Tido Mhando: Awamu ya Hayati Magufuli imechangia 'Comedy Journalism'

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hii ni miongoni mwa Kauli alizotoa Mwenyekiti wa Kamati ya kuchunguza Dhiki au Matatizo ya uchumi yanavyovikabili vyombo vya habari nchini Tanzania , Tido Muhando.

Mhando ameyasema hayo alipotoa hotuba yake kwenye kongamano la Maendeleo ya sekta ya habari linaloendelea Dar es Salaam

Ni nini hasa maana ya Comedy Journalism?

--
Kutokana na mazingira magumu ya sheria na siasa ambavyo vyombo vya habari nchini vimepitia, vyombo hivi, hivi sasa vimejikuta vikijidhibiti kutoa habari ambazo zinasimamia uwajibikaji wa umma (Public Accountability Strories). Matokeo yake ni kwamba vyomo vya habari kubeba maudhui mengi zaidi ya burudani, mapenzi, mziki, michezo, tamthilia, filamu, na vipindi vya mjadala vyenye tija ndogo kwa jamii.

Aina hii ya uandishi inaleta madhara mawili makubwa;

  • "Inadhohofisha uandishi wenye kuzingatia uwajibikaji wa umma ambao ni muhimu sana kwenye jamii na kutengeneza kizazi kufikiria sawasawa kwa kuwa kinayumbishwa na maudhui mepesi sana.
  • "Sasa hivi kumekuwa na comedy journalism, mambo mengi ya mzahamzaha yanaonekana kama vitu vya kawaida. Na yot ehii ni kutokana na wasiwasi ambao waaandishi wa habari wamekuwa wanaogopa kutokana na mazingira magumu ambayo yaliletwa hapo mwanzo.
Sasa tunashukuru kwenye serikali yako mambo haya yameanza kuondoka kidogo kidogo. Lakini kama ulivyokuwa umetoa neno la viongozi hasa wa ngazi za juu za kiasiasa hasa ambao wamekuwa wakiingiza ubabe ubabe katika sekta hii ya uandishi wa habari. Ubababe huo umekuwa mwingi, na tunaomba vile vile ungeweza kutusaidia kukabiliana na suala hili. - Amesema Tido


=====

Kusoma kilichojiri siku ya kwanza ya Kongamano pita hapa:

- Rais Samia akishiriki Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari, Juni 18, 2024


=====
Mwenyekiti wa Kamati ya kufuatilia hali ya uchumi wa vyombo vya Habari, Tido Mhando amesema kutokana na mazingira magumu ya kisheria na kisiasa ambayo vyombo vya habari vimepitia katika Serikali ya awamu ya Tano iliyokuwa chini ya Rais John Magufuli, vyombo vingi vya habari vimejidhibiti kutoa habari za uwajibikaji kwa umma na kuhamia maudhui mepesi ya mzaha ‘comedy journalism.’

Pia amesema vyombo hivyo sasa vimebeba maudhui ya burudani, mapenzi, muziki, michezo, tamthilia na vipindi vyenye tija ndogo kwa jamii.

Mhando ameeleza hayo leo Jumanne wakati akiwasilisha mapendekezo ya kamati yake kwa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ni mgeni rasmi kwenye kongamano la maendeleo ya sekta ya habari.

Mhando amesema aina hiyo ya uandishi inaleta madhara mawili makubwa, kwanza kudhoofisha uandishi unaozongatia uwajibikaji wa umma ambao ni muhimu kwenye jamii lakini pia kutengeneza kizazi kisochoweza kufikiria sawasawa kwa kuwa kinadumazwa na maudhui mepesi.

“Bila shaka sasa hivi tunaelewa kinachoendelea kuna kitu kinaitwa Comedy Journalism kumekuwa na mambo mengi ya mzaha mzaha yote haya yanatokana na wasiwasi waliokuwa nao waandishi, wamekuwa wanaogopa kutokana na mazingira magumu yaliyoletwa hapo mwanzo.

“Tunashukuru kwenye awamu yako hii ya sita yameanza kuondoka kidogo kidogo lakini kama ulivyotoa neno kwa viongozi hawa wa kisiasa wamekuwa wakileta ubabe ubabe katika sekta hii ya habari.

“Ubabe umekuwa mwingi tunaomba utasaidie kukabiliana na suala hili. Nina hakika hakuna chombo cha habari ambacho hakijatikiswa na ubabe huu kutoka kwa baadhi ya viongozi mifano ni mingi lakini nisingependa kuitaja hapa kwa sababu ya muda,” amesema.
 
Hii ni miongoni mwa Kauli alizotoa Mwenyekiti wa Kamati ya kuchunguza Dhiki au Matatizo ya uchumi yanavyovikabili vyombo vya habari nchini Tanzania , Tido Muhando.

Mhando ameyasema hayo alipotoa hotuba yake kwenye kongamano la Maendeleo ya sekta ya habari linaloendelea Dar es Salaam

Ni nini hasa maana ya Comedy Journalism?

View attachment 3019964
CHAWA mchafu huyu mzee
 
Hii ni miongoni mwa Kauli alizotoa Mwenyekiti wa Kamati ya kuchunguza Dhiki au Matatizo ya uchumi yanavyovikabili vyombo vya habari nchini Tanzania , Tido Muhando.

Mhando ameyasema hayo alipotoa hotuba yake kwenye kongamano la Maendeleo ya sekta ya habari linaloendelea Dar es Salaam

Ni nini hasa maana ya Comedy Journalism?

View attachment 3019964
Huo ni ukweli usiofichika. MAGUFULI aliharibu sana. Kama unaweza ukabana demokrasia ya vyama vingi na uhuru wa maoni ambavyo vinatambulika na Katiba iliyokuweka madarakani unakuwa umeturudisha nyuma miaka 35 kwenye chama kimoja
 
Huo ni ukweli usiofichika. MAGUFUKI aliharibu sana. Kama unaweza ukabana demokrasia ya vyama vingi na uhuru wa maoni ambavyo vinatambulika na Katiba iliyokuweka madarakani unakuwa umeturudisha nyuma miaka 35 kwenye chama kimoja
Ashukuriwe Mungu
 
Kutokana na mazingira magumu ya sheria na siasa ambavyo vyombo vya habari nchini vimepitia, vyombo hivi, hivi sasa vimejikuta vikijidhibiti kutoa habari ambazo zinasimamia uwajibikaji wa umma (Public Accountability Strories). Matokeo yake ni kwamba vyomo vya habari kubeba maudhui mengi zaidi ya burudani, mapenzi, mziki, michezo, tamthilia, filamu, na vipindi vya mjadala vyenye tija ndogo kwa jamii.

Aina hii ya uandishi inaleta madhara mawili makubwa;

  • "Inadhohofisha uandishi wenye kuzingatia uwajibikaji wa umma ambao ni muhimu sana kwenye jamii na kutengeneza kizazi kufikiria sawasawa kwa kuwa kinayumbishwa na maudhui mepesi sana.
  • "Sasa hivi kumekuwa na comedy journalism, mambo mengi ya mzahamzaha yanaonekana kama vitu vya kawaida. Na yot ehii ni kutokana na wasiwasi ambao waaandishi wa habari wamekuwa wanaogopa kutokana na mazingira magumu ambayo yaliletwa hapo mwanzo.
Sasa tunashukuru kwenye serikali yako mambo haya yameanza kuondoka kidogo kidogo. Lakini kama ulivyokuwa umetoa neno la viongozi hasa wa ngazi za juu za kiasiasa hasa ambao wamekuwa wakiingiza ubabe ubabe katika sekta hii ya uandishi wa habari. Ubababe huo umekuwa mwingi, na tunaomba vile vile ungeweza kutusaidia kukabiliana na suala hili. - Amesema Tido


=====

Kusoma kilichojiri siku ya kwanza ya Kongamano pita hapa:

- Rais Samia akishiriki Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari, Juni 18, 2024
 
Huyo kastaafu azam anatafuta ukurugenzi ikulu..ni awamu ya Magufuli ndipo lilitoka tamko waandishi lazima wawe na diploma. Lakini awamu ya Magufuli hatukusikia magazeti ya ijumaa, uwazi wala msanii.
Umenikumbusha mbali sana. Haya magazeti bado yapo kweli ama yalikufa? Ijumaa, ijumaa wikienda, uwazi, msanii, Risasi, Kiu ya Jibu(My favorite miaka hiyo).
 
Huyo kastaafu azam anatafuta ukurugenzi ikulu..ni awamu ya Magufuli ndipo lilitoka tamko waandishi lazima wawe na diploma. Lakini awamu ya Magufuli hatukusikia magazeti ya ijumaa, uwazi wala msanii.
Magazeti ya Ijumaa na Uwazi yaliishi kwa scandal/faragha za watu. Kutungwa kwa sheria ulinzi wa faragha ndiyo ilikuwa kitanzi na hatinaye kifi cha magazeti hayo, na sheria hiyo ilitungwa dakika za mwisho za awamu ya JK.
 
Baada ya miaka 5 wataulizwa legacy yao ni nini, watasema ni kumsimanga Magufuli na kusafiri nje ya nchi
Kifo nilikiogopa na kukiheshimu sana kilivyopita na Mzilankede wa Chato bila kupepesa macho!
......Mwamba aendelee kupumzika huko alikotanguliza wengine.
Good news: Wote tutamfuata kila mtu kwa wakati wake.
 
Back
Top Bottom