The so called 'GOD' from religions

The so called 'GOD' from religions

Katika Uumbaji wa Mungu binadamu wa Kwanza aliyeumbwa na Mungu ni Adamu ambaye alipuliziwa pumzi na Mungu na uhai ukaanza...hilo thibitisho la kwanza la uwepo wa Mungu....nataka wanaopinga Uwepo wa Mungu watoe uthibitisho uhai uliingiaje ulimwenguni!
Hujathibitisha, unahadithia hadithi uliyokaririshwa.

Unajuaje hiyo habari ni ya ukweli na si ya kutungwa tu?
 
Hujathibitisha kwamba mungu yupo.

Hujatueleza kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana.
Huko kuumba hivyo alivyoumba,ndio kuonyesha Mungu yupo,na hakuna anaweza kuondoa hivyo alivyoumba yeye,kama wewe huamini kama yupo,ondoa hayo mema na mabaya alitoweka Mungu,tuone kama utaweza.
 
Hujathibitisha, unahadithia hadithi uliyokaririshwa.

Unajuaje hiyo habari ni ya ukweli na si ya kutungwa tu?
Kama ni ya kutunga lete yako,isiyotungwa.Huko kukataa uwepo wa Mungu,ndio uthibitisho wa kuwepo Mungu.
 
Ukisema Mungu hayupo,ndio uthibitisho wa kuwepo Mungu.Huwezi kusema hayupo,ila ni baada ya kuwepo,kama asingekuwako,usingesema hayupo,kwasababu hayupo.Utasemaje hayupo ikiwa hayupo?Ila utasema hayupo kwa kuwepo Yupo.
 
Hujathibitisha, unahadithia hadithi uliyokaririshwa.

Unajuaje hiyo habari ni ya ukweli na si ya kutungwa tu?
Habari ni ya kweli ndomana hadi leo bado unaitwa Binadamu sio sokwe jina ambalo limetokana na mtu wa kwanza kwenye uumbaji ambaye ni adamu!
 
Hujathibitisha, unahadithia hadithi uliyokaririshwa.

Unajuaje hiyo habari ni ya ukweli na si ya kutungwa tu?
jibu swali uhai uliingiaje duniani kwa nyinyi msioamini uwepo wa Mungu
 
Huko kuumba hivyo alivyoumba,ndio kuonyesha Mungu yupo,na hakuna anaweza kuondoa hivyo alivyoumba yeye,kama wewe huamini kama yupo,ondoa hayo mema na mabaya alitoweka Mungu,tuone kama utaweza.
Hujajibu swali nililouliza.

Na kama kuna swali umejibu, silo nililouliza.

Sijasema kina anayeweza kuondoa.

Nimeuliza, unajua kwa nini mungu kaumba hivyo?

Jibu najua, kumba hivyo jwa sababu hii.

Au sijui.

Ukisema alivyoumba hakuna anayeweza kuondoa, unaleta habari ambayo sijaiwekea swali.

Unajibu swali ambalo hujaulizwa.

Ilhali like swali uliloulizwa, la kwa nini mungu huyo kaumba hivi, hujalijibu.
 
jibu swali uhai uliingiaje duniani kwa nyinyi msioamini uwepo wa Mungu
Na wanaopinga kuwepo kwa Mungu ukiwaita masokwe ndio wakwanza,kulalamika,wanavunjiwa haki za kibinadamu.Wakati Mungu ndiye aliyemuumba Adamu,baba wa bin Adam wote.
Na wanakubali kuitwa bin Adam,lakini aliyemuumba huyo Adam,akapatikana yeye,asema hayupo."Akili ni mali"
 
Kama ni ya kutunga lete yako,isiyotungwa.Huko kukataa uwepo wa Mungu,ndio uthibitisho wa kuwepo Mungu.
Kama kukataa kwangu kuwepo kwa mungu ni uthibitisho wa kuwepo kwa mungu, basi kukubali kwako kuwepo kwa mungu ni uthibitisho wa kutokuwepo kwa mungu.

Kwa fikira hizo, mungu huyu yupo na hayupo katika wakati mmoja huu huu.

Hapo ndipo utakapoona jinsi habari uliyoleta ilivyo fyongo.
 
Habari ni ya kweli ndomana hadi leo bado unaitwa Binadamu sio sokwe jina ambalo limetokana na mtu wa kwanza kwenye uumbaji ambaye ni adamu!
Kwa hiyo tukiita binadamu sokwe atageuka sokwe?
 
Kama kukataa kwangu kuwepo kwa mungu ni uthibitisho wa kuwepo kwa mungu, basi kukubali kwako kuwepo kwa mungu ni uthibitisho wa kutokuwepo kwa mungu.

Kwa fikira hizo, mungu huyu yupo na hayupo katika wakati mmoja huu huu.

Hapo ndipo utakapoona jinsi habari uliyoleta ilivyo fyongo.
Huwezi sema hayupo,ila ni kuwa yupo.Kisichokuwepo hakisemwi hakipo.Ila kilichopo ndio husemwa hakipo.kwa kusema Mungu hayupo,ndio uthibitisho wa kuwepo Mungu.
 
Huwezi sema hayupo,ila ni kuwa yupo.Kisichokuwepo hakisemwi hakipo.Ila kilichopo ndio husemwa hakipo.kwa kusema Mungu hayupo,ndio uthibitisho wa kuwepo Mungu.
Kwa hiyo nikisema "pembetatu duara haipo".

Hilo litafanya "pembetatu duara" iwepo?
 
Ukisema Mungu hayupo,ndio uthibitisho wa kuwepo Mungu.Huwezi kusema hayupo,ila ni baada ya kuwepo,kama asingekuwako,usingesema hayupo,kwasababu hayupo.Utasemaje hayupo ikiwa hayupo?Ila utasema hayupo kwa kuwepo Yupo.
Ndo maana Kiranga kakwambia,"You have crazy way of thinking"

Mimi naweza kutunga jina hapa hapa,

Tuseme,Mzee pxkqz

Halafu nikaja kukwambia wewe,huyu mzee pxkqz ndiye aliyekuwa mwalimu wa Alexander mkuu

Na huyu Mzee pxkqz,alikuwa anaishi Afrika

Lakini ukweli ni kuwa,hili jina nimelitunga hapa hapa

Mtu mwenye akili timamu,atahoji

Alexander mkuu,hakuishi Afrika,iweje awe na mwalimu kutoka Afrika?

Baada ya kufikiria kwa kina,akahitimisha kwa kusema mzee pxkqz hayupo

Ina maana baada ya yeye kusema hivyo,atakuwa amethibitisha uwepo wa Mzee pxqz?

Na Mungu yupo hivyo hivyo,ni jina tu lililopewa sifa zinazojipinga.
 
Habari ni ya kweli ndomana hadi leo bado unaitwa Binadamu sio sokwe jina ambalo limetokana na mtu wa kwanza kwenye uumbaji ambaye ni adamu!
Usitumie kigezo cha lugha,kuthibitisha hoja yako

Kiswali,tunaitwa wanaadam

Kingereza, humans,ambayo haina mahusiano yoyote na Adam

Kila lugha inajina lake,kuna kichina,kikorea n.k
 
utamwitaje sokwe wakati sio sokwe?
Kwa hiyo unadhihirisha kuita kitu si lazima kiwe hivyo.

Kwamba, kumuita mtu "binadamu" sio uthibitisho kwanba alikuwapo mtu anaitwa Adamu?

Ndiyo maana nikakuuliza uthibitishe. Maana habari ya "binadamu" tu, inaweza kuwa hadithi. Huko Japan na China mtu haitwi binadamu, ina maana wao kwao vipi hapo?
 
Kwa hiyo unadhihirisha kuita kitu si lazima kiwe hivyo.

Kwamba, kumuita mtu "binadamu" sio uthibitisho kwanba alikuwapo mtu anaitwa Adamu?

Ndiyo maana nikakuuliza uthibitishe. Maana habari ya "binadamu" tu, inaweza kuwa hadithi. Huko Japan na China mtu haitwi binadamu, ina maana wao kwao vipi hapo?
Mi nimekupa uthibitisho huo katika maandiko matakatifu..ila unayapinga nakusema hadithi...unapopinga pinga kwa kuleta ya kwako ambayo sio hadithi kinyume cha hapo unapinga ilimradi kupinga
 
Mi nimekupa uthibitisho huo katika maandiko matakatifu..ila unayapinga nakusema hadithi...unapopinga pinga kwa kuleta ya kwako ambayo sio hadithi kinyume cha hapo unapinga ilimradi kupinga
Unafahamu maana ya kuthibitisha?

Unajua tofauti ya uthibitisho, hadithi na mahubiri?
 
Back
Top Bottom