaa sikioni wote wawili, wakati huo walizidi kuendesha pikipiki zao kwa kasi kuhakikisha Inspekta Jada hawaachi
"Kwa nini?"
"Hivi huku tunakoenda ni wapi, kwa nini tunaendelea kumfuatilia huyu mtu na wala haelekei mahakamani?"
"Huoni kasi yake vipi kama ndio anaenda kumchukua huyu shahidi?"
"Muda utakuwa umekwisha lakini, hataweza kwenda na kurudi ndani ya hizo dakika 15 zilizobaki"
"Kwa nini tusipige risasi taili za gari lake apate ajali aanguke basi kazi iwe imeisha kuliko kukimbizana kama hivi"
"Hapana hilo halipo kwenye mpango wa mheshimiwa, muhimu ni kuhakikisha Osward anashinda kesi yake bila kutokea kizuizi chochote"
"Nina wasiwasi Erica, vipi kama akawa ametuchezea akili tumemfuata huku kumbe shahidi tumemuacha nyumbani kwake!?"
"Mmh hilo nalo neno"

Erica na Elina waliendelea kujadilia wakati huo walishavuka kijiji kimoja na sasa walikuwa wanaingia kijiji cha pili.

Inspekta Jada alishika usukani kwa mkono mmoja mkono mwingine akachukua simu yake na kupiga mahali, simu iliita na mwisho ikapokelewa.

"Tunakaribia afande kaeni tayari" Alieleza kwa ufupi huku akiangalia kwenye site mirror' akawaona Erica na Elina wanazidi kuja kwa kasi.

"Tumezaliwa kupambana na magaidi wa kimataifa kama ninyi" Alijisemea Inspekta Jada huku akizidi kukanyaga mafuta gari ikaendelea kwenda kasi ikipandisha muinuko fulani mdogo hadi alipoanza kutelemka upande wa pili wa muinuko huo. Ghafula mbele na pembeni ya gari la Inspekta Jada yalionekana magari zaidi ya saba ya polisi. Mawili yalikuwa yamesimama upande wa kushoto na kulia wa barabara na moja lilifika na kusimama katikati ya barabara mara tu baada ya Inspekta Jada na gari yake kupita.

Erica na Elina walikuwa bado upande wa nyuma wa muinuko ule walipojitokeza tu upande wa pili walishtushwa na uwepo wa gari nyingi za polisi, lilikuwa ni tukio ambalo hawakuwa wamelitegemea kabisa.
Walifunga breki ghafula na kugeuza pikipiki zao kitaalamu sana lakini tayari walishachelewa yale magari ya polisi pembeni ya barabara yalisogea na kufungua barabara upande wa pili kule walikotokea.
Sasa mapacha hawa Erica na Elina walijikuta wamewekwa kati, mbele gari mbili za polisi nyuma gari tatu za polisi na pembeni yaani kushoto na kulia kulikuwa na gari moja moja.
Polisi zaidi ya 15 walikuwa nje ya gari zao huku wakiwa wamenyoosha siraha zao mbele.
Wakati huo Inspekta Jada alikuwa ameshuka kwenye gari akawa anarudi eneo la tukio huku akijaribu kupiga namba ya simu ndogo aliyompa Annah lakini ikawa haipokelewi.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili simu ilikuwa ikiita kwenye mfuko wa suruali ya Annah lakini hakuwa na uwezo wa kuipokea wakati huo. Alikuwa kwenye pikipiki amesimama huku mguu wake mmoja ukiwa chini uso kwa uso alikuwa akitazamana na Tino ambaye alishuka kwenye gari mara tu baada ya kumtenga Annah kwa mbele.
Sasa Annah anamtia machoni kwa mara nyingine mtu aliyewauwa wazazi wake wote wawili na kisha kumpiga risasi kifuani.
"Ilikuwaje haukufa Annah!?" Tino aliuliza kwa sauti ikiyojaa dharau akachukua sigara na kiberiti cha gesi akawasha kisha akaanza kuvuta. Annah alibaki kimya huku akimtazama kwa macho makali yaliyojaa chuki kubwa aliyokuwanayo dhidi ya mtu huyu.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili mahakamani dakika zilizosalia zilikuwa ni za kuhesabika tu. Mwanasheria Andrea aliikosa amani kabisa kila wakati alikuwa akitazama saa yake ya mkononi kuangalia muda ambao mpaka sasa zilikuwa zimesalia dakika 9 pekee kati ya zile dakika 25 walizopewa.

"Wako wapi hawa mbona hawafiki!?" Andrea alijiuliza huku macho yake yakiwa kwenye geti kuu la kuingia maeneo ya mahakama hiyo. Wakati huo huo macho ya Asia binti kutoka kikosi cha wanawake watatu hatari maarufu kama Kunguru weusi hayakuacha kumfuatilia.

Je, nini kitaendelea?
Erica na Elina wataweza kutoka kwenye mikono ya polisi?
Annah vs Tino nini kitatokea?
Sasa zimebaki dakika 9 tu za kumsubiri Annah mahakamani, atawahi?
Aron Najma wako wapi nini kinaendelea kwao?
ITAENDELEA...

Simulizi ni shillingi 1,000/= lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina saul au Airtel money namba 0788967317 jina saul kisha njoo WhatsApp inbox namba hizo hizo
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya……….44
Mtunzi:saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
“Wako wapi hawa mbona hawafiki?” Andrea alijuliza huku macho yake yakiwa kwenye geti kuu la kuingia maeneo ya mahakama hiyo. Wakati huo huo macho ya Asia binti kutoka kikosi cha wanawake watatu hatari maarufu kama kunguru weusi hayakuacha kumfuatilia.

Je, nini kitafuata?

SASA ENDELEA….
***
Upande wa pili mambo yanakuwa ni magumu sana kwa mapacha Erica na Elina ambao wanajikuta wanaingia kwenye mtego wa polisi uliosukwa na Inspekta Jada mahususi kwa ajili ya kuwakamata.

“Erica hivi ni kweli tunakubali kukamatwa kizembe namna hii?” Aliuliza Elina, wakati huo walikuwa wamezunguukwa na polisi kila upande kushoto kulia mbele na nyuma polisi ambao kila mmoja alikuwa na siraha ya moto mkononi mwake.
“Hakuna namna Elina hawa jamaa wamejipanga sana, tumeshachelewa tukileta ujuaji mwingi hapa watatuua” alijibu Erica na mara wakati huo huo wakasikia sauti ya askari mmoja akiongea kupitia kipaza sauti akiwa nyuma ya gari moja la polisi.

“Toeni siraha zote mlizonazo wekeni chini kisha muweke mikono yenu kichwani na kupiga hatua tatu nyuma”
Baada ya maelezo hayo Elina na Erica walitazamana kisha wakapeana ishara kuwa watii kile walichoambiwa, wakafanya hivyo.

Wakati hayo yakiendelea Inspekta Jada yeye alikuwa bize akijaribu kupiga simu yake aliyompatia Annah lakini simu iliendelea kuita bila kupokelewa. Na mwisho kabisa simu ya Inspekta Jada ilizima baada ya kuisha chaji

“Nini kimempata Annah! au tayari atakuwa amefika mahakamani? Sasa mbona hajaniambia lolote na tulikubaliana akifika tu aniambie” Inspekta Jada alikuwa akijiulza maswali huku hofu yake ikionekana wazi wazi usoni kwake. Hakuwa na uwezo wa kuendelea kuvumilia tena alitamani zoezi la kuwakamata Erica na Elina liende haraka lakini haikuwa hivyo ilikuwa ni lazima wafanye mambo taratibu bila makosa wakiamini Elina na Erica hawakuwa majambazi wa kuwachukulia poa.
***
Upande wa pili barabarani, Annah alikuwa amesimama na pikipiki yake huku mguu mmoja ukiwa chini wakati huo mbele yake alikuwa amezuiwa kupita mara baada ya Tino kumzuia kwa mbele na gari yake.
Tino alikuwa ameshuka kutoka kwenye gari akasimama mbele ya Annah huku akivuta sigara yake taratibu.
“Hivi ilikuwaje haukufa wewe binti, hii ni mara ya pili sasa mara ya kwanza nilikupiga risasi ya kifua mimi mwenyewe inaonekana una roho ya paka” Tino aliongea kwa dharau.
Annah hakusema kitu, alibaki kimya huku akimtazama Tino kwa macho yaliyojaa chuki na hasira kali. Aliikumbuka ile siku mtu huyo alipowaua wazazi wake wote wawili kwa kuwapiga risasi, moyo wake ulimuuma sana lakini akajaribu kujikaza na kutulia kimya. Ukweli ni kwamba hakuwa na cha kufanya wala asingeweza kupambana na mtu huyo ambae aliamini hata pale alipo anayo siraha ya moto.

“Wakati wako utafika, nitakusambaratisha wewe mwanaharamu” aliwaza Annah
“Mbona uko kimya? Hutaki kusema chochote kwa muuaji wa baba yako, usijali leo siwezi kujaribu tena kukua ila utatoka hapa ukiwa salama kama tu utanijibu swali langu kw usahihi” Aliongea Tino wakati huo kijana wake Bosco nae alishuka kwenye gari akaja na kusimama pembeni yake.
“Unataka nini?” Hatimae Annah alifungua kinywa na kuuliza swali
“Nataka kujua sasa hivi unaelekea wapi na ni mpango gani unaendelea kati yako wewe Inspekta Jada na Inspekta Aron ukinijibu hili swali nakuhakikishia wala sito kuumiza” Tino aliongea kwa msisitizo.
“Mbona hao watu siwafahamu” Alijibu Annah kauli iliyomfanya Tino atoe tabasamu lenye dharau kisha akakunja sura yake tena.
“unaleta masihara Annah, ni wazi kuwa ulishajikatia tamaa ya kuishi mara baada ya kuwapoteza wazazi wako” Alisema Tino lakini kabla hajafanya lolote mara Bosco alimshika begani na kuongea haraka haraka.
“Oya bosi hebu toa gari barabarani haraka msara bosi msara”
“Kuna nini?” Aliuliza Tino huku akipeleka macho yake na kutazama kule alikokuwa akitazama kijana wake Bosco akashuhudia msafara wa gari mbili za jeshi ukija taratibu.
Bila hata kusema neno Tino aliingia haraka kwenye gari yake akaliwasha kisha akaendesha na kulisogeza pembeni ya barabara, huo ulikuwa ni wasaa mzuri na nafasi ya pekee kwa Annah ambae nae baada ya kuona msafara wa gari zile za jeshi aliwasha pikipiki yake na kuondoka hata kabla hawajafika. Tino na Bosco wakabaki wanamsindikiza kwa macho huku wakisonya hawakuwa na la kufanya. Baada ya muda kidogo yale magari ya jeshi yalipita taratibu na kuendelea na safari yake.

“Tunafanyaje bosi?” Aliuliza Bosco
“Huyu binti anaelekea mahakamani, naona mipango ya dogo Aron inaendelea licha ya kwamba yeye amekamatwa na polisi”
“Kwa hiyo tumfuate tukamzuie au?”
“Mmh! Hapana acha wapambane na hali zao, Dokta Gongwe ameshakufa kwa nini niendelee kuhangaika na Annah, jambo la msingi kwa sasa ni kujua ni namna gani naweza kuvipata vimelea vya V-COBOS naona kuna mchezo unaendelea hapa, acha tucheze mchezo ndani ya mchezo” Tino aliongea hali akiwa ametuliza akili yake kujaribu kufikili kwa kina ni nini cha kufanya .
***
MAHAKAMANI…
Baada ya kusubiri kwa muda mrefu hatimae zile dakika 25 zilizotolewa kwa ajili ya kumsubiri shahidi ziliisha na Annah alikuwa bado hajawasili mahakamani hapo. Wakili Andrea hakuwa na la kufanya zaidi badala yake aliruhusu taratibu nyingine za mahakama ziendelee.

“Kutokana na upande wa mashataka kushindwa kuwasilisha ushahidi wa kutosha kuthibitisha kuwa bwana Osward matula anahusika na tukio la mauaji lililotokea tarehe kumi na mbili mwezi wa sita mwaka huu, natangaza kuwa kuanzia sasa mahakama inamuachi……..”
“SUBIRIIIIIIIII…..”
Wakati hakimu akitoa maelezo hayo mara kuna sauti kubwa ya mwanamke ilisikika kutoka mlango. Watu wote wakageuka nyuma na kutazama ni nani aliyemkatisha mheshimiwa hakimu wakati anazungumza. Mlangoni kulikuwa binti mmoja mrembo sana ambae alionekana amechoka baada ya kukimbia kwa muda mrefu, huyu hakuwa miwngine bali Annah.

“Mheshimiwa hakimu tafadhali kabla hujatoa hujasoma hukumu yako naomba tumpe nafasi shahidi wangu ndio huyu amefika hivi sasa” Aliaema wakili Andrea kauli iliyoibua minong’ono ya hapa na pale ndani ya mahakama ile.
Hali ilikuwa ni mbaya zaidi kwa Asia na Osward mwenyewe ambao waliamini mambo yalikuwa yameisha na sasa walikuwa wanakwenda kutangazwa kama washindi wa kesi hiyo lakini mambo yanabadilika ghafula pasipo kutegemea. Asia alijikuta anajilaumu na kujiona mzembe kwa nini hakushtuka mapema na kumzuia Annah kabla hajaingia kwenye geti kuu la mahakama hiyo, alikuwa amejihakikishia ushindi lakini ghafula mambo yanakwenda ndivyo sivyo. Hakujua ni nini atamueleza bosi wao Profesa Cosmas Kulolwa Rais mstaafu, wala hakujua ni wapi walipo wenzake kwa wakati huo yaani Elina na Erica.
“Ooh! Shit! Tumefanya nini?” Asia alijisemea mwenyewe huku akiinuka haraka akapiga hatua ndefu ndefu kutika nje ya mahakama hiyo huku akichukua simu yake akapiga namba ya Erica na kuiweka sikioni.
Akiwa nje alisubiri simu hiyo ipokelewe lakini haikupokelewa, akajaribu tena mara ya pili kabla hajapiga simu ya Elina lakini mambo yakawa ni yale yale. Mwisho Asia aliamua kumpigia bosi wao yaani Profesa Cosmas Kulolwa kumueleza kile kilichojili ili waangalie cha kufanya licha ya kwamba asilimia za kushinda zilikuwa ni ndogo sana.
***
Upande mwingine katika hospitali ya taifa Garamukinda watu wawili ambao waligeuka na kuwa maarufu ghafula nchini na nje ya nchi walifikishwa hospitalini hapo kwa ajili ya matibabu huku wakifuatiliwa na kundi la waandishi wa habari waliokuwa wakichukua picha na video kila wakati. Watu hawa walikuwa ni Inspekta Aron ambae ni mtuhumiwa namba moja kwa kesi kubwa iliyotikisa nchi kesi ya kumuua waziri wa afya mheshimiwa Dokta Gongwe. Mtu wa pili alikuwa ni Najma binti mpendwa wa marehemu Dokta Gongwe ambae alipoteza fahamu eneo la tukio mhali mauaji ya baba yake yalipotokea.

Je, nini kitafuata?
Osward atafungwa?
Sultana na jasusi Shadow wanafanya nini?
Hatua ipi atachukua Tino?
Ni nini hatima ya vimelea vya V-COBOS?

ITAENDELEA…..
 
Back
Top Bottom