SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 417
- 1,285
- Thread starter
- #81
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..............45
Mtunzi: Saul David
ILIPOISHIA....
Ikiwa ni katika hatua za mwisho kabisa za kimahakama kabla ya kesi ya Osward kuamuliwa ghafula katikati hali isiyotegemewa Annah ambae ni shahidi pekee aliekuewa akisubiriwa anafika mahakamani hapo.
Upande wa pili Inspekta Aron aliyepigwa risasi ya mguu pamoja na Najma aliyepoteza fahamu wanafikishwa hospitali kwa ajili ya kupata huduma za matibabu.
Je, ni nini kitafuata?
SASA ENDELEA....
"Unamaanisha huyu mwanamke ndio Annah shahidi uliyeomba tumsubiri hapo awali?" Muendesha mashataka aliuliza swali
"Ndiyo, ndio yeye mheshimiwa"wakili Andrea alijibu
Hakimu pamoja na viongozi wengine wa mahakama walionekana kunong'onezana jambo na mwisho wakafikia makubaliano ya pamoja.
"Sawa tutamsikiliza shahidi wako, naomba Annah sogea mbele utaapa kama ilivyo taratibu kisha utahojiwa na mawakili wote wawili" Alisema hakimu.
Annah alipiga hatua kusogea mbele ya mahakama ile, alipokutana na wakili Andrea akasimama
"Pole sana Annah bila shaka umepitia wakati mgumu sana mpaka kufika hapa, lakini tushukuru mungu umefika salama. Hatukupata muda wa kuongea ila najua hauwezi kushindwa kujieleza, ongea kila kitu ulichokiona na kusikia siku hiyo wakati Osward anafanya yale mauaji" Wakili Andrea aliongea haraka haraka kwa sauti ya chini. Annah alitikisa kichwa chake ikiwa ni ishara kuwa amemuelewa wakili. Baadae taratibu zote za kumuapisha zilikamilika na baadae Annah akapandishwa kizimbani upande wa pili tofauti na ule aliopo mshitakiwa Osward, sasa akawa tayari kwa kuhojiwa. Wakili Andrea ndio alikuwa mtu wa kwanza kumuliza maswali shahidi.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili katika nyumba moja kubwa ya kifahari iliyokuwa imejegwa chini ya mlima mdogo pembeni kidogo ya mji, ilikuwa ni nyumba inayomilikiwa na mtoto wa kwanza wa Rais mstaafu Elizabeth Kulolwa ambaye kwa sasa yuko masomoni nchini Marekani. Nyumba hiyo ilijengwa kwa umiliki wake lakini ukweli ni kwamba ilikuwa ni nyumba ambayo inatumiwa sana na baba yake mzazi yaani Profesa Cosmas Kulolwa. Hapa ndipo alikuwa akipanga na kuendesha mipango yake mingi ya siri hata kipindi akiwa madarakani kama Rais.
Leo hii kwa mara nyingine katika nyumba hii yenye ghorofa sita kwenda juu, Profesa Cosmas anapokea ugeni mkubwa kutoka nchini Mexico ugeni ambao ulikuwa ni muhimu sana kwake.
Miongoni mwa wageni hao waliokuwepo wanaume watatu wa miraba minne waliojazia sana na wote walikuwa wamenyoa vipara mmoja kati yao alikuwa mzungu na wawili waafrika. Wageni wengine walikuwa ni wazungu watatu ambao wote walitoka nchini Mexico alikuwepo profesa Fernando Arturo mkurugenzi mtendaji wa maabara ya ZMLST inayomiliki kirusi cha V-COBOS, alikuwepo Dokta Codrado pamoja na mwanamke mmoja mwenye asili ya kihindi aliitwa Sharma Khumal.
Wote kwa pamoja wakiwa na wenyeji wao ambao ni Profesa Cosmas Kulolwa pamoja na Mkemia mkuu wa serikali Andiwelo katabi walikaa na kuizunguuka meza moja ya duara kisha wakawa wanafanya mazungumzo nyeti sana kwa lugha ya kingereza.
"Tumesubiri vya kutosha na katika kusubiri kwetu tumeona kuna mambo yameanza kuharibika na kama tutaendelea kusubiri zaidi basi tunaweza kujikuta tunapoteza kila kitu" Profesa Fernando alianzisha mazungumzo akatulia kwa muda kisha akaendelea.
"Mpango wetu ni ule ule kurudisha heshima ya maabara yetu ya ZMLST kama ilivyokuwa mwanzo na pili ni kutengeneza mabilioni ya pesa. Hivyo vyote vitaenda kwa pamoja na siraha yetu kubwa ni virusi vya V-COBOS. Ilikuwa tufanye hivyo miaka kadhaa iliyopita lakini virusi vya COVID-19 vilikuja na kutuvurugia ratiba hivyo tukasubiri. Korona imepungua kwa sasa ni wakati wetu wa kuitikisa Dunia tutapeleka mambo haraka haraka ikiwa ni pamoja na kuipata chupa ya kijivu ikiyopotea ndio maana tumekuja na kikosi kazi na hawa wanaume wa shoka hapa ni sehemu tu ya kikosi kazi chetu. Tukilazimika kuua tutaua tukilazimika kuchinja tutachinja ilimradi tu jambo letu lifanikiwe. Tunashukuru profesa Cosmas kwa kumuondoa Dunia Dokta Gondwe kwa sababu tayari alishakuwa kikwanzo kwetu tangu mda mrefu, huu ni mfano unaoonyesha ni jinsi gani hili suala halihitaji masihara hata kidogo. Kama akitokea mwingine akazingua ikiwa ni pamoja na kuleta usaliti basi sitosita kuondoa uhai wake mara moja. Kwa sasa naomba Profesa Cosmas utupe maelezo mafupi ni wapi vilipo vimelea vyetu na ni wapi ilipo chupa ya kijivu alafu baada ya hapo tutajua tuanze na nini" aliongea profesa Fernando hapo Rais mstaafu Profesa Cosmas alikohoa kidogo tayari kuzungumza lakini kabla ya kufanya hivyo mara simu yake katika mfuko wa shati iliita kwa kutoa mtikisiko. Profesa Cosmas aliichukua na kutazama namba ya mpigaji shika akainua macho na kuwatazama wenzake.
"Worry out if its important call just pick up"(usiogope kama ni simu ya muhimu pokea) aliongea Sharma Khumal kwa kingereza chenye rafuzi ya kihindi.
Baada ya kusema hivyo Profesa Cosmas alipokea simu ile kutoka kwa Asia mmoja kati ya kikosi hatari cha kunguru weusi.
"Nipe ripoti" aliongea Pro. Cosmas mara tu baada ya kupokea ile simu
"Mheshimiwa mambo yameharibika" Asia aliongea upande wa pili akiwa nje ya mahakama.
"Kivipi?"
"Yule binti, Annah amekuja hapa mahakamani, dakika za mwisho kabisa mkuu"
"Imekuwaje? Kivipi? Wenzio wako wapi?"
"Sijui, naomba uniambie nini cha kufanya la sivyo kila kitu kitaenda hovyo mheshimiwa, tuna dakika chache tu"
"Sawa subiri nákupigia"
Alisema profesa Cosmas kisha akakataka simu, sura yake ikiwa na wasiwasi kiasi na kila mmoja kwenye kikao kile aligundua hilo.
"Kuna nini?" Aliuliza Dokta Codrado
"Kuna kijana wangu mmoja yuko hatarini kufungwa, nilikuwa kwenye harakati za kumsaidia lakini kwa bahati mbaya mambo yameenda tofauti dakika za mwisho"
"Ni mmoja wetu?" aliuliza Profesa Fernando
"Ndio alikuwa chini ya Dokta Gondwe lakini nataka kumfanya awe chini yangu kwa sababu anajua siri yetu pia yuko vizuri kwa kazi"
"Okay, vipi unachochote cha kufanya kuzuia asifungwe kwa muda uliobaki au nikusaidie?"
Aliuliza Profesa Fernando Profesa Cosmas Kulolwa akawa kimya.
"Wewe ni Rais inakuaje suala dogo kama hili likushinde"
"Ni kweli lakini tatizo ni muda nahisi nimechelewa sana, dakika si nyingi hukumu ya huyu kijana itasomwa"
"Okay, nieleze kwa kina kisha tujue tunafanyaje eleza haraka haraka" Alisema Profesa Fernando.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati huo kesi ilianza kusikilizwa mahakamani kwa mara nyingine Annah akiwa kizimbani kama shahidi...
"Annah, ni vipi unamfahamu mtuhumiwa" aliuliza swali hili wakili Andrea
"Nilimuona siku ya birthday yangu, kwenye mgahawa wa Affati"
"Kwa maana hiyo unataka kusema wewe ni mmoja kati ya watu waliokuwepo siku ambayo kulitokea mauaji pale katika mgahawa wa Affati? Tafadhali unaweza kutueleza japo kwa undani kila ulichokiona siku hiyo?"
Andrea aliuliza swali jingine na hapo Annah alieleza kila kitu kuanzia mwanzo mpaka mwisho hakuacha kitu.
"Mheshimiwa hakimu sina swali jingine" wakili Andrea alimaliza huku akiwa na imani kabisa kuwa kwa maelezo aliyoyatoa Annah yalitosha kabisa kumuweka Osward hatiani na nilazima angefungwa
Baada ya hapo hakimu alimruhusu wakili upande wa utetezi kumuuliza shahidi maswali. Kwa ufupi wakili huyu hakuwa amejipanga kumuuliza Annah maswali ya kumbana kitendo cha Annah kuingia ghafula mahakamani hapo kilivuruga kila kitu. Ilibidi tu atumie uzoefu wa kawaida alionao kwani maelezo ya Annah yalikuwa yameshiba.
"Annah unajua kwamba ikibainika unasema uongo mbele ya mahakama kifungo chake ni zaidi ya miaka 15 jela?"
"Najua, yote ninayoyasema ni kweli tupu"
Annah alijibu kwa kujiamini wakati huo kuna askari aliingia ghafula mahakamani hapo akapiga hatua hadi ilipo meza ya hakimu, askari huyu alikuwa na kipande cha karatasi akafika na kumkabidhi hakimu kisha akaondoka. Hii ilikuwa ni kinyume kabisa na utaratibu lakini hakuna aliyehoji. Hakimu alipofungua lile karatasi kulikuwa na picha ndogo kama passport kisha akasoma maelezo yaliyokuwa kwenye karatasi. Ni Andrea pekee ndio aliyeuona mshtuko alioupata hakimu mara baada ya kusoma maelezo yale moja kwa moja akajua kuna kitu hakipo sawa. Wakati huo wakili alizidi kumuuliza maswali Annah ambaye naye aliyajibu kwa ufasaha sana bila kupepesa.
[emoji294][emoji294][emoji294]
NUSU SAA BAADAE..
Gari moja ilifunga breki kali nje ya mahakama ya Ilonga, Inspekta Jada akiwa ndio dereva alishuka upesi na kuanza kupiga hatua kuelekea jengo kuu la mahakama hiyo. Alipotazama mazingira aliona kuna kila dalili kuwa amechewa sana, watu walikuwa ni wachache mno na wengine ndio walikuwa wakimalizaka kuondoka.
Akiwa ameukaribia mlango wa kuingia ndani ya jengo la mahakama Inspekta Jada anakutana na mwanasheria ambaye alikuwa ni wakili wa kesi ile bwana Andrea. Uso wa Andrea uliojaa huzuni ulitosha kabisa kumfanya Inspekta Jada aelewe kuwa mambo sio mazuri.
"Annah alifika?" Hili ndio lilikuwa swali la kwanza kutoka kwa Inspekta Jada.
"Alifika" Andrea alijibu kifupi huku akionekana mtu mwenye kukata tamaa
"Sasa imekuwaje, kwa nini tumeshindwa Andrea?"
"Ni nguvu Inspekta, hatukuwa na nguvu ila haki yetu ilikuwepo wazi" alijibu Andrea
"Una maana gani?"
"Namaanisha kuna nguvu ya ziada imetumika kupindua haki yetu, hakimu alitishiwa katika dakika za mwisho kabisa kabla ya kusoma hukumu kuna kila dalili kuwa watu wazito na wakubwa wameingilia hii kesi" alieleza Andrea japo ilikuwa ni hisia zake tu lakini alichokiongea kilikuwa sahihi kabisa.
Kimya kilitawala huku wote wakionekana kuwa na masikitiko makubwa sana.
" Vipi kuhusu Inspekta Aron" aliuliza Andrea
"Amekamatwa yupo hospitali anatolewa risasi aliyopigwa mguuni"
"Mmh! hali ni mbaya Inspekta Jada"
" Tena sana, Annah yuko wapi sasa?"
"Si..sijui alikuwepo hapa?"
"Hujuii?" Inspekta Jada aliuliza kwa mshangao ulioambatana na wasiwasi.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Annah alionekana maeneo ya mji akikatiza katikati ya barabara ya rami bila kujali magari mengi yaliyokuwa yakipita na kupishana kwenye barabara hiyo. Baadhi ya madereva walimpigia honi mfurulizo huku wengine wakimtukana matusi, nawengine kulazimika kusimama na kumuacha Annah apite kwanza.
"Muache kupenda mkiwa wadogo" Alisikika dereva mmoja wa roli akiongea huku anamchungulia Annah dirishani.
Annah alionekana ni kama mwendawazimu kwa namna alivyokuwa anatembea huku akionekana kuwa mtu mwenye mawazo sana. Annah alijikuta kwenye hali hiyo mara tu baada ya hukumu ya Osward kusomwa kuwa hana hatia, baada ya muda kidogo alipata pia taarifa za kukamatwa kwa mwanaume anaempenda kupita kawaida Inspekta Aron. Annah alijikuta anapatwa na wazimu wa ghafula akaanza kutembea hovyo asijue anakoelekea.
Haya ndio aliyokuwa akiyawaza Annah wakati akizidi kwenda mbele bila kujali kuwa alikuwa akipita katikati ya barabara kuu ya rami yenye gari nyingi.
"Kuna wakati binadamu huwafanya binadamu wenzao kuwa wabaya,nimeamini si kila anaefanya ubaya alipenda kuwa mbaya. Tunaishi katika ulimwengu ambao shida zako zinawapa watu wengine furaha na furaha yako inawapa watu wengine shida. Leo hii mbele ya macho yangu nimeona haki ikipindishwa kwa makusudi kabisa kwa ajili ya manufaa ya watu wachache watu wenye NGUVU watu wenye nyazifa kubwa. Sisi tusio na kitu tunaishia kunyanyasika na kuumizwa kila siku, wamemuua baba wakamuua mama, wanampeleka gerezani mwanaume wangu asiye na hatia. Hiki kilio chetu tukipeleke kwa nani, nani atatusikiliza? nani atasimama kutupigania sisi wanyonge?HAKUNA, NASEMA HAKUNA ni sisi wenyewe tunatakiwa kujipambania. Leo naondoka lakini nitarudi tena nikiwa Annah ambaye hawataamini kama ni Annah yule wanayemjua, nitawaadhibu wote waliohusika kuupindisha ukweli, wote waliohusika kuwaua wazazi wangu, na kamwe sito ruhusu Aron wangu aozee gerezani, ndio mimi Annah nimesema".
ITAENDELEA...
Naam huyo ni ANNAH, bila kusahau tayari timu ya ZMLST kutoka Mexico imeshaingia nchini, vipi kuhusu Inspekta Aron?
Sasa rasmi tunakwenda kuuwasha moto wa SEASON 4, karibu...
0756862047
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..............45
Mtunzi: Saul David
ILIPOISHIA....
Ikiwa ni katika hatua za mwisho kabisa za kimahakama kabla ya kesi ya Osward kuamuliwa ghafula katikati hali isiyotegemewa Annah ambae ni shahidi pekee aliekuewa akisubiriwa anafika mahakamani hapo.
Upande wa pili Inspekta Aron aliyepigwa risasi ya mguu pamoja na Najma aliyepoteza fahamu wanafikishwa hospitali kwa ajili ya kupata huduma za matibabu.
Je, ni nini kitafuata?
SASA ENDELEA....
"Unamaanisha huyu mwanamke ndio Annah shahidi uliyeomba tumsubiri hapo awali?" Muendesha mashataka aliuliza swali
"Ndiyo, ndio yeye mheshimiwa"wakili Andrea alijibu
Hakimu pamoja na viongozi wengine wa mahakama walionekana kunong'onezana jambo na mwisho wakafikia makubaliano ya pamoja.
"Sawa tutamsikiliza shahidi wako, naomba Annah sogea mbele utaapa kama ilivyo taratibu kisha utahojiwa na mawakili wote wawili" Alisema hakimu.
Annah alipiga hatua kusogea mbele ya mahakama ile, alipokutana na wakili Andrea akasimama
"Pole sana Annah bila shaka umepitia wakati mgumu sana mpaka kufika hapa, lakini tushukuru mungu umefika salama. Hatukupata muda wa kuongea ila najua hauwezi kushindwa kujieleza, ongea kila kitu ulichokiona na kusikia siku hiyo wakati Osward anafanya yale mauaji" Wakili Andrea aliongea haraka haraka kwa sauti ya chini. Annah alitikisa kichwa chake ikiwa ni ishara kuwa amemuelewa wakili. Baadae taratibu zote za kumuapisha zilikamilika na baadae Annah akapandishwa kizimbani upande wa pili tofauti na ule aliopo mshitakiwa Osward, sasa akawa tayari kwa kuhojiwa. Wakili Andrea ndio alikuwa mtu wa kwanza kumuliza maswali shahidi.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili katika nyumba moja kubwa ya kifahari iliyokuwa imejegwa chini ya mlima mdogo pembeni kidogo ya mji, ilikuwa ni nyumba inayomilikiwa na mtoto wa kwanza wa Rais mstaafu Elizabeth Kulolwa ambaye kwa sasa yuko masomoni nchini Marekani. Nyumba hiyo ilijengwa kwa umiliki wake lakini ukweli ni kwamba ilikuwa ni nyumba ambayo inatumiwa sana na baba yake mzazi yaani Profesa Cosmas Kulolwa. Hapa ndipo alikuwa akipanga na kuendesha mipango yake mingi ya siri hata kipindi akiwa madarakani kama Rais.
Leo hii kwa mara nyingine katika nyumba hii yenye ghorofa sita kwenda juu, Profesa Cosmas anapokea ugeni mkubwa kutoka nchini Mexico ugeni ambao ulikuwa ni muhimu sana kwake.
Miongoni mwa wageni hao waliokuwepo wanaume watatu wa miraba minne waliojazia sana na wote walikuwa wamenyoa vipara mmoja kati yao alikuwa mzungu na wawili waafrika. Wageni wengine walikuwa ni wazungu watatu ambao wote walitoka nchini Mexico alikuwepo profesa Fernando Arturo mkurugenzi mtendaji wa maabara ya ZMLST inayomiliki kirusi cha V-COBOS, alikuwepo Dokta Codrado pamoja na mwanamke mmoja mwenye asili ya kihindi aliitwa Sharma Khumal.
Wote kwa pamoja wakiwa na wenyeji wao ambao ni Profesa Cosmas Kulolwa pamoja na Mkemia mkuu wa serikali Andiwelo katabi walikaa na kuizunguuka meza moja ya duara kisha wakawa wanafanya mazungumzo nyeti sana kwa lugha ya kingereza.
"Tumesubiri vya kutosha na katika kusubiri kwetu tumeona kuna mambo yameanza kuharibika na kama tutaendelea kusubiri zaidi basi tunaweza kujikuta tunapoteza kila kitu" Profesa Fernando alianzisha mazungumzo akatulia kwa muda kisha akaendelea.
"Mpango wetu ni ule ule kurudisha heshima ya maabara yetu ya ZMLST kama ilivyokuwa mwanzo na pili ni kutengeneza mabilioni ya pesa. Hivyo vyote vitaenda kwa pamoja na siraha yetu kubwa ni virusi vya V-COBOS. Ilikuwa tufanye hivyo miaka kadhaa iliyopita lakini virusi vya COVID-19 vilikuja na kutuvurugia ratiba hivyo tukasubiri. Korona imepungua kwa sasa ni wakati wetu wa kuitikisa Dunia tutapeleka mambo haraka haraka ikiwa ni pamoja na kuipata chupa ya kijivu ikiyopotea ndio maana tumekuja na kikosi kazi na hawa wanaume wa shoka hapa ni sehemu tu ya kikosi kazi chetu. Tukilazimika kuua tutaua tukilazimika kuchinja tutachinja ilimradi tu jambo letu lifanikiwe. Tunashukuru profesa Cosmas kwa kumuondoa Dunia Dokta Gondwe kwa sababu tayari alishakuwa kikwanzo kwetu tangu mda mrefu, huu ni mfano unaoonyesha ni jinsi gani hili suala halihitaji masihara hata kidogo. Kama akitokea mwingine akazingua ikiwa ni pamoja na kuleta usaliti basi sitosita kuondoa uhai wake mara moja. Kwa sasa naomba Profesa Cosmas utupe maelezo mafupi ni wapi vilipo vimelea vyetu na ni wapi ilipo chupa ya kijivu alafu baada ya hapo tutajua tuanze na nini" aliongea profesa Fernando hapo Rais mstaafu Profesa Cosmas alikohoa kidogo tayari kuzungumza lakini kabla ya kufanya hivyo mara simu yake katika mfuko wa shati iliita kwa kutoa mtikisiko. Profesa Cosmas aliichukua na kutazama namba ya mpigaji shika akainua macho na kuwatazama wenzake.
"Worry out if its important call just pick up"(usiogope kama ni simu ya muhimu pokea) aliongea Sharma Khumal kwa kingereza chenye rafuzi ya kihindi.
Baada ya kusema hivyo Profesa Cosmas alipokea simu ile kutoka kwa Asia mmoja kati ya kikosi hatari cha kunguru weusi.
"Nipe ripoti" aliongea Pro. Cosmas mara tu baada ya kupokea ile simu
"Mheshimiwa mambo yameharibika" Asia aliongea upande wa pili akiwa nje ya mahakama.
"Kivipi?"
"Yule binti, Annah amekuja hapa mahakamani, dakika za mwisho kabisa mkuu"
"Imekuwaje? Kivipi? Wenzio wako wapi?"
"Sijui, naomba uniambie nini cha kufanya la sivyo kila kitu kitaenda hovyo mheshimiwa, tuna dakika chache tu"
"Sawa subiri nákupigia"
Alisema profesa Cosmas kisha akakataka simu, sura yake ikiwa na wasiwasi kiasi na kila mmoja kwenye kikao kile aligundua hilo.
"Kuna nini?" Aliuliza Dokta Codrado
"Kuna kijana wangu mmoja yuko hatarini kufungwa, nilikuwa kwenye harakati za kumsaidia lakini kwa bahati mbaya mambo yameenda tofauti dakika za mwisho"
"Ni mmoja wetu?" aliuliza Profesa Fernando
"Ndio alikuwa chini ya Dokta Gondwe lakini nataka kumfanya awe chini yangu kwa sababu anajua siri yetu pia yuko vizuri kwa kazi"
"Okay, vipi unachochote cha kufanya kuzuia asifungwe kwa muda uliobaki au nikusaidie?"
Aliuliza Profesa Fernando Profesa Cosmas Kulolwa akawa kimya.
"Wewe ni Rais inakuaje suala dogo kama hili likushinde"
"Ni kweli lakini tatizo ni muda nahisi nimechelewa sana, dakika si nyingi hukumu ya huyu kijana itasomwa"
"Okay, nieleze kwa kina kisha tujue tunafanyaje eleza haraka haraka" Alisema Profesa Fernando.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati huo kesi ilianza kusikilizwa mahakamani kwa mara nyingine Annah akiwa kizimbani kama shahidi...
"Annah, ni vipi unamfahamu mtuhumiwa" aliuliza swali hili wakili Andrea
"Nilimuona siku ya birthday yangu, kwenye mgahawa wa Affati"
"Kwa maana hiyo unataka kusema wewe ni mmoja kati ya watu waliokuwepo siku ambayo kulitokea mauaji pale katika mgahawa wa Affati? Tafadhali unaweza kutueleza japo kwa undani kila ulichokiona siku hiyo?"
Andrea aliuliza swali jingine na hapo Annah alieleza kila kitu kuanzia mwanzo mpaka mwisho hakuacha kitu.
"Mheshimiwa hakimu sina swali jingine" wakili Andrea alimaliza huku akiwa na imani kabisa kuwa kwa maelezo aliyoyatoa Annah yalitosha kabisa kumuweka Osward hatiani na nilazima angefungwa
Baada ya hapo hakimu alimruhusu wakili upande wa utetezi kumuuliza shahidi maswali. Kwa ufupi wakili huyu hakuwa amejipanga kumuuliza Annah maswali ya kumbana kitendo cha Annah kuingia ghafula mahakamani hapo kilivuruga kila kitu. Ilibidi tu atumie uzoefu wa kawaida alionao kwani maelezo ya Annah yalikuwa yameshiba.
"Annah unajua kwamba ikibainika unasema uongo mbele ya mahakama kifungo chake ni zaidi ya miaka 15 jela?"
"Najua, yote ninayoyasema ni kweli tupu"
Annah alijibu kwa kujiamini wakati huo kuna askari aliingia ghafula mahakamani hapo akapiga hatua hadi ilipo meza ya hakimu, askari huyu alikuwa na kipande cha karatasi akafika na kumkabidhi hakimu kisha akaondoka. Hii ilikuwa ni kinyume kabisa na utaratibu lakini hakuna aliyehoji. Hakimu alipofungua lile karatasi kulikuwa na picha ndogo kama passport kisha akasoma maelezo yaliyokuwa kwenye karatasi. Ni Andrea pekee ndio aliyeuona mshtuko alioupata hakimu mara baada ya kusoma maelezo yale moja kwa moja akajua kuna kitu hakipo sawa. Wakati huo wakili alizidi kumuuliza maswali Annah ambaye naye aliyajibu kwa ufasaha sana bila kupepesa.
[emoji294][emoji294][emoji294]
NUSU SAA BAADAE..
Gari moja ilifunga breki kali nje ya mahakama ya Ilonga, Inspekta Jada akiwa ndio dereva alishuka upesi na kuanza kupiga hatua kuelekea jengo kuu la mahakama hiyo. Alipotazama mazingira aliona kuna kila dalili kuwa amechewa sana, watu walikuwa ni wachache mno na wengine ndio walikuwa wakimalizaka kuondoka.
Akiwa ameukaribia mlango wa kuingia ndani ya jengo la mahakama Inspekta Jada anakutana na mwanasheria ambaye alikuwa ni wakili wa kesi ile bwana Andrea. Uso wa Andrea uliojaa huzuni ulitosha kabisa kumfanya Inspekta Jada aelewe kuwa mambo sio mazuri.
"Annah alifika?" Hili ndio lilikuwa swali la kwanza kutoka kwa Inspekta Jada.
"Alifika" Andrea alijibu kifupi huku akionekana mtu mwenye kukata tamaa
"Sasa imekuwaje, kwa nini tumeshindwa Andrea?"
"Ni nguvu Inspekta, hatukuwa na nguvu ila haki yetu ilikuwepo wazi" alijibu Andrea
"Una maana gani?"
"Namaanisha kuna nguvu ya ziada imetumika kupindua haki yetu, hakimu alitishiwa katika dakika za mwisho kabisa kabla ya kusoma hukumu kuna kila dalili kuwa watu wazito na wakubwa wameingilia hii kesi" alieleza Andrea japo ilikuwa ni hisia zake tu lakini alichokiongea kilikuwa sahihi kabisa.
Kimya kilitawala huku wote wakionekana kuwa na masikitiko makubwa sana.
" Vipi kuhusu Inspekta Aron" aliuliza Andrea
"Amekamatwa yupo hospitali anatolewa risasi aliyopigwa mguuni"
"Mmh! hali ni mbaya Inspekta Jada"
" Tena sana, Annah yuko wapi sasa?"
"Si..sijui alikuwepo hapa?"
"Hujuii?" Inspekta Jada aliuliza kwa mshangao ulioambatana na wasiwasi.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Annah alionekana maeneo ya mji akikatiza katikati ya barabara ya rami bila kujali magari mengi yaliyokuwa yakipita na kupishana kwenye barabara hiyo. Baadhi ya madereva walimpigia honi mfurulizo huku wengine wakimtukana matusi, nawengine kulazimika kusimama na kumuacha Annah apite kwanza.
"Muache kupenda mkiwa wadogo" Alisikika dereva mmoja wa roli akiongea huku anamchungulia Annah dirishani.
Annah alionekana ni kama mwendawazimu kwa namna alivyokuwa anatembea huku akionekana kuwa mtu mwenye mawazo sana. Annah alijikuta kwenye hali hiyo mara tu baada ya hukumu ya Osward kusomwa kuwa hana hatia, baada ya muda kidogo alipata pia taarifa za kukamatwa kwa mwanaume anaempenda kupita kawaida Inspekta Aron. Annah alijikuta anapatwa na wazimu wa ghafula akaanza kutembea hovyo asijue anakoelekea.
Haya ndio aliyokuwa akiyawaza Annah wakati akizidi kwenda mbele bila kujali kuwa alikuwa akipita katikati ya barabara kuu ya rami yenye gari nyingi.
"Kuna wakati binadamu huwafanya binadamu wenzao kuwa wabaya,nimeamini si kila anaefanya ubaya alipenda kuwa mbaya. Tunaishi katika ulimwengu ambao shida zako zinawapa watu wengine furaha na furaha yako inawapa watu wengine shida. Leo hii mbele ya macho yangu nimeona haki ikipindishwa kwa makusudi kabisa kwa ajili ya manufaa ya watu wachache watu wenye NGUVU watu wenye nyazifa kubwa. Sisi tusio na kitu tunaishia kunyanyasika na kuumizwa kila siku, wamemuua baba wakamuua mama, wanampeleka gerezani mwanaume wangu asiye na hatia. Hiki kilio chetu tukipeleke kwa nani, nani atatusikiliza? nani atasimama kutupigania sisi wanyonge?HAKUNA, NASEMA HAKUNA ni sisi wenyewe tunatakiwa kujipambania. Leo naondoka lakini nitarudi tena nikiwa Annah ambaye hawataamini kama ni Annah yule wanayemjua, nitawaadhibu wote waliohusika kuupindisha ukweli, wote waliohusika kuwaua wazazi wangu, na kamwe sito ruhusu Aron wangu aozee gerezani, ndio mimi Annah nimesema".
ITAENDELEA...
Naam huyo ni ANNAH, bila kusahau tayari timu ya ZMLST kutoka Mexico imeshaingia nchini, vipi kuhusu Inspekta Aron?
Sasa rasmi tunakwenda kuuwasha moto wa SEASON 4, karibu...
0756862047